Yeremia 2 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 2:1-37

Israeli Amwacha Mungu

12:1 Isa 38:4; Eze 1:3Neno la Bwana lilinijia kusema, 22:2 Za 71:17; Eze 16:8; Kut 13:21; Hos 2:15; Ufu 2:4; Isa 54:4; Yer 3:4; Kum 1:29“Nenda ukahubiri masikioni mwa watu wa Yerusalemu:

“ ‘Nakumbuka moyo wako wa uchaji katika ujana wako,

jinsi ulivyonipenda kama bibi arusi

na kunifuata katika jangwa lile lote,

katika nchi isiyopandwa mbegu.

32:3 Kut 19:6; Yak 1:18; Kum 7:6; Law 23:9-14; Yer 10:25; Ufu 14:4; Yer 30:16; 50:7Israeli alikuwa mtakatifu kwa Bwana,

kama malimbuko ya kwanza ya mavuno yake;

wote waliowaangamiza walihesabiwa kuwa na hatia,

nayo maafa yaliwakumba,’ ”

asema Bwana.

4Sikia neno la Bwana, ee nyumba ya Yakobo,

nanyi nyote jamaa za nyumba ya Israeli.

52:5 2Fal 17:15; Rum 1:21; Isa 44:9; Kum 32:21; 1Sam 12:21; Za 31:9Hivi ndivyo asemavyo Bwana:

“Je, baba zenu waliona kosa gani kwangu,

hata wakatangatanga mbali nami hivyo?

Walifuata sanamu zisizofaa,

nao wenyewe wakawa hawafai.

62:6 Hos 13:4; Kum 18:5; 32:10; Kut 6:6; Yer 51:43Hawakuuliza, ‘Yuko wapi Bwana,

aliyetupandisha kutoka Misri

na kutuongoza kupitia nyika kame,

kupitia nchi ya majangwa na mabonde,

nchi ya ukame na giza,

nchi ambayo hakuna mtu asafiriye ndani yake

wala hakuna mtu aishiye humo?’

72:7 Hes 13:27; Kum 11:10-12; Za 106:34-39; Kum 8:7-9; Yer 7:30; 16:18; Eze 36:17Niliwaleta katika nchi yenye wingi wa vitu

ili mpate kula matunda yake

na utajiri wa mazao yake.

Lakini mkaja na kuinajisi nchi yangu,

na kuufanya urithi wangu chukizo.

82:8 2Sam 2:12; Rum 2:20; 1Fal 18:22; Yer 23:13; Isa 40:19; Yer 4:22; 3:15; 9:14Makuhani hawakuuliza,

‘Yuko wapi Bwana?’

Wale wanaoshughulikia sheria hawakunijua mimi;

viongozi waliasi dhidi yangu.

Manabii walitabiri kwa jina la Baali,

wakifuata sanamu zisizofaa.

92:9 Isa 3:13; Mik 6:2; Eze 20:35-36; Yer 25:31“Kwa hiyo naleta tena mashtaka dhidi yako,”

asema Bwana.

“Nami nitaleta mashtaka dhidi ya watoto wa watoto wako.

102:10 Mwa 10:4; 25:13Vuka, nenda ngʼambo mpaka pwani ya Kitimu2:10 Kitimu hapa ni Kipro, kisiwa katika Bahari ya Mediterania. nawe uangalie,

tuma watu waende Kedari, wachunguze kwa makini,

uone kama kumekuwepo kitu kama hiki.

112:11 Gal 4:8; Isa 37:19; Za 106:20; Rum 1:23; Kum 4:5-9; 1Sam 4:21; Yer 16:20Je, taifa limebadili miungu yake wakati wowote?

(Hata ingawa hao si miungu kamwe.)

Lakini watu wangu wamebadili Utukufu wao

kwa sanamu zisizofaa kitu.

12Shangaeni katika hili, ee mbingu,

nanyi tetemekeni kwa hofu kuu,”

asema Bwana.

