Walawi 18 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 18:1-30

Uhusiano Wa Kukutana Kimwili Kinyume Cha Sheria

1Bwana akamwambia Mose, 218:2 Mwa 17:7; Eze 20:5; Kut 6:7“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mimi ndimi Bwana Mungu wenu. 318:3 Kut 23:24; Kum 18:9; 2Fal 16:3; 17:8; 1Nya 5:25; Eze 23:8Msifanye kama wafanyavyo huko Misri, mahali mlipokuwa mnaishi, wala msifanye kama wanavyofanya katika nchi ya Kanaani, mahali ninapowapeleka. Msifuate matendo yao. 418:4 Mwa 26:5; Kum 4:1; 1Fal 11:11; Yer 44:10, 23; Eze 11:12Ni lazima mzitii sheria zangu, na mwe waangalifu kuzifuata amri zangu. Mimi ndimi Bwana Mungu wenu. 518:5 Mwa 26:5; Neh 9:20; Isa 55:2; Eze 18:9; 20:11; Amo 5:4-6; Mt 19:17; Rum 10:5; Gal 3:12Zishikeni amri zangu na sheria zangu, kwa maana mtu anayezitii ataishi kwa hizo. Mimi ndimi Bwana.

6“ ‘Hakuna mtu awaye yote atakayemsogelea ndugu wa karibu ili kukutana naye kimwili. Mimi ndimi Bwana.

718:7 Law 20:11; Kum 27:20; Eze 22:10-11“ ‘Usimvunjie heshima baba yako kwa kukutana kimwili na mama yako. Yeye ni mama yako; usiwe na mahusiano kama hayo naye.

818:8 1Kor 5:11; Mwa 35:22; Law 20:11; Kum 22:30; 27:20“ ‘Usikutane kimwili na mke wa baba yako; hiyo itamvunjia heshima baba yako.

918:9 Law 20:17; Kum 27:22; 2Sam 13:13; Eze 22:11“ ‘Usikutane kimwili na dada yako, wala binti wa baba yako, au binti wa mama yako, awe amezaliwa katika nyumba hiyo au mahali pengine.

10“ ‘Usikutane kimwili na binti wa mwanao ama binti wa binti yako; utajivunjia heshima.

11“ ‘Usikutane kimwili na binti wa mke wa baba yako, aliyezaliwa na baba yako; huyo ni dada yako.

1218:12 Law 20:19“ ‘Usikutane kimwili na dada wa baba yako; ni ndugu wa karibu wa baba yako.

1318:13 Law 20:20“ ‘Usikutane kimwili na dada wa mama yako, kwa sababu ni ndugu wa mama yako wa karibu.

14“ ‘Usimvunjie heshima ndugu wa baba yako, kwa kukutana kimwili na mke wake; yeye ni shangazi yako.

1518:15 Mwa 11:31; 38:16; Eze 22:11; Law 20:12“ ‘Usikutane kimwili na mkwe wako, yeye ni mke wa mwanao; usiwe na mahusiano kama hayo naye.

1618:16 Law 20:21; Mt 14:4; Mk 6:18“ ‘Usikutane kimwili na mke wa kaka yako; utamvunjia heshima kaka yako.

1718:17 Law 20:14; Kum 27:23“ ‘Usikutane kimwili na mwanamke kisha na binti yake. Usikutane kimwili na binti wa mwanawe au binti wa binti yake; hao ni ndugu zake wa karibu. Huo ni uovu.

1818:18 Mwa 30:1; Mal 2:15“ ‘Usimchukue dada wa mke wako kuwa mke mwenza, na kukutana naye kimwili wakati bado mke wako anaishi.

1918:19 Law 15:24-30; 20:18; Eze 18:6“ ‘Usimsogelee mwanamke ili kukutana naye kimwili wakati wa unajisi wa siku zake za mwezi.

2018:20 Kut 20:14; Mt 5:27-28; 1Kor 6:9; Ebr 13:4; Mit 6:29“ ‘Usikutane kimwili na mke wa jirani yako na kujitia naye unajisi.

2118:21 Kum 9:4; 12:31; 18:10; 2Fal 16:3; 17:17; 21:6; 23:10; 2Nya 28:1-4; 33:6; Za 106:37-38; Isa 48:11; 57:5; Yer 7:30-31; 19:5; 32:35; Eze 16:20; 22:26; 36:20; Mik 6:7; Law 19:12; 20:2-5; 21:6; Amo 2:7; 1Fal 11:5, 7, 33; Sef 1:5; Mal 1:12; Kut 6:2“ ‘Usimtoe mtoto wako yeyote awe kafara kwa mungu Moleki, kwani hutalinajisi kamwe jina la Mungu wako. Mimi ndimi Bwana.

2218:22 Law 20:13; Kum 23:18; Rum 1:27; 1Kor 6:9; Mwa 19:5“ ‘Usikutane kimwili na mwanaume kama mtu akutanaye na mwanamke; hilo ni chukizo.

2318:23 Kut 22:19; Law 20:15; Kum 27:21“ ‘Usikutane kimwili na mnyama na kujitia unajisi kwake. Mwanamke asijipeleke kwa mnyama ili kukutana naye kimwili; huo ni upotovu.

