Yohana 6 – NEN & SZ-PL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 6:1-71

Yesu Alisha Wanaume 5,000

(Mathayo 14:13-21; Marko 6:30-44; Luka 9:10-17)

16:1 Mt 14:15; Mk 6:35; Lk 9:10, 12Baada ya haya, Yesu alikwenda ngʼambo ya Bahari ya Galilaya, ambayo pia huitwa Bahari ya Tiberia. 26:2 Yn 2:11-13Umati mkubwa wa watu uliendelea kumfuata, kwa sababu waliona ishara nyingi za miujiza alizofanya kwa wagonjwa. 36:3 Yn 6:15Kisha Yesu akapanda mlimani akaketi huko pamoja na wanafunzi wake. 46:4 Yn 11:55Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.

56:5 Yn 1:43Yesu alipotazama na kuuona ule umati mkubwa wa watu ukimjia, akamwambia Filipo, “Tutanunua wapi mikate ili watu hawa wale?” 6Aliuliza swali hili kumpima, kwa maana alishajua la kufanya.

76:7 Hes 11:21, 22Filipo akamjibu, “Hata fedha kiasi cha dinari mia mbili,6:7 Dinari 200 ni sawa na mshahara wa kibarua wa siku 200; mshahara wa kibarua ulikuwa dinari moja kwa siku. hazitoshi kununua mikate ya kuwapa watu hawa ili kila mtu apate kidogo.”

86:8 Yn 1:40Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, ndugu yake Simoni Petro, akamwambia, 96:9 2Fal 4:43“Hapa kuna mvulana mmoja mwenye mikate mitano ya shayiri na samaki wawili wadogo. Lakini hivi vitatosha nini kwa umati huu wote?”

10Yesu akasema, “Waketisheni watu chini.” Palikuwa na majani mengi katika eneo lile, nao watu wakaketi. Palikuwa na wanaume wapatao 5,000. 116:11 Mt 14:19Ndipo Yesu akachukua ile mikate, akamshukuru Mungu na kuwagawia wale watu waliokuwa wameketi. Akafanya vivyo hivyo na wale samaki. Kila mtu akapata kadiri alivyotaka.

12Watu wote walipokwisha kula na kushiba, akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki vya ile mikate, kisipotee chochote.” 13Hivyo wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vya ile mikate mitano ya shayiri na samaki wale wawili wadogo vilivyobakishwa na waliokula.

146:14 Yn 2:11; Kum 18:15-18; Mt 21:11Baada ya watu kuona muujiza ule Yesu aliofanya, walianza kusema, “Hakika huyu ndiye Nabii ajaye ulimwenguni!” 156:15 Yn 18:36; Mt 14:23; Mk 6:46Yesu akijua kwamba walitaka kuja kumfanya awe mfalme wao, kwa nguvu, akajitenga nao akaenda milimani peke yake.

Yesu Atembea Juu Ya Maji

(Mathayo 14:22-33; Marko 6:45-52)

166:16 Mt 14:22-33; Mk 6:45-52Ilipofika jioni, wanafunzi wake waliteremka kwenda baharini. 17Wakaingia kwenye mashua, wakaanza kuvuka bahari kwenda Kapernaumu. Wakati huu kulikuwa tayari giza na Yesu alikuwa hajajumuika nao. 18Bahari ikachafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma. 196:19 Ay 9:8Wanafunzi walipokuwa wamekwenda mwendo wa karibu maili tatu au nne,6:19 Maili tatu au nne ni kama kilomita 5 au 6. walimwona Yesu akitembea juu ya maji akikaribia mashua, nao wakaogopa sana. 206:20 Mt 14:27Lakini Yesu akawaambia, “Ni mimi. Msiogope.” 21Ndipo wakamkaribisha kwa furaha ndani ya mashua, na mara wakafika ufuoni walikokuwa wakienda.