132:13 Za 36:9; Yn 4:14; Yer 17:13; Kum 31:16; Isa 65:11; 12:3“Watu wangu wametenda dhambi mbili:

Wameniacha mimi,

niliye chemchemi ya maji yaliyo hai,

nao wamejichimbia visima vyao wenyewe,

visima vilivyobomoka, visivyoweza kuhifadhi maji.

142:14 Kut 4:22; Yer 31:9Je, Israeli ni mtumishi, yaani mtumwa kwa kuzaliwa?

Kwa nini basi amekuwa mateka?

152:15 Yer 4:7; 50:17; 2Fal 25:9; Law 26:43Simba wamenguruma;

wamemngurumia.

Wameifanya nchi yake kuwa ukiwa;

miji yake imeteketezwa, nayo imeachwa haina watu.

162:16 Isa 19:13; Yer 43:7-9Pia watu wa Memfisi2:16 Memfisi kwa Kiebrania ni Nofu. na Tahpanhesi2:16 Tahpanhesi ni mji katika nchi ya Misri.

wamevunja taji ya kichwa chako.

172:17 Yer 4:18; Isa 1:28; Yer 17:13; 19:4Je, hukujiletea hili wewe mwenyewe

kwa kumwacha Bwana, Mungu wako

alipowaongoza njiani?

182:18 Isa 30:2; Hos 13:3; Eze 17:15; 2Fal 16:7; Hos 5:13; 7:11; Isa 7:20Sasa kwa nini uende Misri

kunywa maji ya Shihori?2:18 Kijito kinachoelekeza maji katika Mto Naili.

Nawe kwa nini kwenda Ashuru

kunywa maji ya Mto Frati?

192:19 Hos 14:4; Isa 59:12; Yer 14:7; Kut 19:5; Ay 20:14; Amo 8:10; Yer 3:11; 19:4Uovu wako utakuadhibu;

kurudi nyuma kwako kutakukemea.

Basi kumbuka, utambue

jinsi lilivyo ovu na chungu kwako

unapomwacha Bwana Mungu wako

na kutokuwa na hofu yangu,”

asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.

202:20 Law 26:13; Yer 3:23; Kum 12:2; Yer 5:5; Ay 21:14; Isa 57:7; Eze 16:15; Isa 1:12“Zamani nilivunja nira yako

na kukatilia mbali vifungo vyako;

ukasema, ‘Sitakutumikia!’

Naam kweli, kwenye kila kilima kirefu

na chini ya kila mti uliotanda matawi yake

ulijilaza kama kahaba.

212:21 Kut 15:17; Za 80:8; Mk 12:1; Isa 5:4Nilikupanda ukiwa mzabibu ulio bora sana,

mkamilifu na wa mbegu nzuri.

Ilikuwaje basi ukawa kinyume nami,

ukaharibika na kuwa mzabibu mwitu?

222:22 Za 51:2; Ay 9:30; Mao 1:8, 17; Yer 17:1Hata ujisafishe kwa magadi

na kutumia sabuni nyingi,

bado doa la hatia yako liko mbele zangu,”

asema Bwana Mwenyezi.

232:23 Yer 23:27; Mwa 3:12-13; Rum 3:19; 2Fal 23:10; Yer 31:22; Mit 30:12; Yer 9:14“Wawezaje kusema, ‘Mimi si najisi,

sijawafuata Mabaali’?

Kumbuka jinsi ulivyotenda kule bondeni;

fikiri uliyoyafanya.

Wewe ni ngamia jike mwenye mbio

ukikimbia hapa na pale,

242:24 Mwa 16:12; Yer 14:6; Ay 39:6punda-mwitu aliyezoea jangwa,

anayenusa upepo katika tamaa yake kubwa:

katika wakati wake wa kuhitaji mbegu

ni nani awezaye kumzuia?

Madume yoyote yanayomfuatilia

hayana haja ya kujichosha;

wakati wa kupandwa kwake watampata tu.

