Yeremia 51 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 51:1-64

151:1 Isa 41:16; Mt 3:12; Yer 50:14; Isa 13:5-951:1 Yer 46:4; Isa 41:25; Yer 50:28, 45; Isa 13:3; Yer 50:9; Isa 21:5; 41:2Hili ndilo asemalo Bwana:

“Tazama nitaamsha roho ya mwangamizi

dhidi ya Babeli na watu wakaao Leb-Kamai.51:1 Leb-Kamai ni Ukaldayo, yaani Babeli, kwa fumbo.

2Nitawatuma wageni Babeli

kumpepeta na kuiharibu nchi yake;

watampinga kila upande

katika siku ya maafa yake.

351:3 Yer 50:29; 46:4Usimwache mpiga upinde afunge kamba upinde wake,

wala usimwache avae silaha zake.

Usiwaonee huruma vijana wake;

angamiza jeshi lake kabisa.

451:4 Isa 13:15-18; Yer 50:30Wataanguka waliouawa katika Babeli,

wakiwa na majeraha ya kutisha barabarani zake.

551:5 Law 26:44; Isa 54:6-8; Za 91:14; Hos 4:1Kwa maana Israeli na Yuda hawajaachwa

na Mungu wao, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

ingawa nchi yao imejaa uovu

mbele zake yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.

651:6 Ufu 18:4; Isa 48:20; Yer 50:8, 15; Ay 21:19; Isa 1:24; Mao 3:64; Hes 16:26“Kimbieni kutoka Babeli!

Okoeni maisha yenu!

Msiangamizwe kwa sababu ya dhambi zake.

Ni wakati wa kisasi cha Bwana,

atamlipa kile anachostahili.

751:7 Isa 51:22; Ufu 17:4; Yer 25:15-16; 49:12; Ufu 14:8-10Babeli alikuwa kikombe cha dhahabu katika mkono wa Bwana;

aliufanya ulimwengu wote ulewe.

Mataifa walikunywa mvinyo wake;

kwa hiyo sasa wameingiwa na wazimu.

851:8 Isa 14:15; Ufu 14:8; Yer 8:22; Ufu 18:9; Yer 46:11; Isa 21:9Babeli ataanguka ghafula na kuvunjika.

Mwombolezeni!

Tafuteni zeri ya kutuliza maumivu yake,

labda anaweza kupona.

951:9 Isa 13:14; 31:9; Ufu 18:4-5; Yer 50:16“ ‘Tungemponya Babeli,

lakini hawezi kuponyeka;

tumwacheni, na kila mmoja wetu aende nchi yake mwenyewe,

kwa kuwa hukumu yake inafika angani,

inapanda juu hadi mawinguni.’

1051:10 Mik 7:8-9; Za 64:9; Yer 50:28“ ‘Bwana amethibitisha haki yetu;

njooni, tutangaze katika Sayuni

kitu ambacho Bwana Mungu wetu amefanya.’

11“Noeni mishale,

chukueni ngao!

Bwana amewaamsha wafalme wa Wamedi,

kwa sababu nia yake ni kuangamiza Babeli.

Bwana atalipiza kisasi,

kisasi kwa ajili ya Hekalu lake.

1251:12 Za 20:5; 2Sam 18:24; Eze 33:2Twekeni bendera juu ya kuta za Babeli!

Imarisheni ulinzi,

wekeni walinzi,

andaeni waviziao!

Bwana atatimiza kusudi lake,

amri yake juu ya watu wa Babeli.

1351:13 Yer 50:38; Ufu 17:15; Eze 22:27; Hab 2:9; Isa 45:3Wewe uishiye kando ya maji mengi

na uliye na wingi wa hazina,

mwisho wako umekuja,

wakati wako wa kukatiliwa mbali.

1451:14 Mwa 22:16; Amo 6:8; Nah 3:15; Yer 50:15Bwana Mwenye Nguvu Zote

ameapa kwa nafsi yake mwenyewe:

‘Hakika nitakujaza na watu, kama kundi la nzige,

nao watapiga kelele za ushindi juu yako.’