Watu Wanamtafuta Yesu

226:22 Yn 6:2; 15:21Siku iliyofuata, wale watu waliokuwa wamebaki ngʼambo waliona kwamba palikuwepo na mashua moja tu na kwamba Yesu hakuwa ameondoka pamoja na wanafunzi wake, ila walikuwa wameondoka peke yao. 236:23 Yn 6:1, 11Lakini zikaja mashua nyingine kutoka Tiberia zikafika karibu na mahali pale walipokula mikate baada ya Bwana kumshukuru Mungu. 24Mara wale watu wakatambua kwamba Yesu hakuwepo hapo, wala wanafunzi wake. Wakaingia kwenye mashua hizo, wakaenda Kapernaumu ili kumtafuta Yesu.

Yesu Ni Mkate Wa Uzima

256:25 Mt 23:7Walipomkuta Yesu ngʼambo ya bahari wakamuuliza, “Rabi, umefika lini huku?”

266:26 Yn 2:11Yesu akawajibu, “Amin, amin nawaambia, ninyi hamnitafuti kwa kuwa mliona ishara na miujiza, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba. 276:27 Mt 25:46; Yn 4:14; Mt 8:20; 2Tim 2:19; Ufu 7:3Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.”

28Ndipo wakamuuliza, “Tufanye nini ili tupate kuitenda kazi ya Mungu?”

296:29 1Yn 3:23; 3:17Yesu akawajibu, “Kazi ya Mungu ndiyo hii: Mwaminini yeye aliyetumwa naye.”

306:30 Yn 2:11; Mt 12:38Hivyo wakamuuliza, “Utafanya ishara gani ya muujiza, ili tuione tukuamini? Utafanya jambo gani? 316:31 Hes 11:7-9; Neh 9:15; Za 105:40Baba zetu walikula mana jangwani, kama ilivyoandikwa, ‘Aliwapa mikate kutoka mbinguni ili wale.’ ”

326:32 Yn 6:49Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, si Mose aliyewapa mikate kutoka mbinguni, bali Baba yangu ndiye anawapa mkate wa kweli kutoka mbinguni. 336:33 Yn 3:13, 31Kwa maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.”

346:34 Yn 4:15Wakamwambia, “Bwana, kuanzia sasa tupatie huo mkate siku zote.”

356:35 Yn 4:14; 6:48; 7:37Yesu akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uzima. Yeye ajaye kwangu, hataona njaa kamwe na yeye aniaminiye, hataona kiu kamwe. 366:36 Yn 6:26, 29Lakini kama nilivyowaambia, mmeniona lakini bado hamwamini. 376:37 Yn 17:2-6, 9, 24Wale wote anipao Baba watakuja kwangu na yeyote ajaye kwangu, sitamfukuzia nje kamwe. 386:38 Yn 3:17; 4:34Kwa kuwa nimeshuka kutoka mbinguni si ili kufanya mapenzi yangu, bali mapenzi yake yeye aliyenituma. 396:39 Isa 27:3; Yn 18:9Haya ndiyo mapenzi yake yeye aliyenituma, kwamba, nisimpoteze hata mmoja wa wale alionipa, bali niwafufue siku ya mwisho. 406:40 Mt 25:26Kwa maana mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mmoja amtazamaye, Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele, nami nitawafufua siku ya mwisho.”

41Wayahudi wakaanza kunungʼunika kwa kuwa alisema, “Mimi ndimi mkate ulioshuka kutoka mbinguni.” 426:42 Lk 4:22; Yn 7:27, 28Wakasema, “Huyu si Yesu, mwana wa Yosefu, ambaye baba yake na mama yake tunawajua? Anawezaje basi sasa kusema, ‘Nimeshuka kutoka mbinguni’?”

43Hivyo Yesu akawaambia, “Acheni kunungʼunikiana ninyi kwa ninyi. 44Hakuna mtu awezaye kuja kwangu kama asipovutwa na Baba aliyenituma, nami nitamfufua siku ya mwisho. 456:45 Isa 54:13; 1Kor 2:13Imeandikwa katika Manabii, ‘Wote watafundishwa na Mungu.’ Yeyote amsikilizaye Baba na kujifunza kutoka kwake, huyo huja kwangu. 466:46 Yn 1:18; 7:29Hakuna mtu yeyote aliyemwona Baba isipokuwa yeye atokaye kwa Mungu, yeye ndiye peke yake aliyemwona Baba. 476:47 Mt 25:46Amin, amin nawaambia, yeye anayeamini anao uzima wa milele. 486:48 Yn 6:35, 51Mimi ni mkate wa uzima. 496:49 Yn 6:3, 58Baba zenu walikula mana jangwani, lakini wakafa. 506:50 Yn 6:33Lakini hapa kuna mkate utokao mbinguni, ambao mtu yeyote akiula, hatakufa. 516:51 Ebr 10:10Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu yeyote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.”

