Walawi 25 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 25:1-55

Mwaka Wa Sabato

(Kumbukumbu 15:1-11)

125:1 Kut 19:11Bwana akamwambia Mose katika Mlima Sinai, 225:2 Kut 23:10; Law 26:34-35; 2Nya 36:21“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapa ninyi, nchi yenyewe ni lazima ishike Sabato kwa ajili ya Bwana. 325:3 Kut 23:10; 25:4Kwa miaka sita mtapanda mazao katika mashamba yenu, nanyi kwa miaka sita mtaikata mizabibu yenu matawi na kuvuna mazao yake. 425:4 Law 26:35; 2Nya 36:21; Isa 36:16; 37:30Lakini mwaka wa saba nchi lazima iwe na Sabato ya mapumziko, Sabato kwa Bwana. Msipande mbegu katika mashamba yenu, wala msikate mizabibu yenu matawi. 525:5 2Fal 19:29; Mwa 40:10; Hes 6:3; 13:20; Kum 23:24; Neh 13:15; Isa 5:2; 37:30Msivune na kuweka akiba kinachoota chenyewe, wala kuvuna na kusindika zabibu ambayo hamkuhudumia mashamba yake. Nchi lazima iwe na mwaka wa mapumziko. 6Chochote nchi itoacho katika mwaka wa Sabato kitakuwa chakula chenu wenyewe, watumishi wenu wa kiume na wa kike, mfanyakazi aliyeajiriwa, na mkazi wa muda anayeishi miongoni mwenu, 725:7 Kut 23:11vilevile malisho ya mifugo yenu na wanyama pori katika nchi yenu. Chochote nchi itakachozalisha kinaweza kuliwa.

Mwaka Wa Yubile

8“ ‘Hesabu Sabato saba za miaka, yaani miaka saba mara saba, ili Sabato saba za miaka utakuwa muda wa miaka arobaini na tisa. 925:9 Law 16:29; 23:24; Hes 10:8; Yos 6:4; Amu 3:27; 7:16; 1Sam 13:3; Isa 27:13; Zek 9:14; Kut 30:10Ndipo tarumbeta itapigwa kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho, piga tarumbeta katika nchi yako yote. 1025:10 Isa 61:1; Yer 34:8, 15, 17; Lk 4:19; Law 27:17, 21; Hes 36:4; Eze 46:17; Kut 20:2; Ezr 6:3; Gal 5:1Mwaka wa hamsini mtauweka wakfu na kutangaza uhuru katika nchi kwa wakazi wake wote. Itakuwa ni yubile25:10 Yubile ni baragumu iliopigwa kila mwaka wa hamsini; ni Sabato ya nchi ya kila mwaka wa hamsini uliokuwa mwaka wa ukombozi, yaani kuachia huru. kwenu; kila mmoja wenu atairudia mali ya jamaa yake, na kila mmoja kurudi kwenye ukoo wake. 11Mwaka wa hamsini utakuwa yubile kwenu, msipande wala msivune kile kiotacho chenyewe, au kuvuna zabibu zisizohudumiwa. 12Kwa kuwa ni yubile, nayo itakuwa takatifu kwenu; mtakula tu kile kilichotoka moja kwa moja mashambani.

13“ ‘Katika huu Mwaka wa Yubile, kila mmoja atarudi kwenye mali yake mwenyewe.

1425:14 Law 19:13; 1Sam 12:3-4; 1Kor 6:8; Za 10:18; Mik 2:2“ ‘Ikiwa utauza ardhi kwa mmoja wa wazawa wa nchi yako, au ukinunua ardhi kutoka kwake, mmoja asimpunje mwingine. 1525:15 Law 27:18, 23Utanunua ardhi kwa mzawa wa nchi yako kwa misingi ya hesabu ya miaka baada ya Yubile. Naye ataiuza kwako kwa misingi ya hesabu ya miaka iliyobaki kwa kuvuna mavuno. 16Miaka inapokuwa mingi, utaongeza bei, nayo miaka ikiwa michache, utapunguza bei, kwa sababu kile anachokuuzia kwa hakika ni hesabu ya mazao. 1725:17 Law 19:13, 14, 32; Ay 31:16; Mit 22:22; Yer 7:5-6; 21:12; 22:3; Zek 7:9-10; 1The 4:6; Mit 14:31; Eze 22:29Mmoja asimpunje mwingine, bali utamcha Mungu wako. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.

