Yohana 11 – NEN & SZ-PL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yohana 11:1-57

Kifo Cha Lazaro

111:1 Mt 21:17; Lk 10:38Basi mtu mmoja jina lake Lazaro alikuwa mgonjwa. Yeye alikuwa akiishi Bethania kijiji cha Maria na Martha dada zake. 211:2 Mk 14:3; Lk 7:38Huyu Maria, ambaye Lazaro kaka yake alikuwa mgonjwa, ndiye yule ambaye alimpaka Bwana mafuta na kuifuta miguu yake kwa nywele zake. 311:3 Yn 11:5, 36Hivyo hawa dada wawili walituma ujumbe kwa Yesu kumwambia, “Bwana, yule umpendaye ni mgonjwa.”

411:4 Yn 11:40Lakini Yesu aliposikia hayo, akasema, “Ugonjwa huu hautaleta mauti bali umetokea ili kudhihirisha utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu apate kutukuzwa kutokana na ugonjwa huu.” 5Pamoja na hivyo, ingawa Yesu aliwapenda Martha, Maria na Lazaro ndugu yao, 611:6 Yn 10:40baada ya kusikia kwamba Lazaro ni mgonjwa, aliendelea kukawia huko alikokuwa kwa siku mbili zaidi.

711:7 Yn 10:40Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Haya, turudi Uyahudi.”

811:8 Mt 23:7; Yn 8:59; 10:31Wanafunzi wake wakamwambia, “Rabi, Wayahudi walikuwa wanataka kukupiga mawe, nawe unataka kurudi huko?”

911:9 Yn 9:4; 12:35Yesu akawajibu, “Si kuna saa kumi na mbili za mchana katika siku moja? Wala watembeao mchana hawawezi kujikwaa kwa maana wanaona nuru ya ulimwengu huu. 1011:10 Yn 12:35Lakini wale watembeao usiku hujikwaa kwa sababu hakuna nuru ndani yao.”

1111:11 Mt 9:24; Lk 8:52Baada ya kusema haya, Yesu akawaambia, “Rafiki yetu Lazaro amelala, lakini naenda kumwamsha.”

12Wanafunzi wakamwambia, “Bwana, kama amelala usingizi ataamka.” 1311:13 Mt 9:24Hata hivyo, Yesu alikuwa anazungumzia kuwa Lazaro amekufa, lakini wanafunzi wake hawakuelewa, walidhani kwamba anasema Lazaro amelala usingizi tu.

14Kwa hiyo Yesu akawaambia waziwazi, “Lazaro amekufa. 15Hata hivyo nafurahi kwa kuwa sikuwepo huko kabla ya Lazaro kufa, ili mpate kuamini. Lakini sasa twendeni kwake.”

1611:16 Mt 10:3; Mdo 1:13Tomaso aliyeitwa Pacha akawaambia wanafunzi wenzake, “Sisi nasi twendeni tukafe pamoja naye.”

Yesu Ndiye Ufufuo Na Uzima

1711:17 Yn 11:6, 39Yesu alipowasili huko alikuta Lazaro amekuwa kaburini siku nne. 1811:18 Yn 11:1; Mt 21:17Basi Bethania ulikuwa karibu na Yerusalemu umbali wa karibu maili mbili,11:18 Maili mbili ni kama kilomita tatu. 1911:19 Yn 11:31; Ay 2:11na Wayahudi wengi walikuwa wamekuja kuwafariji Martha na Maria kwa ajili ya kufiwa na ndugu yao. 2011:20 Lk 10:38-42Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alitoka kwenda kumlaki, ila Maria alibaki nyumbani.

2111:21 Yn 11:32, 37Martha akamwambia Yesu, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa. 2211:22 Yn 11:41, 42Lakini sasa ninajua kuwa chochote utakachomwomba Mungu, atakupa.”

23Yesu akamwambia, “Ndugu yako atafufuka.”

2411:24 Dan 12:2; Mdo 24:15Martha akamjibu, “Ninajua ya kuwa atafufuka wakati wa ufufuo wa wafu siku ya mwisho.”

2511:25 Yn 1:4Yesu akamwambia, “Mimi ndiye huo ufufuo na uzima. Yeye aniaminiye mimi, hata akifa atakuwa anaishi 2611:26 Yn 3:15; Mt 25:46na yeyote aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je, unasadiki haya?”

2711:27 Lk 2:11; Mt 4:3; 16:16; Yn 6:14Martha akamwambia, “Ndiyo Bwana, ninaamini ya kuwa wewe ndiwe Kristo,11:27 Kristo maana yake ni Masiya, yaani Aliyetiwa mafuta. Mwana wa Mungu, yeye ajaye ulimwenguni.”