526:52 Yn 9:16; 10:19Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?”

536:53 Mt 26:26; 8:20; 26:28Hivyo Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. 546:54 Yn 6:39Mtu yeyote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho. 55Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli. 566:56 1Yn 2:24; 3:24Yeyote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake. 576:57 Yn 3:17Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, na kama nami ninavyoishi kwa sababu ya Baba, hivyo anilaye mimi ataishi kwa sababu yangu. 586:58 Yn 3:36; 5:24Huu ndio mkate ushukao kutoka mbinguni, si kama ule mkate baba zenu waliokula nao wakafa. Lakini yeye aulaye mkate huu ataishi milele.” 59Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika sinagogi huko Kapernaumu.

Wafuasi Wengi Wamwacha Yesu

606:60 Yn 6:66; 6:52Wengi wa wafuasi wake waliposikia jambo hili wakasema, “Mafundisho haya ni magumu. Ni nani awezaye kuyapokea?”

616:61 Mt 13:57Yesu alipojua kwamba wafuasi wake wananungʼunika kuhusu mafundisho yake, akawaambia, “Je, jambo hili limewaudhi? 626:62 Mk 16:19; Yn 17:5Ingekuwaje basi kama mngemwona Mwana wa Adamu akipaa kwenda zake huko alipokuwa kwanza? 636:63 2Kor 3:6Roho ndiye atiaye uzima, mwili haufai kitu. Maneno haya niliyowaambia ni Roho tena ni uzima. 646:64 Yn 2:24-25Lakini baadhi yenu hamwamini.” Kwa maana Yesu alifahamu tangu mwanzo wale ambao hawangemwamini miongoni mwao na yule ambaye angemsaliti. 656:65 Mt 13:11Akaendelea kusema, “Hii ndiyo sababu niliwaambia kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.”

666:66 Yn 6:60Tangu wakati huo wafuasi wake wengi wakarejea nyuma wakaacha kumfuata.

676:67 Mt 10:2Hivyo Yesu akawauliza wale wanafunzi wake kumi na wawili, “Je, ninyi pia mnataka kuondoka?”

686:68 Mt 16:16Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tuondoke twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. 696:69 Mk 1:24; Lk 9:20Tunaamini na kujua kuwa wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu.”

706:70 Yn 15:16-19; 13:27; 17:12Ndipo Yesu akajibu, “Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Lakini mmoja wenu ni ibilisi.” 716:71 Mt 26:14; 10:4(Hapa alikuwa anasema juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskariote. Ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili, ndiye ambaye baadaye angemsaliti Yesu.)

Słowo Życia

Jana 6:1-71

Jezus karmi pięć tysięcy mężczyzn

1Potem Jezus przeprawił się na drugą stronę Jeziora Galilejskiego, zwanego też Jeziorem Tyberiadzkim. 2Towarzyszyły Mu tłumy, bo ludzie widzieli, jak w cudowny sposób uzdrawiał chorych. 3Jezus wszedł na górę i usiadł tam ze swoimi uczniami. 4A zbliżało się wtedy żydowskie święto Paschy. 5Gdy Jezus rozejrzał się i zobaczył, nadchodzące ogromne tłumy ludzi, powiedział do Filipa:

—Gdzie kupimy chleb, aby ci ludzie mogli coś zjeść?

6Zapytał o to, aby wystawić go na próbę. Wiedział bowiem, co ma robić.

7—Nawet fortuna nie wystarczyłaby, aby każdy mógł dostać chociaż kawałek chleba—odrzekł Filip.

8Wtedy do rozmowy włączył się inny uczeń—Andrzej, brat Szymona Piotra:

9—Jest tu chłopiec, który ma pięć jęczmiennych chlebów i dwie ryby. Ale co to jest dla takiego tłumu?

10—Każcie wszystkim usiąść!—powiedział Jezus.

