Zaburi 108 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 108:1-13

Zaburi 108

Kuomba Msaada Dhidi Ya Adui

(Zaburi 57:7-11; 60:5-12)

Wimbo. Zaburi ya Daudi.

1108:1 Za 112:7; 119:30, 112; 18:49Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti;

nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.

2108:2 Ay 21:12Amka, kinubi na zeze!

Nitayaamsha mapambazuko.

3Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa;

nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.

4108:4 Hes 14:18; Kum 7:9; Kut 34:6; Za 36:5; Mik 7:18-20Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu;

uaminifu wako unazifikia anga.

5108:5 Za 8:1; 57:5Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,

utukufu wako na uenee duniani kote.

6108:6 Ay 40:14Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume,

ili wale uwapendao wapate kuokolewa.

7108:7 Za 89:35; 68:35; 102:19; Mwa 12:6; 33:17Mungu amenena kutoka patakatifu pake:

“Nitaigawa Shekemu kwa ushindi

na kulipima Bonde la Sukothi.

8108:8 Za 78:68; Mwa 49:10Gileadi ni yangu, Manase ni yangu,

Efraimu ni kofia yangu ya chuma,

nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.

9108:9 Mwa 19:37; 2Sam 8:1, 13-14Moabu ni sinia langu la kunawia,

juu ya Edomu natupa kiatu changu;

nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”

10108:10 Za 60:9Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome?

Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?

11108:11 Za 44:9Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi,

na hutoki tena na majeshi yetu?

12108:12 Isa 10:3; 30:3, 5; 31:3; Yer 2:36; 17:7; Za 118:8; 146:3Tuletee msaada dhidi ya adui,

kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.

13108:13 Za 44:5; Isa 22:5; 63:3, 6; 25:10; Mao 1:15; Mal 4:3; Ufu 14:9Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi,

naye atawaponda adui zetu.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Salmo 108:1-13

Salmo 108

108:1-5Sal 57:7-11

108:6-13Sal 60:5-12

Cántico. Salmo de David.

1Firme está, oh Dios, mi corazón;

¡voy a cantarte salmos, gloria mía!

2¡Despertad, arpa y lira!

¡Haré despertar al nuevo día!

3Te alabaré, Señor, entre los pueblos;

te cantaré salmos entre las naciones.

4Pues tu amor es tan grande que rebasa los cielos;

¡tu verdad llega hasta el firmamento!

5Tú, oh Dios, estás sobre los cielos,

y tu gloria cubre toda la tierra.

6Líbranos con tu diestra, respóndeme

para que tu pueblo amado quede a salvo.

7Dios ha dicho en su santuario:

«Triunfante repartiré a Siquén,

y dividiré el valle de Sucot.

8Mío es Galaad, mío es Manasés;

Efraín es mi yelmo y Judá, mi cetro.

9En Moab me lavo las manos,

sobre Edom arrojo mi sandalia;

sobre Filistea lanzo gritos de triunfo».

10¿Quién me llevará a la ciudad fortificada?

¿Quién me mostrará el camino a Edom?

11¿No es Dios quien nos ha rechazado?

¡Ya no sales, oh Dios, con nuestros ejércitos!

12Bríndanos tu ayuda contra el enemigo,

pues de nada sirve la ayuda humana.

13Con Dios obtendremos la victoria;

¡él pisoteará a nuestros enemigos!