Waebrania 13 – NEN & HHH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waebrania 13:1-25

Huduma Inayompendeza Mungu

113:1 Rum 12:10; 1The 4:9; 1Pet 1:22; 2:17; 3:8; 4:8; 2Pet 1:7; 1Yn 3:11; 4:7Endeleeni kupendana kama ndugu. 213:2 Mt 25:35; Rum 12:13; 1Tim 3:2; 1Pet 4:9; Mwa 18:3; 19:2Msisahau kuwakaribisha wageni, kwa kuwa kwa kufanya hivyo, watu wengine waliwakaribisha malaika pasipo kujua. 313:3 Mt 25:36; Kol 4:18; Ebr 10:34; Rum 12:15; 1Kor 12:26; 1Pet 3:8Wakumbukeni wale waliofungwa gerezani kana kwamba ninyi mmefungwa pamoja nao. Pia wakumbukeni wale wanaotendewa vibaya, kana kwamba ni ninyi wenyewe mnateswa.

413:4 Mal 2:15; 1Kor 7:38; 1Tim 4:3; Kum 22:22; 1Kor 6:9; Efe 5:5; Ufu 22:15Ndoa na iheshimiwe na watu wote, nayo malazi yawe safi, kwa kuwa Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati wote. 513:5 1Tim 3:3; Flp 4:11; Kum 31:6, 8; Yos 1:5; Mwa 28:15; Mt 6:25, 34; 1Nya 28:20; Za 37:25Yalindeni maisha yenu msiwe na tabia ya kupenda fedha, bali mridhike na vile mlivyo navyo, kwa sababu Mungu amesema,

“Kamwe sitakuacha,

wala sitakupungukia.”

613:6 Za 27:1; 56:4; 118:6Kwa hiyo tunaweza kusema kwa ujasiri,

“Bwana ni msaada wangu; sitaogopa.

Mwanadamu anaweza kunitenda nini?”

713:7 Ebr 13:17, 24; 1Kor 16:16; Ebr 4:12; 6:12Wakumbukeni viongozi wenu, wale waliowaambia neno la Mungu. Angalieni matokeo ya mwenendo wa maisha yao mkaiige imani yao. 813:8 Yn 8:58; Ebr 1:12; Za 102:27; Ufu 1:4Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele.

913:9 Efe 4:14; Kol 2:7; 2:16; Ebr 9:10; Rum 14:17; 1Yn 4:1; 1Tim 4:3Msichukuliwe na kila aina ya mafundisho ya kigeni. Ni vyema mioyo yenu iimarishwe kwa neema, wala si kwa sheria kuhusu utaratibu wa vyakula, ambavyo havina faida kwa wale wanaozishika hizo sheria. 1013:10 1Kor 9:13; 10:18Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaohudumu katika hema hawana haki ya kula vile vitu vilivyowekwa juu yake.

1113:11 Law 16:15; Kut 29:14; Law 4:12; 9:11; 16:27; Hes 19:3Kuhani mkuu huchukua damu ya wanyama na kuiingiza Patakatifu pa Patakatifu, kama sadaka ya dhambi, lakini miili ya hao wanyama huteketezwa nje ya kambi. 1213:12 Yn 19:17, 18; Mdo 7:58; Efe 5:26; Rum 3:25Vivyo hivyo, Yesu naye aliteswa nje ya lango la mji ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe. 1313:13 Lk 9:23; Ebr 11:26; 1Pet 4:14Kwa hiyo, basi na tumwendee nje ya kambi, tukiichukua aibu aliyobeba. 1413:14 Mik 2:10; Flp 3:20Kwa kuwa hapa hatuna mji udumuo, bali tunautafuta ule ujao.

1513:15 1Pet 2:5; Isa 57:19; Hos 14:2; Efe 5:20; Law 7:12; Za 50:14, 23; 107:22; 116:17; Hos 14:2Basi kwa njia ya Yesu, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake. 1613:16 Rum 12:13; Flp 4:18; 1Kor 9:12; Ebr 6:10Na msiache kutenda mema na kushirikiana vile vitu mlivyo navyo, kwa kuwa dhabihu kama hizo ndizo zinazompendeza Mungu.

1713:17 Isa 62:6; Mdo 20:28; Ebr 13:7, 24; Flp 2:29; 1The 5:12; 1Tim 5:17; Eze 3:17; 33:2, 7; Mdo 20:26Watiini viongozi wenu na kujinyenyekeza chini ya mamlaka yao. Kwa maana wao wanakesha kwa ajili yenu kama watu watakaopaswa kutoa hesabu. Watiini ili wafanye kazi yao kwa furaha, wala si kama mzigo, maana hiyo haitakuwa na faida kwenu.

1813:18 1The 5:25; Mdo 23:1Tuombeeni. Tuna hakika kuwa tunayo dhamiri safi na shauku ya kuishi kwa uadilifu kwa kila njia. 19Ninawasihi zaidi mniombee ili nipate kurudishwa kwenu upesi.

