Yeremia 17 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 17:1-27

Dhambi Ya Yuda Na Adhabu Yake

117:1 Ay 19:24; 2Kor 3:3; Mit 3:3; Kum 6:6; Kut 27:2“Dhambi ya Yuda imechorwa kwa kalamu ya chuma,

imeandikwa kwa ncha ya almasi,

kwenye vibao vya mioyo yao

na kwenye pembe za madhabahu zao.

217:2 2Nya 24:18; 2Fal 16:4; Yer 2:20Hata watoto wao wanakumbuka madhabahu zao

na nguzo za Ashera,17:2 Ashera ni mungu mke aliyekuwa anaabudiwa na Wakanaani.

kandokando ya miti iliyotanda

na juu ya vilima virefu.

317:3 2Fal 24:13; Yer 15:13; Mik 3:12; Yer 26:18Mlima wangu katika nchi pamoja na utajiri

na hazina zako zote nitazitoa ziwe nyara,

pamoja na mahali pako pa juu pa kuabudia miungu

kwa sababu ya dhambi katika nchi yako yote.

417:4 Mao 5:2; Yer 12:7; 16:13; 22:28; 7:20; 15:14; Kum 28:48Kwa kosa lako mwenyewe utaupoteza

urithi niliokupa.

Nitakufanya mtumwa wa adui zako

katika nchi usiyoijua,

kwa kuwa umeiwasha hasira yangu,

nayo itawaka milele.”

517:5 Za 108:12; Isa 30:1-3; 2:22; 2Kor 1:9Hili ndilo asemalo Bwana:

“Amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu,

ategemeaye mwenye mwili

kwa ajili ya nguvu zake,

ambaye moyo wake

umemwacha Bwana.

617:6 Kum 29:23; Za 107:34; Ay 20:17; 20:17; 30:3; 39:6; Yer 48:9Atakuwa kama kichaka cha jangwani;

hataona mafanikio yatakapokuja.

Ataishi katika sehemu zisizo na maji,

katika nchi ya chumvi ambapo

hakuna yeyote aishiye humo.

717:7 Mit 16:20; Za 146:5; 34:8; 40:4; Yer 39:18“Lakini amebarikiwa mtu ambaye tumaini lake ni katika Bwana,

ambaye matumaini yake ni katika Bwana.

817:8 Yer 14:1-6; Eze 47:12; Ay 14:9; Za 92:12-14; Eze 19:10Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji

uenezao mizizi yake karibu na kijito cha maji.

Hauogopi wakati wa joto ujapo;

majani yake ni mabichi daima.

Hauna hofu katika mwaka wa ukame

na hautaacha kuzaa matunda.”

917:9 Mhu 9:3; Mt 13:15; Mk 7:21-22Moyo ni mdanganyifu kuliko vitu vyote,

ni mwovu kupita kiasi.

Ni nani awezaye kuujua?

1017:10 Yos 22:22; Mit 17:3; Ufu 2:23; Eze 11:5; Rum 8:27; Za 62:12; Yer 32:19; Rum 2:6“Mimi Bwana huchunguza moyo

na kuzijaribu nia,

ili kumlipa mtu kwa kadiri ya mwenendo wake,

kwa kadiri ya matendo yake yanavyostahili.”

1117:11 Lk 12:20Kama kware aanguaye mayai asiyoyataga,

ndivyo alivyo mtu apataye mali kwa njia zisizo za haki.

Maisha yake yafikapo katikati, siku zitamwacha,

na mwishoni atabainika kuwa mpumbavu.

1217:12 Yer 3:17Kiti cha enzi kilichotukuzwa, kilichoinuliwa tangu mwanzo,

ndiyo sehemu yetu ya mahali patakatifu.

1317:13 Za 71:5; 73:27; Yer 14:8; 2:17; Za 69:28; Eze 13:9; Isa 12:3; Yn 4:10Ee Bwana, uliye tumaini la Israeli,

wote wakuachao wataaibika.

Wale wanaogeukia mbali nawe wataandikwa mavumbini

kwa sababu wamemwacha Bwana,

chemchemi ya maji yaliyo hai.

1417:14 Kut 15:2; Isa 30:26; Yer 15:18; Za 109:1; 119:94Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka;

uniokoe nami nitaokoka,

kwa maana wewe ndiwe ninayekusifu.

1517:15 Isa 5:19; Amo 5:18; 2Pet 3:4-5Wao huendelea kuniambia,

“Liko wapi neno la Bwana?

Sasa na litimie!”

16Sijakukimbia na kuacha kuwa mchungaji wako;

unajua sijaitamani siku ya kukata tamaa.

Kile kipitacho midomoni mwangu

ki wazi mbele yako.

1717:17 Za 88:15-16; 46:1; 18:18; Yer 16:19; Nah 1:7Usiwe kwangu kitu cha kunitia hofu kuu;

wewe ndiwe kimbilio langu katika siku ya maafa.

