Zaburi 102 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Zaburi 102:1-28

Zaburi 102

Maombi Ya Mtu Mwenye Taabu

Maombi ya mtu aliyechoka. Anapoteseka na kumimina malalamiko yake kwa Bwana.

1102:1 Za 4:1; Kut 2:23Ee Bwana, usikie maombi yangu,

kilio changu cha kuomba msaada kikufikie.

2102:2 Za 22:24; 31:2; 88:2; 2Fal 19:16Usinifiche uso wako

ninapokuwa katika shida.

Unitegee sikio lako,

ninapoita, unijibu kwa upesi.

3Kwa kuwa siku zangu zinatoweka kama moshi,

mifupa yangu inaungua kama kaa la moto.

4102:4 Za 37:2; 90:5-6; 1Sam 1:7; Ezr 10:6; Ay 33:26Moyo wangu umefifia na kunyauka kama jani,

ninasahau kula chakula changu.

5102:5 Za 6:6Kwa sababu ya kusononeka kwangu kwa uchungu,

nimebakia ngozi na mifupa.

6102:6 Isa 34:11; Sef 2:14; Kum 14:15-17; Ay 30:29Nimekuwa kama bundi wa jangwani,

kama bundi kwenye magofu.

7102:7 Za 77:4; 38:11Nilalapo sipati usingizi,

nimekuwa kama ndege mpweke

kwenye paa la nyumba.

8102:8 Za 31:11; 42:10; Mdo 23:12Mchana kutwa adui zangu hunidhihaki,

wale wanaonizunguka hutumia jina langu kama laana.

9102:9 Isa 44:20; Za 6:6; 42:3; 80:5Ninakula majivu kama chakula changu

na nimechanganya kinywaji changu na machozi

10102:10 Za 7:11; 38:3; 30:7kwa sababu ya ghadhabu yako kuu,

kwa maana umeniinua na kunitupa kando.

11102:11 1Nya 29:15; Ay 14:2; 8:12; Za 39:6; Yak 1:10Siku zangu ni kama kivuli cha jioni,

ninanyauka kama jani.

12102:12 Kut 15:18; 3:15; Isa 55:13; 63:12; 40:2; Za 135:13Lakini wewe, Ee Bwana, umeketi katika kiti chako cha enzi milele,

sifa zako za ukuu zaendelea vizazi vyote.

13102:13 Za 119:126; 44:26; 77:7; Kum 32:36; 1Fal 3:26; Isa 54:8; 60:10; 40:2; Zek 10:6; Kut 13:10; Dan 8:19; Mdo 1:7Utainuka na kuihurumia Sayuni,

kwa maana ni wakati wa kumwonyesha wema;

wakati uliokubalika umewadia.

14102:14 Dan 9:2Kwa maana mawe yake ni ya thamani kwa watumishi wako,

vumbi lake lenyewe hulionea huruma.

15102:15 1Fal 8:43; Isa 2:2; Za 67:7; 76:12; 138:4; 148:11Mataifa wataogopa jina la Bwana,

wafalme wote wa dunia watauheshimu utukufu wako.

16102:16 Za 51:18; 8:1; Isa 60:1, 2Kwa maana Bwana ataijenga tena Sayuni

na kutokea katika utukufu wake.

17102:17 Neh 2:8; 1Fal 8:29; Za 4:1; 6:9Ataitikia maombi ya mtu mkiwa,

wala hatadharau hoja yao.

18102:18 Rum 4:24; 15:4; Za 22:31; 1Kor 10:1; Isa 43:21Hili na liandikwe kwa ajili ya kizazi kijacho,

ili taifa litakaloumbwa baadaye waweze kumsifu Bwana:

19102:19 Kum 26:15; Za 14:2; 53:2Bwana alitazama chini kutoka patakatifu pake palipo juu,

kutoka mbinguni alitazama dunia,

20102:20 Za 68:6; Lk 4:19kusikiliza vilio vya uchungu vya wafungwa

na kuwaweka huru wale waliohukumiwa kufa.”

