Yoshua 18 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yoshua 18:1-28

Mgawanyo Wa Nchi Iliyobaki

118:1 Yos 19:51; 21:2; Amu 18:31; 21:12; 1Sam 1:3; 3:21; 4:3; 1Fal 14:2; Za 78:60; Yer 7:12; 26:6; 41:5; Kut 27:21; 40:2; Mdo 7:45Kusanyiko lote la Waisraeli likakusanyika huko Shilo na kusimamisha Hema la Kukutania. Nchi ikawa chini ya utawala wao, 2lakini palikuwa bado makabila saba ya Israeli ambayo yalikuwa hayajapokea urithi wao.

318:3 Amu 18:9; Sef 3:16; Mt 20:6; Yn 6:27; Flp 3:13-14Hivyo Yoshua akawaambia Waisraeli, “Je, mtasubiri hata lini ili kuingia kumiliki nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa? 418:4 Mik 2:5Chagueni watu watatu kutoka kwenye kila kabila. Nitawatuma hao watu kukagua hiyo nchi na kuniandikia mapendekezo ya mgawanyo wa urithi wa kila kabila. Nao watanirudia. 518:5 Yos 15:1; 16:1-4Mtaigawanya hiyo nchi katika sehemu saba. Yuda atabaki katika eneo lake upande wa kusini na nyumba ya Yosefu katika nchi yake upande wa kaskazini. 618:6 Law 16:8; Yos 14:2Baada ya kuandika maelezo ya hizo sehemu saba za nchi, yaleteni kwangu, nami nitawapigia kura kwa kura mbele za Bwana Mungu wetu. 718:7 Yos 13:33; 13:8Hata hivyo, Walawi hawatakuwa na sehemu miongoni mwenu, kwa maana huduma ya ukuhani kwa Bwana ndio urithi wao. Nao Gadi, Reubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapata urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, ambako Mose mtumishi wa Bwana aliwapa.”

8Watu hao walipokuwa wanaondoka kwenda kuandika vizuri kuhusu hiyo nchi, Yoshua akawaagiza, “Nendeni mkakague hiyo nchi na mwandike maelezo kuihusu. Kisha mrudi kwangu, nami nitawapigia kura hapa Shilo mbele za Bwana.” 9Ndipo hao watu walipoondoka na kupita katika ile nchi. Wakaandika maelezo yake kwenye kitabu, mji kwa mji, katika sehemu saba na kurudisha taarifa kwa Yoshua huko kambini Shilo. 1018:10 Hes 34:13; Yer 7:12; Hes 33:54; Yos 19:51; Mit 16:33Basi Yoshua akawapigia kura huko Shilo mbele za Bwana, na hapo akagawanya ile nchi kwa Waisraeli kufuatana na mgawanyo wa kabila zao.

Mgawo Kwa Benyamini

11Kura iliangukia kabila la Benyamini, ukoo kwa ukoo. Eneo lao walilogawiwa lilikuwa kati ya kabila la Yuda na la Yosefu.

1218:12 Yos 8:15; 7:2Upande wa kaskazini mpaka wao ulianzia pale Yordani, kupitia kaskazini ya mteremko wa Yeriko na kuendelea magharibi kuingia katika nchi ya vilima, ukitokea kwenye jangwa la Beth-Aveni. 1318:13 Mwa 28:19; Yos 12:9; Hes 32:3; Yos 16:5; Amu 1:23; Hes 18:20; Kum 10:9; Eze 44:28Kutoka hapo ulikatiza kwenye mteremko wa kusini mwa Luzu (yaani Betheli) na kushuka hadi Ataroth-Adari katika kilima kusini mwa Beth-Horoni ya Chini.

1418:14 Yos 10:10; 9:17; 1Nya 13:6Kutoka kilima kinachotazamana na Beth-Horoni upande wa kusini mpaka ule ukazunguka kusini kufuatia upande wa magharibi, na ukatokezea Kiriath-Baali (yaani Kiriath-Yearimu), mji wa watu wa Yuda. Huu ndio uliokuwa upande wa magharibi.

