Wimbo 8 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wimbo 8:1-14

18:1 Mit 9:2; Wim 3:4Laiti ungelikuwa kwangu kama ndugu wa kiume,

ambaye aliyanyonya matiti ya mama yangu!

Kisha, kama ningekukuta huko nje,

ningelikubusu,

wala hakuna mtu yeyote angelinidharau.

2Ningelikuongoza na kukuleta

katika nyumba ya mama yangu,

yeye ambaye amenifundisha.

Ningelikupa divai iliyokolezwa unywe,

asali ya maua ya mikomamanga yangu.

38:3 Wim 2:6Mkono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu,

na mkono wake wa kuume unanikumbatia.

48:4 Wim 2:7; 3:5Binti za Yerusalemu, ninawaagiza:

msichochee wala kuamsha mapenzi

hata yatakapotaka yenyewe.

Shairi La Sita

Marafiki

58:5 Wim 3:4-6; Yn 17:14Ni nani huyu anayekuja kutoka nyikani

akimwegemea mpenzi wake?

Mpendwa

Nilikuamsha chini ya mtofaa,

huko mama yako alipotunga mimba yako,

huko yeye alipata utungu akakuzaa.

68:6 Wim 1:2; Hes 5:14; Hag 2:23; Isa 49:16Nitie kama muhuri moyoni mwako,

kama muhuri kwenye mkono wako;

kwa maana upendo una nguvu kama mauti,

wivu wake ni mkatili kama kuzimu.

Unachoma kama mwali wa moto,

kama mwali mkubwa wa moto wa Bwana hasa.

78:7 Mit 6:35Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo,

mito haiwezi kuugharikisha.

Kama mtu angelitoa mali yote ya nyumbani mwake

kwa ajili ya upendo,

angelidharauliwa kabisa.

Marafiki

8Tunaye dada mdogo,

matiti yake hayajakua bado.

Tutafanya nini kwa ajili ya dada yetu

wakati atakapokuja kuposwa?

9Kama yeye ni ukuta,

tutajenga minara ya fedha juu yake.

Na kama yeye ni mlango,

tutamzungushia mbao za mierezi.

Mpendwa

108:10 Kol 2:7; Eze 16:7Mimi ni ukuta,

nayo matiti yangu ni kama minara.

Ndivyo ambavyo nimekuwa machoni pake

kama yule anayeleta utoshelevu.

118:11 Mhu 2:4; Mt 21:33; Isa 7:23Solomoni alikuwa na shamba la mizabibu huko Baal-Hamoni;

alikodisha shamba lake la mizabibu kwa wapangaji.

Kila mmoja angeleta kwa ajili ya matunda yake

shekeli 1,0008:11 Shekeli 1,000 ni kama kilo 11.5. za fedha.

12Lakini shamba langu la mizabibu

ambalo ni langu mwenyewe

ni langu kutoa;

hizo shekeli 1,000 ni kwa ajili yako, ee Solomoni,

na shekeli mia mbili8:12 Shekeli 200 ni kama kilo 2.3. ni kwa ajili

ya wale wanaotunza matunda yake.

Mpenzi

138:13 Wim 2:14Wewe ukaaye bustanini

pamoja na marafiki mliohudhuria,

hebu nisikie sauti yako!

Mpendwa

148:14 Mit 5:19; Wim 2:8-17Njoo, mpenzi wangu,

uwe kama swala

au kama ayala kijana

juu ya milima iliyojaa vikolezo.

Het Boek

Hooglied 8:1-14

1Ach, was je maar een broer van mij, gezoogd door dezelfde moeder als ik. Als ik je dan buiten ontmoette, kon ik je zomaar kussen. Niemand zou dat vreemd vinden.

2Dan kon ik je gewoon naar mijn moeders huis brengen, naar het huis van haar die mij alles leerde. Ik zou je heerlijke wijn aanbieden, jonge wijn van mijn granaatappels.

3Mijn hoofd ligt op zijn linkerarm en met zijn rechterarm omarmt hij mij.

4Meisjes van Jeruzalem, ik zeg het jullie met nadruk! Waarom willen jullie vooruit lopen op de liefde en haar overhaasten als de tijd daarvoor nog niet is aangebroken?

5Wie komt daar uit de woestijn aanlopen, ondersteund door haar liefste?

Onder de appelboom heb ik je gewekt. Daar heeft je moeder je ontvangen, zij heeft jou gebaard.

6Houd mij dicht tegen je aan, ik wil altijd in jouw armen blijven. Want de liefde is zo sterk als de dood. De hartstocht laat niet meer los, net zo min als het dodenrijk dat doet. Het vuur van de hartstocht brandt met hete vlammen, door de Here ontstoken.

7Geen water kan die liefde doven, geen rivier kan de liefde wegspoelen. Zelfs als iemand al zijn bezittingen bood in ruil voor de liefde, zou hem dat niet baten. Met minachting zou hem de deur worden gewezen.

8Wij hebben een klein zusje, zij heeft zelfs nog geen borsten. Wat moeten wij doen als op een dag iemand om haar komt?

9Als zij zich in reinheid bewaart, zullen wij haar daarvoor prijzen. Maar als zij zich te gemakkelijk geeft, zullen wij dat verhinderen.

10Ik heb mijzelf in reinheid bewaard tot nu toe. Nu ben ik voor hem degene die zich volkomen geven wil.

11Salomo had in Baäl-Hamon een wijngaard. Hij liet die bewaken, omdat hij van grote waarde was.

12Mijn wijngaard is voor mijzelf alleen. Al uw overvloed laat ik u, Salomo.

13Mijn allerliefste, die in een lusthof woont, laat mij je stem horen. Mijn vrienden luisteren mee.

14Mijn liefste, kom snel naar mij toe. Doe als de gazelle of als een jong hert op bergen vol heerlijk struikgewas.