252:25 Isa 57:10; Kum 32:16; Yer 3:13; 14:10Usikimbie hadi miguu yako iwe haina viatu,

na koo lako liwe limekauka.

Lakini ulisema, ‘Haina maana!

Ninaipenda miungu ya kigeni,

nami lazima niifuatie.’

26“Kama vile mwizi aaibikavyo wakati amekamatwa,

hivyo ndivyo nyumba ya Israeli inavyoaibishwa:

wao wenyewe, wafalme wao na maafisa wao,

makuhani wao na manabii wao.

272:27 Yer 32:33; Eze 7:22; Isa 26:16; Yer 10:8; 9:3; 1Fal 14:9; 2Nya 29:9Wanaiambia miti, ‘Wewe ndiwe baba yangu,’

nalo jiwe, ‘Wewe ndiwe uliyenizaa.’

Wamenipa visogo vyao

wala hawakunigeuzia nyuso zao;

lakini wakiwa katika taabu, wanasema,

‘Njoo utuokoe!’

282:28 Isa 45:20; Kum 32:37; 2Fal 17:29; Isa 40:19Iko wapi basi ile miungu mliyojitengenezea?

Yenyewe na ije kama inaweza kuwaokoa

wakati mko katika taabu!

Kwa maana mna miungu mingi

kama mlivyo na miji, ee Yuda.

292:29 Dan 9:11; Mik 3:11; Yer 6:13; Mik 7:2“Kwa nini mnaleta mashtaka dhidi yangu?

Ninyi nyote mmeniasi,”

asema Bwana.

302:30 Neh 9:26; 2Nya 36:16; Mdo 7:52; 1The 2:15; Yer 11:21; Law 26:23“Nimeadhibu watu wako bure tu,

hawakujirekebisha.

Upanga wako umewala manabii wako

kama simba mwenye njaa.

312:31 Isa 45:19; Ay 21:14“Enyi wa kizazi hiki, tafakarini neno la Bwana:

“Je, nimekuwa jangwa kwa Israeli

au nchi ya giza kuu?

Kwa nini watu wangu wanasema, ‘Sisi tuko huru kuzurura,

hatutarudi kwako tena’?

32Je, mwanamwali husahau vito vyake,

au bibi arusi mapambo yake ya arusi?

Lakini watu wangu wamenisahau mimi,

tena kwa siku zisizo na hesabu.

33Je, wewe una ustadi kiasi gani katika kufuatia mapenzi!

Hata wale wanawake wabaya kuliko wote

wanaweza kujifunza kutokana na njia zako.

342:34 Yer 19:4; Mit 6:17; Kut 22:2; 2Fal 21:16Katika nguo zako watu huona

damu ya uhai ya maskini wasio na hatia,

ingawa hukuwakamata wakivunja nyumba.

Lakini katika haya yote

352:35 Mit 28:13; Eze 17:20; 2Sam 12:13; 1Yn 1:8-10; Mit 30:12; Isa 66:16; Yer 25:31unasema, ‘Sina hatia;

Mungu hajanikasirikia.’

Lakini nitakuhukumu kwa sababu unasema,

‘Mimi sijatenda dhambi.’

362:36 Yer 31:22; Hos 5:13; Za 108:12; Isa 30:2-7; Yer 37:7Kwa nini unatangatanga sana,

kubadili njia zako?

Utakatishwa tamaa na Misri

kama ulivyokatishwa na Ashuru.

372:37 2Sam 13:19; Yer 37:7Pia utaondoka mahali hapo

ukiwa umeweka mikono kichwani,

kwa kuwa Bwana amewakataa wale unaowatumainia;

hutasaidiwa nao.

Hoffnung für Alle

Jeremia 2:1-37

Mein Volk läuft nutzlosen Götzen nach

1Der Herr gab mir wieder eine Botschaft und befahl: 2»Geh nach Jerusalem und rufe den Menschen dort zu: So spricht der Herr: Ich denke daran, Israel, wie du mir treu gewesen bist, als du noch jung warst. Du liebtest mich wie eine Braut ihren Bräutigam. Selbst durch die Wüste bist du mit mir gegangen, dorthin, wo man weder sät noch erntet. 3Du gehörtest mir allein, so wie die ersten Früchte der Ernte mir gehören. Wer sich an dir vergriff, machte sich schuldig, und ich brachte Unheil über ihn.