1825:18 Mwa 26:5; Law 26:4-5; Kum 12:10; 33:28; Ay 5:22; Za 4:8; Yer 23:6; 30:10; 32:37; 33:16; Eze 28:26; 34:25; 38:14“ ‘Fuateni amri zangu, mwe waangalifu kutii amri zangu, nanyi mtaishi salama katika nchi. 1925:19 Law 26:4; Kum 11:14; 28:12; Isa 55:10; Mt 6:25; Hes 11:4-13; 2Fal 6:15Kisha nchi itazaa matunda yake, nanyi mtakula na kushiba na kuishi humo kwa salama. 20Mwaweza kuuliza, “Tutakula nini katika mwaka wa saba ikiwa hatutapanda wala kuvuna mazao yetu?” 2125:21 Kum 28:8-12; Za 133:3; 134:3; 147:13; Eze 44:30; Hag 2:19; Mal 3:10; Kut 16:5Nitawapelekeeni baraka ya pekee katika mwaka wa sita, kwamba nchi itazalisha mazao ya kutosha kwa miaka mitatu. 2225:22 Law 26:10; 2Fal 19:29; Yos 5:11Mnapopanda mwaka wa nane, mtakula mavuno ya miaka iliyopita. Pia mtaendelea kuyala mazao hayo hadi mvune mavuno ya mwaka wa tisa.

2325:23 Hes 36:7; 1Fal 21:3; Eze 46:18; Kut 19:5; Mwa 23:4; Ebr 11:13“ ‘Kamwe ardhi isiuzwe kwa mkataba wa kudumu, kwa sababu nchi ni mali yangu, nanyi ni wageni na wapangaji wangu. 2425:24 Rut 4:7; Yer 32:8Katika nchi yote mtakayoshika kuwa milki yenu, ni lazima mtoe ukombozi wa ardhi.

2525:25 Rut 2:20; 4:4; Yer 32:7; Law 27:13-31“ ‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini na akauza baadhi ya mali yake, ndugu yake wa karibu atakuja na kukomboa kile ndugu yako alichokiuza. 26Iwapo mtu huyo hana jamaa wa karibu wa kukomboa mali hiyo kwa ajili yake, lakini yeye mwenyewe akafanikiwa na kupata mali itoshayo kuikomboa, 27ataamua tena thamani yake kwa miaka tangu alipoiuza, na kurudisha kiasi kilichobaki cha thamani kwa mtu ambaye alikuwa amemuuzia mali hiyo, naye ataweza kuirudia mali yake. 28Lakini kama hatapata njia ya kumlipa mnunuzi, ile mali aliyouza itabaki kumilikiwa na mnunuzi mpaka Mwaka wa Yubile. Mali hiyo itarudishwa mwaka wa Yubile, naye ataweza kuirudia mali yake.

29“ ‘Ikiwa mtu atauza nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta, yeye anayo haki ya kuikomboa mwaka mzima baada ya mauzo ya hiyo nyumba. Wakati huo anaweza kuikomboa. 30Ikiwa haikukombolewa kabla ya mwaka mmoja kamili kupita, nyumba iliyo ndani ya mji uliozungukwa kwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya mnunuzi na wazao wake. Haitarudishwa mwaka wa Yubile. 31Lakini nyumba zilizo vijijini bila ya kuwa na kuta zilizozizunguka zitahesabiwa kama mashamba. Zinaweza kukombolewa, nazo zirudishwe katika mwaka wa Yubile.

3225:32 Hes 35:1-8; Yos 21:2“ ‘Walawi siku zote wana haki ya kukomboa nyumba zao katika miji ya Walawi wanayoimiliki. 33Kwa hiyo mali ya Mlawi inaweza kukombolewa, yaani nyumba iliyouzwa katika mji wowote wanaoushikilia itarudishwa mwaka wa Yubile, kwa sababu nyumba zilizo katika miji ya Walawi ni mali yao miongoni mwa Waisraeli. 3425:34 Hes 35:2-5; Eze 48:14; Mdo 4:36Lakini nchi ya malisho iliyo mali ya miji yao kamwe isiuzwe, ni milki yao ya kudumu.

