Waebrania 10 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waebrania 10:1-39

Dhabihu Ya Kristo Ni Mara Moja Tu

110:1 Kol 2:17; Ebr 8:5; 9:23; 9:11; 9:9; 9:14Sheria ni kivuli tu cha mambo mema yajayo, wala si uhalisi wa mambo yenyewe. Kwa sababu hii, haiwezekani kamwe kwa njia ya dhabihu zitolewazo mwaka hadi mwaka kuwakamilisha wale wanaokaribia ili kuabudu. 210:2 Ebr 9:9Kama dhabihu hizo zingeweza kuwakamilisha, hazingeendelea kutolewa tena. Kwa kuwa hao waabuduo wangekuwa wametakaswa mara moja tu, wala wasingejiona tena kuwa na dhambi. 310:3 Law 16:21; 16:34; Ebr 9:7Lakini zile dhabihu zilikuwa ukumbusho wa dhambi kila mwaka, 410:4 Mik 6:6, 7; Ebr 9:13; 9:11kwa sababu haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.

510:5 Ebr 1:6; 2:14; 1Pet 2:24; Za 40:6; 50:8; Isa 1:11; Yer 6:20; Amo 5:21, 22Kwa hiyo, Kristo alipokuja duniani, alisema:

“Dhabihu na sadaka hukuzitaka,

bali mwili uliniandalia;

6sadaka za kuteketezwa na za dhambi

hukupendezwa nazo.

710:7 Ezr 6:2; Yer 36:2; Za 40:6-8; Mt 26:39Ndipo niliposema, ‘Mimi hapa, nimekuja,

imeandikwa kunihusu katika kitabu:

Nimekuja kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu.’ ”

810:8 Ebr 10:5, 6; Mk 12:33Kwanza alisema, “Dhabihu na sadaka, sadaka za kuteketezwa na za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo” (ingawa sheria iliagiza zitolewe). 910:9 Ebr 10:7Kisha akasema “Mimi hapa, nimekuja kuyafanya mapenzi yako.” Aondoa lile Agano la kwanza ili kuimarisha la pili. 1010:10 Ebr 10:14; Efe 5:26; Ebr 2:14; 7:27; 1Pet 2:24Katika mapenzi hayo sisi tumetakaswa na kufanywa watakatifu kwa njia ya sadaka ya mwili wa Yesu Kristo alioutoa mara moja tu.

1110:11 Ebr 5:1; 10:1, 4; Hes 28:3; Ebr 7:27Kila kuhani husimama siku kwa siku akifanya huduma yake ya ibada, na kutoa tena na tena dhabihu zile zile ambazo haziwezi kamwe kuondoa dhambi. 1210:12 Ebr 5:1; Mk 16:19; Ebr 1:3; Kol 3:1Lakini huyu kuhani akiisha kutoa dhabihu moja kwa ajili ya dhambi kwa wakati wote, aliketi mkono wa kuume wa Mungu. 1310:13 Yos 10:24; Ebr 1:13; Za 110:1; Mdo 2:35; 1Kor 15:25Tangu wakati huo anangoja mpaka adui zake wawekwe chini ya miguu yake, 1410:14 Ebr 10:1; Efe 5:26kwa sababu kwa dhabihu moja amewafanya kuwa wakamilifu milele wale wote wanaotakaswa.

1510:15 Ebr 3:7Pia Roho Mtakatifu anatushuhudia kuhusu jambo hili. Kwanza anasema:

1610:16 Yer 31:33; Ebr 8:10“Hili ndilo Agano nitakalofanya nao

baada ya siku hizo, asema Bwana.

Nitaziweka sheria zangu mioyoni mwao,

na kuziandika katika nia zao.”

1710:17 Yer 31:34; Ebr 8:12Kisha aongeza kusema:

“Dhambi zao na kutokutii kwao

sitakumbuka tena.”

18Basi haya yakiisha kusamehewa, hakuna tena dhabihu yoyote inayotolewa kwa ajili ya dhambi.