1551:15 Ay 9:8; Isa 40:26; Mdo 14:15; Za 104:24; 136:5“Aliiumba dunia kwa uweza wake;

akaweka misingi ya ulimwengu kwa hekima yake

na akazitandaza mbingu kwa ufahamu wake.

1651:16 Za 18:11-13; Kum 28:12; Yn 1:12; Ay 28:26; Za 135:7Atoapo sauti yake, maji yaliyo katika mbingu hunguruma,

huyafanya mawingu yainuke kutoka miisho ya dunia.

Hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua,

naye huuleta upepo kutoka ghala zake.

1751:17 Isa 44:20; Hab 2:18-19; Yer 50:2“Kila mtu ni mjinga na hana maarifa;

kila sonara ameaibishwa na sanamu zake.

Vinyago vyake ni vya udanganyifu,

havina pumzi ndani yavyo.

1851:18 Yer 18; 15; Yn 2:8Havifai kitu, ni vitu vya kufanyia mzaha,

hukumu yavyo itakapowadia, vitaangamia.

1951:19 Za 119:57; Kut 34:9Yeye Aliye Fungu la Yakobo sivyo alivyo,

kwani ndiye Muumba wa vitu vyote,

pamoja na kabila la urithi wake:

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.

2051:20 Isa 10:5; Zek 9:13; Mik 4:13; Ay 34:24; Isa 45:1“Wewe ndiwe rungu langu la vita,

silaha yangu ya vita:

kwa wewe navunjavunja mataifa,

kwa wewe naangamiza falme,

2151:21 Kut 15:1; Isa 43:17; Yer 50:37kwa wewe navunjavunja

farasi na mpanda farasi,

kwa wewe navunjavunja

gari la vita na mwendeshaji wake,

2251:22 2Nya 36:17; Isa 13:17-18kwa wewe napondaponda

mwanaume na mwanamke,

kwa wewe napondaponda

mzee na kijana,

kwa wewe napondaponda

kijana wa kiume na mwanamwali,

23kwa wewe nampondaponda

mchungaji na kundi,

kwa wewe nampondaponda

mkulima na maksai,

kwa wewe nawapondaponda

watawala na maafisa.

2451:24 Kum 32:41; Mao 3:64; Yer 50:15; Isa 45:1“Mbele ya macho yako nitamlipiza Babeli na wote waishio Ukaldayo kwa ajili ya makosa yote waliyofanya katika Sayuni,” asema Bwana.

2551:25 Yer 21:13; 50:23; Kut 3:20; Zek 4:7“Mimi niko kinyume nawe, ee mlima unaoharibu,

wewe uangamizaye dunia yote,”

asema Bwana.

“Nitanyoosha mkono wangu dhidi yako,

nikuvingirishe kutoka kwenye kilele cha mwamba,

na kukufanya mlima ulioteketezwa kwa moto.

2651:26 Isa 13:19-22; Yer 50:12Hakuna jiwe litakalochukuliwa kutoka kwako

kwa ajili ya kufanywa jiwe la pembeni,

wala jiwe lolote kwa ajili ya msingi,

kwa maana utakuwa ukiwa milele,”

asema Bwana.

2751:27 Isa 13:2; Za 20:5; Mwa 8:4; 10:3; Yer 25:14“Twekeni bendera katika nchi!

Pigeni tarumbeta katikati ya mataifa!

Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake,

iteni falme hizi dhidi yake:

Ararati, Mini na Ashkenazi.

Wekeni jemadari dhidi yake,

pelekeni farasi wengi kama kundi la nzige.

28Andaeni mataifa kwa ajili ya vita dhidi yake,

wafalme wa Wamedi,

watawala wao na maafisa wao wote,

pamoja na nchi zote wanazotawala.

