Warumi 5 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Warumi 5:1-21

Matokeo Ya Kuhesabiwa Haki

15:1 Rum 3:28; Isa 32:17; Yn 16:33Kwa hiyo, kwa kuwa tumekwisha kuhesabiwa haki kwa imani, tuna amani na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo, 25:2 Efe 2:18; 3:12; 1Kor 15:1; Ebr 3:5; Mt 5:12ambaye kwa kupitia kwake tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo ndani yake sasa tunasimama, nasi twafurahia katika tumaini letu la kushiriki utukufu wa Mungu. 35:3 Ebr 10:36; Yak 1:2-3; Ebr 3:6; 1Yn 3:2-3; Mdo 10:43Si hivyo tu, bali twafurahi pia katika mateso, kwa sababu tunajua kuwa mateso huleta saburi, 45:4 Yak 1:12nayo saburi huleta uthabiti wa moyo, na uthabiti wa moyo huleta tumaini, 55:5 Flp 1:20; Ebr 3:6; Yn 3:2, 3; Rum 5:8; Yn 3:16; Rum 8:39; Tit 3:3, 6wala tumaini halitukatishi tamaa, kwa sababu Mungu amekwisha kumimina pendo lake mioyoni mwetu kwa njia ya Roho Mtakatifu ambaye ametupatia.

65:6 Mk 1:15; Efe 1:10; Rum 4:25Kwa maana hata tulipokuwa dhaifu, wakati ulipowadia, Kristo alikufa kwa ajili yetu sisi wenye dhambi. 7Hakika, ni vigumu mtu yeyote kufa kwa ajili ya mwenye haki, ingawa inawezekana mtu akathubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema. 85:8 Yn 3:16; 1Yn 4:10Lakini Mungu anaudhihirisha upendo wake kwetu kwamba: Tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.

95:9 Rum 3:25; Kum 1:18Basi, kwa kuwa sasa tumehesabiwa haki kwa damu yake, si zaidi sana tutaokolewa kutoka ghadhabu ya Mungu kupitia kwake! 105:10 Rum 11:28; 1Kor 1:21; 2Kor 5:18, 19; Kol 1:20, 22; Ebr 7:25Kwa kuwa kama tulipokuwa adui wa Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kifo cha Mwanawe, si zaidi sana tukiisha kupatanishwa, tutaokolewa kwa uzima wake. 115:11 Rum 5:10; 2:17; 3:29, 30; Gal 4:9Lakini zaidi ya hayo, pia tunafurahi katika Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kupitia kwake tumepata upatanisho.

Adamu Alileta Kifo, Yesu Ameleta Uzima

125:12 Mwa 3:1-7; 1Kor 15:21, 22; Mwa 3:19; Rum 6:23Kwa hiyo kama vile dhambi ilivyoingia ulimwenguni kupitia kwa mtu mmoja, na kupitia dhambi hii mauti ikawafikia watu wote, kwa sababu wote wamefanya dhambi: 135:13 Rum 4:15kwa maana kabla sheria haijatolewa, dhambi ilikuwepo ulimwenguni. Lakini dhambi haihesabiwi wakati hakuna sheria. 145:14 1Kor 15:22, 45Hata hivyo, tangu wakati wa Adamu hadi wakati wa Mose, mauti ilitawala watu wote, hata wale ambao hawakutenda dhambi kwa kuvunja amri, kama alivyofanya Adamu, ambaye alikuwa mfano wa yule atakayekuja.

155:15 Mdo 15:11Lakini ile karama iliyotolewa haikuwa kama lile kosa. Kwa maana ikiwa watu wengi walikufa kwa sababu ya kosa la mtu mmoja, zaidi sana neema ya Mungu na ile karama iliyokuja kwa neema ya mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo, imezidi kuwa nyingi kwa ajili ya wengi. 16Tena, ile karama ya Mungu si kama matokeo ya ile dhambi. Hukumu ilikuja kwa njia ya mtu mmoja, ikaleta adhabu, bali karama ya neema ya Mungu ilikuja kwa njia ya makosa mengi, ikaleta kuhesabiwa haki. 17Kwa maana ikiwa kutokana na kosa la mtu mmoja, mauti ilitawala kupitia huyo mtu mmoja, zaidi sana wale wanaopokea wingi wa neema ya Mungu na karama yake ya kuhesabiwa haki, watatawala katika uzima kwa njia ya huyo mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo.

