Yeremia 17 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 17:1-27

Dhambi Ya Yuda Na Adhabu Yake

117:1 Ay 19:24; 2Kor 3:3; Mit 3:3; Kum 6:6; Kut 27:2“Dhambi ya Yuda imechorwa kwa kalamu ya chuma,

imeandikwa kwa ncha ya almasi,

kwenye vibao vya mioyo yao

na kwenye pembe za madhabahu zao.

217:2 2Nya 24:18; 2Fal 16:4; Yer 2:20Hata watoto wao wanakumbuka madhabahu zao

na nguzo za Ashera,17:2 Ashera ni mungu mke aliyekuwa anaabudiwa na Wakanaani.

kandokando ya miti iliyotanda

na juu ya vilima virefu.

317:3 2Fal 24:13; Yer 15:13; Mik 3:12; Yer 26:18Mlima wangu katika nchi pamoja na utajiri

na hazina zako zote nitazitoa ziwe nyara,

pamoja na mahali pako pa juu pa kuabudia miungu

kwa sababu ya dhambi katika nchi yako yote.

417:4 Mao 5:2; Yer 12:7; 16:13; 22:28; 7:20; 15:14; Kum 28:48Kwa kosa lako mwenyewe utaupoteza

urithi niliokupa.

Nitakufanya mtumwa wa adui zako

katika nchi usiyoijua,

kwa kuwa umeiwasha hasira yangu,

nayo itawaka milele.”

517:5 Za 108:12; Isa 30:1-3; 2:22; 2Kor 1:9Hili ndilo asemalo Bwana:

“Amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu,

ategemeaye mwenye mwili

kwa ajili ya nguvu zake,

ambaye moyo wake

umemwacha Bwana.

617:6 Kum 29:23; Za 107:34; Ay 20:17; 20:17; 30:3; 39:6; Yer 48:9Atakuwa kama kichaka cha jangwani;

hataona mafanikio yatakapokuja.

Ataishi katika sehemu zisizo na maji,

katika nchi ya chumvi ambapo

hakuna yeyote aishiye humo.

717:7 Mit 16:20; Za 146:5; 34:8; 40:4; Yer 39:18“Lakini amebarikiwa mtu ambaye tumaini lake ni katika Bwana,

ambaye matumaini yake ni katika Bwana.

817:8 Yer 14:1-6; Eze 47:12; Ay 14:9; Za 92:12-14; Eze 19:10Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji

uenezao mizizi yake karibu na kijito cha maji.

Hauogopi wakati wa joto ujapo;

majani yake ni mabichi daima.

Hauna hofu katika mwaka wa ukame

na hautaacha kuzaa matunda.”

917:9 Mhu 9:3; Mt 13:15; Mk 7:21-22Moyo ni mdanganyifu kuliko vitu vyote,

ni mwovu kupita kiasi.

Ni nani awezaye kuujua?

1017:10 Yos 22:22; Mit 17:3; Ufu 2:23; Eze 11:5; Rum 8:27; Za 62:12; Yer 32:19; Rum 2:6“Mimi Bwana huchunguza moyo

na kuzijaribu nia,

ili kumlipa mtu kwa kadiri ya mwenendo wake,

kwa kadiri ya matendo yake yanavyostahili.”

1117:11 Lk 12:20Kama kware aanguaye mayai asiyoyataga,

ndivyo alivyo mtu apataye mali kwa njia zisizo za haki.

Maisha yake yafikapo katikati, siku zitamwacha,

na mwishoni atabainika kuwa mpumbavu.

1217:12 Yer 3:17Kiti cha enzi kilichotukuzwa, kilichoinuliwa tangu mwanzo,

ndiyo sehemu yetu ya mahali patakatifu.

1317:13 Za 71:5; 73:27; Yer 14:8; 2:17; Za 69:28; Eze 13:9; Isa 12:3; Yn 4:10Ee Bwana, uliye tumaini la Israeli,

wote wakuachao wataaibika.

Wale wanaogeukia mbali nawe wataandikwa mavumbini

kwa sababu wamemwacha Bwana,

chemchemi ya maji yaliyo hai.

