Yeremia 52 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 52:1-34

Anguko La Yerusalemu

(2 Wafalme 24:18–25:30)

152:1 2Fal 24:17-18; Yos 10:29; Hes 33:20; 2Fal 8:22Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna. 252:2 Yer 36:30Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu. 352:3 Eze 17:12-16; Kut 33:15; Mwa 4:14Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake.

Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.

452:4 Zek 8:19; 2Fal 25:1-7; Yer 34:1; Eze 24:1-2; Kum 28:52-57Hivyo katika mwaka wa tisa wa utawala wa Sedekia, katika siku ya kumi ya mwezi wa kumi, Nebukadneza mfalme wa Babeli akiwa na jeshi lake lote alifanya vita dhidi ya Yerusalemu. Wakapiga kambi nje ya mji na kuuzunguka mji pande zote. 5Mji ulizungukwa na jeshi mpaka mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Mfalme Sedekia.

652:6 Law 26:26; Mao 1:11; Eze 4:16Ilipowadia siku ya tisa ya mwezi wa nne, njaa ikazidi kuwa kali sana ndani ya mji, hadi hapakuwa na chakula kwa ajili ya watu. 752:7 Mao 4:19Kisha ukuta wa mji ukavunjwa na jeshi lote likakimbia. Wakaondoka mjini usiku kupitia lango lililokuwa kati ya kuta mbili karibu na bustani ya mfalme, ingawa Wakaldayo walikuwa wameuzunguka mji. Wakakimbia kuelekea Araba. 8Lakini jeshi la Wakaldayo likamfuatia Mfalme Sedekia na kumpata katika sehemu tambarare za Yeriko. Askari wake wote wakatengwa naye na kutawanyika, 952:9 Yer 21:7; 32:4; Hes 34:11; 13:21naye akakamatwa.

Akapelekwa kwa mfalme wa Babeli huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mahali ambapo alimtangazia hukumu. 1052:10 Yer 22:30; 39:6-7Huko Ribla mfalme wa Babeli aliwachinja wana wa Sedekia mbele ya macho yake. Pia akawaua maafisa wote wa Yuda. 1152:11 Eze 12:13; 17:16; Yer 34:4Kisha akayangʼoa macho ya Sedekia, akamfunga kwa pingu za shaba na kumpeleka Babeli, alipomweka gerezani mpaka siku ya kifo chake.

1252:12 Zek 8:19; Yer 39:9; Zek 7:5Mnamo siku ya kumi ya mwezi wa tano, katika mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mfalme wa Babeli, Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme, aliyemtumikia mfalme wa Babeli, alikuja Yerusalemu. 1352:13 2Nya 36:19; Kum 29:24; Mik 3:12; Za 74:8; Yer 19:13; Kum 13:16; Mao 2:6Alichoma moto Hekalu la Bwana, jumba la kifalme, na nyumba zote za Yerusalemu. Aliteketeza kila jengo muhimu. 14Jeshi lote la Wakaldayo chini ya jemadari wa askari walinzi wa mfalme walivunja kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu. 1552:15 2Fal 24:1; Yer 38:19; 1:3Nebuzaradani, jemadari wa askari walinzi, akawapeleka uhamishoni baadhi ya watu maskini sana na wale waliobaki katika mji, pamoja na mabaki ya watu wa kawaida, na wale waliojisalimisha kwa mfalme wa Babeli. 16Lakini Nebuzaradani akawaacha mabaki ya wale watu maskini kabisa ili watunze mashamba ya mizabibu na mashamba mengine.

1752:17 1Fal 7:15, 27-37; Yer 27:19-22Wakaldayo walivunja vipande zile nguzo za shaba, vile vishikilio vya shaba vilivyohamishika, na ile Bahari ya shaba, ambavyo vyote vilikuwa katika Hekalu la Bwana. Hivyo wakaichukua hiyo shaba yote na kuipeleka Babeli. 1852:18 Kut 27:3; 1Fal 7:45; Hes 4:14Wakachukua pia vyungu, masepetu, mikasi ya kusawazishia tambi, mabakuli ya kunyunyizia, sahani na vyombo vyote vya shaba vilivyotumika katika huduma ya Hekalu. 1952:19 Law 10:1; 1Fal 7:50; Hes 3:31; Kut 25:29; Hes 4:7; Dan 5:2; Ezr 1:7Jemadari wa askari walinzi wa mfalme akachukua yale masinia, vile vyetezo, yale mabakuli ya kunyunyizia, zile sufuria, vile vinara vya taa, zile sahani na yale mabakuli yaliyotumika kwa sadaka za vinywaji, vitu vyote vile vilivyokuwa vimetengenezwa kwa dhahabu safi au fedha.