2951:29 Isa 13:20; Yer 50:13; Amu 5:4; Yer 49:21; Za 33:11; Yer 48:9Nchi inatetemeka na kugaagaa,

kwa kuwa makusudi ya Bwana dhidi ya Babeli yanasimama:

yaani, kuangamiza nchi ya Babeli

ili pasiwe na yeyote atakayeishi humo.

3051:30 Yer 50:24; 2Sam 19:16; Mao 2:9; Nah 3:13; Isa 47:14; 45:2Mashujaa wa Babeli wameacha kupigana,

wamebaki katika ngome zao.

Nguvu zao zimekwisha,

wamekuwa kama wanawake.

Makazi yake yameteketezwa kwa moto,

makomeo ya malango yake yamevunjika.

3151:31 Yer 50:24; 2Sam 18:19-31; Dan 5:30Tarishi mmoja humfuata mwingine,

na mjumbe humfuata mjumbe,

kumtangazia mfalme wa Babeli

kwamba mji wake wote umetekwa,

3251:32 Isa 47:14; Yer 50:36Vivuko vya mito vimekamatwa,

mabwawa yenye mafunjo yametiwa moto,

nao askari wameingiwa na hofu kuu.”

3351:33 Isa 21:10; 17:5; Hos 6:11; Mt 13:30; Isa 13:22Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:

“Binti Babeli ni kama sakafu ya kupuria

wakati inapokanyagwa;

wakati wa kumvuna utakuja upesi.”

3451:34 Yer 50:17; Nah 2:12; Hos 8:8“Nebukadneza mfalme wa Babeli ametula,

ametufanya tuchangayikiwe,

ametufanya tuwe gudulia tupu.

Kama nyoka ametumeza

na kujaza tumbo lake kwa vyakula vyetu vizuri,

kisha akatutapika.

35Jeuri iliyofanyiwa miili yetu51:35 Au: Jeuri tuliyofanyiwa sisi na watoto wetu. na iwe juu ya Babeli,”

ndivyo wasemavyo wakaao Sayuni.

“Damu yetu na iwe juu ya wale waishio Babeli,”

asema Yerusalemu.

3651:36 Za 140:12; Mao 3:58; Yer 20:12; Rum 12:19; Hos 13:15; Yer 50:34; Isa 11:15Kwa hiyo, hili ndilo Bwana asemalo:

“Tazama, nitatetea shauri lako

na kulipiza kisasi kwa ajili yako;

nitaikausha bahari yake

na kuzikausha chemchemi zake.

3751:37 Isa 13:22; Ufu 12:8; Yer 50:39; 18:16; Ufu 18:2; Nah 3:6; Mal 2:9Babeli utakuwa lundo la magofu

na makao ya mbweha,

kitu cha kutisha na kudharauliwa,

mahali asipoishi mtu.

38Watu wake wote wananguruma kama simba wadogo,

wanakoroma kama wana simba.

3951:39 Isa 21:5; Yer 50:24; Za 13:3Lakini wakati wakiwa wameamshwa,

nitawaandalia karamu

na kuwafanya walewe,

ili wapige kelele kwa kicheko,

kisha walale milele na wasiamke,”

asema Bwana.

40“Nitawateremsha kama wana-kondoo waendao machinjoni,

kama kondoo dume na mbuzi.

4151:41 Yer 25:26; Isa 13:19; Dan 4:30; Yer 50:13“Tazama jinsi Sheshaki51:41 Sheshaki ni Babeli kwa fumbo. atakamatwa,

majivuno ya dunia yote yatakavyonyakuliwa.

Babeli atakuwa mwenye hofu kiasi gani

kati ya mataifa!

4251:42 Za 18:4; Isa 8:7-8Bahari itainuka juu ya Babeli;

mawimbi yake yenye kunguruma yatamfunika.

4351:43 Isa 13:20; Yer 2:6; Isa 21:1Miji yake itakuwa ukiwa,

kame na jangwa,

nchi ambayo hakuna yeyote anayeishi ndani yake,

ambayo hakuna mtu anayepita humo.

4451:44 Isa 21:9; 2Fal 25:4; Isa 25:12; 46:1; Yer 50:15Nitamwadhibu Beli katika Babeli,

na kumfanya atapike kile alichokimeza.

Mataifa hayatamiminika tena kwake.

Nao ukuta wa Babeli utaanguka.

4551:45 Ufu 18:4; Yer 50:8; Isa 48:20; Za 76:10; 79:6“Tokeni ndani yake, enyi watu wangu!

Okoeni maisha yenu!

Ikimbieni hasira kali ya Bwana.

4651:46 Yer 46:27; 2Fal 19:7; Za 18:45Msikate tamaa wala msiogope tetesi

zitakaposikika katika nchi;

tetesi moja inasikika mwaka huu,

nyingine mwaka unaofuata;

tetesi juu ya jeuri katika nchi,

na ya mtawala dhidi ya mtawala.

4751:47 Isa 46:1-2; Yer 50:12; 27:7; 50:12Kwa kuwa hakika wakati utawadia

nitakapoziadhibu sanamu za Babeli;

nchi yake yote itatiwa aibu,

na watu wake wote waliouawa

wataangukia ndani yake.

4851:48 Isa 44:23; Ufu 18:20; Yer 25:26; Isa 41:25; Za 149:2; Ay 3:7Ndipo mbingu na dunia na vyote vilivyomo ndani yake

vitapiga kelele za shangwe juu ya Babeli,

kwa kuwa kutoka kaskazini

waharabu watamshambulia,”

asema Bwana.

4951:49 Za 137:8; Yer 50:29“Babeli ni lazima aanguke kwa sababu ya kuwaua Waisraeli,

kama vile waliouawa duniani kote

walivyoanguka kwa sababu ya Babeli.

50Wewe uliyepona upanga,

ondoka wala usikawie!

Mkumbuke Bwana ukiwa katika nchi ya mbali,

na utafakari juu ya Yerusalemu.”

5151:51 Za 44:13-16; 79:4; Mao 1:10“Tumetahayari, kwa maana tumetukanwa

na aibu imefunika nyuso zetu,

kwa sababu wageni wameingia

mahali patakatifu pa nyumba ya Bwana.”

5251:52 Ay 24:12“Lakini siku zinakuja,” asema Bwana,

“nitakapoadhibu sanamu zake,

na katika nchi yake yote

waliojeruhiwa watalia kwa maumivu makali.

5351:53 Mwa 11:4; Isa 14:13-14; Ay 15:21; Yer 49:16Hata kama Babeli ikifika angani

na kuziimarisha ngome zake ndefu,

nitatuma waharabu dhidi yake,”

asema Bwana.

54“Sauti ya kilio inasikika kutoka Babeli,

sauti ya uharibifu mkuu

kutoka nchi ya Wakaldayo.

5551:55 Za 18:4; Isa 25:5Bwana ataiangamiza Babeli,

atanyamazisha makelele ya kishindo chake.

Mawimbi ya adui yatanguruma kama maji makuu,

ngurumo ya sauti zao itavuma.

5651:56 Ay 15:21; Mwa 4:24; Za 46:9; Hab 2:8; Za 94:1-2Mharabu atakuja dhidi ya Babeli,

mashujaa wake watakamatwa,

nazo pinde zao zitavunjwa.

Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa kisasi,

yeye atalipiza kikamilifu.

5751:57 Za 76:5; Yer 25:27; Isa 6:5; Yer 46:18; Ay 5:13; Isa 21:7Nitawafanya maafisa wake na wenye busara walewe,

watawala wao, maafisa, pamoja na wapiganaji wao;

watalala milele na hawataamka,”

asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote.

5851:58 2Fal 25:4; Isa 15:4; 47:14; Hab 2:13; Isa 13:2Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo:

“Ukuta mnene wa Babeli utasawazishwa,

na malango yaliyoinuka yatateketezwa kwa moto;

mataifa yanajichosha bure,

taabu ya mataifa ni nishati tu ya miali ya moto.”

5951:59 Yer 36:4; 52:1; 28:1Huu ndio ujumbe Yeremia aliompa afisa Seraya mwana wa Neria mwana wa Maaseya, alipokwenda Babeli pamoja na Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne wa utawala wake. 6051:60 Kut 17:14; Yer 30:2; 36:2Yeremia alikuwa ameandika ndani ya kitabu kuhusu maafa yote yatakayoipata Babeli, yaani yote yaliyokuwa yameandikwa kuhusu Babeli. 61Yeremia akamwambia Seraya, “Utakapofika Babeli, hakikisha kwamba umesoma maneno haya yote kwa sauti kubwa. 6251:62 Isa 13:20; Yer 9:11; 50:13Kisha sema, ‘Ee Bwana, umesema utaangamiza mahali hapa ili mtu wala mnyama asiishi ndani yake, napo patakuwa ukiwa milele.’ 6351:63 Mwa 2:14Utakapomaliza kusoma hiki kitabu, kifungie jiwe kisha ukitupe ndani ya Mto Frati. 6451:64 Ay 31:40; Za 18:21; Eze 26:21; 28:19Kisha sema, ‘Hivi ndivyo Babeli utakavyozama na usiinuke tena, kwa sababu ya maafa nitakayoleta juu yake. Nao watu wake wataanguka.’ ”

Maneno ya Yeremia yanaishia hapa.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Jeremías 51:1-64

1Así dice el Señor:

«Voy a levantar un viento destructor

contra Babilonia y la gente de Leb Camay.51:1 Leb Camay es un criptograma que alude a Caldea, es decir, Babilonia.

2Enviaré contra Babilonia

gente que la lance por los aires,

que la aviente como se avienta el trigo,

hasta dejarla vacía.

En el día de su calamidad

la atacarán por todas partes.

3Que no tense el arquero su arco,51:3 Que no tense el arquero su arco. Frase de difícil traducción.

ni se vista la coraza.

No perdonéis a sus jóvenes;

destruid a su ejército por completo.

4Caerán muertos en el país de los babilonios;

serán traspasados en las calles.

5Aunque Israel y Judá están llenos de culpa

delante del Santo de Israel,

no han sido abandonados por su Dios,

el Señor Todopoderoso.

6»¡Huid de Babilonia!

¡Sálvese quien pueda!

No perezcáis por causa de su iniquidad.

Porque ha llegado la hora

de que el Señor tome venganza;

¡él le dará su merecido!

7En la mano del Señor

Babilonia era una copa de oro

que embriagaba a toda la tierra.

Las naciones bebieron de su vino

y enloquecieron.

8Pero de pronto Babilonia cayó hecha pedazos.

¡Gemid por ella!

Traed bálsamo para su dolor;

tal vez pueda ser curada.

9»“Quisimos curar a Babilonia,

pero no pudo ser sanada;

abandonémosla, y regrese cada uno a su país,

porque llega su condena hasta los cielos;

¡se eleva hasta las nubes!”

10»“¡El Señor nos ha vindicado!

Venid, que en Sión daremos a conocer

lo que ha hecho el Señor, nuestro Dios”.

11»¡Afilad las flechas!

¡Armaos con escudos!

El Señor ha despertado el espíritu

de los reyes de Media

para destruir a Babilonia.

Esta es la venganza del Señor,

la venganza por su templo.

12¡Levantad el estandarte

contra los muros de Babilonia!

¡Reforzad la guardia!

¡Poned centinelas!

¡Preparad la emboscada!

El Señor cumplirá su propósito;

cumplirá su decreto contra los babilonios.

13Tú, que habitas junto a muchas aguas

y eres rica en tesoros,

has llegado a tu fin,

al final de tu existencia.

14El Señor Todopoderoso ha jurado por sí mismo:

“Te llenaré de enemigos, como de langostas,

y sobre ti lanzarán gritos de victoria”.

15»Con su poder hizo el Señor la tierra;

con su sabiduría afirmó el mundo;

con su inteligencia extendió los cielos.

