Yeremia 20 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 20:1-18

Yeremia Ateswa Na Pashuri

120:1 1Nya 24:14; 2Fal 25:18; Lk 22:52Ikawa kuhani Pashuri mwana wa Imeri, mkuu wa maafisa wa Hekalu la Bwana, alipomsikia Yeremia akitoa unabii juu ya mambo haya, 220:2 Kum 25:2-3; 2Kor 11:24; Ay 13:27; Zek 14:10; Ay 29:7; Yer 15:15; 37:15; 29:26; Mdo 16:24; Ebr 11:36akaamuru Yeremia nabii apigwe na kufungwa kwenye mkatale katika Lango la Juu la Benyamini huko Hekaluni la Bwana. 3Siku ya pili Pashuri alipomwachia kutoka kwenye mkatale, Yeremia akamwambia, “Bwana hakukuita jina lako kuwa Pashuri bali Magor-Misabibu.20:3 Magor-Misabibu maana yake hapa ni Vitisho pande zote. 420:4 Ay 18:11; Yer 29:21; 25:9; 52:27; 39:9; 21:10; 13:19Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitakufanya kuwa hofu kuu kwako wewe mwenyewe na rafiki zako wote, na kwa macho yako mwenyewe utawaona wakianguka kwa upanga wa adui zao. Nitawatia Yuda wote mikononi mwa mfalme wa Babeli, ambaye atawachukua na kuwapeleka Babeli, ama awaue kwa upanga. 520:5 2Fal 25:15; Yer 17:3; 3:24; 2Fal 20:17Nitatia utajiri wote wa mji huu kwa adui zao: yaani mazao yao yote, vitu vyao vyote vya thamani, na hazina zote za wafalme wa Yuda. Watavitwaa kwa nyara na kuvipeleka Babeli. 620:6 Yer 14:15; Mao 2:14; Yer 28:15Nawe Pashuri pamoja na wote waishio katika nyumba yako mtakwenda uhamishoni Babeli. Mtafia humo na kuzikwa, wewe na rafiki zako wote ambao umewatabiria uongo.’ ”

Malalamiko Ya Yeremia

720:7 Kut 5:23; 22:16; Isa 8:11; 1Kor 9:16; Ay 12:4Ee Bwana, umenidanganya,

nami nikadanganyika;

wewe una nguvu kuniliko,

nawe umenishinda.

Ninadharauliwa mchana kutwa,

kila mmoja ananidhihaki.

820:8 Yer 28:8; 2Nya 36:16; Yer 6:7-10Kila ninenapo, ninapiga kelele

nikitangaza ukatili na uharibifu.

Kwa hiyo neno la Bwana limeniletea matukano

na mashutumu mchana kutwa.

920:9 Za 39:3; Yer 4:19; Amo 3:8; Mdo 4:20; 18:5; Yer 44:16Lakini kama nikisema, “Sitamtaja

wala kusema tena kwa jina lake,”

neno lake linawaka ndani ya moyo wangu kama moto,

moto uliofungwa ndani ya mifupa yangu.

Nimechoka sana kwa kulizuia ndani mwangu;

kweli, siwezi kujizuia.

1020:10 Yer 6:25; Neh 6:6-13; Ay 19:14; Lk 11:54; Za 57:4Ninasikia minongʼono mingi,

“Hofu iko pande zote!

Mshtakini! Twendeni tumshtaki!”

Rafiki zangu wote wananisubiri niteleze,

wakisema,

“Labda atadanganyika;

kisha tutamshinda

na kulipiza kisasi juu yake.”

1120:11 Rum 8:31; Yer 15:15; 17:18; 23:40; 7:19; Za 129:2Lakini Bwana yu pamoja nami

kama shujaa mwenye nguvu;

hivyo washtaki wangu watajikwaa

na kamwe hawatashinda.

Watashindwa, nao wataaibika kabisa;

kukosa adabu kwao hakutasahauliwa.

1220:12 Yer 17:10; Za 54:7; Rum 12:19; Za 62:8; Yer 11:20; Za 7:9; Kum 32:35Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote,

wewe umjaribuye mwenye haki

na kupima moyo na nia,

hebu nione ukilipiza kisasi juu yao,

kwa maana kwako

nimeliweka shauri langu.

1320:13 Za 35:10; Yak 2:5-6; Isa 12:6; Za 34:6; 97:10Mwimbieni Bwana!

