Yeremia 46 – NEN & CARST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 46:1-28

Ujumbe Kuhusu Misri

146:1 Yer 25:15-38; 1:10Hili ni neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu mataifa:

246:2 2Fal 23:29; 2Nya 35:20; Mwa 2:14Kuhusu Misri:

Huu ni ujumbe dhidi ya jeshi la Farao Neko mfalme wa Misri, lililoshindwa huko Karkemishi kwenye Mto Frati na Nebukadneza mfalme wa Babeli, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda:

346:3 Isa 21:5; Yer 51:11-12; Isa 8:9-10; Yoe 3:9-10“Wekeni tayari ngao zenu, kubwa na ndogo,

mtoke kwa ajili ya vita!

446:4 Eze 21:9-11; 2Nya 26:14; Neh 4:16; 1Sam 17:5, 38Fungieni farasi lijamu,

pandeni farasi!

Shikeni nafasi zenu

mkiwa mmevaa chapeo!

Isugueni mikuki yenu,

vaeni dirii vifuani!

546:5 Yer 48:44; Za 31:13; Yer 49:29; Ufu 6:15-17Je, ninaona nini?

Wametiwa hofu,

wanarudi nyuma,

askari wao wameshindwa.

Wanakimbia kwa haraka

pasipo kutazama nyuma,

tena kuna hofu kuu kila upande,”

asema Bwana.

646:6 Isa 30:16; Za 20:8; Dan 11:19; Mwa 2:14; 15:18Walio wepesi na wenye mbio hawawezi kukimbia,

wala wenye nguvu hawawezi kutoroka.

Kaskazini, kando ya Mto Frati,

wanajikwaa na kuanguka.

746:7 Dan 11:22; Yer 47:2“Ni nani huyu ajiinuaye kama Mto Naili,

kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi?

846:8 Dan 11:10; Eze 29:3, 9; 30:12; Amo 8:8Misri hujiinua kama Mto Naili,

kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi.

Husema, ‘Nitainuka na kufunika dunia,

nitaiangamiza miji na watu wake.’

946:9 Mwa 10:6; Yer 47:3; Isa 66:19; Eze 26:10Songeni mbele, enyi farasi!

Endesheni kwa ukali, enyi magari ya farasi,

Endeleeni mbele, enyi mashujaa:

watu wa Kushi46:9 Kushi ni Naili ya Juu; sasa ni Sudan. na Putu46:9 Putu sasa ni Libya. wachukuao ngao,

watu wa Ludi46:9 Nchi iliyo Afrika ya Kaskazini, magharibi ya Mto Naili; sasa ni Libya. wavutao upinde.

1046:10 Eze 32:10; Mao 1:15; Hes 31:3; 2Fal 23:29-30; Law 3:9; Isa 34:6Lakini ile siku ni ya Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

siku ya kulipiza kisasi,

kisasi juu ya adui zake.

Upanga utakula hata utakapotosheka,

hadi utakapozima kiu yake kwa damu.

Kwa maana Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatoa dhabihu

kwenye nchi ya kaskazini, kando ya Mto Frati.

1146:11 Yer 8:22; Mwa 37:35; 2Fal 19:21; Isa 47:1; Yer 30:13“Panda hadi Gileadi ukapate zeri,

ee Bikira Binti wa Misri.

Lakini umetumia dawa nyingi bila mafanikio;

huwezi kupona.

1246:12 Isa 19:4; Nah 3:8-10Mataifa yatasikia juu ya aibu yako,

kilio chako kitaijaza dunia.

Shujaa mmoja atajikwaa juu ya mwingine,

nao wataanguka chini pamoja.”

1346:13 Yer 43:10; Isa 19:1; Yer 27:7; Eze 32:11Huu ndio ujumbe Bwana aliomwambia nabii Yeremia kuhusu kuja kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ili kuishambulia Misri:

1446:14 Yer 43:8; Isa 19:13; 2Sam 2:26; Kum 32:42; Yer 24:8“Tangaza hili katika Misri, nawe ulihubiri katika Migdoli,

hubiri pia katika Memfisi46:14 Memfisi kwa Kiebrania ni Nofu. na Tahpanhesi:46:14 Ni mji katika Misri.

‘Shikeni nafasi zenu na mwe tayari,

kwa kuwa upanga unawala wale wanaokuzunguka.’

1546:15 Yos 23:5; Isa 66:15-16Kwa nini mashujaa wako wamesombwa

na kupelekwa mbali?

