Warumi 11 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Warumi 11:1-36

Mabaki Ya Israeli

111:1 Law 26:46; Za 94:14; 2Kor 11:22; Flp 3:5Basi nauliza: Je, Mungu amewakataa watu wake? La, hasha! Mimi mwenyewe ni Mwisraeli, tena uzao wa Abrahamu kutoka kabila la Benyamini. 211:2 Rum 8:29; 11:1; 1Fal 19:10, 14Mungu hajawakataa watu wake, ambao yeye aliwajua tangu mwanzo. Je, hamjui yale Maandiko yasemayo kuhusu Eliya, jinsi alivyomlalamikia Mungu kuhusu Israeli? 311:3 1Fal 19:10, 14Alisema, “Bwana, wamewaua manabii wako na kuzibomoa madhabahu zako, nimebaki mimi peke yangu, nao wanataka kuniua?” 411:4 1Fal 19:18Je, Mungu alimjibuje? “Nimejibakizia watu elfu saba ambao hawajapiga magoti kumwabudu Baali.” 511:5 Rum 9:27; 3:24Vivyo hivyo pia, sasa wapo mabaki waliochaguliwa kwa neema ya Mungu. 611:6 Rum 4:4; Gal 3:18Lakini ikiwa wamechaguliwa kwa neema, si tena kwa msingi wa matendo. Kama ingekuwa kwa matendo, neema isingekuwa neema tena.

711:7 Rum 9:31; 9:18Tuseme nini basi? Kile kitu ambacho Israeli alikitafuta kwa bidii hakukipata. Lakini waliochaguliwa walikipata. Waliobaki walifanywa wagumu, 811:8 Mt 13:13-15; Kum 29:4; Isa 29:10kama ilivyoandikwa:

“Mungu aliwapa bumbuazi la mioyo,

macho ili wasiweze kuona,

na masikio ili wasiweze kusikia,

hadi leo.”

911:9 Za 69:22, 23; 35:8Naye Daudi anasema:

“Karamu zao na ziwe tanzi na mtego wa kuwanasa,

kitu cha kuwakwaza waanguke, na adhabu kwao.

1011:10 Za 69:22, 23; Rum 11:8Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona,

nayo migongo yao iinamishwe daima.”

Matawi Yaliyopandikizwa

1111:11 Mdo 13:46; Rum 10:19; 11:1Hivyo nauliza tena: Je, Waisraeli walijikwaa ili waanguke na kuangamia kabisa? La, hasha! Lakini kwa sababu ya makosa yao, wokovu umewafikia watu wa Mataifa, ili kuwafanya Waisraeli waone wivu. 1211:12 Rum 11:25Basi ikiwa kukosa kwao kumekuwa utajiri mkubwa kwa ulimwengu, tena kama kuangamia kwao kumeleta utajiri kwa watu wa Mataifa, kurudishwa kwao kutaleta utajiri mkuu zaidi.

1311:13 Mdo 9:15Sasa ninasema nanyi watu wa Mataifa. Maadamu mimi ni mtume kwa watu wa Mataifa, naitukuza huduma yangu 1411:14 1Kor 10:33; 1The 2:16; Mt 1:21; Lk 2:11ili kuwafanya watu wangu waone wivu na hivyo kuwaokoa baadhi yao. 1511:15 Rum 5:10; Lk 15:24, 32Kwa kuwa ikiwa kukataliwa kwao ni kupatanishwa kwa ulimwengu, kukubaliwa kwao si kutakuwa ni uhai baada ya kufa? 1611:16 Law 23:10, 17; Hes 15:18-21Kama sehemu ya donge la unga uliotolewa kuwa limbuko ni mtakatifu, basi unga wote ni mtakatifu, nalo shina kama ni takatifu, vivyo hivyo na matawi nayo.

1711:17 Yer 11:16; Yn 15:2; Mdo 2:39; Efe 2:11-13Lakini kama baadhi ya matawi yalikatwa, nawe chipukizi la mzeituni mwitu ukapandikizwa mahali pao ili kushiriki unono pamoja na matawi mengine kutoka shina la mzeituni, 1811:18 Yn 4:22; 1Kor 10:12basi usijivune juu ya hayo matawi. Kama ukijivuna, kumbuka jambo hili: si wewe unayelishikilia shina, bali ni shina linalokushikilia wewe. 19Basi utasema, “Matawi yale yalikatwa ili nipate kupandikizwa katika hilo shina.” 2011:20 1Kor 10:12; 2Kor 1:24; Rum 12:16; 1Tim 6:17; 1Pet 1:17Hii ni kweli. Matawi hayo yalikatwa kwa sababu ya kutokuamini kwake, lakini wewe umesimama tu kwa sababu ya imani. Kwa hiyo usijivune, bali simama kwa kuogopa. 21Kwa maana kama Mungu hakuyahurumia matawi ya asili, wala hatakuhurumia wewe.