3525:35 Kum 24:14-15; 15:8; Za 37:21-26; Mit 21:26; Lk 6:35; Mdo 11:29; Rum 12:18; 1Yn 3:17; Kum 15:7“ ‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini, naye akashindwa kujitegemeza mwenyewe katikati yako, msaidie kama vile ambavyo ungelimsaidia mgeni au kama mkazi wa muda, ili aweze kuendelea kuishi katikati yako. 3625:36 Kut 22:25; Yer 15:10; Law 19:32; Kum 23:19; Neh 5:7; Za 15:5; Mit 28:8; Eze 18:8Usichukue riba wala faida yoyote kutoka kwake, bali utamwogopa Mungu wako, ili mzawa wa nchi yako aweze kuendelea kuishi katikati yako. 3725:37 Kut 22:25Usimkopeshe fedha ili alipe na riba, wala usimuuzie chakula kwa faida. 3825:38 Mwa 10:19; 17:7; Law 11:45Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekuleta kutoka nchi ya Misri nikupe nchi ya Kanaani, nami niwe Mungu wako.

3925:39 1Fal 5:13; 9:23; Yer 34:14; Kut 21:2; 22:3; Kum 15:12“ ‘Ikiwa mmoja wa wazawa wa nchi yako amekuwa maskini katikati yako, naye akajiuza kwako, usimfanye atumike kama mtumwa. 40Atatendewa kama mfanyakazi aliyeajiriwa, au kama mkazi wa muda katikati yako, naye atatumika mpaka Mwaka wa Yubile. 41Ndipo yeye na watoto wake wataachiwa, naye atarudi kwa watu wa ukoo wake, na kwenye mali ya baba zake. 4225:42 Rum 6:22; 1Kor 7:23Kwa sababu Waisraeli ni watumishi wangu niliowaleta kutoka nchi ya Misri, kamwe wasiuzwe kama watumwa. 4325:43 Kut 1:13; Eze 34:4; Kol 4:1; Mwa 42:18; Isa 47:6; Efe 6:9; Kum 25:18; Mal 3:5Usiwatawale kwa ukatili, lakini utamcha Mungu wako.

44“ ‘Watumwa wako wa kiume na wa kike watatoka katika mataifa yanayokuzunguka; kutoka kwao waweza kununua watumwa. 45Pia waweza kununua baadhi ya wakazi wa muda wanaoishi katikati yako, na jamaa ya koo zao waliozaliwa katika nchi yako, nao watakuwa mali yako. 46Hao waweza kuwarithisha watoto wako kuwa urithi wao, na wanaweza kuwafanya watumwa maisha yao yote, lakini usiwatawale ndugu zako Waisraeli kwa ukatili.

4725:47 Neh 5:5; Ay 24:9“ ‘Ikiwa mgeni au mkazi wa muda katikati yako atakuwa tajiri, na mmoja wa wazawa wa nchi yako akawa maskini, naye akajiuza kwa yule mgeni anayeishi katikati yako, au kwa mmoja wa jamaa wa koo za wageni, 48anayo haki ya kukombolewa baada ya kujiuza. Mmoja wa jamaa zake aweza kumkomboa: 49Mjomba wake, au binamu yake, au yeyote aliye ndugu wa damu katika ukoo wake aweza kumkomboa. Au ikiwa atafanikiwa, anaweza kujikomboa mwenyewe. 5025:50 Ay 7:1; 14:6; Isa 16:14; 21:16Yeye na huyo aliyemnunua watahesabu muda kuanzia mwaka aliojiuza hadi Mwaka wa Yubile. Mahali pa kuanzia bei ya kuachiwa kwake itakadiriwa kwa ujira unaolipwa mfanyakazi aliyeajiriwa kwa idadi ya hiyo miaka. 51Ikiwa imebaki miaka mingi, ni lazima atalipia ukombozi wake fungu kubwa la bei iliyolipwa kumnunua yeye. 52Ikiwa miaka iliyobaki ni michache kufikia Mwaka wa Yubile, atafanya hesabu yake, naye atalipa malipo yanayostahili kwa ajili ya ukombozi wake. 5325:53 Kol 4:1Atatendewa kama mtu wa kuajiriwa mwaka hadi mwaka; lazima uone kwamba yule aliyemnunua hamtawali kwa ukatili.