Wito Wa Kuvumilia

1910:19 Efe 3:12; Law 16:2; Efe 2:18; Ebr 9:8, 12, 25Kwa hiyo, ndugu zangu, kwa kuwa tunao ujasiri wa kupaingia Patakatifu pa Patakatifu kwa damu ya Yesu, 2010:20 Ebr 9:8; 6:19; 9:3kwa njia mpya iliyo hai tuliyofunguliwa kwa ajili yetu kupitia kwenye lile pazia, yaani, mwili wake, 2110:21 Ebr 2:17; 3:6basi kwa kuwa tunaye Kuhani Mkuu juu ya nyumba ya Mungu, 2210:22 Ebr 10:1; 7:19; 3:12; Yak 1:6; 1Yn 3:21; Eze 36:25; 2Kor 7:1; 1Pet 1:2; Mdo 22:16sisi na tumkaribie Mungu kwa moyo mnyofu kwa imani timilifu, mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa damu ya Kristo na kuwa safi kutokana na dhamiri mbaya nayo miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi. 2310:23 Ebr 3:6; 3; 1; 1Kor 1:9Tushike kwa uthabiti lile tumaini la ukiri wetu bila kuyumbayumba, kwa maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu. 2410:24 Tit 2:14Tuangaliane na kuhimizana sisi kwa sisi katika upendo na katika kutenda mema. 2510:25 Mdo 2:42; Ebr 3:13; 1Kor 3:13Wala tusiache kukutana pamoja, kama wengine walivyo na desturi, bali tuhimizane sisi kwa sisi kadiri tuonavyo Siku ile inakaribia.

2610:26 Kut 21:14; Hes 15:30; Ebr 5:2; 6:4-8; 2Pet 2:20; 1Tim 2:4Kama tukiendelea kutenda dhambi kwa makusudi baada ya kupokea ufahamu wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi. 2710:27 Isa 26:11; 2The 1:7; Ebr 9:27; 12:29Lakini kinachobaki ni kungoja kwa hofu hukumu ya moto uwakao, utakaowaangamiza adui za Mungu. 2810:28 Kum 17:6, 7; Mt 18:16; Ebr 2:2; Yn 8:17Yeyote aliyeikataa sheria ya Mose alikufa pasipo huruma kwa ushahidi wa watu wawili au watatu. 2910:29 Ebr 2:3; 12:25; 1Kor 11:29; Mt 12:32; Efe 4:30; Mt 4:3; Ufu 1:5; Ebr 6:6; Mt 26:28Je, mnadhani ni adhabu kali kiasi gani anayostahili kupewa mtu aliyemkanyaga Mwana wa Mungu chini ya nyayo zake, yeye aliyeifanya damu ya Agano iliyomtakasa kuwa kitu najisi na kumtendea maovu Roho wa neema? 3010:30 Kum 32:35; Rum 12:19; Kum 32:36; Za 135:14Kwa kuwa tunamjua yeye aliyesema, “Ni juu yangu kulipiza kisasi; nitalipiza.” Tena asema, “Bwana atawahukumu watu wake.” 3110:31 2Kor 5:11; Isa 19:16; Mt 16:16Ni jambo la kutisha kuanguka mikononi mwa Mungu aliye hai.

3210:32 Ebr 6:4; Flp 1:9, 30; Gal 3:4; 2Yn 8; Kol 2:1Kumbukeni siku zile za kwanza, ambazo mkiisha kutiwa nuru mlistahimili mashindano makali ya maumivu. 33Wakati mwingine mlitukanwa na kuteswa hadharani; wakati mwingine mlikuwa radhi kuungana na wale waliofanyiwa hivyo. 3410:34 Ebr 13:3; 11:16; 1Pet 1:4, 5Mliwahurumia wale waliokuwa kifungoni, mkikubali kwa furaha kunyangʼanywa mali zenu kwa maana mlijua kwamba mnayo mali iliyo bora zaidi idumuyo.

3510:35 Efe 3:12; Mt 5:12; 10:32Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kubwa mno. 3610:36 Rum 5:3; Ebr 5:11; 12:1; Yak 1:3, 4, 12; 2Pet 1:6; Ebr 6:15; 9:15Inawapasa kuvumilia ili mkiisha kufanya mapenzi ya Mungu mpate kile alichoahidi. 3710:37 Mt 11:3; Ufu 22:20; Lk 18:8; 2Pet 3:9; Hab 2:3, 4Kwa kuwa bado kitambo kidogo tu,

“Yeye ajaye atakuja wala hatakawia.

