Yohana 21 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 21:1-25

Yesu Awatokea Wanafunzi Saba

121:1 Yn 21:14; 20:19, 26Baada ya haya Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kando ya Bahari ya Tiberia.21:1 Yaani Bahari ya Galilaya. Yeye alijionyesha kwao hivi: 221:2 Yn 11:16; 1:4; 2:1; Mt 4:21Simoni Petro, Tomaso aitwaye Didimasi, yaani Pacha, Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja. 321:3 Lk 5:5Simoni Petro akawaambia wenzake, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua, lakini usiku ule hawakupata chochote.

421:4 Lk 24:16; Yn 20:14Mara baada ya kupambazuka, Yesu akasimama ufuoni, lakini wanafunzi hawakumtambua kwamba alikuwa Yesu.

521:5 Lk 24:41Yesu akawaambia, “Wanangu, je, mna samaki wowote?”

Wakamjibu, “La.”

621:6 Lk 5:4-7Akawaambia, “Shusheni nyavu upande wa kuume wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Wakashusha nyavu na tazama wakapata samaki wengi mno hata wakashindwa kuvutia zile nyavu zilizojaa samaki ndani ya mashua.

721:7 Yn 13:23Yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, “Huyu ni Bwana!” Simoni Petro aliposikia haya, akajifunga nguo yake kwa kuwa alikuwa uchi, naye akajitosa baharini. 8Wale wanafunzi wengine wakaja kwa ile mashua huku wakikokota ule wavu uliyojaa samaki, maana hawakuwa mbali na nchi kavu, ilikuwa yapata dhiraa 20021:8 Dhiraa 200 ni kama mita 90. 921:9 Yn 18:18; 21:10, 13Walipofika ufuoni, wakaona moto wa makaa na samaki wakiokwa juu yake na mikate.

10Yesu akawaambia, “Leteni baadhi ya hao samaki mliovua sasa hivi.”

11Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuukokota ule wavu pwani. Ulikuwa umejaa samaki wakubwa 153. Ingawa samaki walikuwa wengi kiasi hicho, ule wavu haukuchanika. 1221:12 Mdo 10:41Yesu akawaambia, “Njooni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyethubutu kumuuliza, “Wewe ni nani?” Kwa sababu walijua ya kuwa ni Bwana. 1321:13 Yn 21:9Yesu akaja, akachukua ule mkate, akawapa na vivyo hivyo akawagawia pia wale samaki. 1421:14 Yn 20:19, 26Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada yake kufufuliwa kutoka kwa wafu.

Yesu Amuuliza Petro Kama Anampenda

1521:15 Lk 24:41Walipokwisha kula, Yesu akamuuliza Simoni Petro, “Je, Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?”

Yeye akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.”

Yesu akamwambia, “Lisha wana-kondoo wangu.”

1621:16 2Sam 5:2; Mt 2:6Yesu akamwambia tena, “Simoni, mwana wa Yohana, wanipenda?”

Petro akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.”

Yesu akamwambia, “Chunga kondoo zangu.”

1721:17 Yn 2:24, 25; 16:30Kwa mara ya tatu Yesu akamuuliza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?”

Petro akahuzunika sana kwa kuwa Yesu alimuuliza mara ya tatu, “Unanipenda?” Akamjibu, “Bwana, wewe unajua yote, unajua ya kuwa ninakupenda.”

Yesu akamwambia, “Lisha kondoo wangu. 18Amin, amin nakuambia, ulipokuwa kijana ulivaa na kwenda unakotaka, lakini utakapokuwa mzee utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvika na kukupeleka usipotaka kwenda.” 1921:19 Yn 12:33; 18:32Yesu alisema haya ili kuashiria ni kifo cha aina gani Petro atakachomtukuza nacho Mungu. Kisha Yesu akamwambia Petro, “Nifuate!”

2021:20 Yn 16:22; 21:7; 13:23Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akiwafuata. (Huyu ndiye yule mwanafunzi aliyeegama kifuani mwa Yesu walipokula naye chakula cha mwisho na kuuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”) 21Petro alipomwona huyo mwanafunzi, akamuuliza Yesu, “Bwana na huyu je?”

2221:22 Mt 16:27, 28; 25:31; 1Kor 4; 5; 11:26; Ufu 2:25; 3:11; 22:7, 20Yesu akamjibu, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini? Wewe inakupasa unifuate!” 2321:23 Mdo 1:16Kwa sababu ya maneno haya ya Yesu, uvumi ukaenea miongoni mwa ndugu kwamba huyu mwanafunzi hangekufa. Lakini Yesu hakusema kuwa hangekufa. Yeye alisema tu kwamba, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini?”