2211:22 Rum 2:4; Ebr 3:6; Yn 15:2Angalia basi wema na ukali wa Mungu: Kwa wale walioanguka, ukali, bali kwako wewe wema wa Mungu, kama utadumu katika wema wake. La sivyo, nawe utakatiliwa mbali. 2311:23 2Kor 3:16Wao nao wasipodumu katika kutokuamini kwao, watapandikizwa tena kwenye shina, kwa maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena kwenye hilo shina. 2411:24 Yer 11:16Ikiwa wewe ulikatwa kutoka kile ambacho kwa asili ni mzeituni mwitu na kupandikizwa kinyume cha asili kwenye mzeituni uliopandwa, si rahisi zaidi matawi haya ya asili kupandikizwa tena kwenye shina lake la mzeituni!

Israeli Wote Wataokolewa

2511:25 Rum 1:13; 1Kor 10:1; 12:1; 2Kor 1:8; 1The 4:13; Rum 12:16; Lk 21:24Ndugu zangu, ili msije mkajidai kuwa wenye hekima kuliko mlivyo, nataka mfahamu siri hii: Ugumu umewapata Israeli kwa sehemu hadi idadi ya watu wa Mataifa watakaoingia itimie. 2611:26 Isa 45:17; Yer 31:34Hivyo Israeli wote wataokolewa. Kama ilivyoandikwa:

“Mkombozi atakuja kutoka Sayuni;

ataondoa kutokumcha Mungu katika Yakobo.

2711:27 Isa 59:20, 21; 27; 9; Ebr 8:10, 12Hili ndilo agano langu nao

nitakapoziondoa dhambi zao.”

2811:28 Rum 5:10; Kum 7:8; 10:15; Rum 9:5Kwa habari ya Injili, wao ni adui wa Mungu kwa ajili yenu, lakini kuhusu kule kuteuliwa kwao ni wapendwa, kwa ajili ya mababa zao wa zamani, 2911:29 Rum 8:28; Ebr 7:21kwa maana akishawapa watu karama, Mungu haziondoi, wala wito wake. 3011:30 Efe 2:2; Kol 3:7Kama vile ninyi wakati fulani mlivyokuwa waasi kwa Mungu lakini sasa mmepata rehema kwa sababu ya kutokutii kwao, 31hivyo nao Waisraeli wamekuwa waasi ili kwamba wao nao sasa waweze kupata rehema kwa ajili ya rehema za Mungu kwenu. 3211:32 Rum 3:9; Gal 3:22; 1Tim 2:4Kwa maana Mungu amewafunga wanadamu wote kwenye kuasi ili apate kuwarehemu wote.

Wimbo Wa Shukrani

3311:33 Rum 2:4; Mhu 8:17; Efe 3:10; Kol 2:3; Za 92:5; 139:6; Isa 40:28Tazama jinsi kilivyo kina cha utajiri

wa hekima na maarifa ya Mungu!

Tazama jinsi ambavyo hukumu zake hazichunguziki,

na ambavyo njia zake zisivyotafutikana!

3411:34 Isa 40:13, 14; Ay 15:8; 36:22; Yer 23:18; 1Kor 2:16“Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana?

Au ni nani ambaye amekuwa mshauri wake?”

3511:35 Ay 41:11; 35:7“Au ni nani aliyempa chochote

ili arudishiwe?”

3611:36 1Kor 8:6; 11:12; Kol 1:16; 1Pet 5:11; 1Tim 1:17; Ebr 2:10; Efe 3:21; Rum 16:27; Yud 25; Ufu 5:13Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, viko kwake na kwa ajili yake.

Utukufu ni wake milele! Amen.