1817:18 Za 35:1-8; Isa 40:2; Yer 12:3Watesi wangu na waaibishwe,

lakini nilinde mimi nisiaibike;

wao na watiwe hofu kuu,

lakini unilinde mimi na hofu kuu.

Waletee siku ya maafa;

waangamize kwa maangamizi maradufu.

Kuiadhimisha Sabato

1917:19 Yer 7:2; 26:2Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ukasimame kwenye lango la watu, mahali ambako wafalme wa Yuda huingilia na kutokea, simama pia kwenye malango mengine yote ya Yerusalemu. 2017:20 Yer 19:3; 22:2; Za 49:1Waambie, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda, nanyi watu wote wa Yuda, na kila mmoja aishiye Yerusalemu apitaye katika malango haya. 2117:21 Kum 5:14; Yn 5:10; Neh 13:15-21; Hes 15:32-36Hili ndilo asemalo Bwana: Jihadharini msije mkabeba mzigo siku ya Sabato, wala kuingiza mzigo kupitia malango ya Yerusalemu. 2217:22 Eze 20:12; Kut 20:8; Mwa 2:3; Isa 56:2-6Msitoe mizigo nje ya nyumba zenu wala kufanya kazi yoyote wakati wa Sabato, lakini itakaseni siku ya Sabato, kama nilivyowaamuru baba zenu. 2317:23 Yer 7:26; 19:15; 2Nya 28:22; Zek 7:11; Yer 7:28Hata hivyo hawakusikiliza wala kujali, walishupaza shingo zao, na hawakutaka kusikia wala kukubali adhabu. 24Lakini mkiwa waangalifu kunitii, asema Bwana, nanyi msipoleta mzigo wowote kupitia malango ya mji huu wakati wa Sabato, lakini mkaitakasa siku ya Sabato kwa kutofanya kazi siku hiyo, 2517:25 2Sam 7:13; Lk 1:32; Yer 22:2; 30:10; 33:19; Isa 6:6-7; Eze 28:26ndipo wafalme wakaao juu ya kiti cha enzi cha Daudi wataingia kupitia malango ya mji huu, pamoja na maafisa wao. Wao na maafisa wao watakuja wakiwa wamepanda magari na farasi, wakiandamana na watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, nao mji huu utakaliwa na watu daima. 2617:26 Yer 33:14; Zek 7:7; Yer 32:44Watu watakuja kutoka miji ya Yuda na vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, kutoka nchi ya Benyamini na chini ya vilima vya magharibi, kutoka nchi ya vilima na Negebu, wakileta sadaka za kuteketezwa na dhabihu, sadaka za nafaka, uvumba na sadaka za shukrani kwenye nyumba ya Bwana. 2717:27 Yer 22:5; 7:20; Hos 8:14; Amo 2:5; Neh 10:31; 2Fal 25:9; 1Fal 9:6Lakini ikiwa hamtanitii mimi kwa kuitakasa Sabato na kwa kutochukua mzigo wowote mnapoingia katika malango ya Yerusalemu wakati wa Sabato, basi nitawasha moto usiozimika katika malango ya Yerusalemu utakaoteketeza ngome zake.’ ”

Hoffnung für Alle

Jeremia 17:1-27

Glücklich ist, wer mir vertraut

1»Volk von Juda, eure Sünde ist tief in euer Herz und auf die Ecken17,1 Wörtlich: Hörner. – Diese ragten an den vier oberen Ecken der Altäre hervor und wurden mit dem Blut der Opfertiere bestrichen, um ihn von der Sünde zu reinigen. – Vgl. 3. Mose 16,18‒19. eurer Altäre geschrieben. Unauslöschlich ist sie eingraviert, wie von einem Eisengriffel mit einer Spitze aus Diamant. 2Selbst eure Kinder denken schon an die Opferaltäre und an die Pfähle, die der Göttin Aschera geweiht sind. Unter den dicht belaubten Bäumen, auf den Hügeln 3und auf den Bergen – überall habt ihr sie aufgestellt. Darum gebe ich euren Besitz und eure Schätze den Feinden zur Plünderung preis,17,3 So nach einigen alten Übersetzungen. Der hebräische Text lautet: Unter den dicht belaubten Bäumen und auf den hohen Hügeln habt ihr sie aufgestellt. Meinen Berg im Land, euren Besitz und eure Schätze gebe ich der Plünderung preis. ebenso all eure Opferstätten, denn im ganzen Land habt ihr dort gegen mich gesündigt.

4Ich hatte euch dieses Land für immer geschenkt; doch ihr werdet es wieder verlieren, und daran seid ihr selbst schuld! In einem Land, das ihr nicht kennt, werdet ihr euren Feinden dienen müssen. Denn ihr habt meinen Zorn herausgefordert, er brennt wie ein unauslöschliches Feuer.

