Yeremia 35 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 35:1-19

Warekabi Wasifiwa

135:1 Yer 22:18; 2Nya 36:5Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana, wakati wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda: 235:2 2Fal 10:15; 1Nya 2:55; 1Fal 6:5; Kum 15:12“Nenda kwa jamaa ya Warekabi, uwaalike waje kwenye moja ya vyumba vya pembeni vya nyumba ya Bwana, na uwape divai wanywe.”

3Basi nikaenda kumwita Yaazania mwana wa Yeremia, mwana wa Habazinia, na ndugu zake na wanawe wote, yaani jamaa nzima ya Warekabi. 435:4 Kum 33:1; 1Nya 9:19; 2Fal 12:9; 23:4Nikawaleta katika nyumba ya Bwana, ndani ya chumba cha wana wa Hanani mwana wa Igdalia mtu wa Mungu. Kilikuwa karibu na chumba cha maafisa, ambacho kilikuwa juu ya kile cha Maaseya mwana wa Shalumu, aliyekuwa bawabu. 5Kisha nikaweka mabakuli yaliyojaa divai na baadhi ya vikombe mbele ya watu wa jamaa ya Warekabi na kuwaambia, “Kunyweni divai.”

635:6 Hes 6:2-4; Lk 1:15; Yer 35:2; 2Fal 10:15; Law 10:9Lakini wao wakajibu, “Sisi hatunywi divai, kwa sababu baba yetu Yonadabu mwana wa Rekabu, alitupa agizo hili: ‘Ninyi wala wazao wenu kamwe msinywe divai. 735:7 Ebr 11:9; Kut 20:12; Efe 6:2-3; Kum 4:40Pia msijenge nyumba kamwe, wala kuotesha mbegu au kupanda mashamba ya mizabibu. Kamwe msiwe na kitu chochote katika hivi, lakini siku zote lazima muishi kwenye mahema. Ndipo mtakapoishi kwa muda mrefu katika nchi ambayo ninyi ni wahamiaji.’ 835:8 Kol 3:20; Mit 1:8Tumetii kila kitu ambacho baba yetu Yonadabu mwana wa Rekabu alituamuru. Sisi wenyewe wala wake zetu wala wana wetu na binti zetu kamwe hatujanywa divai 935:9 1Tim 6:6wala kujenga nyumba za kuishi au kuwa na mashamba ya mizabibu, mashamba au mazao. 10Tumeishi katika mahema na tumetii kikamilifu kila kitu alichotuamuru baba yetu Yonadabu. 1135:11 2Fal 24:1; Yer 8:14; Yos 10:20Lakini wakati Nebukadneza mfalme wa Babeli alipoivamia nchi hii, tulisema, ‘Njooni, lazima twende Yerusalemu ili kukimbia majeshi ya Wakaldayo na ya Washamu.’ Kwa hiyo tumeishi Yerusalemu.”

12Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia kusema: 1335:13 Yer 6:10; 32:33; 11:6“Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliye Mungu wa Israeli, asemalo: Nenda ukawaambie watu wa Yuda na watu wa Yerusalemu, ‘Je, hamwezi kujifunza kutoka kwa wana wa Rekabu, na kuyatii maneno yangu?’ asema Bwana. 1435:14 Yer 7:13; 25:3; Isa 30:9‘Yonadabu mwana wa Rekabu aliwaagiza wanawe wasinywe divai, na agizo hilo wamelishika mpaka leo hawanywi divai, kwa sababu wanatii amri ya baba yao. Lakini nimenena nanyi tena na tena, lakini hamkunitii mimi. 1535:15 Yer 7:25; 26:3; 6:10; 25:5; 7:25; 2Fal 17:13; Eze 14:6; Isa 59:20Tena na tena nimewatuma watumishi wangu wote manabii kwenu. Wakasema, “Kila mmoja wenu ni lazima ageuke na kuacha njia zake mbaya, na kuyatengeneza matendo yake. Msifuate miungu mingine ili kuitumikia. Ndipo mtakapoishi katika nchi niliyowapa ninyi na baba zenu.” Lakini hamkujali wala kunisikiliza. 1635:16 Law 20:9; Mal 1:6Wazao wa Yonadabu mwana wa Rekabu walitimiza amri ambayo baba yao aliwapa, lakini watu hawa hawakunitii mimi.’