1417:14 Kut 15:2; Isa 30:26; Yer 15:18; Za 109:1; 119:94Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka;

uniokoe nami nitaokoka,

kwa maana wewe ndiwe ninayekusifu.

1517:15 Isa 5:19; Amo 5:18; 2Pet 3:4-5Wao huendelea kuniambia,

“Liko wapi neno la Bwana?

Sasa na litimie!”

16Sijakukimbia na kuacha kuwa mchungaji wako;

unajua sijaitamani siku ya kukata tamaa.

Kile kipitacho midomoni mwangu

ki wazi mbele yako.

1717:17 Za 88:15-16; 46:1; 18:18; Yer 16:19; Nah 1:7Usiwe kwangu kitu cha kunitia hofu kuu;

wewe ndiwe kimbilio langu katika siku ya maafa.

1817:18 Za 35:1-8; Isa 40:2; Yer 12:3Watesi wangu na waaibishwe,

lakini nilinde mimi nisiaibike;

wao na watiwe hofu kuu,

lakini unilinde mimi na hofu kuu.

Waletee siku ya maafa;

waangamize kwa maangamizi maradufu.

Kuiadhimisha Sabato

1917:19 Yer 7:2; 26:2Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ukasimame kwenye lango la watu, mahali ambako wafalme wa Yuda huingilia na kutokea, simama pia kwenye malango mengine yote ya Yerusalemu. 2017:20 Yer 19:3; 22:2; Za 49:1Waambie, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda, nanyi watu wote wa Yuda, na kila mmoja aishiye Yerusalemu apitaye katika malango haya. 2117:21 Kum 5:14; Yn 5:10; Neh 13:15-21; Hes 15:32-36Hili ndilo asemalo Bwana: Jihadharini msije mkabeba mzigo siku ya Sabato, wala kuingiza mzigo kupitia malango ya Yerusalemu. 2217:22 Eze 20:12; Kut 20:8; Mwa 2:3; Isa 56:2-6Msitoe mizigo nje ya nyumba zenu wala kufanya kazi yoyote wakati wa Sabato, lakini itakaseni siku ya Sabato, kama nilivyowaamuru baba zenu. 2317:23 Yer 7:26; 19:15; 2Nya 28:22; Zek 7:11; Yer 7:28Hata hivyo hawakusikiliza wala kujali, walishupaza shingo zao, na hawakutaka kusikia wala kukubali adhabu. 24Lakini mkiwa waangalifu kunitii, asema Bwana, nanyi msipoleta mzigo wowote kupitia malango ya mji huu wakati wa Sabato, lakini mkaitakasa siku ya Sabato kwa kutofanya kazi siku hiyo, 2517:25 2Sam 7:13; Lk 1:32; Yer 22:2; 30:10; 33:19; Isa 6:6-7; Eze 28:26ndipo wafalme wakaao juu ya kiti cha enzi cha Daudi wataingia kupitia malango ya mji huu, pamoja na maafisa wao. Wao na maafisa wao watakuja wakiwa wamepanda magari na farasi, wakiandamana na watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, nao mji huu utakaliwa na watu daima. 2617:26 Yer 33:14; Zek 7:7; Yer 32:44Watu watakuja kutoka miji ya Yuda na vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, kutoka nchi ya Benyamini na chini ya vilima vya magharibi, kutoka nchi ya vilima na Negebu, wakileta sadaka za kuteketezwa na dhabihu, sadaka za nafaka, uvumba na sadaka za shukrani kwenye nyumba ya Bwana. 2717:27 Yer 22:5; 7:20; Hos 8:14; Amo 2:5; Neh 10:31; 2Fal 25:9; 1Fal 9:6Lakini ikiwa hamtanitii mimi kwa kuitakasa Sabato na kwa kutochukua mzigo wowote mnapoingia katika malango ya Yerusalemu wakati wa Sabato, basi nitawasha moto usiozimika katika malango ya Yerusalemu utakaoteketeza ngome zake.’ ”