4Hört, was ich euch sage, ihr Nachkommen von Jakob, all ihr Sippen Israels: 5Was habe ich euren Vorfahren Böses getan, dass sie sich so weit von mir entfernten? Sie liefen nichtigen Götzen nach und wurden dadurch selbst zunichte. 6Von mir, dem Herrn, wollten sie nichts mehr wissen, dabei hatte ich sie doch aus Ägypten geführt. Durch die Wüste hatte ich sie geleitet, durch ein dürres und zerklüftetes Land, das trocken und dunkel ist, das niemand durchwandert und kein Mensch bewohnt. 7Ich brachte euch in ein fruchtbares Land, damit ihr seine besten Früchte genießen könnt. Doch kaum wart ihr angekommen, da habt ihr es entweiht; mein eigenes Land habt ihr zu einem Ort gemacht, den ich verabscheue. 8Die Priester haben nicht nach mir gefragt, sie, die mit dem Gesetz vertraut sein sollten, kannten mich nicht einmal! Die Führer2,8 Wörtlich: Hirten. – So auch in Kapitel 3,15 und 22,22. meines Volkes haben sich gegen mich aufgelehnt, und die Propheten haben im Namen des Gottes Baal geweissagt, nutzlosen Götzen sind sie nachgelaufen! 9Darum muss ich euch weiterhin anklagen, euch und sogar noch eure Enkel! Darauf gebe ich, der Herr, mein Wort.

10Fahrt doch einmal übers Meer nach Zypern, oder sendet Boten bis ins Wüstenland Kedar und forscht nach, ob es so etwas jemals gab: 11Hat eines dieser Völker je seine Götter gewechselt? Und dabei sind sie doch gar keine Götter! Mein Volk aber hat seinen herrlichen Gott mit nutzlosen Götzen vertauscht, die ihm nicht helfen können! 12Entsetzt euch darüber, ihr Himmel, zittert vor Schreck und Empörung! Das sage ich, der Herr. 13Denn mein Volk hat eine doppelte Sünde begangen: Erst haben sie mich verlassen, die Quelle mit Leben spendendem Wasser, und dann haben sie sich rissige Zisternen ausgehauen, die überhaupt kein Wasser halten.«

Deine Untreue bringt dich zu Fall

14»Israel, bist du denn ein Knecht, schon als Sklave geboren, dass jeder dich als Beute nimmt? 15Deine Feinde brüllen wie die Löwen, sie brüllen und verwüsten dein Land, die Städte sind niedergebrannt und menschenleer. 16Und nun werden auch noch die Ägypter aus Memfis und Tachpanhes kommen und dir den Kopf kahl scheren.

17Das alles hast du dir selbst zuzuschreiben, weil du mich, den Herrn, verlassen hast, deinen Gott, der dich so sicher geführt hat! 18Was versprichst du dir davon, nach Ägypten und Assyrien zu reisen? Willst du etwa aus dem Nil und aus dem Euphrat trinken?2,18 Gemeint ist: sich durch ein Bündnis mit diesen Ländern stärken. 19Deine eigene Bosheit wird dich strafen, deine Untreue bringt dich zu Fall: Erkenne doch, wie schmerzlich und bitter es ist, dass du mich, den Herrn, deinen Gott, verlassen hast und mir keine Ehrfurcht mehr erweist. Das sage ich, der allmächtige Herr und Gott.

