Yeremia 30 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 30:1-24

Kurudishwa Kwa Israeli

1Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana: 230:2 Isa 30:8; Yer 36:2“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Andika katika kitabu maneno yote niliyonena na wewe. 330:3 Yer 29:14; 16:15; Amo 9:14; Yer 24:6Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘nitakapowaleta watu wangu Israeli na Yuda kutoka uhamishoni, na kuwarudisha katika nchi niliyowapa baba zao ili kuimiliki,’ asema Bwana.”

4Haya ndiyo maneno Bwana aliyoyanena kuhusu Israeli na Yuda: 530:5 Yer 6:25“Hili ndilo asemalo Bwana:

“ ‘Vilio vya woga vinasikika:

hofu kuu, wala si amani.

630:6 Yer 4:31; Isa 29:22Ulizeni na mkaone:

Je, mwanaume aweza kuzaa watoto?

Kwa nini basi ninaona kila mwanaume mwenye nguvu

ameweka mikono yake tumboni

kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa,

kila uso ukigeuka rangi kabisa?

730:7 Isa 2:12; Amo 5:18; Yoe 2:11; Isa 22:5; Sef 1:15; Yer 23:3Tazama jinsi ile siku itakavyokuwa ya kutisha!

Hakutakuwa na nyingine mfano wake.

Utakuwa wakati wa dhiki kwa Yakobo,

lakini ataokolewa kutoka hiyo.

830:8 Isa 9:4; Yer 25:14; Eze 34:27; Yer 27:7; Za 107:14“ ‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote,

‘nitaivunja nira kutoka shingoni mwao

na kuvipasua vifungo vyao;

wageni hawatawafanya tena watumwa.

930:9 Isa 55:3-4; 1Sam 13:14; Hos 1:11; 3:5; Yer 33:15; Eze 34:23-24Badala yake, watamtumikia Bwana, Mungu wao

na Daudi mfalme wao,

nitakayemwinua kwa ajili yao.

1030:10 Isa 41:10-13; 43:5; Yer 29:14; Isa 35:9; Yer 17:25; Isa 29:22; Eze 34:25-28“ ‘Hivyo usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu,

usifadhaike, ee Israeli,’

asema Bwana.

‘Hakika, nitakuokoa kutoka mbali,

wazao wako kutoka nchi ya uhamisho wao.

Yakobo atakuwa tena na amani na usalama,

wala hakuna atakayemtia hofu.

1130:11 Law 26:44; Yer 4:27; 10:24; Hos 11:9; Amo 9:8; Yer 5:18; Isa 29:22; Eze 34:25-28Mimi niko pamoja nawe, nami nitakuokoa,’

asema Bwana.

‘Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote

ambamo miongoni mwao nimewatawanya,

sitawaangamiza ninyi kabisa.

Nitawaadhibu, lakini kwa haki.

Sitawaacha kabisa bila adhabu.’

1230:12 Yer 8:22; 15:18; Ay 6:4; Yer 10:19“Hili ndilo asemalo Bwana:

“ ‘Kidonda chako hakina dawa,

jeraha lako haliponyeki.

1330:13 Nah 3:19; Amu 6:31; Yer 14:19; 8:22; 46:11Hakuna yeyote wa kukutetea shauri lako,

hakuna dawa ya kidonda chako,

wewe hutapona.

1430:14 Yer 22:20; Ay 13:24; 30:21; Yer 25:7; Mao 1:2Wale walioungana nawe wote wamekusahau,

hawajali chochote kukuhusu wewe.

Nimekupiga kama vile adui angelifanya,

na kukuadhibu kama vile mtu mkatili angelifanya,

kwa sababu hatia yako ni kubwa mno

na dhambi zako ni nyingi sana.

1530:15 Yer 10:19; Mit 1:31Kwa nini unalia kwa ajili ya jeraha lako,

yale maumivu yako yasiyoponyeka?

Kwa sababu ya uovu wako mkubwa na dhambi zako nyingi

nimekufanyia mambo haya.

1630:16 Kum 23:22; Yoe 3:4-8; Isa 29:8; Yer 10:25; Isa 14:2; Yer 49:2; 50:10“ ‘Lakini watu wote wakuangamizao wataangamizwa;

adui zako wote watakwenda uhamishoni.

Wale wote wakutekao nyara watatekwa nyara;

wote wakufanyao mateka nitawafanya mateka.

1730:17 Isa 6:12; Yer 33:24; Kut 15:26; Za 142:4Lakini nitakurudishia afya yako

na kuyaponya majeraha yako,’

asema Bwana,

‘kwa sababu umeitwa mwenye kutupwa,

Sayuni ambaye hakuna yeyote anayekujali.’

1830:18 Kum 30:3; Yer 32:44; Za 103:13; Eze 39:25; 36:10; Yer 31:23; Hes 24:5“Hili ndilo asemalo Bwana:

“ ‘Nitarudisha baraka za mahema ya Yakobo,

na kuhurumia maskani yake.