21102:21 Za 22:22; 9:14Kwa hiyo jina la Bwana latangazwa huko Sayuni

na sifa zake katika Yerusalemu,

22102:22 Hos 1:11; Za 22:27; Isa 49:22, 23; Zek 8:20-23wakati mataifa na falme zitakapokusanyika

ili kumwabudu Bwana.

23102:23 Za 39:5Katika kuishi kwangu alivunja nguvu zangu,

akafupisha siku zangu.

24102:24 Mwa 21:33; Ay 36:26; Za 90:2; Hab 1:12; Ufu 1:4, 8Ndipo niliposema:

“Ee Mungu wangu, usinichukue katikati ya siku zangu;

miaka yako inaendelea vizazi vyote.

25102:25 Mwa 1:1; Ebr 1:10; 2Nya 2:12; Za 8:3; Kut 20:11; Ay 38:4-7Hapo mwanzo uliweka misingi ya dunia,

nazo mbingu ni kazi ya mikono yako.

26102:26 Rum 8:20; Isa 51:6; 13:10, 13; 66:21; 34:4; Mt 24:35; Yoe 2:10; Eze 32:8; 2Pet 3:7-10; Ufu 20:11Hizi zitatoweka, lakini wewe utadumu,

zote zitachakaa kama vazi.

Utazibadilisha kama nguo

nazo zitaondoshwa.

27102:27 Hes 23:19; Ebr 13:8; Mal 3:6; Yak 1:17; Za 9:7Lakini wewe, U yeye yule,

nayo miaka yako haikomi kamwe.

28102:28 Za 69:36; 25:13; 89:4Watoto wa watumishi wako wataishi mbele zako;

wazao wao wataimarishwa mbele zako.”

Ketab El Hayat

مزمور 102:1-28

الْمَزْمُورُ الْمِئَةُ وَالثَّانِي

صَلاةُ الْمِسْكِينِ إِذَا أَعْيَا وَسَكَبَ شَكْوَاهُ أَمَامَ الرَّبِّ

1يَا رَبُّ اسْتَمِعْ صَلاتِي وَلْيَصِلْ إِلَيْكَ صُرَاخِي. 2لَا تَحْجُبْ وَجْهَكَ عَنِّي فِي يَوْمِ ضِيقِي، بَلْ أَمِلْ نَحْوِي أُذُنَكَ. اسْتَجِبْ لِي سَرِيعاً يَوْمَ أَدْعُوكَ، 3لأَنَّ أَيَّامِي قَدْ تَبَدَّدَتْ كَالدُّخَانِ، وَعِظَامِي اضْطَرَمَتْ كَالْوَقِيدِ. 4قَلْبِي مَنْكُوبٌ وَيَابِسٌ كَالْعُشْبِ الْجَافِّ، حَتَّى غَفِلْتُ عَنْ أَكْلِ طَعَامِي. 5الْتَصَقَتْ عِظَامِي بِلَحْمِي مِنْ جَرَّاءِ أَنَّاتِي الْمُرْتَفِعَةِ. 6صِرْتُ أَشْبَهَ بِبَجْعِ الْبَرَارِي، وَمِثْلَ بُومَةِ الْخَرَائِبِ. 7أَرِقْتُ، وَصِرْتُ كَالْعُصْفُورِ الْمُنْفَرِدِ عَلَى السَّطْحِ. 8عَيَّرَنِي أَعْدَائِي طُولَ النَّهَارِ، وَالسَّاخِرُونَ الْحَانِقُونَ عَلَيَّ، جَعَلُوا اسْمِي لَعْنَةً، 9فَقَدْ أَكَلْتُ الرَّمَادَ كَالْخُبْزِ، وَمَزَجْتُ شَرَابِي بِالدُّمُوعِ، 10بِسَبَبِ غَضَبِكَ وَسَخَطِكَ لأَنَّكَ قَدْ رَفَعْتَنِي ثُمَّ طَرَحْتَنِي بِعُنْفٍ. 11عُمْرِي أَشْبَهُ بِظِلٍّ مُتَقَلِّصٍ، وَأَنَا مِثْلُ الْعُشْبِ أَذْوِي.