Hawawezi kusimama, kwa maana Bwana

atawasukuma awaangushe chini.

1646:16 Law 26:37; Isa 13:14; Yer 25:38Watajikwaa mara kwa mara,

wataangukiana wao kwa wao.

Watasema, ‘Amka, turudi

kwa watu wetu na nchi yetu,

mbali na upanga wa mtesi.’

1746:17 Isa 19:11-16; 1Fal 20:10-11Huko watatangaza,

‘Farao mfalme wa Misri ni makelele tu,

amekosa wasaa wake.’

1846:18 Yer 48:15; Yos 19:22; 1Fal 18:42“Kwa hakika kama niishivyo,” asema Mfalme,

ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote,

“mmoja atakuja ambaye ni kama Tabori miongoni mwa milima,

kama Karmeli kando ya bahari.

1946:19 Yer 48:18; Isa 20:4; 19:13; Eze 29:10-12; 35:7Funga mizigo yako kwenda uhamishoni,

wewe ukaaye Misri,

kwa kuwa Memfisi utaangamizwa

na kuwa magofu pasipo mkazi.

2046:20 Isa 14:31; Hos 10:11; Yer 47:2“Misri ni mtamba mzuri,

lakini kipanga anakuja dhidi yake kutoka kaskazini.

2146:21 2Fal 7:6; Ay 20:24; Za 18:18; Yer 18:17; Lk 15:27; Ay 18:20; Za 37:13Askari wake waliokodiwa katika safu zake

wako kama ndama walionenepeshwa.

Wao pia watageuka na kukimbia pamoja,

hawataweza kuhimili vita,

kwa maana siku ya msiba inakuja juu yao,

wakati wao wa kuadhibiwa.

2246:22 Za 74:5Misri atatoa sauti kama ya nyoka anayekimbia

kadiri adui anavyowasogelea na majeshi,

watakuja dhidi yake wakiwa na mashoka,

kama watu wakatao miti.

2346:23 Isa 29:4; Amo 7:12; Za 74:5; Kum 28:42Wataufyeka msitu wake,”

asema Bwana,

“hata kama umesongamana kiasi gani.

Ni wengi kuliko nzige,

hawawezi kuhesabika.

2446:24 2Fal 24:7; Yer 1:15Binti wa Misri ataaibishwa,

atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.”

2546:25 Eze 30:14; Nah 3:4; Yer 43:12; Isa 20:6; Eze 30:22; 2Fal 24:7Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asema: “Nakaribia kuleta adhabu juu ya Amoni mungu wa Thebesi,46:25 Thebesi kwa Kiebrania ni No (au No-Amoni), mji katika Misri. na juu ya Farao, Misri na miungu yake, na wafalme wake, pamoja na wale wanaomtegemea Farao. 2646:26 Yer 44:30; Isa 19:4; Eze 32:11; 29:11-16Nitawatia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wao, yaani Nebukadneza mfalme wa Babeli na maafisa wake. Hatimaye, hata hivyo, Misri itakaliwa kama nyakati zilizopita,” asema Bwana.

2746:27 Yer 29:14; Isa 41:13; Yer 51:46; Isa 11:11; 43:5; 41:8; Yer 50:19“Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu,

usifadhaike, ee Israeli.

Hakika nitakuokoa kutoka nchi za mbali,

uzao wako kutoka nchi ya uhamisho wao.

Yakobo atakuwa tena na amani na salama,

wala hakuna hata mmoja atakayewatia hofu.

2846:28 Kut 14:22; Hes 14:9; Yer 4:27; Isa 8:9-10Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu,

kwa maana mimi niko pamoja nawe,”

asema Bwana.

“Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote

ambayo miongoni mwake nimekutawanya,

sitakuangamiza wewe kabisa.

Nitakurudi, lakini kwa haki tu,

wala sitakuacha kabisa bila kukuadhibu.”

Священное Писание (Восточный перевод), версия для Таджикистана

Иеремия 46:1-28

Пророчество о Египте

1Вот слово Вечного, которое было к Иеремии о судьбах других народов.

2О Египте, о войске египетского фараона Нехо46:2 Нехо II, правивший Египтом с 610 по 595 гг. до н. э., пошёл на помощь Ашшурубаллиту II, последнему царю Ассирии, воевавшему с Вавилоном., которое было разбито Навуходоносором, царём Вавилона, при Каркемише на реке Евфрат в четвёртом году правления иудейского царя Иоакима, сына Иосии (в 605 г. до н. э.).