King James Version

Jeremiah 17:1-27

1The sin of Judah is written with a pen of iron, and with the point of a diamond: it is graven upon the table of their heart, and upon the horns of your altars;17.1 point: Heb. nail 2Whilst their children remember their altars and their groves by the green trees upon the high hills. 3O my mountain in the field, I will give thy substance and all thy treasures to the spoil, and thy high places for sin, throughout all thy borders. 4And thou, even thyself, shalt discontinue from thine heritage that I gave thee; and I will cause thee to serve thine enemies in the land which thou knowest not: for ye have kindled a fire in mine anger, which shall burn for ever.17.4 thyself: Heb. in thyself

5¶ Thus saith the LORD; Cursed be the man that trusteth in man, and maketh flesh his arm, and whose heart departeth from the LORD. 6For he shall be like the heath in the desert, and shall not see when good cometh; but shall inhabit the parched places in the wilderness, in a salt land and not inhabited. 7Blessed is the man that trusteth in the LORD, and whose hope the LORD is. 8For he shall be as a tree planted by the waters, and that spreadeth out her roots by the river, and shall not see when heat cometh, but her leaf shall be green; and shall not be careful in the year of drought, neither shall cease from yielding fruit.17.8 drought: or, restraint

9¶ The heart is deceitful above all things, and desperately wicked: who can know it? 10I the LORD search the heart, I try the reins, even to give every man according to his ways, and according to the fruit of his doings. 11As the partridge sitteth on eggs, and hatcheth them not; so he that getteth riches, and not by right, shall leave them in the midst of his days, and at his end shall be a fool.17.11 sitteth…: or, gathereth young which she hath not brought forth

12¶ A glorious high throne from the beginning is the place of our sanctuary. 13O LORD, the hope of Israel, all that forsake thee shall be ashamed, and they that depart from me shall be written in the earth, because they have forsaken the LORD, the fountain of living waters. 14Heal me, O LORD, and I shall be healed; save me, and I shall be saved: for thou art my praise.

15¶ Behold, they say unto me, Where is the word of the LORD? let it come now. 16As for me, I have not hastened from being a pastor to follow thee: neither have I desired the woeful day; thou knowest: that which came out of my lips was right before thee.17.16 to…: Heb. after thee 17Be not a terror unto me: thou art my hope in the day of evil. 18Let them be confounded that persecute me, but let not me be confounded: let them be dismayed, but let not me be dismayed: bring upon them the day of evil, and destroy them with double destruction.17.18 destroy…: Heb. break them with a double breach

19¶ Thus said the LORD unto me; Go and stand in the gate of the children of the people, whereby the kings of Judah come in, and by the which they go out, and in all the gates of Jerusalem; 20And say unto them, Hear ye the word of the LORD, ye kings of Judah, and all Judah, and all the inhabitants of Jerusalem, that enter in by these gates: 21Thus saith the LORD; Take heed to yourselves, and bear no burden on the sabbath day, nor bring it in by the gates of Jerusalem; 22Neither carry forth a burden out of your houses on the sabbath day, neither do ye any work, but hallow ye the sabbath day, as I commanded your fathers. 23But they obeyed not, neither inclined their ear, but made their neck stiff, that they might not hear, nor receive instruction. 24And it shall come to pass, if ye diligently hearken unto me, saith the LORD, to bring in no burden through the gates of this city on the sabbath day, but hallow the sabbath day, to do no work therein; 25Then shall there enter into the gates of this city kings and princes sitting upon the throne of David, riding in chariots and on horses, they, and their princes, the men of Judah, and the inhabitants of Jerusalem: and this city shall remain for ever. 26And they shall come from the cities of Judah, and from the places about Jerusalem, and from the land of Benjamin, and from the plain, and from the mountains, and from the south, bringing burnt offerings, and sacrifices, and meat offerings, and incense, and bringing sacrifices of praise, unto the house of the LORD. 27But if ye will not hearken unto me to hallow the sabbath day, and not to bear a burden, even entering in at the gates of Jerusalem on the sabbath day; then will I kindle a fire in the gates thereof, and it shall devour the palaces of Jerusalem, and it shall not be quenched.