Wakolosai 2 – NEN & PEV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wakolosai 2:1-23

12:1 Kol 1:29; 4:12; 4:13, 15, 16; Ufu 1:11Nataka mjue jinsi ninavyojitaabisha kwa ajili yenu na kwa ajili ya wale walioko Laodikia, na pia kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona mimi binafsi. 22:2 Efe 6:22; Kol 4:8; Rum 16:25Kusudi langu ni watiwe moyo na kuunganishwa katika upendo, ili wapate ule utajiri wa ufahamu mkamilifu, ili waijue siri ya Mungu, yaani, Kristo mwenyewe, 32:3 Isa 11:2; Yer 23:5; Rum 11:33; 1Kor 1:24, 30ambaye ndani yake kumefichwa hazina zote za hekima na maarifa. 42:4 Rum 16:18Nawaambia mambo haya ili mtu yeyote asiwadanganye kwa maneno ya kuwashawishi. 52:5 1Kor 5:4; 1The 2:17Kwa kuwa ingawa mimi siko pamoja nanyi kimwili, lakini niko pamoja nanyi kiroho, nami nafurahi kuuona utaratibu wenu na jinsi uthabiti wa imani yenu katika Kristo ulivyo.

Ukamilifu Wa Maisha Katika Kristo

62:6 Yn 13:13; Kol 1:10Hivyo basi, kama vile mlivyompokea Kristo Yesu kuwa Bwana, endeleeni kukaa ndani yake, 72:7 Efe 3:17; 4:22mkiwa na mizizi, na mmejengwa ndani yake, mkiimarishwa katika imani kama mlivyofundishwa, na kufurika kwa wingi wa shukrani.

82:8 1Tim 6:20; Kol 2:20; Gal 4:2Angalieni mtu yeyote asiwafanye ninyi mateka kwa elimu batili na madanganyo matupu yanayotegemea mapokeo ya wanadamu na mafundisho ya ulimwengu badala ya Kristo.

92:9 Yn 1:16Maana ukamilifu wote wa Uungu umo ndani ya Kristo katika umbile la mwili wa kibinadamu, 102:10 Efe 1:22; Mt 28:18nanyi mmepewa ukamilifu ndani ya Kristo, ambaye ndiye mkuu juu ya kila enzi na kila mamlaka. 112:11 Rum 2:29; Flp 3:3; Gal 5:24Katika Kristo pia mlitahiriwa kwa kutengwa mbali na asili ya dhambi, si kwa tohara inayofanywa kwa mikono ya wanadamu, bali kwa ile tohara iliyofanywa na Kristo, 122:12 Mt 28:19; Rum 6:5; Mdo 2:24mkiwa mmezikwa pamoja naye katika ubatizo, na kufufuliwa pamoja naye kwa njia ya imani yenu katika uweza wa Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu.

132:13 Efe 2:15; 2:5; 4:32Mlipokuwa wafu katika dhambi zenu na kutokutahiriwa katika asili yenu ya dhambi, Mungu aliwafanya mwe hai pamoja na Kristo. Alitusamehe dhambi zetu zote, 142:14 Efe 2:15; 1Pet 2:24akiisha kuifuta ile hati yenye mashtaka yaliyokuwa yanatukabili, pamoja na maagizo yake. Aliiondoa isiwepo tena, akiigongomea kwenye msalaba wake. 152:15 Kol 2:10; Efe 6:12; Mt 12:29; Lk 10:18; Yn 12:31Mungu akiisha kuzivua enzi na mamlaka, alizifanya kuwa kitu cha fedheha hadharani kwa kuziburura kwa ujasiri, akizishinda katika msalaba wa Kristo.

162:16 Rum 14:3, 4; Mk 7:19; Rum 14:17; Law 23:2; Rum 14:5Kwa hiyo mtu asiwahukumu ninyi kuhusu vyakula au vinywaji, au kuhusu kuadhimisha sikukuu za dini, au Sikukuu za Mwezi Mwandamo au siku ya Sabato. 172:17 Ebr 8:5; 10:1Hizi zilikuwa kivuli cha mambo ambayo yangekuja, lakini ile iliyo halisi imo ndani ya Kristo. 182:18 Kol 2:23; 1Kor 9:24; Flp 3:14Mtu yeyote asiwaondolee thawabu yenu kwa kusisitiza kunyenyekea kwake na kuabudu malaika. Mtu kama huyo hudumu katika maono yake, akijivuna bila sababu katika mawazo ya kibinadamu. 192:19 Efe 1:22; 1Kor 2:8; Gal 4:3, 9, 14, 16Yeye amepoteza ushirikiano na Kichwa, ambaye kutoka kwake mwili wote unalishwa na kushikamanishwa pamoja kwa viungo na mishipa, nao hukua kwa ukuaji utokao kwa Mungu.