2421:24 Yn 15:27; 19:35Huyu ndiye yule mwanafunzi anayeshuhudia mambo haya na ndiye ambaye ameandika habari hizi. Nasi tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.

2521:25 Yn 20:30Lakini kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya. Kama yote yangeliandikwa, nadhani hata ulimwengu wote usingekuwa na nafasi ya kutosha kuweka vitabu vyote ambavyo vingeandikwa. Amen.

Knijga O Kristu

Ivan 21:1-25

Isus se pojavljuje pred sedmoricom učenika

1Poslije se Isus opet javio učenicima uz Tiberijsko jezero. Evo kako se to dogodilo: 2Ondje ih je bila nekolicina: Šimun Petar, Toma zvani Blizanac, Natanael iz Kane Galilejske, Zebedejevi sinovi te još dvojica učenika.

3“Idem loviti ribu”, reče Šimun Petar.

“Idemo i mi”, rekli su oni i pošli s njim, ali cijele noći nisu ništa ulovili.

4U zoru je Isus stajao na obali, ali učenici ga nisu prepoznali. 5“Zar nemate ribe, djeco?” dovikne im on.

“Nemamo!” odgovore.

6On reče: “Bacite mrežu s desne strane lađe i uhvatit ćete ih!” Tako su i učinili. Nisu mogli izvući mrežu zbog mnoštva riba koje su uhvatili.

7Učenik kojega je Isus osobito volio reče Petru: “To je Gospodin!” Nato Šimun Petar opaše gornju haljinu jer je bio slabo obučen, skoči u vodu i otpliva do obale. 8Drugi su ostali u lađi. Dovuku mrežu punu riba do obale udaljene stotinjak metara.21:8 U grčkome: dvjesto lakata. 9Kad su izišli na obalu, ugledaju ribu kako se peče na razgorjelu žaru i kruh.

10“Donesite malo riba koje ste uhvatili”, reče im Isus. 11Šimun Petar ode i izvuče mrežu punu velikih riba na obalu: sto pedeset i tri velike ribe. Mreža se ipak nije rastrgala.

12“Dođite doručkovati!” reče im Isus. Nitko se od njih nije usuđivao pitati ga je li on uistinu Gospodin jer su znali da jest. 13Isus uzme kruh, pa im ga dade. To učini i s ribom. 14To je bilo već treći put Isus da se javio učenicima otkad je uskrsnuo od mrtvih.

Isusov razgovor s Petrom

15Nakon doručka Isus upita Šimuna Petra: “Šimune, Ivanov sine, ljubiš li me više nego ovi?”

“Da”, odgovori Petar. “Ti znaš da te volim.”

“Onda pasi moje jaganjce”, reče mu Isus.

16Ponovno ga upita: “Šimune, Ivanov sine, ljubiš li me?”

“Da, Gospodine,” reče Petar “znaš da te volim.”

“Onda pasi moje ovce”, reče mu Isus.

17Još ga jedanput upita: “Šimune, Ivanov sine, voliš li me?”

Petar se ražalosti što ga Isus i treći put pita voli li ga. “Gospodine, ti sve znaš; znaš da te volim”, reče.

“Onda pasi moje ovce”, reče mu Isus. 18“Zaista ti kažem, kad si bio mlad, mogao si činiti što si htio i ići kamo si želio; ali kad ostariš, raširit ćeš ruke i drugi će te opasati i voditi onamo kamo ne želiš ići.” 19Isus mu je to rekao da bi mu navijestio kakvom će smrću proslaviti Boga. Zatim mu reče: “Slijedi me!”

20Petar se okrene i opazi da učenik kojega je Isus osobito volio, onaj koji se pri večeri nagnuo i upitao Isusa: “Učitelju, koji će te od nas izdati?” ide za njim. 21Petar upita Isusa: “A što će biti s njime, Gospodine?”

22Isus mu odgovori: “Ako hoću da on ostane dok ja ne dođem, što se to tebe tiče? Ti me slijedi!” 23Tako se među braćom raširio glas da onaj učenik neće umrijeti. Ali Isus nije rekao da on neće umrijeti, već samo: “Ako hoću da on ostane dok ja ne dođem, što se to tebe tiče!”

24Ovo je taj učenik koji je vidio te događaje i ovdje ih zabilježio. A svi mi znamo da je zapis tih događaja točan i istinit.

25Isus je učinio još mnogo toga i kad bi se sve redom zapisalo, mislim da sve te knjige ne bi stale ni u cijeli svijet!