Yeremia 37 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 37:1-21

Yeremia Gerezani

137:1 2Fal 14:17; 1Nya 3:16; Eze 17:13; 2Nya 36:10; 24:8, 12; Yer 22:24Sedekia mwana wa Yosia akafanywa kuwa mfalme wa Yuda na Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye akatawala mahali pa Yehoyakini37:1 Yehoyakini ni jina jingine la Yekonia au Konia. mwana wa Yehoyakimu. 237:2 2Fal 24:19; 2Nya 36:12-14; Mit 29:12Lakini sio Sedekia, wala watumishi wake, wala watu wa nchi walisikiliza maneno ya Bwana aliyonena kupitia kwa nabii Yeremia.

337:3 2Fal 25:18; Yer 52:24; Hes 21:7; 1Sam 12:19; Yer 38:14; Kut 8:28; 1Fal 13:6Hata hivyo, Mfalme Sedekia akamtuma Yehukali mwana wa Shelemia, pamoja na kuhani Sefania mwana wa Maaseya kwa nabii Yeremia na ujumbe huu: “Tafadhali utuombee kwa Bwana, Mungu wetu.”

437:4 Yer 32:2Wakati huu Yeremia alikuwa huru kuingia na kutoka katikati ya watu, kwa sababu alikuwa bado hajatiwa gerezani. 537:5 Mwa 15; 18; Yer 34:21; 31:1; Isa 30:5; 2Fal 24:7; Eze 17:15Jeshi la Farao lilikuwa limetoka Misri, nao Wakaldayo waliokuwa wameuzunguka Yerusalemu kwa majeshi waliposikia taarifa kuhusu jeshi hilo walijiondoa Yerusalemu.

6Ndipo neno la Bwana likamjia nabii Yeremia kusema: 737:7 Mwa 25:22; 2Fal 22:18; 18:21; Yer 2:12; 36; Mao 4:17“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: Mwambie mfalme wa Yuda aliyekutuma uniulize mimi, ‘Jeshi la Farao lililotoka kuja kukusaidia litarudi katika nchi yake yenyewe, yaani Misri. 837:8 Yer 21:10; 39; 8; Mit 21:30; Yer 38:3, 8Kisha Wakaldayo watarudi na kushambulia mji huu, watauteka na kuuchoma moto.’

937:9 Yer 29:8; Mk 13:5“Hili ndilo Bwana asemalo: Msijidanganye wenyewe mkifikiri, ‘Hakika Wakaldayo watatuacha na kwenda zao.’ Hakika hawatawaacha! 1037:10 Law 26:36-38; Isa 30:17; Yer 21:4-5, 10Hata kama mngelishinda jeshi lote la Wakaldayo linalowashambulia ninyi, na wakawa ni watu waliojeruhiwa tu waliobaki kwenye mahema yao, wangetoka na kuuchoma mji huu moto.”

11Baada ya jeshi la Wakaldayo kujiondoa kutoka Yerusalemu kwa sababu ya jeshi la Farao, 1237:12 Yer 32:9Yeremia akaanza kuondoka mjini ili kwenda nchi ya Benyamini ili akapate sehemu yake ya milki miongoni mwa watu huko. 1337:13 Yer 20:2; 21:9Lakini alipofika kwenye Lango la Benyamini, mkuu wa walinzi, ambaye jina lake lilikuwa Iriya mwana wa Shelemia mwana wa Hanania, akamkamata Yeremia na kusema, “Wewe unakwenda kujiunga na Wakaldayo!”

1437:14 Isa 58:6; Yer 40:4Yeremia akasema, “Hiyo si kweli, mimi sijiungi na Wakaldayo.” Lakini Iriya hakumsikiliza; badala yake, akamkamata Yeremia na kumpeleka kwa maafisa. 1537:15 Yer 20:2; 38:26; Ebr 11:36; Mdo 5:40; 12:6; 1Fal 22:27Wakamkasirikia Yeremia, wakaamuru apigwe, na akafungwa katika nyumba ya Yonathani mwandishi waliyokuwa wameifanya gereza.

16Yeremia akawekwa kwenye chumba kilichofukuliwa chini, kilichojengwa kwa zege ndani ya gereza chini ya ngome, akakaa huko kwa muda mrefu. 1737:17 Yer 15:11; 38:16; 21:7; Mwa 25:22Kisha Mfalme Sedekia akatumana aletwe katika jumba la kifalme, mahali alipomuuliza kwa siri, “Je, kuna neno lolote kutoka kwa Bwana?”

Yeremia akajibu, “Ndiyo, utatiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli.”