5Ich, der Herr, sage: Mein Fluch lastet auf dem, der sich von mir abwendet, seine Hoffnung auf Menschen setzt und nur auf menschliche Kraft vertraut. 6Er ist wie ein kahler Strauch in der Wüste, der vergeblich auf Regen wartet. Er steht in einem dürren, unfruchtbaren Land, wo niemand wohnt. 7Doch ich segne jeden, der seine Hoffnung auf mich, den Herrn, setzt und mir ganz vertraut. 8Er ist wie ein Baum, der nah am Bach gepflanzt ist und seine Wurzeln zum Wasser streckt: Die Hitze fürchtet er nicht, denn seine Blätter bleiben grün. Auch wenn ein trockenes Jahr kommt, sorgt er sich nicht, sondern trägt Jahr für Jahr Frucht.

9Nichts ist so undurchschaubar wie das menschliche Herz, es ist unheilbar krank. Wer kann es ergründen? 10Ich, der Herr, durchschaue es; ich prüfe jeden Menschen ganz genau und gebe ihm, was er für seine Taten verdient.

11Wer auf unehrliche Weise zu Reichtum gekommen ist, gleicht einem Vogel17,11 Wörtlich: Rebhuhn., der Eier ausbrütet, die er nicht gelegt hat. In der Mitte seines Lebens wird er seinen Reichtum verlieren, und am Ende steht er als Narr da!«

12Unser Tempel ist der herrliche Thron Gottes, seit jeher hoch erhaben. 13Herr, du bist Israels Hoffnung! Wer dich verlässt, der wird scheitern. Wer sich von dir abwendet, dessen Name vergeht so schnell wie ein Wort, das man in den Sand schreibt. Denn er hat dich verlassen, die Quelle mit Leben spendendem Wasser.

Herr, du hast mich berufen – hilf mir jetzt!

14Heile du mich, Herr, dann werde ich geheilt, hilf mir, dann ist mir geholfen! Dich allein will ich preisen! 15Immer wieder fragen sie mich: »Wo bleibt das Unheil, das der Herr uns angedroht hat? Soll es doch eintreffen!« 16Gott, du hast mich zum Hirten deines Volkes berufen, und diesem Auftrag bin ich nicht ausgewichen. Ich habe ihnen nie den Untergang gewünscht – das weißt du! Alles, was ich verkündigt habe, ist dir bekannt. 17Stürze mich nicht in Angst und Schrecken! Du bist doch meine Zuflucht, wenn das Unheil hereinbricht! 18Bring Schande über meine Verfolger, aber nicht über mich! Sorg dafür, dass sie das Entsetzen packt, doch mich verschone! Lass den Tag des Unheils über sie hereinbrechen, sie sollen ein für alle Mal vom Erdboden verschwinden!

Der Sabbat – ein heiliger Tag

19Der Herr sprach zu mir: »Stell dich ans Volkstor17,19 Möglicherweise ist das Haupttor von Jerusalem gemeint. Ein Tor dieses Namens wird sonst nirgendwo in der Bibel erwähnt., durch das die Könige von Juda ein- und ausziehen! Stell dich auch an die anderen Stadttore von Jerusalem 20und ruf: Hört die Botschaft des Herrn, ihr Könige von Juda, ihr Bewohner von Jerusalem und ganz Juda, die ihr durch diese Tore geht!

21So spricht der Herr: Wenn euch euer Leben lieb ist, dann hütet euch davor, am Sabbat irgendeine Last durch diese Tore hereinzutragen! 22Tragt an diesem Tag auch nichts aus euren Häusern, verrichtet am Sabbat keine Arbeit, sondern ehrt ihn als einen Tag, der mir allein geweiht ist. So habe ich es euren Vorfahren befohlen, 23aber sie gehorchten mir nicht, ja, sie hörten nicht einmal hin! Sie haben sich stur gestellt und wollten sich nichts sagen lassen.

24Ich, der Herr, verspreche euch: Wenn ihr wirklich auf mich hört und am Sabbat keine Lasten durch die Tore dieser Stadt bringt, wenn ihr diesen Tag als heilig achtet und keine Arbeit verrichtet, 25dann werden in dieser Stadt auch weiterhin Könige regieren, die Nachkommen von David sind. Mit Pferden und Wagen werden sie durch die Tore ein- und ausziehen, begleitet von ihren obersten Beamten und den Bewohnern von Juda und Jerusalem. Dann wird diese Stadt für immer bewohnt bleiben. 26Aus dem ganzen Land werden Menschen hierherkommen: aus den Städten von Juda und den Dörfern um Jerusalem, aus dem Gebiet von Benjamin, vom Hügelland an der Westküste, aus dem Bergland und aus der Wüste Negev im Süden. Sie werden ihre Opfer zum Tempel bringen: Brand- und Schlachtopfer, Speiseopfer, Weihrauch und Dankopfer. 27Wenn ihr aber mein Gebot nicht befolgt, wenn ihr den Sabbat nicht als heilig achtet, sondern euch an diesem Tag Lasten aufladet und sie durch die Stadttore von Jerusalem hereintragt, dann werde ich in den Toren ein Feuer entfachen, das die Paläste der Stadt verzehrt. Keiner kann dieses Feuer löschen!«