Walawi 17 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 17:1-16

Kunywa Damu Kumekatazwa

1Bwana akamwambia Mose, 217:2 Law 10:6, 12“Sema na Aroni na wanawe, pamoja na Waisraeli wote, uwaambie: ‘Hili ndilo Bwana aliloagiza: 317:3 Law 3:7; 7:23Mwisraeli yeyote atakayetoa dhabihu ya maksai, mwana-kondoo au mbuzi ndani ya kambi au nje yake, 417:4 1Fal 8:4; 2Nya 1:3; Kum 12:5-21; Mwa 17:14badala ya kuileta kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili kuileta kama sadaka kwa Bwana mbele ya Maskani ya Bwana, mtu huyo atahesabiwa kuwa na hatia ya kumwaga damu; ni lazima akatiliwe mbali na watu wake. 517:5 Law 3:1; Eze 43:27; Mwa 21:33; 22:2; 1Fal 14:22-23Hii ni ili Waisraeli wamletee Bwana dhabihu wanazozifanya sasa mahali pa wazi mashambani. Ni lazima wazilete kwa makuhani, yaani kwa Bwana, katika ingilio la Hema la Kukutania, na kutoa dhabihu kama sadaka za amani. 6Kuhani atanyunyiza damu kwenye madhabahu ya Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania, na kuyateketeza mafuta ya hiyo dhabihu kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. 717:7 Kut 12:14; 22:20; 34:15; 34:15; Yer 3:6-9; Eze 23:3; 1Kor 10:20; Mwa 9:12; Kum 32:17; 2Nya 11:15; Za 106:37Hawatatoa kamwe dhabihu zao kwa sanamu za mbuzi ambazo wamekuwa wakijifanyia nazo ukahaba. Hili litakuwa agizo la kudumu kwao na kwa ajili ya vizazi vijavyo.’

8“Waambie: ‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi miongoni mwao atakayetoa sadaka ya kuteketezwa au dhabihu 917:9 Law 1:3; 3:7bila kuileta kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili kutoa dhabihu kwa Bwana, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.

1017:10 Mwa 9:4; Kum 12:16, 23; 1Sam 14:33; Law 26:17; Yer 44:11; Eze 15:7“ ‘Mwisraeli yeyote au mgeni anayeishi miongoni mwao ambaye atakunywa damu yoyote, nitakuwa kinyume cha mtu huyo atakayekunywa damu na kumkatilia mbali na watu wake. 1117:11 Mwa 9:4; Ebr 9:22Kwa kuwa uhai wa kiumbe uko ndani ya damu, nami nimewapa hiyo damu ili mfanyie upatanisho kwa ajili yenu wenyewe juu ya madhabahu; damu ndiyo ifanyayo upatanisho kwa ajili ya maisha ya mtu. 12Kwa hiyo, ninawaambia Waisraeli, “Hakuna hata mmoja wenu anayeruhusiwa kunywa damu, wala mgeni anayeishi miongoni mwenu haruhusiwi kunywa damu.”

1317:13 Law 7:26; Eze 24:7; 33:25; Mdo 15:20; Kum 12:16“ ‘Mwisraeli yeyote au mgeni anayeishi miongoni mwenu ambaye atamwinda mnyama au ndege anayeruhusiwa kuliwa ni lazima aimwage damu na kuifunika kwa udongo, 1417:14 Mwa 9:4; Law 7:24; 14:8; 11:40; Kol 1:14; Kum 14:21; Kut 22:31; Mk 14:24; Rum 5:9kwa sababu uhai wa kila kiumbe ni katika damu yake. Ndiyo sababu nimewaambia Waisraeli, “Kamwe msinywe damu ya kiumbe chochote, kwa sababu uhai wa kila kiumbe ni katika damu yake; yeyote atakayekunywa damu ni lazima akatiliwe mbali.”

1517:15 Kut 22:31; Kum 14:2; Eze 4:14“ ‘Mtu yeyote, awe mzawa au mgeni, ambaye atakula mzoga wa kitu chochote ama kilichouawa na wanyama mwitu ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada mpaka jioni, kisha atakuwa safi. 1617:16 Law 5:1; Hes 19:20; Ebr 9:28Lakini kama hakufua nguo zake na kuoga, atakuwa na hatia kwa kosa hilo.’ ”

New International Reader’s Version

Leviticus 17:1-16

Do Not Eat Meat With Blood in It

1The Lord said to Moses, 2“Speak to Aaron and his sons. Speak to all the Israelites. Tell them, ‘Here is what the Lord has commanded. He has said, 3“Suppose someone sacrifices an ox, a lamb or a goat. They sacrifice it in the camp or outside of it. 4They do it instead of bringing the animal to the entrance to the tent of meeting. They sacrifice it instead of giving it as an offering to me in front of my holy tent. Then they will be thought of as guilty of spilling blood. Because they have done that, they must be separated from their people. 5The Israelites are now making sacrifices in the open fields. But they must bring their sacrifices to the priest. They must bring them to me at the entrance to the tent of meeting. There they must sacrifice them as friendship offerings. 6The priest must splash the blood against my altar. It is the altar at the entrance to the tent of meeting. He must burn the fat. Its smell will please me. 7The Israelites must stop offering any of their sacrifices to statues of gods that look like goats. When they offer sacrifices to those statues, they are not faithful to me. This is a law for them that will last for all time to come.” ’

8“Tell them, ‘Suppose someone offers a burnt offering or sacrifice. It does not matter whether they are an Israelite or an outsider. 9And suppose they do not bring it to the entrance to the tent of meeting to sacrifice it to me. Then they must be separated from their people.

10“ ‘Suppose someone eats meat that still has blood in it. It does not matter whether they are an Israelite or an outsider. I will turn against them if they eat it. I will separate them from their people. 11The life of each creature is in its blood. So I have given you the blood of animals to pay for your sin on the altar. Blood is life. That is why blood pays for your sin. 12So I say to the Israelites, “You must not eat meat that still has blood in it. And an outsider who lives among you must not eat it either.”

13“ ‘Suppose any of you hunts any animal or bird that can be eaten. It does not matter whether you are an Israelite or an outsider. You must let the blood flow out of the animal or bird. You must cover the blood with dirt. 14That is because every creature’s life is its blood. And that is why I have said to the Israelites, “You must not eat any creature’s meat that still has blood in it. Every creature’s life is its blood. Anyone who eats that kind of meat must be separated from the community of Israel.”

15“ ‘Suppose someone eats anything found dead or torn apart by wild animals. It does not matter whether they are an Israelite or an outsider. They must wash their clothes. They must take a bath. They will be “unclean” until evening. After that, they will be “clean.” 16But suppose they do not wash their clothes. And suppose they do not take a bath. Then they will be held responsible for what they have done.’ ”