Wakolosai 3 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wakolosai 3:1-25

Kanuni Za Kuishi Maisha Matakatifu

13:1 Rum 6:5; Mk 16:19Basi, kwa kuwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo alikoketi mkono wa kuume wa Mungu. 23:2 Flp 3:19, 20Yafikirini mambo yaliyo juu, wala si ya duniani. 33:3 Rum 6:2; 2Kor 5:14Kwa maana ninyi mlikufa, nao uhai wenu sasa umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu. 43:4 1Kor 1:7; 1Pet 1:13; 1Yn 3:2; Gal 2:20; 1Kor 1:7; 1Pet 1:13; Yn 3:2Wakati Kristo, aliye uzima wenu, atakapotokea, ndipo nanyi mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.

53:5 Efe 5:3-5; Rum 6:2; Efe 4:22; Gal 5:24; 1Kor 6:18; Efe 5:3; Gal 5:19-21Kwa hiyo, ueni kabisa chochote kilicho ndani yenu cha asili ya kidunia: yaani uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya na ulafi, ambayo ndiyo ibada ya sanamu. 63:6 Rum 1:18Kwa sababu ya mambo haya, ghadhabu ya Mungu inakuja. 73:7 Efe 2:2Ninyi pia zamani mlienenda katika mambo haya mlipoishi maisha hayo. 83:8 Efe 4:22-31Lakini sasa yawekeni mbali nanyi mambo kama haya yote: yaani hasira, ghadhabu, uovu, masingizio na lugha chafu kutoka midomoni mwenu. 93:9 Efe 4:22-25Msiambiane uongo, kwa maana mmevua kabisa utu wenu wa kale pamoja na matendo yake, 103:10 Rum 1:22; 2Kor 4:16; Efe 2:10nanyi mmevaa utu mpya, unaofanywa upya katika ufahamu sawasawa na mfano wa Muumba wake. 113:11 Rum 10:12; 1Kor 7:19; Gal 3:28; Efe 1:23Hapa hakuna Myunani wala Myahudi, aliyetahiriwa wala asiyetahiriwa, asiyestaarabika wala aliyestaarabika, mtumwa wala mtu huru, bali Kristo ni yote, na ndani ya wote.

123:12 Flp 2:3; 2Kor 6:6; Gal 5:22, 23; Efe 4:2Kwa hiyo, kwa kuwa ninyi mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao sana, jivikeni moyo wa huruma, utu wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu. 133:13 Efe 4:2, 32; 4:32Vumilianeni na kusameheana mtu akiwa na lalamiko lolote dhidi ya mwenzake. Sameheaneni kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi. 143:14 1Kor 13:1-13; Efe 4:3Zaidi ya maadili haya yote jivikeni upendo, ambao ndio unaofunga kila kitu pamoja katika umoja mkamilifu.

153:15 Yn 14:27Amani ya Kristo na itawale mioyoni mwenu, kwa kuwa ninyi kama viungo vya mwili mmoja mmeitiwa amani. Tena kuweni watu wa shukrani. 163:16 Rum 10:17; Kol 1:28; Efe 5:19Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu, mkifundishana na kuonyana katika hekima yote, mkimwimbia Mungu zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, huku mkiwa na shukrani mioyoni mwenu. 173:17 Efe 5:20-22Lolote mfanyalo, ikiwa ni kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba katika yeye.

Kanuni Katika Madaraka Ya Nyumbani

18Ninyi wake, watiini waume zenu, kama inavyostahili katika Bwana.

193:19 Efe 5:25, 28, 33; 1Pet 3:7; Efe 4:31Ninyi waume, wapendeni wake zenu, wala msiwe na uchungu dhidi yao.

203:20 Efe 6:1; 5:24; Tit 2:9Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana hivi ndivyo inavyompendeza Bwana.

213:21 Efe 6:4Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.

223:22 Efe 6:5; 1Tim 6:1; Tit 2:9; 1Pet 2:18Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu wa hapa duniani katika mambo yote. Fanyeni hivyo si wakiwepo tu, wala si kwa kutafuta upendeleo wao, bali kwa moyo mnyofu na kumcha Bwana. 233:23 Efe 6:6, 7Lolote mfanyalo, fanyeni kwa moyo kama watu wanaomtumikia Bwana, na si wanadamu, 243:24 Mdo 20:32kwa kuwa mnajua kwamba mtapokea urithi wenu kutoka kwa Bwana ukiwa thawabu yenu. Ni Bwana Yesu Kristo mnayemtumikia. 253:25 Mdo 10:34Yeyote atendaye mabaya atalipwa kwa ajili ya mabaya yake, wala hakuna upendeleo.

King James Version

Colossians 3:1-25

1If ye then be risen with Christ, seek those things which are above, where Christ sitteth on the right hand of God. 2Set your affection on things above, not on things on the earth. 3For ye are dead, and your life is hid with Christ in God. 4When Christ, who is our life, shall appear, then shall ye also appear with him in glory.

5Mortify therefore your members which are upon the earth; fornication, uncleanness, inordinate affection, evil concupiscence, and covetousness, which is idolatry: 6For which things’ sake the wrath of God cometh on the children of disobedience: 7In the which ye also walked some time, when ye lived in them. 8But now ye also put off all these; anger, wrath, malice, blasphemy, filthy communication out of your mouth. 9Lie not one to another, seeing that ye have put off the old man with his deeds; 10And have put on the new man, which is renewed in knowledge after the image of him that created him: 11Where there is neither Greek nor Jew, circumcision nor uncircumcision, Barbarian, Scythian, bond nor free: but Christ is all, and in all. 12Put on therefore, as the elect of God, holy and beloved, bowels of mercies, kindness, humbleness of mind, meekness, longsuffering; 13Forbearing one another, and forgiving one another, if any man have a quarrel against any: even as Christ forgave you, so also do ye. 14And above all these things put on charity, which is the bond of perfectness. 15And let the peace of God rule in your hearts, to the which also ye are called in one body; and be ye thankful. 16Let the word of Christ dwell in you richly in all wisdom; teaching and admonishing one another in psalms and hymns and spiritual songs, singing with grace in your hearts to the Lord. 17And whatsoever ye do in word or deed, do all in the name of the Lord Jesus, giving thanks to God and the Father by him.

18Wives, submit yourselves unto your own husbands, as it is fit in the Lord. 19Husbands, love your wives, and be not bitter against them. 20Children, obey your parents in all things: for this is well pleasing unto the Lord. 21Fathers, provoke not your children to anger, lest they be discouraged. 22Servants, obey in all things your masters according to the flesh; not with eyeservice, as menpleasers; but in singleness of heart, fearing God: 23And whatsoever ye do, do it heartily, as to the Lord, and not unto men; 24Knowing that of the Lord ye shall receive the reward of the inheritance: for ye serve the Lord Christ. 25But he that doeth wrong shall receive for the wrong which he hath done: and there is no respect of persons.