1837:18 1Sam 16:18; Yn 10:32; Mdo 25:8Kisha Yeremia akamwambia Mfalme Sedekia, “Nimefanya kosa gani dhidi yako na maafisa wako au watu hawa, hata ukanitia gerezani? 1937:19 Yer 14:13; Eze 13:2Wako wapi manabii wako waliokutabiria wakisema, ‘Mfalme wa Babeli hatakushambulia wewe wala nchi hii?’ 20Lakini sasa, bwana wangu mfalme, tafadhali sikiliza. Niruhusu nilete maombi yangu mbele yako, usinirudishe kwenye nyumba ya Yonathani mwandishi, nisije nikafia humo.”

2137:21 Law 26:26; 2Kor 4; 6; Isa 33:16; 2Fal 25:3; Yer 52:6; 39:13-14Ndipo Mfalme Sedekia akatoa maagizo Yeremia awekwe katika ua wa walinzi, na apewe mkate kutoka mitaa ya waokaji kila siku mpaka mikate yote katika mji itakapokwisha. Kwa hiyo Yeremia akabaki katika ua wa walinzi.

King James Version

Jeremiah 37:1-21

1And king Zedekiah the son of Josiah reigned instead of Coniah the son of Jehoiakim, whom Nebuchadrezzar king of Babylon made king in the land of Judah. 2But neither he, nor his servants, nor the people of the land, did hearken unto the words of the LORD, which he spake by the prophet Jeremiah.37.2 by…: Heb. by the hand of the prophet 3And Zedekiah the king sent Jehucal the son of Shelemiah and Zephaniah the son of Maaseiah the priest to the prophet Jeremiah, saying, Pray now unto the LORD our God for us. 4Now Jeremiah came in and went out among the people: for they had not put him into prison. 5Then Pharaoh’s army was come forth out of Egypt: and when the Chaldeans that besieged Jerusalem heard tidings of them, they departed from Jerusalem.

6¶ Then came the word of the LORD unto the prophet Jeremiah, saying, 7Thus saith the LORD, the God of Israel; Thus shall ye say to the king of Judah, that sent you unto me to enquire of me; Behold, Pharaoh’s army, which is come forth to help you, shall return to Egypt into their own land. 8And the Chaldeans shall come again, and fight against this city, and take it, and burn it with fire. 9Thus saith the LORD; Deceive not yourselves, saying, The Chaldeans shall surely depart from us: for they shall not depart.37.9 yourselves: Heb. your souls 10For though ye had smitten the whole army of the Chaldeans that fight against you, and there remained but wounded men among them, yet should they rise up every man in his tent, and burn this city with fire.37.10 wounded: Heb. thrust through

11¶ And it came to pass, that when the army of the Chaldeans was broken up from Jerusalem for fear of Pharaoh’s army,37.11 broken…: Heb. made to ascend 12Then Jeremiah went forth out of Jerusalem to go into the land of Benjamin, to separate himself thence in the midst of the people.37.12 separate…: or, to slip away from thence in the midst of the people 13And when he was in the gate of Benjamin, a captain of the ward was there, whose name was Irijah, the son of Shelemiah, the son of Hananiah; and he took Jeremiah the prophet, saying, Thou fallest away to the Chaldeans. 14Then said Jeremiah, It is false; I fall not away to the Chaldeans. But he hearkened not to him: so Irijah took Jeremiah, and brought him to the princes.37.14 false: Heb. falsehood, or, a lie 15Wherefore the princes were wroth with Jeremiah, and smote him, and put him in prison in the house of Jonathan the scribe: for they had made that the prison.

16¶ When Jeremiah was entered into the dungeon, and into the cabins, and Jeremiah had remained there many days;37.16 cabins: or, cells 17Then Zedekiah the king sent, and took him out: and the king asked him secretly in his house, and said, Is there any word from the LORD? And Jeremiah said, There is: for, said he, thou shalt be delivered into the hand of the king of Babylon. 18Moreover Jeremiah said unto king Zedekiah, What have I offended against thee, or against thy servants, or against this people, that ye have put me in prison? 19Where are now your prophets which prophesied unto you, saying, The king of Babylon shall not come against you, nor against this land? 20Therefore hear now, I pray thee, O my lord the king: let my supplication, I pray thee, be accepted before thee; that thou cause me not to return to the house of Jonathan the scribe, lest I die there.37.20 let…: Heb. let my supplication fall 21Then Zedekiah the king commanded that they should commit Jeremiah into the court of the prison, and that they should give him daily a piece of bread out of the bakers’ street, until all the bread in the city were spent. Thus Jeremiah remained in the court of the prison.