20Schon seit jeher hast du dich geweigert, mir zu dienen, du hast dich losgerissen, dich von mir befreit wie von einem drückenden Joch. Und dann warfst du dich anderen Göttern an den Hals wie eine Hure. Auf allen Hügeln und unter jedem dicht belaubten Baum bautest du deine Altäre auf. 21Ich hatte dich als edlen Weinstock eingepflanzt, als Rebe aus bester Züchtung. Wie kommt es dann, dass du zu einem wilden Weinstock wurdest, zu so einer schlechten Rebe? 22Du kannst dich waschen, so viel du willst, mit Seife, sogar mit Natronlauge – den Schmutz deiner Schuld wirst du nicht los, das sage ich, der Herr!

23Wie kannst du da behaupten: ›Ich habe nichts getan! Niemals bin ich anderen Göttern nachgelaufen‹? Führ dir doch vor Augen, was du da unten im Hinnomtal treibst, denk über deine Taten nach! Du bist wie eine brünstige Kamelstute, die ständig hin und her läuft, 24wie eine wilde Eselin, die jeden Pfad in der Wüste kennt; vor Gier schnappt sie nach Luft, und niemand kann sie zurückhalten. Kein Hengst, der sie sucht, muss sich müde laufen: In ihrer Brunstzeit lässt sie sich schnell von ihm finden. 25Israel, lauf dir nicht die Füße wund, sieh zu, dass du nicht verdurstest, wenn du den Göttern hinterherrennst! Du aber sagst: ›Es hat keinen Zweck, mich zu ermahnen! Ich liebe sie nun einmal, die anderen Götter, und hinter ihnen bin ich her!‹

26Doch wie ein Dieb, der auf frischer Tat ertappt wird, kleinlaut dasteht, so muss sich auch Israel schämen: die Könige und führenden Männer, die Priester und Propheten, 27alle, die zu einer Holzstatue sagen: ›Du bist mein Vater!‹, und zu einer Steinsäule: ›Du hast mir das Leben geschenkt!‹ Mir kehren sie nur noch den Rücken zu. Doch wenn sie in Not geraten, dann schreien sie zu mir: ›O Herr, rette uns!‹ 28Ihr Judäer, wo sind nun eure Götter, die ihr euch selbst angefertigt habt? Sollen sie doch kommen und euch aus dem Unglück retten! Denn ihr habt so viele Götter wie Städte im Land! 29Warum klagt ihr mich an?, frage ich euch. Schließlich habt ihr alle mich verlassen! 30Vergeblich habe ich euch geschlagen, ihr wolltet euch nicht ändern. Ich sandte Propheten zu euch, doch ihr habt euch auf sie gestürzt wie wilde Löwen und sie mit euren Schwertern umgebracht.

31Was seid ihr doch für ein Volk! Hört, was ich, der Herr, euch sage: War ich etwa gefährlich für euch wie die Wüste, wie ein Land, in dem Finsternis herrscht? Warum ruft ihr denn: ›Wir wollen weg von dir und kehren nie wieder zurück!‹ 32Vergisst ein Mädchen seinen Schmuck oder eine Braut ihr Hochzeitskleid? Niemals! Mein Volk jedoch hat mich seit langer Zeit vergessen!

33Überall hast du nach Liebhabern gesucht, Israel – das kannst du wirklich gut! Dabei schreckst du selbst vor Verbrechen nicht zurück.2,33 Oder: Dabei kann selbst eine Prostituierte von dir noch etwas lernen. 34Das Blut unschuldiger, armer Menschen klebt an deinen Kleidern. Sie waren keine Einbrecher, du hast sie nicht in Notwehr getötet. Doch trotz allem 35behauptest du: ›Ich habe nichts getan! Gott wird schon nicht länger zornig auf mich sein!‹ Aber glaub mir, ich werde dich vor Gericht bringen, gerade weil du dich für unschuldig hältst!

36Warum läufst du ständig umher und suchst einen neuen Bündnispartner? Ägypten wird dich genauso bitter enttäuschen, wie Assyrien es tat! 37Auch von dort wirst du völlig verzweifelt zurückkehren. Denn ich, der Herr, will von diesen Völkern, auf die du dein Vertrauen setzt, nichts wissen; du wirst mit ihnen kein Glück haben!«