Waamuzi 18 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waamuzi 18:1-31

Wadani Wahamia Laishi

118:1 Amu 17:6; Yos 19:47; Amu 1:34Katika siku hizo Israeli walikuwa hawana mfalme.

Katika siku hizo kabila la Wadani walikuwa wanatafuta mahali pao wenyewe pa kuishi, kwa sababu walikuwa hawajafika kwenye urithi wao miongoni mwa makabila ya Israeli. 218:2 Mwa 30:6; Hes 21:32; Yos 2:1; Amu 17:1Hivyo Wadani wakatuma mashujaa watano kutoka Sora na Eshtaoli ili kupeleleza nchi na kuichunguza. Hawa watu waliwakilisha koo zao zote. Waliwaambia, “Nendeni mkaichunguze hiyo nchi.”

Watu hao wakaingia katika nchi ya vilima ya Efraimu, nao wakafika nyumba ya Mika, ambako walilala usiku huo. 318:3 Amu 17:7Walipofika karibu na nyumba ya Mika, waliitambua sauti ya yule kijana Mlawi; hivyo wakaingia humo na kumuuliza, “Ni nani aliyekuleta hapa? Unafanya nini mahali hapa? Kwa nini uko hapa?”

418:4 Amu 17:12Akawaeleza yale Mika aliyomtendea, naye akasema, “Ameniajiri nami ni kuhani wake.”

518:5 Mwa 25:22; Amu 20:18, 23, 27; 1Sam 14:18; 2Sam 5:19; 2Fal 1:2; 8:8Kisha wakamwambia, “Tafadhali tuulizie kwa Mungu kama safari yetu itafanikiwa.”

618:6 1Fal 22:6Yule kuhani akawajibu, “Enendeni kwa amani. Safari yenu ina kibali cha Bwana.”

718:7 Yos 19:47; Mwa 34:25; Yos 11:8Basi hao watu watano wakaondoka na kufika Laishi, mahali ambapo waliwakuta watu wanaishi salama, kama Wasidoni, kwa utulivu na bila mashaka. Nchi yao haikupungukiwa na kitu chochote, hivyo wakawa tajiri. Pia walikaa mbali sana na Wasidoni, wala hawakushughulika na mtu yeyote.

8Waliporudi kwa ndugu zao huko Sora na Eshtaoli, ndugu zao wakawauliza, “Mlionaje mambo huko?”

918:9 Hes 13:30; 1Fal 22:3Wakajibu, “Twendeni, tukapigane nao! Tumeona kuwa nchi ni nzuri sana. Je, hamtafanya chochote? Msisite kupanda ili kuimiliki. 1018:10 Kum 8:9; 1Nya 4:40Mtakapokwenda huko mtakuta watu waliotulia walio salama, nayo nchi hiyo ni kubwa na Mungu ameitia mikononi mwenu, nayo ni nchi ambayo haikupungukiwa na kitu chochote kilicho duniani.”

1118:11 Amu 13:2Ndipo watu 600 toka ukoo wa Wadani, waliojifunga silaha za vita, wakaondoka Sora na Eshtaoli. 1218:12 Yos 9:17; Amu 13:25Walipokuwa wakisafiri wakapiga kambi huko Kiriath-Yearimu katika Yuda. Hii ndiyo sababu sehemu ya magharibi ya Kiriath-Yearimu inaitwa Mahane-Dani18:12 Mahane-Dani maana yake Kambi ya Dani. mpaka leo. 1318:13 Amu 17:6Kutoka hapo wakaendelea mbele mpaka nchi ya vilima ya Efraimu na kufika katika nyumba ya Mika.

1418:14 Yos 19:47; Amu 8:27; