Yeremia 47 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 47:1-7

Ujumbe Kuhusu Wafilisti

147:1 Zek 9:5-7; Sef 2:4-5; Amo 1:6; Mwa 10:14-19Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Wafilisti, kabla Farao hajaishambulia Gaza:

247:2 Isa 8:7; 14:31; 15:3Hili ndilo asemalo Bwana:

“Tazama jinsi maji yanavyoinuka huko kaskazini,

yatakuwa mafuriko yenye nguvu sana.

Yataifurikia nchi na vitu vyote vilivyomo ndani yake,

miji na wale waishio ndani yake.

Watu watapiga kelele;

wote waishio katika nchi wataomboleza

347:3 Yer 46:9; Eze 23:24; Yer 50:43; Eze 7:17; 21:7kwa sauti ya kwato za farasi waendao mbio,

kwa sauti ya magari ya adui

na mngurumo wa magurudumu yake.

Baba hawatageuka kuwasaidia watoto wao,

mikono yao italegea.

447:4 Isa 23:1; Amo 1:9-10; Mwa 10:14-15; Yer 25:22; Yoe 3:4; Kum 2:23; Za 9:2-4Kwa maana siku imewadia

kuwaangamiza Wafilisti wote

na kuwakatilia mbali walionusurika wote

ambao wangeweza kusaidia Tiro na Sidoni.

Bwana anakaribia kuwaangamiza Wafilisti,

mabaki toka pwani za Kaftori.47:4 Kaftori ndio Krete.

547:5 Yer 41:5; Mik 1:16; Yer 25:20; Law 19:28Gaza atanyoa kichwa chake katika kuomboleza,

Ashkeloni atanyamazishwa.

Enyi mabaki kwenye tambarare,

mtajikatakata wenyewe mpaka lini?

647:6 Isa 34:5; Yer 12:12; Eze 21:3; Yer 48:10; 50:35“Mnalia, ‘Aa, upanga wa Bwana,

utaendelea mpaka lini ndipo upumzike?

Rudi ndani ya ala yako;

acha na utulie.’

747:7 Eze 25:15-17Lakini upanga utatuliaje

wakati Bwana ameuamuru,

wakati ameuagiza kuishambulia Ashkeloni

pamoja na pwani yake?”

Hoffnung für Alle

Jeremia 47:1-7

Die Philister werden ausgerottet

1Ehe der Pharao die Stadt Gaza eroberte, empfing der Prophet Jeremia vom Herrn eine Botschaft für die Philister:

2»So spricht der Herr: Seht, aus dem Norden droht eine Flut; das Wasser wird zum reißenden Strom, der über die Ufer tritt. Er überschwemmt das Land und die Felder, er reißt Städte und Menschen mit fort. Die Bewohner rufen um Hilfe, im ganzen Land schreien sie laut! 3Denn sie hören Pferde galoppieren, Räder rasseln, Streitwagen herandonnern. Die Väter fliehen und sehen sich nicht mehr nach ihren Kindern um, die Angst hat sie gepackt! 4Der Tag ist gekommen, an dem das Land der Philister verwüstet wird; die letzten Verbündeten von Tyrus und Sidon werden ausgerottet. Ja, ich, der Herr, lösche die restlichen Philister aus, die einst von der Insel Kreta gekommen sind.

5Die Einwohner von Gaza sind verzweifelt und scheren sich den Kopf kahl, die Menschen in Aschkelon wurden alle umgebracht. Wie lange ritzt ihr euch vor Trauer die Haut blutig, ihr Nachkommen der Enakiter47,5 So nach der griechischen Übersetzung. Der hebräische Text lautet: ihr restlichen Bewohner der Talebene.? 6Ihr schreit: ›Ach, du Schwert des Herrn, wie lange willst du noch zustechen? Hör auf damit, kehr zurück in deine Scheide und lass uns endlich in Ruhe!‹ 7Doch wie kann das Schwert ruhen, wenn ich, der Herr, ihm einen Auftrag gegeben habe? Ich selbst habe ihm befohlen, Aschkelon und das Gebiet an der Küste zu zerstören!«