Mji utajengwa tena juu ya magofu yake,

nalo jumba la kifalme litasimama mahali pake halisi.

1930:19 Neh 8:12; Mwa 15:5; Isa 51:3, 11; 60:9; Yer 31:4; Isa 35:10; 44:23; Zek 2:4Nyimbo za kushukuru zitatoka kwao

na sauti ya furaha.

Nitaiongeza idadi yao

wala hawatapungua,

nitawapa heshima

na hawatadharauliwa.

2030:20 Isa 54:13-14; Zek 8:5; Yer 31:17; Kut 23:22Watoto wao watakuwa kama walivyokuwa

siku za zamani,

nayo jumuiya yao itaimarishwa mbele yangu;

nitawaadhibu wale wote wawaoneao.

2130:21 Yer 23:5-6; Hes 16:5; Kum 17:15Mmoja wao atakuwa kiongozi wao;

mtawala wao atainuka miongoni mwao.

Nitamleta karibu nami,

naye atanikaribia mimi,

kwa maana ni nani yule atakayejitolea

kuwa karibu nami?’

asema Bwana.

2230:22 Isa 19:25; Hos 2:23; Law 26:12‘Kwa hiyo ninyi mtakuwa watu wangu,

nami nitakuwa Mungu wenu.’ ”

2330:23 Yer 23:19; 25:32Tazama, tufani ya Bwana

italipuka kwa ghadhabu,

upepo wa kisulisuli uendao kasi

utashuka juu ya vichwa vya waovu.

2430:24 Yer 4:8; Mao 1:12; Yer 4:28; 23:19-20Hasira kali ya Bwana haitarudi nyuma

mpaka atakapotimiza makusudi yote ya moyo wake.

Siku zijazo

mtayaelewa haya.

New International Version

Jeremiah 30:1-24

Restoration of Israel

1This is the word that came to Jeremiah from the Lord: 2“This is what the Lord, the God of Israel, says: ‘Write in a book all the words I have spoken to you. 3The days are coming,’ declares the Lord, ‘when I will bring my people Israel and Judah back from captivity30:3 Or will restore the fortunes of my people Israel and Judah and restore them to the land I gave their ancestors to possess,’ says the Lord.”

4These are the words the Lord spoke concerning Israel and Judah: 5“This is what the Lord says:

“ ‘Cries of fear are heard—

terror, not peace.

6Ask and see:

Can a man bear children?

Then why do I see every strong man

with his hands on his stomach like a woman in labor,

every face turned deathly pale?

7How awful that day will be!

No other will be like it.

It will be a time of trouble for Jacob,

but he will be saved out of it.

8“ ‘In that day,’ declares the Lord Almighty,

‘I will break the yoke off their necks

and will tear off their bonds;

no longer will foreigners enslave them.

9Instead, they will serve the Lord their God

and David their king,

whom I will raise up for them.

10“ ‘So do not be afraid, Jacob my servant;

do not be dismayed, Israel,’

declares the Lord.

‘I will surely save you out of a distant place,

your descendants from the land of their exile.

Jacob will again have peace and security,

and no one will make him afraid.

11I am with you and will save you,’

declares the Lord.

‘Though I completely destroy all the nations

among which I scatter you,

I will not completely destroy you.

I will discipline you but only in due measure;

I will not let you go entirely unpunished.’

12“This is what the Lord says:

“ ‘Your wound is incurable,

your injury beyond healing.

13There is no one to plead your cause,

no remedy for your sore,

no healing for you.

14All your allies have forgotten you;

they care nothing for you.

I have struck you as an enemy would

and punished you as would the cruel,

because your guilt is so great

and your sins so many.

15Why do you cry out over your wound,

your pain that has no cure?

Because of your great guilt and many sins

I have done these things to you.

16“ ‘But all who devour you will be devoured;

all your enemies will go into exile.

Those who plunder you will be plundered;

all who make spoil of you I will despoil.

17But I will restore you to health

and heal your wounds,’

declares the Lord,

‘because you are called an outcast,

Zion for whom no one cares.’

18“This is what the Lord says:

“ ‘I will restore the fortunes of Jacob’s tents

and have compassion on his dwellings;

the city will be rebuilt on her ruins,

and the palace will stand in its proper place.

19From them will come songs of thanksgiving

and the sound of rejoicing.

I will add to their numbers,

and they will not be decreased;

I will bring them honor,

and they will not be disdained.

20Their children will be as in days of old,

and their community will be established before me;

I will punish all who oppress them.

21Their leader will be one of their own;

their ruler will arise from among them.

I will bring him near and he will come close to me—

for who is he who will devote himself

to be close to me?’

declares the Lord.

22“ ‘So you will be my people,

and I will be your God.’ ”

23See, the storm of the Lord

will burst out in wrath,

a driving wind swirling down

on the heads of the wicked.

24The fierce anger of the Lord will not turn back

until he fully accomplishes

the purposes of his heart.

In days to come

you will understand this.