Yesu Alia

2811:28 Mt 26:18; Yn 13:13Baada ya kusema haya Martha alikwenda, akamwita Maria dada yake faraghani na kumwambia, “Mwalimu yuko hapa anakuita.” 29Maria aliposikia hivyo, akaondoka upesi akaenda mpaka alipokuwa Yesu. 3011:30 Yn 11:20; 13:13Yesu alikuwa hajaingia kijijini, bali alikuwa bado yuko mahali pale alipokutana na Martha. 3111:31 Yn 11:19; 8:59Wale Wayahudi waliokuwa pamoja na Maria nyumbani wakimfariji walipoona ameondoka haraka na kutoka nje, walimfuata wakidhani ya kwamba alikuwa anakwenda kule kaburini kulilia huko.

3211:32 Yn 11:21; 5:18Maria alipofika mahali pale Yesu alipokuwa, alipiga magoti miguuni Pake na kusema, “Bwana, kama ungalikuwa hapa, ndugu yangu hangalikufa.”

3311:33 Yn 11:38; 12:27; 13:21Yesu alipomwona Maria akilia na wale Wayahudi waliokuja pamoja naye pia wakilia, Yesu alisikia uchungu moyoni, akafadhaika sana. 34Akauliza, “Mmemweka wapi?”

Wakamwambia, “Bwana, njoo upaone.”

3511:35 Lk 19:41Yesu akalia machozi.

3611:36 Yn 11:3Ndipo Wayahudi wakasema, “Tazama jinsi alivyompenda Lazaro!”

3711:37 Yn 9:6, 7; 11:21, 32Lakini wengine wakasema, “Je, yule aliyefungua macho ya kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?”

Yesu Amfufua Lazaro

3811:38 Yn 11:33; Mt 27:60; Lk 24:2; Yn 20:1Yesu kwa mara nyingine akiwa amefadhaika sana, akafika penye kaburi. Hilo kaburi lilikuwa pango ambalo jiwe lilikuwa limewekwa kwenye ingilio lake. 3911:39 Yn 11:17Yesu akasema, “Liondoeni hilo jiwe.”

Martha ndugu yake yule aliyekuwa amekufa akasema, “Lakini Bwana, wakati huu atakuwa ananuka kwani amekwisha kuwa kaburini siku nne.”

4011:40 Yn 11:23-25Yesu akamwambia, “Sikukuambia kwamba kama ukiamini utauona utukufu wa Mungu?”

4111:41 Yn 17:1; Mt 11:25Kwa hiyo wakaliondoa lile jiwe kutoka kaburini. Yesu akainua macho yake juu akasema, “Baba, ninakushukuru kwa kuwa wanisikia. 4211:42 Yn 12:30; 3:17Ninajua ya kuwa wewe hunisikia siku zote, lakini nimesema haya kwa ajili ya umati huu uliosimama hapa, ili wapate kuamini ya kuwa wewe umenituma.”

4311:43 Lk 7:14Baada ya kusema haya, Yesu akapaza sauti yake akaita, “Lazaro, njoo huku!” 4411:44 Yn 19:40; 20:7Yule aliyekuwa amekufa akatoka nje, mikono yake na miguu yake ikiwa imeviringishiwa vitambaa vya kitani na leso usoni pake.

Yesu akawaambia, “Mfungueni, mwacheni aende zake.”

Shauri La Kumuua Yesu

(Mathayo 26:1-5; Marko 14:1-2; Luka 22:1-2)

4511:45 Yn 11:19; 2:23; 14Hivyo Wayahudi wengi waliokuwa wamekuja kumfariji Maria, walipoona yale Yesu aliyoyatenda wakamwamini. 46Lakini baadhi yao wakaenda kwa Mafarisayo na kuwaambia mambo Yesu aliyoyafanya. 4711:47 Yn 2:11Kwa hiyo viongozi wa makuhani na Mafarisayo wakaita mkutano wa baraza.

Wakaulizana, “Tufanyeje? Huyu mtu anafanya ishara nyingi. 48Kama tukimwacha aendelee hivi, kila mtu atamwamini, nao Warumi watakuja na kupaharibu mahali petu patakatifu na taifa letu.”

4911:49 Lk 3:2; Yn 18:14; Mdo 4:6Mmoja wao aliyeitwa Kayafa, ambaye alikuwa kuhani mkuu mwaka huo, akasema, “Ninyi hamjui kitu chochote! 5011:50 Yn 18:14Hamjui kwamba ni afadhali mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, kuliko taifa lote liangamie?”