3– Готовьте щиты, и большие, и малые,

и выступайте в бой!

4Седлайте коней и садитесь на них!

Надевайте шлемы и становитесь в строй!

Точите копья и надевайте кольчуги!

5Но что Я вижу?

Они испугались,

они отступают,

их воины побеждены.

Они бегут без оглядки,

и ужас со всех сторон, –

возвещает Вечный. –

6Быстрый не сможет убежать,

и сильный не спасётся.

На севере у реки Евфрат

они споткнутся и упадут.

7Кто там вздымается, как Нил,

как реки с бурными водами?

8Египет вздымается, как Нил,

как реки с бурными водами,

говоря: «Поднимусь и покрою землю;

погублю города и их жителей».

9Скачите, кони!

Мчитесь, колесничие!

Выступайте, сильные воины:

воины Эфиопии и Ливии46:9 Букв.: «Пута»., держащие щиты,

и воины Лидии, натягивающие луки.

10Это день Владыки Вечного, Повелителя Сил,

день возмездия для отмщения Его врагам.

Будет меч пожирать, пока не насытится,

пока не утолит жажду кровью.

Это жертва Владыке Вечному, Повелителю Сил,

в северных землях у реки Евфрат.

11– Пойди в Галаад и возьми бальзам46:11 Галаад славился своим целебным бальзамом из смолы мастикового дерева.,

девственная дочь Египта46:11 Девственная дочь Египта – олицетворение Египта. Также в ст. 24..

Напрасно ты лечишься многими снадобьями –

нет тебе исцеления.

12Народы услышали про твой позор;

твой крик наполнил землю.

Споткнулся о воина воин,

и упали оба разом.

13Вот слово, которое Вечный сказал пророку Иеремии о будущем вторжении Навуходоносора, царя Вавилона, в Египет:

14– Объявляйте в Египте,

возвещайте в Мигдоле;

возвещайте и в Мемфисе46:14 Букв.: «Нофе»; так же в ст. 19., и в Тахпанхесе:

«Становись и готовься, Египет:

меч уже пожирает тех, кто вокруг тебя».

15Почему твои воины будут повержены?

Они не смогут выстоять,

потому что Вечный повергнет их.

16Они будут спотыкаться снова и снова,

будут падать один на другого и говорить:

«Вставайте, давайте вернёмся

к своему народу, на нашу родину,

подальше от меча притеснителя».

17Они воскликнут:

«Фараон, царь Египта, – крикун,

упустивший свою возможность».

18Верно, как и то, что Я живу, – возвещает Царь,

Чьё имя Вечный, Повелитель Сил, –

придёт тот, кто велик, как гора Фавор среди гор

и как гора Кармил у моря.

19Собирайте свои пожитки

и готовьтесь к изгнанию, жители Египта,

потому что Мемфис подвергнется разорению,

станет необитаемой развалиной.

20Египет – прекрасная телица,

но с севера летит к ней слепень.

21Даже наёмники в войске Египта

как тучные быки.

Но они повернутся и вместе пустятся в бегство

и не устоят,

потому что настал день их бедствий,

время их наказания.

22Зашипит Египет, как уползающий змей,

так как близятся вражьи войска,

и пойдут они на него с топорами,

как дровосеки.

23Они вырубят его лес, –

возвещает Вечный, –

как бы ни был он густ,

ведь они многочисленнее саранчи,

нет им числа.

24Дочь Египта будет опозорена,

отдана в руки северного народа.

25Вечный, Повелитель Сил, Бог Исроила говорит:

– Я накажу Амона, бога города Фивы46:25 Букв.: «города Но»., и фараона, и Египет, и всех его богов и царей, и тех, кто полагается на фараона. 26Я отдам их в руки тех, кто ищет их смерти, – Навуходоносору, царю Вавилона, и его слугам. Потом Египет будет снова населён людьми, как и в прежние времена, – возвещает Вечный.

27– А ты не бойся, раб Мой Якуб;

не пугайся, Исроил.

Я вызволю тебя из далёкого края,

твоё потомство – из земли его пленения.

Якуб вернётся к спокойной и мирной жизни,

и никто не будет его устрашать.

28Не бойся же, раб Мой Якуб,

потому что Я с тобой, –

возвещает Вечный. –

Я истреблю все народы,

среди которых рассеял тебя,

а тебя не истреблю.

Я накажу тебя по справедливости,

но безнаказанным не оставлю тебя.