Mpeni Bwana sifa!

Yeye huokoa uhai wa mhitaji

kutoka mikononi mwa waovu.

1420:14 Yer 15:10; Ay 3:8, 16Ilaaniwe siku niliyozaliwa!

Nayo isibarikiwe ile siku

mama yangu aliyonizaa!

15Alaaniwe mtu yule aliyemletea baba yangu habari,

yule aliyemfanya afurahi sana, akisema,

“Mtoto amezaliwa kwako,

tena mtoto wa kiume!”

1620:16 Mwa 19:25; Yer 18:22; 6:26Mtu huyo na awe kama miji ile

ambayo Bwana Mungu

aliiangamiza bila huruma.

Yeye na asikie maombolezo asubuhi

na kilio cha vita adhuhuri.

1720:17 Ay 3:10-16; 10:18-19Kwa sababu hakuniua nikiwa tumboni,

hivyo mama yangu angekuwa kaburi langu,

nalo tumbo lake la uzazi

lingebaki kuwa kubwa daima.

1820:18 1Fal 19:4; Za 102:3; Ay 3:20; 3:10-11; Mhu 4:2; Mwa 3:17; Ay 5:7; Za 90:9Kwa nini basi nilitoka tumboni

ili kuona taabu na huzuni,

na kuzimaliza siku zangu katika aibu?

New International Reader’s Version

Jeremiah 20:1-18

Jeremiah and Pashhur

1Pashhur the priest was the official in charge of the Lord’s temple. He was the son of Immer. Pashhur heard Jeremiah prophesying that Jerusalem would be destroyed. 2So he had Jeremiah the prophet beaten. Then Pashhur put him in prison at the Upper Gate of Benjamin at the Lord’s temple. 3The next day Pashhur set him free. Jeremiah said to him, “The Lord’s name for you isn’t Pashhur. The Lord’s name for you is Terror on Every Side. 4The Lord says to you, ‘I will make you a terror to yourself. You will also be a terror to all your friends. With your own eyes you will see them die. Their enemies will kill them with swords. I will hand over all the people of Judah to the king of Babylon. He will carry them away to Babylon or kill them with swords. 5I will hand over all the wealth of this city to Judah’s enemies. I will give them all its products and everything of value. I will turn over to them all the treasures that belonged to the kings of Judah. They will take these things and carry them off to Babylon. 6Pashhur, you and everyone who lives in your house will also be forced to go there. You have prophesied lies to all your friends. So all of you will die and be buried in Babylon.’ ”

Jeremiah Complains to the Lord

7You tricked me, Lord, and I was tricked.

You overpowered me and won.

People make fun of me all day long.

Everyone laughs at me.

8Every time I speak, I cry out.

All you ever tell me to talk about

is fighting and trouble.

Your message has brought me nothing but dishonor.

It has made me suffer shame all day long.

9Sometimes I think, “I won’t talk about his message anymore.

I’ll never speak in his name again.”

But then your message burns in my heart.

It’s like a fire deep inside my bones.

I’m tired of holding it in.

In fact, I can’t.

10I hear many people whispering,

“There is terror on every side!

Bring charges against Jeremiah! Let’s bring charges against him!”

All my friends

are waiting for me to slip.

They are saying, “Perhaps he will be tricked

into making a mistake.

Then we’ll win out over him.

We’ll get even with him.”

11But you are with me like a mighty warrior.

So those who are trying to harm me will trip and fall.

They won’t win out over me.

They will fail. They’ll be totally put to shame.

Their dishonor will never be forgotten.

12Lord, you rule over all.

You test those who do what is right.

You see what is in people’s hearts and minds.

So pay them back for what they’ve done.

I’ve committed my cause to you.

13Sing to the Lord, you people!

Give praise to him!

He saves the lives of people in need.

He saves them from the power of sinful people.

14May the day I was born be cursed!

May the day I was born to my mother not be blessed!

15May the man who brought my father the news be cursed!

He’s the one who made my father very glad.

He said, “You have had a baby! It’s a boy!”

16May that man be like the towns

the Lord destroyed without pity.

May that man hear loud weeping in the morning.

May he hear a battle cry at noon.

17He should have killed me in my mother’s body.

He should have made my mother my grave.

He should have let her body stay large forever.

18Why did I ever come out of my mother’s body?

I’ve seen nothing but trouble and sorrow.

My days will end in shame.