Maonyo Dhidi Ya Walimu Wa Uongo

20Kwa kuwa mlikufa pamoja na Kristo, mkayaacha yale mafundisho ya msingi ya ulimwengu huu, kwa nini bado mnaishi kama ninyi ni wa ulimwengu? Kwa nini mnajitia chini ya amri: 212:21 1Tim 4:3“Msishike! Msionje! Msiguse!”? 222:22 1Kor 6:13; Isa 29:13; Mt 15:9; Tit 1:14Haya yote mwisho wake ni kuharibika yanapotumiwa, kwa sababu msingi wake ni katika maagizo na mafundisho ya wanadamu. 232:23 Kol 2:18Kwa kweli amri kama hizo huonekana kama zina hekima, katika namna za ibada walizojitungia wenyewe, na unyenyekevu wa uongo na kuutawala mwili kwa ukali, lakini hayafai kitu katika kuzuia tamaa za mwili.

La Parola è Vita

Colossesi 2:1-23

1Voglio che sappiate quanto ho lottato, pregando per voi, per la chiesa di Laodicèa e per i tanti altri amici che non mi hanno mai conosciuto personalmente. 2Questo è ciò che ho chiesto a Dio per voi: che siate incoraggiati e, uniti nellʼamore, possiate fare lʼesperienza straordinaria di conoscere Cristo fino in fondo, con la piena convinzione dellʼintelligenza. Perché il piano segreto di Dio finalmente ora è stato rivelato: è Cristo stesso. 3In lui stanno nascosti tutti i tesori della sapienza e della scienza.

Che nessuno sciupi la vostra fede

4Vi dico queste cose, perché temo che qualcuno possa imbrogliarvi con dei bei discorsi. 5Anche se sono lontano da voi, il mio cuore è con voi, e sono felice di sapere che vi comportate bene e che restate ben fermi nella fede in Cristo. 6Ora come avete creduto che Cristo vi salva, così camminate in Lui. Mantenetevi in unione vitale con Cristo. 7Come alberi che hanno in lui le loro radici, prendete da lui il vostro nutrimento; come case che hanno in lui le loro fondamenta, tenete salda in lui la vostra fede, tanto da diventare forti e vigorosi nella verità che avete imparato. La vostra vita sia piena di gioia e di gratitudine per tutto ciò che Dio ha fatto per voi.

8State attenti che nessuno rovini la vostra fede e la vostra gioia con la filosofia e con i ragionamenti inutili e sbagliati che si basano sui pensieri e le tradizioni degli uomini, anziché su ciò che Cristo ha detto. 9In Cristo cʼè corporalmente la pienezza della divinità, 10perciò quando avete Cristo, avete tutto e, strettamente uniti a lui, siete riempiti di Dio. È lui il Signore di tutti i signori, dominatore di ogni potenza.

11Quando voi avete accettato Cristo, egli vi ha liberato dalla debolezza davanti al peccato, e non per mezzo della circoncisione, un semplice intervento sul corpo, ma con un intervento spirituale, fatto da Cristo. 12Perché nel battesimo avete sepolto con Cristo la vostra vecchia natura corrotta, per poi risorgere con lui ad una nuova vita, per mezzo della fede nella potenza di Dio, che ha resuscitato Cristo dalla morte.

13A causa dei vostri peccati e della vostra vecchia natura corrotta, di fatto, voi eravate come morti. Ma Dio vi ha fatto rivivere con Cristo; egli ha perdonato tutti i nostri peccati, 14eliminando lʼatto di accusa contro di noi: lʼelenco dei comandamenti che noi non abbiamo osservato. Dio ha tolto di mezzo le accuse contro di noi, inchiodandole alla croce di Cristo. 15In questo modo Dio ha disarmato ogni autorità e ogni potenza, e le ha esposte allo scherno della gente, dopo averle vinte per mezzo della croce di Cristo.

16Perciò, nessuno ha il diritto di criticarvi per ciò che mangiate o bevete, né se osservate o meno le feste ebraiche, le cerimonie del sabato o per la luna nuova. 17Perché queste sono state soltanto regole provvisorie, che hanno avuto fine con lʼarrivo di Cristo. Erano soltanto lʼombra delle cose reali, e cioè, di Cristo stesso. 18Non lasciate che chiunque che si compiace nella falsa umiltà e nellʼadorare gli angeli, vi dica che perderete il premio. Magari vi raccontano di aver avuto delle visioni, e per questo vorrebbero obbligarvi. Costoro sono soltanto degli esaltati, 19ma una cosa è certa: non sono uniti a Cristo, il capo a cui siamo uniti tutti noi, che siamo il suo corpo. E questo corpo, tenuto ben saldo dalle giunture e dalle articolazioni, può crescere soltanto se prende nutrimento da Cristo, un nutrimento che viene da Dio. 20Se davvero fate conto di essere morti con Cristo, e ciò vi ha liberati dalla ricerca della salvezza per mezzo degli insegnamenti di questo mondo, perché allora continuate a seguirli, restando legati a certi precetti? 21Perché vi lasciate dire: «Questo non si può prendere, quello non si può assaggiare, o questʼaltro non si può toccare?» 22Questi precetti non sono né più né meno che insegnamenti umani, destinati a scomparire con lʼuso. 23È vero che tali regole possono anche sembrare sagge perché, oltre a richiedere grande devozione, umiliano e fanno soffrire il corpo, ma in realtà non servono a niente per dominare i pensieri e i desideri carnali. Anzi, servono soltanto a renderci orgogliosi.