1518:15 Yos 15:9Upande wa kusini mpaka ulianzia kwenye viunga vya Kiriath-Yearimu kwa upande wa magharibi, nao ukatokeza kwenye chemchemi ya maji ya Neftoa. 1618:16 Yos 17:15; 15:7-8; 2Fal 23:10; 2Nya 28:3; 33:6; Isa 30:33; Yer 19:2; Yos 15:8Mpaka ukateremka hadi shefela inayotazamana na Bonde la Ben-Hinomu, kaskazini mwa Bonde la Refaimu. Ukaendelea chini kwenye Bonde la Hinomu sambamba na mteremko wa kusini mwa mji mkubwa wa Wayebusi na kisha hadi En-Rogeli. 1718:17 Yos 22:10; 15:6-7Kisha ukapinda kuelekea kaskazini, ukaenda hadi En-Shemeshi na kuendelea mpaka Gelilothi, inayotazamana na Njia ya Adumimu, ukateremka hadi kwenye Jiwe la Bohani mwana wa Reubeni. 1818:18 Yos 15:6; 11:2; 16:1Ukaendelea upande wa mteremko wa kaskazini wa Beth-Araba ukateremka hadi Araba. 1918:19 Yos 15:6; Mwa 14:3Kisha ukaenda mpaka kwenye mteremko wa kaskazini wa Beth-Hogla na kujitokeza kwenye ghuba ya kaskazini ya Bahari ya Chumvi, kwenye maingilio ya Yordani upande wa kusini. Huo ulikuwa mpaka wa kusini.

2018:20 1Sam 9:1; Yos 21:4, 17Nayo Yordani ikawa ndio mpaka wa upande wa mashariki.

Hii ilikuwa ndiyo mipaka iliyoonyesha urithi wa koo za Benyamini pande zote.

2118:21 Yos 6:26; 1Fal 16:34; Lk 10:30Kabila ya Benyamini, ukoo kwa ukoo, ilikuwa na miji mikubwa ifuatayo:

Yeriko, Beth-Hogla, Emeki-Kesisi, 2218:22 Yos 15:6; 2Nya 13:4; Yos 16:1Beth-Araba, Semaraimu, Betheli, 2318:23 Kum 2:23; Amu 6:11, 24; 8:27, 32; 9:6; 1Sam 13:17Avimu, Para na Ofra, 2418:24 Yos 21:17; 1Sam 13:3, 16; 14:5; 1Fal 15:22; 2Fal 23:8; Isa 10:29; Amu 19:12-16; Ezr 2:26Kefar-Amoni, Ofni, na Geba; miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.

2518:25 Yos 10:40; Amu 4:5; 19:13; 1Sam 2:11; 7:17; 25:1; Neh 11:33; 1Fal 15:17, 21; Neh 7:29Gibeoni, Rama na Beerothi, 2618:26 Yer 11:3; Yos 9:17; Ezr 2:25; Neh 7:29Mispa, Kefira, Moza, 27Rekemu, Irpeeli, Tarala, 2818:28 2Sam 21:14; Yos 15:8; 10:1; 15:57; 9:17; Eze 48:23; Mwa 46:21; Mdo 17:26Zela, Elefu, mji wa Wayebusi (yaani Yerusalemu), Gibea na Kiriathi; miji kumi na minne pamoja na vijiji vyake.

Huu ndio uliokuwa urithi wa Benyamini kwa ajili ya koo zake.

Swedish Contemporary Bible

Josua 18:1-28

Spioner sänds ut för att utforska de områden som ännu inte erövrats

1Israels hela menighet samlades i Shilo och satte upp uppenbarelsetältet. De hade nu kontroll över hela landet, 2men sju av stammarna hade ännu inte fått sin landegendom.