185:18 Rum 4:25Kwa hiyo, kama vile kosa la mtu mmoja lilivyoleta adhabu kwa watu wote, vivyo hivyo pia kwa tendo la haki la mtu mmoja lilileta kuhesabiwa haki ambako huleta uzima kwa wote. 195:19 Flp 2:8Kwa maana kama vile kwa kutokutii kwa yule mtu mmoja wengi walifanywa wenye dhambi, vivyo hivyo kwa kutii kwa mtu mmoja wengi watafanywa wenye haki.

205:20 Rum 3:20; Gal 3:19; Rum 6:1; 1Tim 1:13, 14Zaidi ya hayo, sheria ilikuja, ili uvunjaji wa sheria uongezeke. Lakini dhambi ilipoongezeka, neema iliongezeka zaidi, 215:21 Rum 6:16ili kwamba kama vile dhambi ilivyotawala kwa njia ya mauti, vivyo hivyo neema iweze kutawala kwa njia ya kuhesabiwa haki hata kuleta uzima wa milele katika Yesu Kristo Bwana wetu.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

羅馬書 5:1-21

與上帝和好

1我們既然因信而被稱為義人,就藉著我們的主耶穌基督與上帝和好了。 2我們又靠著祂,藉著信進入現在所站的這恩典中,歡歡喜喜地盼望分享上帝的榮耀。 3不但如此,我們在苦難中也歡喜,因為知道苦難使人生忍耐, 4忍耐生品格,品格生盼望。 5這種盼望不會落空,因為上帝的愛藉著所賜給我們的聖靈已傾注在我們心中。

6當我們還軟弱無助的時候,基督就在所定的日期為罪人死了。 7為義人死,是罕見的;為好人死,也許有敢做的; 8但基督卻在我們還做罪人的時候為我們死!上帝的愛就這樣顯明了。

9現在,我們既然因祂所流的血而被稱為義人,豈不更要靠著祂免受上帝的烈怒嗎? 10如果我們還與上帝爲敵的時候,尚且可以藉著上帝兒子的死亡與上帝和好,和好後的我們豈不更要藉著祂兒子的生命得到拯救嗎? 11不但如此,我們藉著主耶穌基督與上帝和好之後,還要藉著祂在上帝面前歡喜。

亞當與基督

12因此,罪怎樣從一個人進入世界並帶來了死亡,死亡也怎樣臨到了全人類,因為全人類都犯了罪。 13沒有律法之前,罪已經在世上了;但沒有律法,罪也不算為罪。 14事實上,從亞當摩西的時代,死亡一直辖制著人類,甚至連那些不與亞當犯同樣罪的人也不能倖免。亞當是將要來的那位的預表。

15然而,上帝的洪恩遠超過亞當的過犯。若因一人的過犯,眾人都要死亡,那麼上帝的恩典,也就是通過耶穌基督一人所賜的恩典,豈不要更豐富地臨到眾人嗎? 16再者,上帝的恩賜不同於一人犯罪的後果。一人犯罪便帶來審判和定罪,恩賜卻使眾人罪惡得赦、被稱為義人。 17如果因一人的過犯,死亡就藉著那人作了王,那麼接受上帝洪恩又得到祂所賜之義的人,豈不更要藉著耶穌基督一人在生命中作王嗎?

18如此說來,因為一人的過犯,眾人都被定罪;照樣,因為一人的義行,眾人都被稱為義人,得到生命。 19因為一人的悖逆,眾人成為罪人;照樣,因為一人的順服,眾人將被稱為義人。 20律法是後來頒佈的,使過犯更多地顯出來,只是哪裡的罪越多,哪裡的恩典就顯得越豐富。 21罪怎樣掌權帶來死亡5·21 罪怎樣掌權帶來死亡」或譯「罪怎樣藉著死亡掌權」。,恩典也照樣藉著義掌權,為要藉著我們主耶穌基督帶來永生。