Maombi Ya Kuwatakia Baraka

20Basi Mungu wa amani, ambaye kwa damu ya Agano la milele alimleta tena kutoka kwa wafu Bwana wetu Yesu, yule Mchungaji Mkuu wa kondoo, 21awafanye ninyi wakamilifu mkiwa mmekamilishwa katika kila jambo jema ili mpate kutenda mapenzi yake, naye atende ndani yetu kile kinachompendeza machoni Pake, kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu una yeye milele na milele. Amen.

Maneno Ya Mwisho Na Salamu

2213:22 1Pet 5:12; Yak 1:21Ndugu zangu, nawasihi mchukuliane na maneno yangu ya maonyo, kwa kuwa nimewaandikia waraka mfupi tu.

2313:23 1The 3:2; Mdo 16:1; 1Tim 6:12Nataka ninyi mjue kwamba ndugu yetu Timotheo amefunguliwa kutoka gerezani. Akifika mapema, nitakuja pamoja naye kuwaona.

2413:24 Ebr 13:7, 17; Mdo 18:2Wasalimuni viongozi wenu wote na watakatifu wote. Wale wa kutoka Italia wanawasalimu.

2513:25 Tit 3:15; Kol 4:18Neema iwe nanyi nyote. Amen.

Habrit Hakhadasha/Haderekh

האיגרת אל-העברים 13:1-25

1המשיכו לאהוב איש את אחיו באמת ובתמים. 2אל תשכחו להכניס אורחים, כי יש כאלה שאירחו מלאכים בביתם בלי שידעו זאת. 3זכרו את האסירים בכלא; השתתפו בסבלם כאילו אתם עצמכם אסורים יחד אתם. השתתפו בכאבם של הסובלים כאילו התייסרתם יחד איתם.

4כבדו את נשואיכם ושמרו על נאמנותכם וטוהר גופכם, כי אלוהים יעניש את כל הזונים והנואפים.

5התרחקו מאהבת כסף ושמחו בחלקכם, כי אלוהים אמר: ”לעולם לא אאכזב ולא אעזוב אותך!“13‏.5 יג 5 תרגום חופשי של יהושע א 5 6משום כך יכולים אנו לומר בביטחון וללא ספק: ”ה׳ בעוזרי ואיני פוחד מאיש!“13‏.6 יג 6 תרגום חופשי של תהלים קיח 6

7זכרו את מנהיגיכם אשר לימדו אתכם את דבר ה׳; חישבו על דרך חייהם והשתדלו לבטוח בה׳ כמוהם.

8ישוע המשיח אינו משתנה; כפי שהיה בעבר כך הוא בהווה, וכך גם יישאר לנצח! 9אל תלכו שולל אחרי רעיונות זרים וחדשים, כי מוטב לחזק את לבנו בחסד אלוהים, מאשר להקדיש את כל תשומת לבנו לטקסי־מאכל שלא הועילו למשתתפים בהם. 10יש לנו מזבח שאינו מועיל לאלה שממשיכים לחפש ישועה באמצעות קיום התורה. 11לפי חוקי התורה הביא הכהן הגדול את דם הבהמות אל הקודש כדי לכפר על החטא, ואילו גוף הבהמה נשרף מחוץ למחנה. 12משום כך גם ישוע סבל ומת מחוץ לעיר. 13לכן, הבה נצא לקראתו אל מחוץ לעיר (כלומר, מחוץ לענייני העולם הזה) ונהיה מוכנים לשאת את חרפתו. 14כי העולם הזה אינו ביתנו; אנו מצפים לעיר שעתידה לבוא.

15בעזרת המשיח נקריב לאלוהים בכל עת זבח תודה, כלומר, נודה לו בפינו ונכריז על נאמנותנו לשמו. 16אל תשכחו לעשות מעשים טובים ולשתף את העניים במה שיש לכם, כי קורבנות כאלה רצויים לה׳.

17צייתו למנהיגיכם וכבדו את סמכותם, כי הם דואגים לכם ללא ליאות, כמי שעתידים למסור על כך דין וחשבון. הקלו עליהם; אפשרו להם לבצע את תפקידם בשמחה, ללא צער וללא כאב, כי אחרת תסבלו גם אתם. 18התפללו בעדנו, כי מצפוננו נקי וברצוננו לשמור עליו כך. 19במיוחד עתה אני זקוק לתפילתכם, כדי שאוכל לשוב אליכם במהרה.

20ואלוהי השלום, אשר בדם הברית החדשה והנצחית העלה מן המתים את רועה הצאן הגדול – את ישוע המשיח אדוננו – 21יצייד אתכם בכל מה שדרוש לכם כדי למלא את רצונו, ויעשה בכם את הרצוי בעיניו על־ידי ישוע המשיח, אשר לו הכבוד לעולמי עולמים. – אמן.

22אחים יקרים, אנא, הקשיבו בסבלנות למה שכתבתי במכתבי זה, שהרי זהו מכתב קצר. 23אני רוצה להביא לידיעתכם שאחינו טימותיוס שוחרר מהכלא. אם הוא יבוא לכאן בקרוב, אבוא יחד איתו לבקר אתכם.

24מסרו דרישת־שלום לכל מנהיגיכם ולכל המאמינים שנמצאים שם. המאמינים באיטליה שואלים לשלומכם. 25חסד אלוהים עם כולכם. – אמן.