Ludzie usiedli więc na trawie, a samych tylko mężczyzn było tam około pięciu tysięcy. 11Jezus wziął chleby, podziękował za nie Bogu i polecił rozdać je siedzącym—każdemu tyle, ile chciał. To samo zrobił z rybami.

12Gdy już wszyscy się najedli, powiedział uczniom:

—Pozbierajcie resztki, aby nic się nie zmarnowało.

13I z pięciu jęczmiennych chlebów zebrano aż dwanaście koszy resztek chleba! 14Gdy ludzie uświadomili sobie, jakiego cudu dokonał Jezus, zaczęli wołać:

—To na pewno jest ten prorok, który miał nadejść!

15Lecz Jezus zorientował się, że chcą Go zabrać i obwołać królem. Dlatego samotnie oddalił się na górę.

Jezus chodzi po wodzie

16Wieczorem uczniowie zeszli na brzeg, 17wsiedli do łodzi i popłynęli w kierunku Kafarnaum. 18Wkrótce zerwał się silny wiatr i jezioro bardzo się wzburzyło. 19Intensywnie wiosłując, przepłynęli jakieś pięć kilometrów. Nagle zobaczyli Jezusa idącego po wodzie i będącego już blisko łodzi. Przerazili się, 20lecz On zawołał:

—Nie bójcie się, to Ja!

21Chcieli Go wziąć do łodzi, ale okazało się, że właśnie dobijają do brzegu—do miejsca, do którego płynęli.

22Następnego dnia, tłum ludzi, zebrany na przeciwległym brzegu, zorientował się, że poza jedną łodzią, którą odpłynęli uczniowie, nie było innej. Wiedzieli też, że Jezus nie wsiadł do łodzi z uczniami, bo odpłynęli sami. 23Tymczasem na miejsce, w którym Jezus nakarmił ludzi chlebem, przypłynęły z Tyberiady inne łodzie. 24Gdy ludzie zauważyli, że nie ma ani Jezusa, ani uczniów, wsiedli do łodzi i popłynęli do Kafarnaum, aby Go odnaleźć.

Jezus chlebem życia

25Gdy Go znaleźli, zapytali:

—Nauczycielu! Kiedy zdążyłeś tu przybyć?

26—Zapewniam was, że szukacie Mnie nie dlatego, że ujrzeliście cud, lecz dlatego, że najedliście się do syta—odpowiedział Jezus. 27—Starajcie się jednak nie o ten nietrwały pokarm, ale o pokarm dający życie wieczne, który Ja, Syn Człowieczy, mogę wam zapewnić. Po to właśnie posłał Mnie Bóg Ojciec!

28—A co mamy zrobić, żeby wypełnić wolę Boga?—pytali.

29—Wolą Boga jest to, abyście wierzyli Temu, którego On posłał—odparł Jezus.

30—Jakiego cudu dokonasz więc, abyśmy mogli go zobaczyć i uwierzyć ci? 31Nasi przodkowie codziennie jedli mannę na pustyni. Pismo mówi: „Dał im do jedzenia chleb z nieba”.

32—Zapewniam was, że to nie Mojżesz dawał chleb z nieba—odrzekł Jezus—ale mój Ojciec daje wam teraz prawdziwy chleb z nieba. 33Chlebem od Boga jest bowiem Ten, który przychodzi z nieba—to On daje światu życie.

34—Panie, dawaj nam zawsze ten chleb—prosili Go.

35—To Ja jestem chlebem życia!—odpowiedział Jezus. —Kto do Mnie przychodzi, nie będzie głodny. A kto wierzy Mi, nie zazna pragnienia. 36Ale nie pierwszy raz o tym mówię, a wy patrzycie na Mnie i nadal nie wierzycie. 37Jednak ci wszyscy, których dał Mi Ojciec, przyjdą do Mnie. A Ja nikogo z nich nie odtrącę. 38Przyszedłem bowiem z nieba nie po to, aby działać na własną rękę, lecz żeby wypełnić wolę Ojca, który Mnie posłał. 39On nie chce, abym kogoś stracił, ale pragnie, abym wszystkich ożywił w dniu ostatecznym. 40Wolą mojego Ojca jest to, aby każdy, kto widzi Syna i wierzy Mu, miał życie wieczne i abym ożywił go w dniu ostatecznym.