2052:20 1Fal 7:25, 47Shaba iliyotokana na zile nguzo mbili, ile Bahari na wale mafahali kumi na mawili wa shaba waliokuwa chini yake, pamoja na vile vishikilio vilivyohamishika, ambavyo Mfalme Solomoni alikuwa ametengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana, ilikuwa na uzito usioweza kupimika. 21Kila nguzo ilikuwa na urefu wa dhiraa kumi na nane, kimo chake na mzunguko dhiraa kumi na mbili, na unene wa nyanda nne, na zote zilikuwa wazi ndani. 2252:22 1Fal 7:15-16, 20, 47; Kut 28:33Sehemu ya shaba juu ya ile nguzo moja ilikuwa na urefu wa dhiraa tano, na ilikuwa imepambwa kwa wavu na makomamanga ya shaba kuizunguka kote. Ile nguzo nyingine pamoja na makomamanga yake ilifanana na hiyo ya kwanza. 23Kulikuwa na makomamanga tisini na sita pembeni; jumla ya makomamanga juu ya wavu uliokuwa umezunguka yalikuwa mia moja.

2452:24 2Fal 25:18; Yer 37:3; 21:1; 2Fal 12:9Yule jemadari wa askari walinzi akawachukua kama wafungwa Seraya kuhani mkuu, kuhani Sefania aliyefuata kwa cheo, na mabawabu watatu. 2552:25 Yer 36:10Miongoni mwa wale watu waliokuwa wamesalia katika mji, alimchukua afisa kiongozi wa wapiganaji, na washauri saba wa mfalme. Akamchukua pia mwandishi aliyesimamia uandikishaji wa watu wa nchi, pamoja na watu wake sitini waliopatikana ndani ya mji. 26Nebuzaradani jemadari akawachukua hao wote na kuwapeleka kwa mfalme wa Babeli huko Ribla. 2752:27 Yer 20:4; Law 26:33; Hes 34:11Huko Ribla, katika nchi ya Hamathi, mfalme wa Babeli akaamuru wanyongwe.

Hivyo Yuda wakaenda utumwani, mbali na nchi yao. 2852:28 2Fal 24:14-16; Neh 1:2; 2Nya 36:20; Kum 28:36Hii ndiyo hesabu ya watu ambao Nebukadneza aliwachukua kwenda uhamishoni:

katika mwaka wa saba,

Wayahudi 3,023;

29katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza,

watu 832 kutoka Yerusalemu;

3052:30 Yer 43:3; 13:19katika mwaka wa ishirini na tatu wa utawala wake,

Wayahudi 745 walichukuliwa kwenda uhamishoni na Nebuzaradani jemadari wa askari walinzi wa mfalme.

Jumla ya watu wote walikuwa 4,600.

Yehoyakini Anaachiwa Huru

3152:31 2Fal 25:27-30; Mwa 40:13-20Katika mwaka wa thelathini na saba tangu Yehoyakini mfalme wa Yuda apelekwe uhamishoni, katika mwaka ule ambao Evil-Merodaki52:31 Pia aliitwa Ameli-Mariduki. alifanyika mfalme wa Babeli, alimwacha huru Yehoyakini mfalme wa Yuda, na kumfungua kutoka gerezani siku ya ishirini na tano ya mwezi wa kumi na mbili. 32Alizungumza naye kwa upole na kumpa kiti cha heshima zaidi kuliko wale wafalme wengine aliokuwa nao huko Babeli. 3352:33 2Sam 9:7, 13Hivyo Yehoyakini akayavua mavazi yake ya mfungwa, na siku zote za maisha yake zilizobaki alikula mezani mwa mfalme. 3452:34 2Sam 9:10Siku kwa siku mfalme wa Babeli alimpa Yehoyakini posho siku zote za maisha yake, hadi siku ya kifo chake.

La Bible du Semeur

Jérémie 52:1-34

Appendice historique

La prise de Jérusalem

1Sédécias avait vingt et un ans à son avènement. Il régna onze ans à Jérusalem. Sa mère s’appelait Hamoutal, elle était fille de Jérémie, de Libna52.1 Ce chapitre reproduit presque intégralement 2 R 24.18-20 ; 25.1-21, 25-30. Pour les notes, voir ces chapitres de 2 Rois.. 2Il fit ce que l’Eternel considère comme mal, tout comme Yehoyaqim. 3Tout cela arriva parce que l’Eternel était en colère contre Jérusalem et Juda, au point de les chasser loin de lui.

Or, Sédécias se révolta contre le roi de Babylone. 4La neuvième année de son règne, le dixième jour du dixième mois, Nabuchodonosor, roi de Babylone, vint avec toute son armée attaquer Jérusalem. Ils établirent leur camp devant la ville et construisirent des terrassements tout autour.

5La ville resta assiégée jusqu’à la onzième année du règne de Sédécias.