54“ ‘Hata ikiwa hakukombolewa kwa njia mojawapo ya hizi, yeye na watoto wake wataachiwa katika Mwaka wa Yubile, 5525:55 Law 11:44-45kwa maana Waisraeli ni mali yangu kama watumishi. Wao ni watumishi wangu, niliowatoa kutoka nchi ya Misri. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.

King James Version

Leviticus 25:1-55

1And the LORD spake unto Moses in mount Sinai, saying, 2Speak unto the children of Israel, and say unto them, When ye come into the land which I give you, then shall the land keep a sabbath unto the LORD.25.2 keep: Heb. rest 3Six years thou shalt sow thy field, and six years thou shalt prune thy vineyard, and gather in the fruit thereof; 4But in the seventh year shall be a sabbath of rest unto the land, a sabbath for the LORD: thou shalt neither sow thy field, nor prune thy vineyard. 5That which groweth of its own accord of thy harvest thou shalt not reap, neither gather the grapes of thy vine undressed: for it is a year of rest unto the land.25.5 of thy vine…: Heb. of thy separation 6And the sabbath of the land shall be meat for you; for thee, and for thy servant, and for thy maid, and for thy hired servant, and for thy stranger that sojourneth with thee, 7And for thy cattle, and for the beast that are in thy land, shall all the increase thereof be meat.

8¶ And thou shalt number seven sabbaths of years unto thee, seven times seven years; and the space of the seven sabbaths of years shall be unto thee forty and nine years. 9Then shalt thou cause the trumpet of the jubile to sound on the tenth day of the seventh month, in the day of atonement shall ye make the trumpet sound throughout all your land.25.9 of the jubile: Heb. loud of sound 10And ye shall hallow the fiftieth year, and proclaim liberty throughout all the land unto all the inhabitants thereof: it shall be a jubile unto you; and ye shall return every man unto his possession, and ye shall return every man unto his family. 11A jubile shall that fiftieth year be unto you: ye shall not sow, neither reap that which groweth of itself in it, nor gather the grapes in it of thy vine undressed. 12For it is the jubile; it shall be holy unto you: ye shall eat the increase thereof out of the field. 13In the year of this jubile ye shall return every man unto his possession. 14And if thou sell ought unto thy neighbour, or buyest ought of thy neighbour’s hand, ye shall not oppress one another: 15According to the number of years after the jubile thou shalt buy of thy neighbour, and according unto the number of years of the fruits he shall sell unto thee: 16According to the multitude of years thou shalt increase the price thereof, and according to the fewness of years thou shalt diminish the price of it: for according to the number of the years of the fruits doth he sell unto thee. 17Ye shall not therefore oppress one another; but thou shalt fear thy God: for I am the LORD your God.

18¶ Wherefore ye shall do my statutes, and keep my judgments, and do them; and ye shall dwell in the land in safety. 19And the land shall yield her fruit, and ye shall eat your fill, and dwell therein in safety. 20And if ye shall say, What shall we eat the seventh year? behold, we shall not sow, nor gather in our increase: 21Then I will command my blessing upon you in the sixth year, and it shall bring forth fruit for three years. 22And ye shall sow the eighth year, and eat yet of old fruit until the ninth year; until her fruits come in ye shall eat of the old store.

23¶ The land shall not be sold for ever: for the land is mine; for ye are strangers and sojourners with me.25.23 for ever: or, to be quite cut off: Heb. for cutting off 24And in all the land of your possession ye shall grant a redemption for the land.