41Słysząc to, ludzie zaczęli się oburzać, ponieważ powiedział: „To Ja jestem chlebem, który zstąpił z nieba”.

42—Przecież to tylko Jezus, syn Józefa!—wykrzykiwali. —Znamy jego ojca i matkę. Jak on może mówić: „Zstąpiłem z nieba?”.

43—Dlaczego jesteście oburzeni?—zapytał Jezus. 44—Nikt nie może do Mnie przyjść, jeśli nie zostanie przyprowadzony przez Ojca, który Mnie posłał. Tych zaś, którzy przyjdą do Mnie, ożywię w dniu ostatecznym. 45W księgach proroków napisano przecież: „Oni wszyscy będą uczniami Boga”. Każdy więc, kto słuchał Ojca i uczył się od Niego, przyjdzie do Mnie. 46Nie znaczy to, że ktokolwiek widział Boga Ojca—oprócz Tego, który od Niego przyszedł. 47Raz jeszcze zapewniam was: Kto wierzy, ma życie wieczne! 48Ja jestem chlebem życia! 49Wasi przodkowie jedli wprawdzie mannę na pustyni, ale poumierali. 50Natomiast każdy, kto je ten chleb z nieba, nie umrze. 51To Ja jestem chlebem życia, przysłanym z nieba. Kto się nim posili, będzie żyć na wieki. Chlebem tym jest moje ciało, które poświęcam, aby dać światu życie.

52Wtedy słuchający Go zaczęli się między sobą sprzeczać:

—Jak on może dać nam do jedzenia swoje ciało?

53—Zapewniam was: Jeżeli nie spożyjecie ciała i krwi Syna Człowieczego—odpowiedział Jezus—nie będziecie mieć w sobie życia. 54Kto spożywa moje ciało i krew, już ma życie wieczne, a Ja go ożywię w dniu ostatecznym. 55Ciało moje to prawdziwy pokarm, a moja krew to prawdziwy napój. 56Kto spożywa moje ciało i krew, jest trwale połączony ze Mną, a Ja—z nim. 57Ja żyję dzięki żyjącemu Ojcu, który Mnie posłał. Tak samo ten, kto się Mną karmi, będzie żyć dzięki Mnie. 58To właśnie jest chleb z nieba—nie taki, jaki jedli wasi przodkowie i poumierali. Każdy, kto spożywa ten chleb, będzie żył wiecznie.

59Tego wszystkiego Jezus nauczał w synagodze w Kafarnaum.

Wielu uczniów opuszcza Jezusa

60Słysząc to, wielu Jego uczniów, mówiło:

—To jest zbyt trudne! Któż jest w stanie to pojąć?

61Jezus wiedział, że im się to nie podoba. Spytał więc:

—Jesteście zniechęceni tym? 62Co w takim razie powiecie, gdy zobaczycie Mnie, Syna Człowieczego, wracającego tam, skąd przyszedłem? 63Zrozumcie: to Duch daje życie—ludzkie wysiłki nie mają znaczenia. Słowa, które wam powiedziałem, pochodzą właśnie od Ducha i prowadzą do życia. 64Ale niektórzy z was nadal Mi nie wierzą.

Jezus od początku wiedział bowiem, kto Mu nie wierzy oraz kto Go zdradzi. 65Powiedział więc:

—To właśnie miałem na myśli, mówiąc, że nikt nie jest w stanie przyjść do Mnie, jeśli go nie przyprowadzi Ojciec.

66Po tych słowach wielu uczniów opuściło Jezusa i już z Nim nie chodziło. 67Wtedy On zwrócił się do Dwunastu:

—Czy i wy chcecie odejść?

68—Panie, a do kogo pójdziemy?—odpowiedział Szymon Piotr. —Twoje słowa prowadzą do życia wiecznego! 69Uwierzyliśmy Ci i wiemy, że jesteś Świętym Synem Boga.

70—Wybrałem was Dwunastu—rzekł Jezus—ale jeden z was jest sługą diabła.

71Mówiąc to, miał na myśli Judasza, syna Szymona z Kariotu. To on bowiem, jako należący do grona Dwunastu, miał Go później zdradzić.