New International Reader’s Version

Romans 11:1-36

The Israelites Who Are Faithful

1So here is what I ask. Did God turn his back on his people? Not at all! I myself belong to Israel. I am one of Abraham’s children. I am from the tribe of Benjamin. 2God didn’t turn his back on his people. After all, he chose them. Don’t you know what Scripture says about Elijah? He complained to God about Israel. 3He said, “Lord, they have killed your prophets. They have torn down your altars. I’m the only one left. And they are trying to kill me.” (1 Kings 19:10,14) 4How did God answer him? God said, “I have kept 7,000 people for myself. They have not bowed down to Baal.” (1 Kings 19:18) 5Some are also faithful today. They have been chosen by God’s grace. 6And if they are chosen by grace, then they can’t work for it. If that were true, grace wouldn’t be grace anymore.

7What should we say then? The people of Israel did not receive what they wanted so badly. Those Israelites who were chosen did receive it. But the rest of the people were made stubborn. 8It is written,

“God made it hard for them to understand.

He gave them eyes that could not see.

He gave them ears that could not hear.

And they are still like that today.” (Deuteronomy 29:4; Isaiah 29:10)

9David says,

“Let their feast be a trap and a snare.

Let them trip and fall. Let them get what’s coming to them.

10Let their eyes grow dark so they can’t see.

Let their backs be bent forever.” (Psalm 69:22,23)

Two Kinds of Olive Branches

11Again, here is what I ask. The Israelites didn’t trip and fall once and for all time, did they? Not at all! Because Israel sinned, the Gentiles can be saved. That will make Israel jealous of them. 12Israel’s sin brought riches to the world. Their loss brings riches to the Gentiles. So then what greater riches will come when all Israel turns to God!

13I am talking to you who are not Jews. I am the apostle to the Gentiles. So I take pride in the work I do for God and others. 14I hope somehow to stir up my own people to want what you have. Perhaps I can save some of them. 15When they were not accepted, it became possible for the whole world to be brought back to God. So what will happen when they are accepted? It will be like life from the dead. 16The first handful of dough that is offered is holy. This makes all of the dough holy. If the root is holy, so are the branches.

17Some of the natural branches have been broken off. You are a wild olive branch. But you have been joined to the tree with the other branches. Now you enjoy the life-giving sap of the olive tree root. 18So don’t think you are better than the other branches. Remember, you don’t give life to the root. The root gives life to you. 19You will say, “Some branches were broken off so that I could be joined to the tree.” 20That’s true. But they were broken off because they didn’t believe. You stand only because you do believe. So don’t be proud, but tremble. 21God didn’t spare the natural branches. He won’t spare you either.

22Think about how kind God is! Also think about how firm he is! He was hard on those who stopped following him. But he is kind to you. So you must continue to live in his kindness. If you don’t, you also will be cut off. 23If the people of Israel do not continue in their unbelief, they will again be joined to the tree. God is able to join them to the tree again. 24After all, weren’t you cut from a wild olive tree? Weren’t you joined to an olive tree that was taken care of? And wasn’t that the opposite of how things should be done? How much more easily will the natural branches be joined to their own olive tree!

All Israel Will Be Saved

25Brothers and sisters, here is a mystery I want you to understand. It will keep you from being proud. Part of Israel has refused to obey God. That will continue until the full number of Gentiles has entered God’s kingdom. 26In this way all Israel will be saved. It is written,

“The God who saves will come from Mount Zion.

He will remove sin from Jacob’s family.

27Here is my covenant with them.

I will take away their sins.” (Isaiah 59:20,21; 27:9; Jeremiah 31:33,34)

28As far as the good news is concerned, the people of Israel are enemies. This is for your good. But as far as God’s choice is concerned, the people of Israel are loved. This is because of God’s promises to the founders of our nation. 29God does not take back his gifts. He does not change his mind about those he has chosen. 30At one time you did not obey God. But now you have received mercy because Israel did not obey. 31In the same way, Israel has not been obeying God. But now they receive mercy because of God’s mercy to you. 32God has found everyone guilty of not obeying him. So now he can have mercy on everyone.

Praise to God

33How very rich are God’s wisdom and knowledge!

How he judges is more than we can understand!

The way he deals with people is more than we can know!

34“Who can ever know what the Lord is thinking?

Or who can ever give him advice?” (Isaiah 40:13)

35“Has anyone ever given anything to God,

so that God has to pay them back?” (Job 41:11)

36All things come from him.

All things are directed by him.

All things are for his praise.

May God be given the glory forever! Amen.