Yeremia 17 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 17:1-27

Dhambi Ya Yuda Na Adhabu Yake

117:1 Ay 19:24; 2Kor 3:3; Mit 3:3; Kum 6:6; Kut 27:2“Dhambi ya Yuda imechorwa kwa kalamu ya chuma,

imeandikwa kwa ncha ya almasi,

kwenye vibao vya mioyo yao

na kwenye pembe za madhabahu zao.

217:2 2Nya 24:18; 2Fal 16:4; Yer 2:20Hata watoto wao wanakumbuka madhabahu zao

na nguzo za Ashera,17:2 Ashera ni mungu mke aliyekuwa anaabudiwa na Wakanaani.

kandokando ya miti iliyotanda

na juu ya vilima virefu.

317:3 2Fal 24:13; Yer 15:13; Mik 3:12; Yer 26:18Mlima wangu katika nchi pamoja na utajiri

na hazina zako zote nitazitoa ziwe nyara,

pamoja na mahali pako pa juu pa kuabudia miungu

kwa sababu ya dhambi katika nchi yako yote.

417:4 Mao 5:2; Yer 12:7; 16:13; 22:28; 7:20; 15:14; Kum 28:48Kwa kosa lako mwenyewe utaupoteza

urithi niliokupa.

Nitakufanya mtumwa wa adui zako

katika nchi usiyoijua,

kwa kuwa umeiwasha hasira yangu,

nayo itawaka milele.”

517:5 Za 108:12; Isa 30:1-3; 2:22; 2Kor 1:9Hili ndilo asemalo Bwana:

“Amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu,

ategemeaye mwenye mwili

kwa ajili ya nguvu zake,

ambaye moyo wake

umemwacha Bwana.

617:6 Kum 29:23; Za 107:34; Ay 20:17; 20:17; 30:3; 39:6; Yer 48:9Atakuwa kama kichaka cha jangwani;

hataona mafanikio yatakapokuja.

Ataishi katika sehemu zisizo na maji,

katika nchi ya chumvi ambapo

hakuna yeyote aishiye humo.

717:7 Mit 16:20; Za 146:5; 34:8; 40:4; Yer 39:18“Lakini amebarikiwa mtu ambaye tumaini lake ni katika Bwana,

ambaye matumaini yake ni katika Bwana.

817:8 Yer 14:1-6; Eze 47:12; Ay 14:9; Za 92:12-14; Eze 19:10Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji

uenezao mizizi yake karibu na kijito cha maji.

Hauogopi wakati wa joto ujapo;

majani yake ni mabichi daima.

Hauna hofu katika mwaka wa ukame

na hautaacha kuzaa matunda.”

917:9 Mhu 9:3; Mt 13:15; Mk 7:21-22Moyo ni mdanganyifu kuliko vitu vyote,

ni mwovu kupita kiasi.

Ni nani awezaye kuujua?

1017:10 Yos 22:22; Mit 17:3; Ufu 2:23; Eze 11:5; Rum 8:27; Za 62:12; Yer 32:19; Rum 2:6“Mimi Bwana huchunguza moyo

na kuzijaribu nia,

ili kumlipa mtu kwa kadiri ya mwenendo wake,

kwa kadiri ya matendo yake yanavyostahili.”

1117:11 Lk 12:20Kama kware aanguaye mayai asiyoyataga,

ndivyo alivyo mtu apataye mali kwa njia zisizo za haki.

Maisha yake yafikapo katikati, siku zitamwacha,

na mwishoni atabainika kuwa mpumbavu.

1217:12 Yer 3:17Kiti cha enzi kilichotukuzwa, kilichoinuliwa tangu mwanzo,

ndiyo sehemu yetu ya mahali patakatifu.

1317:13 Za 71:5; 73:27; Yer 14:8; 2:17; Za 69:28; Eze 13:9; Isa 12:3; Yn 4:10Ee Bwana, uliye tumaini la Israeli,

wote wakuachao wataaibika.

Wale wanaogeukia mbali nawe wataandikwa mavumbini

kwa sababu wamemwacha Bwana,

chemchemi ya maji yaliyo hai.

1417:14 Kut 15:2; Isa 30:26; Yer 15:18; Za 109:1; 119:94Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka;

uniokoe nami nitaokoka,

kwa maana wewe ndiwe ninayekusifu.

1517:15 Isa 5:19; Amo 5:18; 2Pet 3:4-5Wao huendelea kuniambia,

“Liko wapi neno la Bwana?

Sasa na litimie!”

16Sijakukimbia na kuacha kuwa mchungaji wako;

unajua sijaitamani siku ya kukata tamaa.

Kile kipitacho midomoni mwangu

ki wazi mbele yako.

1717:17 Za 88:15-16; 46:1; 18:18; Yer 16:19; Nah 1:7Usiwe kwangu kitu cha kunitia hofu kuu;

wewe ndiwe kimbilio langu katika siku ya maafa.

1817:18 Za 35:1-8; Isa 40:2; Yer 12:3Watesi wangu na waaibishwe,

lakini nilinde mimi nisiaibike;

wao na watiwe hofu kuu,

lakini unilinde mimi na hofu kuu.

Waletee siku ya maafa;

waangamize kwa maangamizi maradufu.

