Ujumbe Kuhusu Wafilisti
147:1 Zek 9:5-7; Sef 2:4-5; Amo 1:6; Mwa 10:14-19Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Wafilisti, kabla Farao hajaishambulia Gaza:
247:2 Isa 8:7; 14:31; 15:3Hili ndilo asemalo Bwana:
“Tazama jinsi maji yanavyoinuka huko kaskazini,
yatakuwa mafuriko yenye nguvu sana.
Yataifurikia nchi na vitu vyote vilivyomo ndani yake,
miji na wale waishio ndani yake.
Watu watapiga kelele;
wote waishio katika nchi wataomboleza
347:3 Yer 46:9; Eze 23:24; Yer 50:43; Eze 7:17; 21:7kwa sauti ya kwato za farasi waendao mbio,
kwa sauti ya magari ya adui
na mngurumo wa magurudumu yake.
Baba hawatageuka kuwasaidia watoto wao,
mikono yao italegea.
447:4 Isa 23:1; Amo 1:9-10; Mwa 10:14-15; Yer 25:22; Yoe 3:4; Kum 2:23; Za 9:2-4Kwa maana siku imewadia
kuwaangamiza Wafilisti wote
na kuwakatilia mbali walionusurika wote
ambao wangeweza kusaidia Tiro na Sidoni.
Bwana anakaribia kuwaangamiza Wafilisti,
mabaki toka pwani za Kaftori.47:4 Kaftori ndio Krete.
547:5 Yer 41:5; Mik 1:16; Yer 25:20; Law 19:28Gaza atanyoa kichwa chake katika kuomboleza,
Ashkeloni atanyamazishwa.
Enyi mabaki kwenye tambarare,
mtajikatakata wenyewe mpaka lini?
647:6 Isa 34:5; Yer 12:12; Eze 21:3; Yer 48:10; 50:35“Mnalia, ‘Aa, upanga wa Bwana,
utaendelea mpaka lini ndipo upumzike?
Rudi ndani ya ala yako;
acha na utulie.’
747:7 Eze 25:15-17Lakini upanga utatuliaje
wakati Bwana ameuamuru,
wakati ameuagiza kuishambulia Ashkeloni
pamoja na pwani yake?”
关于非利士的预言
1在法老攻打迦萨之前,耶和华告诉了耶利米先知有关非利士人的事。
2耶和华说:
“看啊,大水将从北方涨溢,
形成一道洪流,
淹没大地和地上的一切,
吞噬城邑和其中的居民。
人们必呼喊,
地上的居民必哀哭。
3一听见马蹄嗒嗒、
战车隆隆、车轮滚滚的声音,
做父亲的就吓得手脚发软,
无力照顾儿女。
4因为毁灭所有非利士人的日子到了,
铲除泰尔和西顿剩余帮手的日子到了。
耶和华要灭绝迦斐托岛剩余的非利士人。
5迦萨一片荒凉,
亚实基伦沦为废墟。
谷中的余民啊!
你们要割伤身体到何时呢?
6你们大喊,‘耶和华的刀啊,
你何时才停下来呢?
求你入鞘吧!停下来吧!’
7但耶和华已命令它攻击亚实基伦和沿海一带,
它怎能停下来呢?”