Yona 2 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yona 2:1-10

Maombi Ya Yona Katika Tumbo La Nyangumi

1Akiwa ndani ya tumbo la nyangumi, Yona alimwomba Bwana Mungu wake. 22:2 Za 18:6; 120:1; 86:13; Mao 3:55Akasema:

“Katika shida yangu nalimwita Bwana,

naye akanijibu.

Kutoka kina cha kaburi2:2 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. niliomba msaada,

nawe ukasikiliza kilio changu.

32:3 Za 88:6; 42:7; 2Sam 22:5Ulinitupa kwenye kilindi,

ndani kabisa ya moyo wa bahari,

mikondo ya maji ilinizunguka,

mawimbi yako yote na viwimbi

vilipita juu yangu.

42:4 Za 31:22; Yer 7:15; Isa 49:14; 1Fal 8:38, 48Nikasema, ‘Nimefukuziwa

mbali na uso wako,

hata hivyo nitatazama tena

kuelekea Hekalu lako takatifu.’

52:5 Za 69:1-2Maji yaliyonimeza yalinitisha,

kilindi kilinizunguka;

mwani2:5 Mwani hapa maana yake ni magugu yaotayo kwenye sakafu ya kilindi cha bahari. ulijisokota kichwani pangu.

62:6 Ay 28:9; 17:16; 33:18; Za 30:3Nilizama chini sana mpaka pande za mwisho za milima,

makomeo ya hiyo nchi yalinifungia hata milele.

Lakini uliuleta uhai wangu kutoka shimoni,

Ee Bwana Mungu wangu.

72:7 Za 11:4; 18:6; 77:11-12; 34:6; 130:2; Yer 2:13; 2Nya 30:27“Wakati uhai wangu ulipokuwa unatoka,

nilikukumbuka wewe, Bwana,

nayo maombi yangu yalikufikia wewe,

katika Hekalu lako takatifu.

82:8 1Sam 12:21; Yer 10:8; 2Fal 17:15; Za 31:6; Kum 32:21“Wale watu wanaongʼangʼana na sanamu zisizofaa

hupoteza neema ile ambayo ingekuwa yao.

92:9 Hos 14:2; Ebr 13:15; Hes 30:2; Kut 15:2; Za 50:14; 116:14; 66:13-15; 3:8; 42:4Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani,

nitakutolea dhabihu.

Lile nililowekea nadhiri nitalitimiza.

Wokovu watoka kwa Bwana.”

102:10 Yn 1:17; Mt 8:9Basi Bwana akamwamuru yule nyangumi, naye akamtapika Yona katika nchi kavu.

Hoffnung für Alle

Jona 2:1-11

Jonas Dankgebet

1Der Herr ließ einen großen Fisch kommen, der Jona verschlang. Drei Tage und drei Nächte war Jona im Bauch des Fisches. 2Dort betete er zum Herrn, seinem Gott:

3»Ich schrie zum Herrn,

als ich nicht mehr aus noch ein wusste,

und er antwortete mir in meiner Not.

Ich war dem Tode nah,

doch du, Herr, hast meinen Hilferuf gehört!

4In die Tiefe hattest du mich geworfen,

mitten ins Meer,

rings um mich türmten sich die Wellen auf;

die Fluten rissen mich mit und spülten mich fort.

5Ich dachte schon,

du hättest mich aus deiner Nähe verstoßen

und ich würde deinen heiligen Tempel nie wiedersehen2,5 Oder: doch ich würde deinen heiligen Tempel einst wiedersehen..

6Ja, die Strudel zogen mich in die Tiefe,

bis ich fast ertrank.

Seetang schlang sich mir um den Kopf;

7bis zu den Fundamenten der Berge sank ich hinab

in ein Land, dessen Tore

sich auf ewig hinter mir schließen sollten.

Aber du, Herr, mein Gott,

hast mich heraufgezogen

und mir das Leben neu geschenkt!

8Als ich schon alle Hoffnung aufgegeben hatte,

dachte ich an dich,

und mein Gebet drang zu dir in deinen heiligen Tempel.

9Wer sein Heil bei anderen Göttern sucht,

die ja doch nicht helfen können,

verspielt die Gnade, die er bei dir finden kann.

10Ich aber will dir Danklieder singen

und dir meine Opfer darbringen.

Was ich dir versprochen habe,

das will ich erfüllen.

Ja, der Herr allein kann retten!«

11Da befahl der Herr dem Fisch, Jona am Meeresufer auszuspeien.