16Ante su trueno, braman las lluvias en el cielo,

y desde los confines de la tierra

hace que suban las nubes;

entre relámpagos desata la lluvia,

y saca de sus depósitos el viento.

17»Todo hombre es necio e ignorante;

todo orfebre se avergüenza de sus ídolos.

Sus ídolos son una mentira;

no tienen aliento de vida.

18Son absurdos, objetos de burla;

en el tiempo del juicio serán destruidos.

19La porción de Jacob no es como aquellos;

su Dios es el creador de todas las cosas.

Su nombre es el Señor Todopoderoso;

Israel es la tribu de su heredad.

20»Tú eres mi mazo, mi arma de guerra;

contigo destrozo naciones y reinos.

21Contigo destrozo jinetes y caballos;

contigo destrozo aurigas y carros de guerra.

22Contigo destrozo hombres y mujeres;

contigo destrozo jóvenes y ancianos,

contigo destrozo jóvenes y doncellas.

23Contigo destrozo pastores y rebaños;

contigo destrozo labradores y yuntas,

contigo destrozo jefes y gobernantes.

24»Pero en vuestra presencia daré su merecido a Babilonia y a todos sus habitantes por todo el mal que han hecho en Sión —afirma el Señor—.

25»Estoy en contra de ti,

monte del exterminio,

que destruyes toda la tierra —afirma el Señor—.

Extenderé mi mano contra ti;

te haré rodar desde los peñascos

y te convertiré en monte quemado.

26No volverán a tomar de ti piedra angular,

ni piedra de cimiento,

porque para siempre quedarás desolada

—afirma el Señor—.

27»¡Levantad la bandera en el país!

¡Tocad la trompeta entre las naciones!

¡Convocad contra ella

a los reinos de Ararat, Mini y Asquenaz!

¡Poned al frente un general!

¡Que avancen los caballos cual plaga de langostas!

28¡Convocad contra ella a las naciones,

a los reyes de Media,

y a sus gobernadores y oficiales!

¡Convocad a todo su imperio!

29La tierra tiembla y se sacude;

se cumplen los planes de Dios contra Babilonia,

al convertirla en un desierto desolado

donde nadie ha de habitar.

30Dejaron de combatir los guerreros de Babilonia;

se escondieron en las fortalezas.

Sus fuerzas se agotaron;

se volvieron como mujeres.

Sus moradas fueron incendiadas

y destrozados sus cerrojos.

31Corre un emisario tras el otro;

un mensajero sigue a otro mensajero,

para anunciar al rey de Babilonia

que toda la ciudad ha sido conquistada.

32Los vados han sido ocupados,

e incendiados los cañaverales;

llenos de pánico quedaron los guerreros».

33Porque así dice el Señor Todopoderoso, el Dios de Israel:

«La bella Babilonia es como una era

en el momento de la trilla;

¡ya le llega el tiempo de la cosecha!»

34«Nabucodonosor, el rey de Babilonia,

me devoró, me confundió;

me dejó como un plato vacío.

Me tragó como un monstruo marino,

con mis delicias se ha llenado el estómago

para luego vomitarme.

35Dice Jerusalén:

“¡Que recaiga sobre Babilonia

la violencia que me hizo!”

Dice la moradora de Sión:

“¡Que mi sangre se derrame

sobre los babilonios!”»

36Por eso, así dice el Señor:

«Voy a defender tu causa,

y llevaré a cabo tu venganza;

voy a secar el agua de su mar,

y dejaré secos sus manantiales.

37Babilonia se convertirá en un montón de ruinas,

en guarida de chacales,

en objeto de horror y de burla,

en un lugar sin habitantes.

38Juntos rugen como leones;

gruñen como cachorros de león.

39Cuando entren en calor, les serviré bebida;

los embriagaré para que se diviertan.

Así dormirán un sueño eterno

del que ya no despertarán

—afirma el Señor—.

40Voy a llevarlos al matadero,

como si fueran corderos;

como carneros y chivos.