5111:51 Mwa 50:20; Kut 28:30; Hes 27:21Hakusema haya kutokana na mawazo yake mwenyewe bali kama kuhani mkuu mwaka huo, alitabiri kuwa Yesu angelikufa kwa ajili ya taifa la Wayahudi, 5211:52 Isa 49:6; Yn 10:16wala si kwa ajili ya taifa hilo pekee, bali pia kwa ajili ya watoto wa Mungu waliotawanyika, ili kuwaleta pamoja na kuwafanya wawe wamoja. 5311:53 Mt 12:14Hivyo tangu siku hiyo wakawa wanafanya mipango ili wamuue Yesu.

5411:54 Yn 7:1Kwa hiyo Yesu akawa hatembei hadharani miongoni mwa Wayahudi, bali alijitenga akaenda sehemu iliyo karibu na jangwa kwenye kijiji kiitwacho Efraimu. Akakaa huko na wanafunzi wake.

5511:55 Kut 12:13, 23, 27; Mk 14:1; 2Nya 30:17-18Basi Pasaka ya Wayahudi ilipokuwa imekaribia, watu wengi walitoka vijijini wakaenda Yerusalemu kabla ya Pasaka ili wakajitakase. 5611:56 Yn 7:11; 17:7Watu wakawa wanamtafuta Yesu, nao waliposimama kwenye eneo la Hekalu waliulizana, Je, mtu huyu hatakuja kamwe kwenye Sikukuu? 57Viongozi wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kuwa yeyote atakayejua mahali Yesu aliko, lazima atoe taarifa ili wapate kumkamata.

Słowo Życia

Jana 11:1-57

Śmierć Łazarza

1Pewnego dnia zachorował Łazarz, brat Marii i Marty z Betanii. 2Maria była tą kobietą, która namaściła olejkiem stopy Pana i wytarła je swoimi włosami. 3Siostry wysłały do Jezusa wiadomość: „Panie, Twój bliski przyjaciel zachorował”. 4Gdy Jezus to usłyszał, powiedział:

—Ta choroba nie zakończy się śmiercią, lecz przyniesie chwałę Bogu i Ja, Syn Człowieczy, również zostanę dzięki niej otoczony chwałą.

5Jezus bardzo kochał całą trójkę: Martę, jej siostrę—Marię oraz Łazarza. 6Jednak jeszcze dwa dni pozostał tam, gdzie zastała Go ta wiadomość. 7Dopiero wtedy oznajmił uczniom:

—Chodźmy jeszcze raz do Judei.

8—Nauczycielu! Przecież tamtejsi przywódcy chcieli Cię zabić, a Ty znowu tam idziesz?—zaprotestowali.

9—Czy dzień nie ma dwunastu godzin?—odpowiedział Jezus. —Kto chodzi w ciągu dnia, nie potknie się, bo jest jasno. 10Kto zaś chodzi nocą, potyka się, bo panuje ciemność. 11Nasz przyjaciel Łazarz zasnął, muszę więc pójść, aby go obudzić.

12—Panie! Jeśli zasnął, to znaczy, że powraca do zdrowia—ucieszyli się uczniowie.

13Jezus jednak miał na myśli śmierć Łazarza. Oni natomiast myśleli, że mówi o zwykłym śnie. 14Wyjaśnił im więc:

—Łazarz umarł. 15Ale ze względu na was cieszę się, że Mnie tam nie było. Chcę bowiem, abyście uwierzyli. Chodźmy do niego!

16—Chodźmy więc! Najwyżej umrzemy razem z nim—odezwał się Tomasz, zwany Bliźniakiem.

Jezus pociesza siostry

17Gdy Jezus dotarł na miejsce, Łazarz już od czterech dni spoczywał w grobie. 18A Betania leżała blisko Jerozolimy, w odległości niecałych trzech kilometrów, 19dlatego wielu ludzi z Jerozolimy przyszło do Marty i Marii, aby wyrazić im swoje współczucie po stracie brata. 20Gdy Marta dowiedziała się, że nadchodzi Jezus, wybiegła Mu na spotkanie. Maria zaś została w domu. 21Spotkawszy Jezusa, Marta powiedziała:

—Panie, gdybyś tu był, mój brat by nie umarł! 22Ale jestem przekonana, że nawet teraz Bóg da Ci to, o co Go poprosisz.

23—Twój brat zmartwychwstanie—powiedział Jezus.

24—Tak, wiem o tym—odrzekła Marta. —Ożyje w dniu ostatecznego zmartwychwstania.

25—To Ja jestem zmartwychwstaniem i życiem—oznajmił Jezus. —Kto wierzy Mi, choćby umarł, będzie żyć. 26A każdy, kto żyje i wierzy Mi, nigdy nie umrze. Czy wierzysz w to?