12أَمَّا أَنْتَ يَا رَبُّ فَجَالِسٌ عَلَى عَرْشِكَ إِلَى الأَبَدِ، وَذِكْرُكَ بَاقٍ مَدَى الدَّهْرِ. 13أَنْتَ تَقُومُ وَتَرْحَمُ صِهْيَوْنَ لأَنَّهُ قَدْ أَزِفَ وَقْتُ إِظْهَارِ رِضَاكَ، 14فَإِنَّ عَبِيدَكَ يُسَرُّونَ بِحِجَارَتِهَا، يَشْتَاقُونَ إِلَى ذَرَّاتِ تُرَابِهَا. 15فَتَخْشَى الأُمَمُ اسْمَ الرَّبِّ، وَيَهَابُ جَمِيعُ مُلُوكِ الأَرْضِ مَجْدَكَ. 16لأَنَّ الرَّبَّ بَنَى صِهْيَوْنَ وَتَجَلَّى فِي مَجْدِهِ. 17الْتَفَتَ إِلَى صَلاةِ الْبَائِسِينَ وَلَمْ يَرْفُضْ دُعَاءَ الْمُتَضَايِقِينَ. 18يُكْتَبُ هَذَا لِلْجِيلِ الآتِي الَّذِي سَيُخْلَقُ فَيُسَبِّحُ الرَّبَّ. 19تَطَلَّعَ الرَّبُّ مِنْ عَلْيَاءِ مَقْدِسِهِ، مِنَ السَّمَاوَاتِ نَظَرَ إِلَى الأَرْضِ، 20لِيَسْمَعَ أَنِينَ شَعْبِهِ الأَسِيرِ وَيُحَرِّرَ الْمَقْضِيَّ عَلَيْهِمْ بِالْمَوْتِ. 21لِكَيْ يُذَاعَ اسْمُ الرَّبِّ فِي صِهْيَوْنَ، وَيُسَبَّحَ أَيْضاً فِي أُورُشَلِيمَ، 22عِنْدَمَا تَجْتَمِعُ الشُّعُوبُ وَالْمَمَالِكُ جَمِيعاً لِيَعْبُدُوا الرَّبَّ.

23الرَّبُّ أَضْعَفَنِي وَأَنَا فِي رَيْعَانِ قُوَّتِي وَقَصَّرَ أَيَّامِي. 24حَتَّى قُلْتُ: «يَا رَبُّ أَنْتَ حَيٌّ إِلَى الأَبَدِ. لَا تَقْصِفْنِي فِي مُنْتَصَفِ عُمْرِي، قَبْلَ أَنْ أَبْلُغَ الشَّيْخُوخَةَ. 25مِنْ قِدَمٍ أَسَّسْتَ الأَرْضَ، وَالسَّمَاوَاتُ هِيَ صُنْعُ يَدَيْكَ. 26هِيَ زَائِلَةٌ أَمَّا أَنْتَ فَبَاقٍ. تَبْلَى كُلُّهَا كَالثَّوْبِ. وَتَسْتَبْدِلُهَا كَمَا يُسْتَبْدَلُ الرِّدَاءُ القَدِيمُ بِالجَدِيدِ. 27لَكِنَّكَ أَنْتَ الدَّائِمُ الْخَالِدُ، وَسِنُوكَ لَنْ تَنْتَهِيَ. 28أَبْنَاءُ عَبِيدِكَ يَدُومُونَ، وَنَسْلُهُمْ يَظَلُّ ثَابِتاً أَمَامَكَ».