1735:17 Yos 23:15; 1Fal 13:34; Mit 1:24; Rum 10:21; Isa 66:4; 65:12; Yer 21:4-7“Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Sikilizeni! Nitaleta juu ya Yuda na juu ya kila mmoja aishiye Yerusalemu kila aina ya maafa niliyotamka dhidi yao. Nilinena nao, lakini hawakusikiliza. Niliwaita, lakini hawakujibu.’ ”

1835:18 Mwa 31:35Kisha Yeremia akaiambia jamaa ya Warekabi, “Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: ‘Mmetii amri ya baba yenu Yonadabu, na mmefuata mafundisho yake yote na mmefanya kila kitu alichowaamuru.’ 1935:19 Isa 48:19; Yer 33:17; 15:19Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Yonadabu mwana wa Rekabu hatakosa kamwe kuwa na mtu wa kunitumikia mimi.’ ”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

耶利米书 35:1-19

顺服的利甲族和悖逆的犹大人

1犹大约西亚的儿子约雅敬执政期间,耶和华对耶利米说: 2“你去利甲族那里,邀请他们到耶和华殿的一间厢房,给他们酒喝。” 3于是,我将哈巴洗尼雅的孙子、雅利米雅的儿子雅撒尼亚,以及雅撒尼亚的弟兄和儿子等利甲全族的人, 4领到耶和华的殿,进入上帝的仆人伊基大利之子哈难众儿子的房间。这房间靠近官长的房间,在殿门守卫沙龙的儿子玛西雅的房间上面。 5我把盛满酒的杯和壶摆在利甲全族面前,请他们喝酒。 6他们却说:“我们不喝酒,因为我们的祖先利甲的儿子约拿达曾吩咐我们和我们的子孙永远不可喝酒、 7盖房、撒种、栽植葡萄或拥有葡萄园,一辈子都要住帐篷,以便在异乡长久居住。 8我们遵守他的一切吩咐,我们和我们的妻子儿女从不喝酒, 9不盖房,也没有葡萄园、田地和种子。 10我们住帐篷,遵守我们祖先约拿达的一切吩咐。 11但当巴比伦尼布甲尼撒进攻这里的时候,我们决定来耶路撒冷躲避迦勒底亚兰的军队。因此,我们现在住在耶路撒冷。”

12耶和华对耶利米说: 13“这是以色列的上帝——万军之耶和华的话,你去把我的话告诉犹大人和耶路撒冷的居民,‘耶和华说,你们要听从我的教导。 14利甲的儿子约拿达吩咐他的子孙不可喝酒,他们直到现在都不喝酒。但我屡次告诫你们,你们却不听我的话。 15我再三差遣我的仆人——众先知劝你们改邪归正,不要追随、祭拜别的神明,以便你们可以在我赐给你们和你们祖先的土地上安居乐业,你们却充耳不闻,毫不理会。 16利甲的儿子约拿达的子孙尚且听从他们祖先的吩咐,你们却不听从我的话。 17因此,以色列的上帝——万军之耶和华说,我要给犹大耶路撒冷的居民降下我说过的灾祸。因为我对他们说话,他们不听;我呼唤他们,他们不理会。’”

18然后,耶利米利甲族人说:“以色列的上帝——万军之耶和华说,‘你们听从祖先利甲的儿子约拿达的吩咐,遵守他的一切命令, 19因此,利甲的儿子约拿达的子孙必永远事奉我。这是以色列的上帝——万军之耶和华说的。’”