27—Tak, Panie—odrzekła Marta—wierzę, że jesteś Synem Boga, Mesjaszem, który miał przyjść na świat.

28Po tych słowach odeszła. Zawołała siostrę, Marię, i na osobności powiedziała jej:

—Nauczyciel już przyszedł i chce się z tobą zobaczyć.

29Maria natychmiast wstała i pobiegła do Niego. 30Jezus nie wszedł jeszcze do wsi, ale czekał tam, gdzie Go spotkała Marta. 31Przybysze z Jerozolimy, którzy byli z Marią w domu i pocieszali ją, zauważyli, że w pośpiechu wstała i wyszła. Pomyśleli więc, że idzie wypłakać się przy grobie Łazarza, dlatego poszli za nią. 32Gdy Maria doszła do Jezusa i zobaczyła Go, upadła Mu do nóg i powiedziała:

—Panie, gdybyś tu był, mój brat by nie umarł.

33Jezus zobaczył, jak Maria płacze, a wraz z nią ci, którzy za nią przyszli. Wtedy głęboko się wzruszył i zasmucił.

34—Gdzie go pochowaliście?—zapytał.

—Panie, chodź i zobacz—odpowiedzieli.

35Wtedy Jezus zapłakał.

36—Musiał być mu bardzo bliski!—zauważyli przybysze z Jerozolimy.

37—Przecież przywrócił wzrok niewidomemu! Nie mógł więc sprawić, żeby Łazarz nie umarł?—mówili z wyrzutem niektórzy.

Jezus wskrzesza Łazarza

38Poruszony do głębi, Jezus dotarł do grobowca. Była to grota, a jej wejście zamykał głaz.

39—Odsuńcie głaz!—polecił Jezus.

—Panie, ciało już cuchnie! Leży tam już bowiem od czterech dni—zawołała Marta, siostra zmarłego.

40—Przecież powiedziałem ci, że jeśli uwierzysz, ujrzysz Bożą chwałę—odpowiedział Jezus.

41Odsunięto więc głaz. A Jezus podniósł oczy ku górze i rzekł:

—Ojcze, dziękuję Ci, że Mnie wysłuchałeś. 42Ja wiem, że zawsze Mnie wysłuchujesz, ale mówię to ze względu na tych ludzi, aby uwierzyli, że to Ty Mnie posłałeś.

43Potem zawołał donośnym głosem:

—Łazarzu! Wyjdź!

44Wtedy zmarły wyszedł z grobu. Jego stopy i ręce były jeszcze powiązane płóciennymi opaskami, a twarz owinięta chustą.

—Rozwiążcie go i pozwólcie mu chodzić—rzekł Jezus.

Spisek przeciwko Jezusowi

45Wówczas wielu ludzi z Jerozolimy, którzy przyszli z Marią i zobaczyli ten cud, uwierzyło Jezusowi. 46Niektórzy jednak odeszli stamtąd i powiadomili o wszystkim faryzeuszy. 47Ci zaś, razem z najwyższymi kapłanami, zwołali posiedzenie Wysokiej Rady.

—Co robić?—zastanawiali się. —Ten człowiek dokonuje tak wielu cudów. 48Jeżeli nic z nim nie zrobimy, wszyscy Mu uwierzą! A wtedy nadciągną Rzymianie i odbiorą nam świątynię i władzę nad krajem.

49W tym momencie głos zabrał niejaki Kajfasz, który tego roku sprawował urząd najwyższego kapłana:

—Nic nie rozumiecie! 50Przecież lepiej będzie, jeśli jeden człowiek umrze za naród, niż miałby zginąć cały naród.

51Nie powiedział tego sam od siebie. Jako najwyższy kapłan wypowiedział proroctwo, że Jezus ma umrzeć za cały naród. 52I nie tylko za naród, lecz również po to, aby zgromadzić razem wszystkie Boże dzieci rozproszone po świecie. 53Tego dnia przywódcy postanowili więc, że zabiją Jezusa. 54Dlatego przestał On jawnie poruszać się po Judei. Skierował się natomiast wraz z uczniami do Efraim, miasteczka położonego blisko pustyni, i tam się zatrzymał. 55Zbliżało się właśnie święto Paschy. I mnóstwo ludzi z całego kraju napływało do Jerozolimy jeszcze przed świętem, aby dopełnić ceremonii oczyszczenia. 56Wszyscy wypatrywali także Jezusa i będąc w świątyni pytali siebie nawzajem:

—Jak myślicie, czy przyjdzie na uroczystości?

57Najwyżsi kapłani i faryzeusze publicznie ogłosili wtedy, że każdy, kto zobaczy Jezusa, ma ich natychmiast o tym poinformować, aby można Go było aresztować.