3810:38 Rum 1:17; Gal 3:11; Hab 2:3, 4Lakini mwenye haki wangu

ataishi kwa imani.

Naye kama akisitasita,

sina furaha naye.”

3910:39 2Pet 2:20, 21; Mdo 16:30, 31; 1The 5:9; 2The 2:14Lakini sisi hatumo miongoni mwa hao wanaositasita na kuangamia, bali tuko miongoni mwa hao wenye imani na hivyo tunaokolewa.

King James Version

Hebrews 10:1-39

1For the law having a shadow of good things to come, and not the very image of the things, can never with those sacrifices which they offered year by year continually make the comers thereunto perfect. 2For then would they not have ceased to be offered? because that the worshippers once purged should have had no more conscience of sins. 3But in those sacrifices there is a remembrance again made of sins every year. 4For it is not possible that the blood of bulls and of goats should take away sins. 5Wherefore when he cometh into the world, he saith, Sacrifice and offering thou wouldest not, but a body hast thou prepared me: 6In burnt offerings and sacrifices for sin thou hast had no pleasure. 7Then said I, Lo, I come (in the volume of the book it is written of me,) to do thy will, O God. 8Above when he said, Sacrifice and offering and burnt offerings and offering for sin thou wouldest not, neither hadst pleasure therein; which are offered by the law; 9Then said he, Lo, I come to do thy will, O God. He taketh away the first, that he may establish the second. 10By the which will we are sanctified through the offering of the body of Jesus Christ once for all. 11And every priest standeth daily ministering and offering oftentimes the same sacrifices, which can never take away sins: 12But this man, after he had offered one sacrifice for sins for ever, sat down on the right hand of God; 13From henceforth expecting till his enemies be made his footstool. 14For by one offering he hath perfected for ever them that are sanctified. 15Whereof the Holy Ghost also is a witness to us: for after that he had said before, 16This is the covenant that I will make with them after those days, saith the Lord, I will put my laws into their hearts, and in their minds will I write them; 17And their sins and iniquities will I remember no more. 18Now where remission of these is, there is no more offering for sin.

19Having therefore, brethren, boldness to enter into the holiest by the blood of Jesus, 20By a new and living way, which he hath consecrated for us, through the veil, that is to say, his flesh; 21And having an high priest over the house of God; 22Let us draw near with a true heart in full assurance of faith, having our hearts sprinkled from an evil conscience, and our bodies washed with pure water. 23Let us hold fast the profession of our faith without wavering; (for he is faithful that promised;) 24And let us consider one another to provoke unto love and to good works: 25Not forsaking the assembling of ourselves together, as the manner of some is; but exhorting one another: and so much the more, as ye see the day approaching. 26For if we sin wilfully after that we have received the knowledge of the truth, there remaineth no more sacrifice for sins, 27But a certain fearful looking for of judgment and fiery indignation, which shall devour the adversaries. 28He that despised Moses’ law died without mercy under two or three witnesses: 29Of how much sorer punishment, suppose ye, shall he be thought worthy, who hath trodden under foot the Son of God, and hath counted the blood of the covenant, wherewith he was sanctified, an unholy thing, and hath done despite unto the Spirit of grace? 30For we know him that hath said, Vengeance belongeth unto me, I will recompense, saith the Lord. And again, The Lord shall judge his people. 31It is a fearful thing to fall into the hands of the living God. 32But call to remembrance the former days, in which, after ye were illuminated, ye endured a great fight of afflictions; 33Partly, whilst ye were made a gazingstock both by reproaches and afflictions; and partly, whilst ye became companions of them that were so used. 34For ye had compassion of me in my bonds, and took joyfully the spoiling of your goods, knowing in yourselves that ye have in heaven a better and an enduring substance. 35Cast not away therefore your confidence, which hath great recompence of reward. 36For ye have need of patience, that, after ye have done the will of God, ye might receive the promise. 37For yet a little while, and he that shall come will come, and will not tarry. 38Now the just shall live by faith: but if any man draw back, my soul shall have no pleasure in him. 39But we are not of them who draw back unto perdition; but of them that believe to the saving of the soul.