2418:24 Law 20:23; Kum 9:4; 18:12; Mt 15:18; 1Kor 3:17“ ‘Msijitie unajisi kwa njia yoyote katika hizi, kwa sababu hivi ndivyo mataifa nitakayoyafukuza mbele yenu yalivyojitia unajisi. 2518:25 Hes 35:34; Kum 9:5; 12:31; 18:12; 21:23; Law 20:23; Ay 20:15; Yer 51:34Hata nchi ilitiwa unajisi, hivyo nikaiadhibu kwa dhambi zake, nayo nchi ikawatapika wakazi wake. 2618:26 Mwa 26:5; 18:28; Law 20:22; Ezr 9:11; Mao 1:17Lakini ni lazima uzitunze amri zangu na sheria zangu. Mzawa na wageni waishio miongoni mwenu kamwe wasifanye mambo yoyote ya machukizo haya, 27kwa kuwa mambo haya yote yalifanywa na watu walioishi katika nchi hii kabla yenu, na nchi ikawa najisi. 28Kama mkiinajisi nchi, itawatapika kama ilivyowatapika mataifa yaliyowatangulia.

29“ ‘Kila mtu atakayefanya mojawapo ya machukizo haya, watu hao ni lazima wakatiliwe mbali na watu wao. 3018:30 Law 8:35; Kum 11:1; 19:2; Hes 14:5; Za 68:26; Kut 20:2; 15:11; 1Pet 1:16; Law 11:44; 20:26Shikeni maagizo yangu, wala msifuate desturi za machukizo yoyote yaliyofanywa kabla hamjafika katika nchi hii, na kujitia unajisi kwa hayo. Mimi ndimi Bwana Mungu wako.’ ”

Korean Living Bible

레위기 18:1-30

불법적인 성관계를 금함

1여호와께서 모세를 통하여 이스라엘 백성에게 말씀하셨다. “나는 여

2호와 너희 하나님이다.

3너희는 오랫동안 살았던 이집트 땅의 풍습을 좇지 말고 내가 너희를 인도할 가나안 땅의 풍습도 좇지 말아라.

4너희는 내 법에 순종하고 내가 명령한 것을 그대로 준수하라. 나는 너희 하나님 여호와이다.

5그러므로 너희는 나의 법과 규정을 지켜야 한다. 사람이 이것을 행하면 살 것이다. 나는 여호와이다.

6“너희는 가까운 친척과 성관계를 하지 말아라. 나는 여호와이다.

7너희 자녀들은 부모에게 절대로 부끄러운 짓을 해서는 안 된다.

8또 너희는 아버지의 첩에게 부끄러운 짓을 하지 말아라.

9너희는 친자매이든 의붓자매이든, 그들이 너희와 한집에서 태어났든지 다른 곳에서 태어났든지 일체 그들과 성관계를 해서는 안 된다.

10너희는 친손녀나 외손녀를 욕보이지 말아라. 그들은 가까운 친척이다.

11너희는 의붓누이와 성관계를 하지 말아라. 그녀도 역시 너희 자매이다.

12너희는 너희 고모에게 부끄러운 짓을 하지 말아라. 그녀는 너희 아버지와 가까운 친척이다.

13너희는 너희 이모에게 부끄러운 짓을 하지 말아라. 그녀는 너희 어머니와 가까운 친척이다.

14너희는 너희 아버지 형제의 아내를 가까이하여 부끄러운 짓을 하지 말아라. 그들은 너희 백모와 숙모이다.

15너희는 너희 며느리를 욕보이지 말아라. 그녀는 너희 아들의 아내이다.

16너희는 너희 형제의 아내와 성관계를 하지 말아라. 그들은 너희 형수와 제수이다.

17너희는 너희가 성관계를 가진 여인의 딸이나 손녀를 욕보이지 말아라. 그들은 피를 함께 나눈 자들이므로 이런 짓은 악한 행위이다.

18너희는 아내가 살아 있는 동안 그녀의 자매를 또 다른 아내로 맞아 그들이 서로 시기하는 일이 없도록 하라.

19“너희는 월경중에 있는 부정한 여자와 성관계를 하지 말아라.

20또 너희는 남의 아내와 간통하여 너희 자신을 더럽히지 말아라.

21“너희는 너희 자녀를 이방 신 몰렉에게 주어 불로 태우는 제물이 되게 함으로써 너희 하나님의 이름을 욕되게 하지 말아라. 나는 여호와이다.

22너희는 절대로 동성 연애를 해서는 안 된다. 이것은 추잡한 짓이다.

23남자이든 여자이든 누구든지 짐승과 음란한 짓을 하여 자신을 더럽히지 말아라. 이것은 무서운 죄이다.

24“너희는 이런 추잡한 일로 자신을 더럽히지 말아라. 내가 너희 앞에서 쫓아낼 이방 민족들이 이런 죄로 더럽혀졌고

25그들의 온 땅도 더럽혀졌으므로 내가 그 땅에 사는 사람들을 벌하여 18:25 또는 ‘그 땅이 그 거민을 토하여 낼 것이다’그 곳에서 쫓아낼 것이다.

26-27그들은 이런 악한 짓을 하여 그 땅을 더럽혔으나 너희만은 그렇게 해서는 안 된다. 너희는 이스라엘 사람이건 너희 가운데 사는 외국인이건 모두 나 여호와의 법과 규정을 따르고 지켜야 한다.

28너희가 만일 그 땅을 더럽히면 내가 쫓아낼 민족과 마찬가지로 너희도 그 땅에서 쫓아내겠다.

29누구든지 이런 악한 일을 하나라도 범하는 자는 내 백성 가운데서 제거될 것이다.

30그러므로 너희는 내 명령에 순종해야 하며 이런 악습을 따라서는 안 된다. 너희는 앞으로 들어가 살 그 땅의 백성들이 행하는 악한 풍습을 좇아 너희 자신을 더럽히지 말아라. 나는 너희 하나님 여호와이다.”