41»¡Cómo ha sido capturada Sesac!51:41 Sesac es un criptograma que alude a Babilonia.

¡Cómo ha sido conquistado

el orgullo de toda la tierra!

Babilonia se ha convertido

en un horror para las naciones.

42El mar ha subido contra Babilonia;

agitadas olas la han cubierto.

43Desoladas han quedado sus ciudades:

como un sequedal, como un desierto.

Nadie habita allí;

nadie pasa por ese lugar.

44Voy a castigar al dios Bel en Babilonia;

haré que vomite lo que se ha tragado.

Ya no acudirán a él las naciones,

ni quedará en pie el muro de Babilonia.

45»¡Huye de ella, pueblo mío!

¡Sálvese quien pueda de mi ardiente ira!

46No desfallezcáis, no os acobardéis

por los rumores que corren por el país.

Año tras año surgen nuevos rumores;

cunde la violencia en el país,

y un gobernante se levanta contra otro.

47Se acercan ya los días

en que castigaré a los ídolos de Babilonia.

Toda su tierra será avergonzada;

caerán sus víctimas en medio de ella.

48Entonces el cielo y la tierra,

y todo lo que hay en ellos,

lanzarán gritos de júbilo contra Babilonia,

porque del norte vendrán sus destructores

—afirma el Señor—.

49»Babilonia tiene que caer

por las víctimas de Israel,

así como en toda la tierra

cayeron las víctimas de Babilonia.

50Vosotros, los que escapasteis de la espada,

huid sin demora.

Invocad al Señor en tierras lejanas,

y no dejéis de pensar en Jerusalén».

51«Sentimos vergüenza por los insultos;

estamos cubiertos de deshonra,

porque han penetrado extranjeros

en el santuario del Señor».

52«Por eso, vienen días

en que castigaré a sus ídolos;

a lo largo de todo el país

gemirán sus heridos

—afirma el Señor—.

53Aunque Babilonia suba hasta los cielos,

y en lo alto fortifique sus baluartes,

yo enviaré destructores contra ella

—afirma el Señor—.

54»Se oyen clamores por la gran destrucción

del país de Babilonia.

55El Señor la destruye por completo;

pone fin a su bullicio.

Rugen sus enemigos como olas agitadas;

resuena el estruendo de su voz.

56Llega contra Babilonia el destructor;

sus guerreros serán capturados,

y sus arcos serán hechos pedazos.

Porque el Señor es un Dios

que a cada cual le da su merecido.

57Voy a embriagar a sus jefes y a sus sabios;

a sus gobernadores, oficiales y guerreros;

y dormirán un sueño eterno,

del que no despertarán»,

afirma el Rey,

cuyo nombre es el Señor Todopoderoso.

58Así dice el Señor Todopoderoso:

«Los anchos muros de Babilonia

serán derribados por completo;

sus imponentes puertas serán incendiadas.

Los pueblos se agotan en vano,

y las naciones se fatigan

por lo que se desvanece como el humo».

59Este es el mandato que el profeta Jeremías dio a Seraías, hijo de Nerías y nieto de Maseías, cuando fue a Babilonia con Sedequías, rey de Judá, durante el año cuarto de su reinado. Seraías era el jefe de este viaje. 60Jeremías había descrito en un rollo todas las calamidades que le sobrevendrían a Babilonia, es decir, todo lo concerniente a ella. 61Jeremías le dijo a Seraías: «En cuanto llegues a Babilonia, asegúrate de leerles todas estas palabras. 62Luego diles: “Señor, tú has dicho que vas a destruir este lugar, y que lo convertirás en una desolación perpetua, hasta que no quede en él un solo habitante, ni hombre ni animal”. 63Cuando termines de leer el rollo, átale una piedra y arrójalo al Éufrates. 64Luego diles: “Así se hundirá Babilonia, y nunca más se levantará del desastre que voy a traer sobre ella”».

Aquí concluyen las palabras de Jeremías.