Kuiadhimisha Sabato

1917:19 Yer 7:2; 26:2Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ukasimame kwenye lango la watu, mahali ambako wafalme wa Yuda huingilia na kutokea, simama pia kwenye malango mengine yote ya Yerusalemu. 2017:20 Yer 19:3; 22:2; Za 49:1Waambie, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda, nanyi watu wote wa Yuda, na kila mmoja aishiye Yerusalemu apitaye katika malango haya. 2117:21 Kum 5:14; Yn 5:10; Neh 13:15-21; Hes 15:32-36Hili ndilo asemalo Bwana: Jihadharini msije mkabeba mzigo siku ya Sabato, wala kuingiza mzigo kupitia malango ya Yerusalemu. 2217:22 Eze 20:12; Kut 20:8; Mwa 2:3; Isa 56:2-6Msitoe mizigo nje ya nyumba zenu wala kufanya kazi yoyote wakati wa Sabato, lakini itakaseni siku ya Sabato, kama nilivyowaamuru baba zenu. 2317:23 Yer 7:26; 19:15; 2Nya 28:22; Zek 7:11; Yer 7:28Hata hivyo hawakusikiliza wala kujali, walishupaza shingo zao, na hawakutaka kusikia wala kukubali adhabu. 24Lakini mkiwa waangalifu kunitii, asema Bwana, nanyi msipoleta mzigo wowote kupitia malango ya mji huu wakati wa Sabato, lakini mkaitakasa siku ya Sabato kwa kutofanya kazi siku hiyo, 2517:25 2Sam 7:13; Lk 1:32; Yer 22:2; 30:10; 33:19; Isa 6:6-7; Eze 28:26ndipo wafalme wakaao juu ya kiti cha enzi cha Daudi wataingia kupitia malango ya mji huu, pamoja na maafisa wao. Wao na maafisa wao watakuja wakiwa wamepanda magari na farasi, wakiandamana na watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, nao mji huu utakaliwa na watu daima. 2617:26 Yer 33:14; Zek 7:7; Yer 32:44Watu watakuja kutoka miji ya Yuda na vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, kutoka nchi ya Benyamini na chini ya vilima vya magharibi, kutoka nchi ya vilima na Negebu, wakileta sadaka za kuteketezwa na dhabihu, sadaka za nafaka, uvumba na sadaka za shukrani kwenye nyumba ya Bwana. 2717:27 Yer 22:5; 7:20; Hos 8:14; Amo 2:5; Neh 10:31; 2Fal 25:9; 1Fal 9:6Lakini ikiwa hamtanitii mimi kwa kuitakasa Sabato na kwa kutochukua mzigo wowote mnapoingia katika malango ya Yerusalemu wakati wa Sabato, basi nitawasha moto usiozimika katika malango ya Yerusalemu utakaoteketeza ngome zake.’ ”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

耶利米書 17:1-27

猶大的罪與罰

1猶大人的罪是用鐵筆記錄的,用鑽石鐫刻的,寫在了他們心坎上和祭壇角上。 2他們的兒女沒有忘記綠樹下、高崗上、 3山野間的祭壇和亞舍拉神像。因為他們境內的罪惡,我必使敵人擄掠他們的財寶和神廟。 4他們必失去我賜給他們的產業,被敵人擄到異鄉做奴隸,因為他們激起了我的怒火,永難熄滅。」

5耶和華說:

「信靠世人、倚靠血肉之軀、

背叛耶和華的人該受咒詛!

6這樣的人毫無福樂,

像沙漠中的灌木。

他要住在曠野中乾旱無人的鹽鹼地。

7信靠耶和華、倚靠耶和華的人有福了!

8這樣的人像一棵栽在水邊的樹,

根扎入水中,

不怕炎熱,不怕乾旱,

綠葉如蔭,不斷結果。

9「人心比什麼都詭詐,

無可救藥,

誰能識透呢?

10我耶和華鑒察人心,

察看人的意念,

按照人的行為報應人。」

11謀取不義之財的人就像孵其他鳥蛋的鷓鴣,

他中年便會失去不義之財,

最後成了愚昧之人。

12我們的聖殿是從太初就矗立在高處的榮耀寶座。

13耶和華啊,你是以色列的盼望。

背棄你的人必蒙羞,

背叛你的人必像寫在塵土上的名字一樣消逝,

因為他們背棄了耶和華——活水的源泉。

14耶和華啊,

你醫治我,我必痊癒;

你拯救我,我必脫離危難,

因為你是我所讚美的。

15人們常譏諷我說:「耶和華說的那些事在哪裡?

怎麼還沒有實現呢?」

16但我並沒有逃避牧養你子民的工作,

也沒有求你降禍給他們。

你知道我說的每一句話。

17你是我患難中的避難所,

求你不要使我恐懼。

18願你使那些迫害我的人蒙羞,

不要使我蒙羞;

願你使他們驚慌,

不要使我驚慌。

求你使他們大禍臨頭,

徹底毀滅他們。

遵守安息日

19耶和華對我說:「你去站在猶大君王出入的城門前和耶路撒冷的各城門前, 20宣告,『從這些城門進出的猶大君王、百姓以及耶路撒冷的居民啊,你們都要聽耶和華的話。 21耶和華說,如果你們想保住性命,就要小心,不要在安息日帶貨物進耶路撒冷的城門, 22也不要從家中運出貨物,不要在安息日做任何工作。要按照我對你們祖先的吩咐守安息日為聖日。 23然而,他們卻不聽,毫不理會,頑固不化,不肯受教。

24「『耶和華說,你們要留心聽我的話,在安息日不可運貨物進耶路撒冷的城門,不可做任何工作,要守安息日為聖日。 25這樣,坐大衛寶座的君王及其官員必乘車騎馬和猶大人以及耶路撒冷的居民從城門出入。這城必永遠有人居住。 26人們必帶著燔祭、平安祭、素祭、乳香和感恩祭從猶大的城邑、耶路撒冷四周、便雅憫地區、丘陵、山區和南地去耶和華的殿。 27但如果你們不聽我的話,不守安息日為聖日,仍在安息日運貨物進耶路撒冷的城門,我必在各城門點起無法撲滅的大火,燒毀耶路撒冷的宮殿。』」