25¶ If thy brother be waxen poor, and hath sold away some of his possession, and if any of his kin come to redeem it, then shall he redeem that which his brother sold. 26And if the man have none to redeem it, and himself be able to redeem it;25.26 himself…: Heb. his hand hath attained and found sufficiency 27Then let him count the years of the sale thereof, and restore the overplus unto the man to whom he sold it; that he may return unto his possession. 28But if he be not able to restore it to him, then that which is sold shall remain in the hand of him that hath bought it until the year of jubile: and in the jubile it shall go out, and he shall return unto his possession. 29And if a man sell a dwelling house in a walled city, then he may redeem it within a whole year after it is sold; within a full year may he redeem it. 30And if it be not redeemed within the space of a full year, then the house that is in the walled city shall be established for ever to him that bought it throughout his generations: it shall not go out in the jubile. 31But the houses of the villages which have no wall round about them shall be counted as the fields of the country: they may be redeemed, and they shall go out in the jubile.25.31 they may…: Heb. redemption belongeth unto it 32Notwithstanding the cities of the Levites, and the houses of the cities of their possession, may the Levites redeem at any time. 33And if a man purchase of the Levites, then the house that was sold, and the city of his possession, shall go out in the year of jubile: for the houses of the cities of the Levites are their possession among the children of Israel.25.33 a man…: or, one of the Levites redeem them 34But the field of the suburbs of their cities may not be sold; for it is their perpetual possession.

35¶ And if thy brother be waxen poor, and fallen in decay with thee; then thou shalt relieve him: yea, though he be a stranger, or a sojourner; that he may live with thee.25.35 fallen…: Heb. his hand faileth25.35 relieve: Heb. strengthen 36Take thou no usury of him, or increase: but fear thy God; that thy brother may live with thee. 37Thou shalt not give him thy money upon usury, nor lend him thy victuals for increase. 38I am the LORD your God, which brought you forth out of the land of Egypt, to give you the land of Canaan, and to be your God.

39¶ And if thy brother that dwelleth by thee be waxen poor, and be sold unto thee; thou shalt not compel him to serve as a bondservant:25.39 compel…: Heb. serve thyself with him with the service, etc 40But as an hired servant, and as a sojourner, he shall be with thee, and shall serve thee unto the year of jubile: 41And then shall he depart from thee, both he and his children with him, and shall return unto his own family, and unto the possession of his fathers shall he return. 42For they are my servants, which I brought forth out of the land of Egypt: they shall not be sold as bondmen.25.42 as…: Heb. with the sale of a bondman 43Thou shalt not rule over him with rigour; but shalt fear thy God. 44Both thy bondmen, and thy bondmaids, which thou shalt have, shall be of the heathen that are round about you; of them shall ye buy bondmen and bondmaids. 45Moreover of the children of the strangers that do sojourn among you, of them shall ye buy, and of their families that are with you, which they begat in your land: and they shall be your possession. 46And ye shall take them as an inheritance for your children after you, to inherit them for a possession; they shall be your bondmen for ever: but over your brethren the children of Israel, ye shall not rule one over another with rigour.25.46 they…: Heb. ye shall serve yourselves with them

47¶ And if a sojourner or stranger wax rich by thee, and thy brother that dwelleth by him wax poor, and sell himself unto the stranger or sojourner by thee, or to the stock of the stranger’s family:25.47 wax rich…: Heb. his hand obtain, etc 48After that he is sold he may be redeemed again; one of his brethren may redeem him: 49Either his uncle, or his uncle’s son, may redeem him, or any that is nigh of kin unto him of his family may redeem him; or if he be able, he may redeem himself. 50And he shall reckon with him that bought him from the year that he was sold to him unto the year of jubile: and the price of his sale shall be according unto the number of years, according to the time of an hired servant shall it be with him. 51If there be yet many years behind, according unto them he shall give again the price of his redemption out of the money that he was bought for. 52And if there remain but few years unto the year of jubile, then he shall count with him, and according unto his years shall he give him again the price of his redemption. 53And as a yearly hired servant shall he be with him: and the other shall not rule with rigour over him in thy sight. 54And if he be not redeemed in these years, then he shall go out in the year of jubile, both he, and his children with him.25.54 in these…: or, by these means 55For unto me the children of Israel are servants; they are my servants whom I brought forth out of the land of Egypt: I am the LORD your God.