6Le neuvième jour du quatrième mois, alors que la famine sévissait durement dans la ville et que la population du pays n’avait plus rien à manger, 7une brèche fut ouverte dans le rempart de la ville et tous les soldats52.7 Le texte parallèle de Jr 39.4 mentionne le roi Sédécias avec les soldats. Il figurera aussi dans le présent texte au verset 8. Il est donc possible que l’omission du roi au v. 7 soit due à une erreur de copiste. de Juda s’enfuirent : ils s’échappèrent de la ville, de nuit, par la porte qui se trouvait entre les deux remparts et qui donnait sur le jardin du roi, tandis que la ville était encerclée par les Chaldéens, et ils prirent le chemin de la vallée du Jourdain. 8Mais l’armée des Chaldéens se lança à la poursuite du roi, et rattrapa Sédécias dans la plaine de Jéricho. Alors tous ses soldats se dispersèrent loin de lui. 9Les Chaldéens se saisirent du roi et l’amenèrent au roi de Babylone à Ribla, dans le pays de Hamath, et celui-ci prononça son jugement contre lui. 10Le roi de Babylone fit égorger les fils de Sédécias sous ses yeux. Il fit aussi égorger à Ribla tous les ministres de Juda. 11Puis il fit crever les yeux à Sédécias et le fit lier avec une double chaîne de bronze. Après cela, le roi de Babylone le déporta à Babylone où il l’enferma en prison. Sédécias y resta jusqu’à sa mort.

12Le dixième jour du cinquième mois – c’était la dix-neuvième année du règne de Nabuchodonosor, roi de Babylone – Nebouzaradân, chef de la garde impériale qui était attaché au service personnel du roi de Babylone, fit son entrée à Jérusalem. 13Il mit le feu au temple de l’Eternel, au palais royal, à toutes les maisons et à tous les édifices importants de la ville. 14Les troupes chaldéennes, sous le commandement du chef de la garde, démantelèrent les remparts qui entouraient la ville.

15Nebouzaradân, chef de la garde impériale, déporta une partie des gens les plus pauvres et le reste de la population qui était demeurée dans la ville, ceux qui s’étaient déjà rendus au roi de Babylone et ce qui restait des artisans. 16Mais il laissa une partie des gens pauvres du pays pour cultiver les vignes et les champs.

17Les Chaldéens mirent en pièces les colonnes de bronze du temple de l’Eternel, les chariots et la grande cuve de bronze qui étaient dans le parvis du Temple, et ils emportèrent tout le bronze à Babylone. 18Ils prirent aussi les chaudrons, les pelles, les couteaux, les coupes à aspersion, les autres coupes et tous les autres objets de bronze employés pour le culte. 19Le chef de la garde s’empara de tous les objets d’or et d’argent massif : les bassins, les brasiers, les coupes à aspersion, les chaudrons, les chandeliers, les autres coupes et les bols.

20On ne saurait évaluer le poids du bronze des deux colonnes, de la grande cuve et des douze bœufs de bronze qui soutenaient les chariots, que le roi Salomon avait fait faire pour le temple de l’Eternel. 21Chaque colonne avait neuf mètres de haut, sa circonférence était de six mètres, le bronze avait près de huit centimètres d’épaisseur, la colonne étant creuse à l’intérieur. 22Elle était surmontée d’un chapiteau de bronze de deux mètres cinquante de haut, entouré d’un treillis décoré de grenades. Le tout était en bronze. 23Il y avait quatre-vingt-seize grenades en relief, et en tout, cent grenades autour du treillis.

24Le chef de la garde fit prisonnier le grand-prêtre Seraya, Sophonie, le prêtre en second, et les trois prêtres chargés de surveiller l’entrée du Temple. 25Il arrêta aussi, dans la ville, un haut responsable militaire, sept conseillers du roi, qui étaient restés dans la ville, le secrétaire du chef de l’armée chargé de recruter les soldats dans le pays, ainsi que soixante Judéens qui se trouvaient à l’intérieur de la ville. 26Nebouzaradân, chef de la garde, emmena tous ces prisonniers au roi de Babylone, à Ribla. 27Celui-ci les fit exécuter à Ribla, dans le pays de Hamath. Ainsi, la population de Juda fut déportée loin de sa patrie.

28Voici le nombre des captifs que Nabuchodonosor emmena en exil : 3 023 Judéens, la septième année de son règne52.28 En 597 av. J.-C. : 29832 habitants de Jérusalem la dix-huitième année52.29 En 587 av. J.-C.. 30Puis, la vingt-troisième année du règne de Nabuchodonosor52.30 En 582 av. J.-C., Nebouzaradân, le chef de la garde, déporta encore 745 Judéens ; ce qui donne un total de 4 600 déportés.

Un signe d’espoir : Yehoyakîn gracié

31La trente-septième année52.31 En 561 av. J.-C. de la déportation de Yehoyakîn52.31 Voir 2 R 24.10-17 ; Jr 22.24-27., roi de Juda, le vingt-cinquième jour du douzième mois, Evil-Merodak, roi de Babylone, gracia Yehoyakîn, roi de Juda, l’année de son accession au trône de Babylone, et le fit sortir de prison.

32Il le traita avec bonté et lui accorda une situation supérieure à celle des autres rois exilés avec lui à Babylone. 33Il lui fit quitter ses vêtements de prisonnier et l’admit à prendre ses repas à sa table jusqu’à la fin de sa vie. 34Le roi de Babylone pourvut à son entretien régulier, jour après jour, aussi longtemps qu’il vécut.