3Då frågade Josua: ”Hur länge tänker ni vänta innan ni intar det land som Herren, era förfäders Gud, har gett er? 4Utse tre män från varje stam, så ska jag skicka iväg dem för att utforska landet och göra en beskrivning av de olika områdena och sedan komma till mig. 5Männen får dela upp landet i sju delar. Juda ska vara kvar i sitt område i söder och likadant Josef i sitt område i norr. 6När ni gjort en beskrivning över de sju delarna av landet, ska ni komma till mig och sedan ska jag kasta lott för er inför Herren, vår Gud. 7Leviterna ska inte ha något område som ni andra, för deras del är att vara Herrens präster.18:7 Prästerna fick behålla en del av offret när de andra stammarna offrade till Herren. De fick även städer att bo i och andra gåvor av folket. Se 13:14; 21:1-42; 5 Mos 18:1-8. Gads och Rubens stammar och ena halvan av Manasses stam har redan fått sina områden på östra sidan av Jordan, den arvedel som Herrens tjänare Mose gav dem.”

8Männen gav sig alltså iväg och Josua befallde dem att kartlägga landet. Han sa: ”Vandra igenom landet, gör en beskrivning av det och kom tillbaka till mig, så ska jag kasta lott för er inför Herren i Shilo.”

9Männen gick och vandrade igenom landet och beskrev de sju delarna i en bok och antecknade alla städerna i de olika områdena. Sedan återvände de till Josua i lägret vid Shilo. 10Josua kastade sedan lott för dem i Shilo och fördelade landet åt de olika stammarna, så att de alla fick sin del.

Benjamins stam

11Det landområde som lotten tilldelade Benjamins stam, med alla dess släkter, låg mellan de områden som Judas och Josefs stammar tidigare fått.

12Den norra gränslinjen började vid floden Jordan och gick vid bergssluttningen norr om Jeriko. Sedan fortsatte den västerut genom bergsbygden och öknen vid Bet Aven.

13Därifrån gick gränsen söder om Lus vid den södra bergssluttningen, dvs. Betel, och fortsatte ner till Atarot Addar nära berget som ligger söder om Nedre Bet Horon. 14Där svängde gränslinjen på västsidan mot söder, passerade berget vid Bet Horon och slutade vid Kirjat-Baal, dvs. Kirjat-Jearim, en av Judas stams städer. Detta var den västra sidan.

15Den södra gränsen sträckte sig från Kirjat-Jearims utkant till Neftoachkällan 16och ner till bergsfoten vid Hinnoms sons dal norrut i Refaimdalen. Därifrån fortsatte den tvärs igenom Hinnoms dal och gick söder om bergssluttningen där jevuséerna bodde och fortsatte ner till Rogelkällan.

17Därifrån gick gränslinjen mot nordost till Shemeshkällan och vidare till Gelilot som ligger mitt emot Adummimshöjden. Därefter gick den ner till Bohans, Rubens sons, sten, 18vidare utmed norra kanten av Bet Haarava ner i dalen 19och förbi Bet-Hoglas höjd i norr för att sluta vid Döda havets norra vik som utgör södra änden av floden Jordan. Detta var sydgränsen.

20I öster utgjordes gränsen av floden Jordan.

Detta var benjaminiternas områden med deras gränser.

21Följande städer ingick också i det land som Benjamins stam fick, efter sina släkter:

Jeriko, Bet-Hogla, Emek Kesis, 22Bet Haarava, Semarajim, Betel, 23Avvim, Para, Ofra, 24Kefar Haammoni, Ofni och Geva, tolv städer med kringliggande byar, 25Givon, Rama, Beerot, 26Mispa, Kefira, Mosa, 27Rekem, Jirpeel, Tarala, 28Sela, Elef, Jevus, dvs. Jerusalem, Giva och Kirjat-Jearim, fjorton städer med kringliggande byar.

Detta är benjaminiternas områden, efter deras släkter.