Yeremia 47 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 47:1-7

Ujumbe Kuhusu Wafilisti

147:1 Zek 9:5-7; Sef 2:4-5; Amo 1:6; Mwa 10:14-19Hili ndilo neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu Wafilisti, kabla Farao hajaishambulia Gaza:

247:2 Isa 8:7; 14:31; 15:3Hili ndilo asemalo Bwana:

“Tazama jinsi maji yanavyoinuka huko kaskazini,

yatakuwa mafuriko yenye nguvu sana.

Yataifurikia nchi na vitu vyote vilivyomo ndani yake,

miji na wale waishio ndani yake.

Watu watapiga kelele;

wote waishio katika nchi wataomboleza

347:3 Yer 46:9; Eze 23:24; Yer 50:43; Eze 7:17; 21:7kwa sauti ya kwato za farasi waendao mbio,

kwa sauti ya magari ya adui

na mngurumo wa magurudumu yake.

Baba hawatageuka kuwasaidia watoto wao,

mikono yao italegea.

447:4 Isa 23:1; Amo 1:9-10; Mwa 10:14-15; Yer 25:22; Yoe 3:4; Kum 2:23; Za 9:2-4Kwa maana siku imewadia

kuwaangamiza Wafilisti wote

na kuwakatilia mbali walionusurika wote

ambao wangeweza kusaidia Tiro na Sidoni.

Bwana anakaribia kuwaangamiza Wafilisti,

mabaki toka pwani za Kaftori.47:4 Kaftori ndio Krete.

547:5 Yer 41:5; Mik 1:16; Yer 25:20; Law 19:28Gaza atanyoa kichwa chake katika kuomboleza,

Ashkeloni atanyamazishwa.

Enyi mabaki kwenye tambarare,

mtajikatakata wenyewe mpaka lini?

647:6 Isa 34:5; Yer 12:12; Eze 21:3; Yer 48:10; 50:35“Mnalia, ‘Aa, upanga wa Bwana,

utaendelea mpaka lini ndipo upumzike?

Rudi ndani ya ala yako;

acha na utulie.’

747:7 Eze 25:15-17Lakini upanga utatuliaje

wakati Bwana ameuamuru,

wakati ameuagiza kuishambulia Ashkeloni

pamoja na pwani yake?”

Bibelen på hverdagsdansk

Jeremiasʼ Bog 47:1-7

Profeti imod filistrene

1Det følgende budskab om filistrene i Gaza modtog jeg, før byen blev erobret af egypterhæren.

2Herren siger: „En flodbølge fra nord vil oversvømme filistrenes land, og den vil ødelægge byerne med alle deres indbyggere. Folk vil skrige af rædsel, og alle i landet vil græde. 3Hør hestenes trampen og vognhjulenes rumlen, mens de suser fremad. Forældre vil springe for livet uden at få deres hjælpeløse børn med. 4Nu er timen kommet, hvor filistrene og deres forbundsfæller fra Tyrus og Sidon skal udryddes. Ja, Herren udrydder filistrene, den sidste rest af indvandrerne fra Kreta. 5Gazas indbyggere rager håret af i sorg. Ashkalons folk er stumme af rædsel. Resten af det tidligere så mægtige folk snitter sig i huden af bar fortvivlelse.

6Det hjælper ikke, at de råber til mig om at standse fjendens nedslagtninger, 7for det er mig, der har sendt dem. Jeg har beordret dem til at slå ned på Ashkalon, ja, alle dem, der bor langs havet.”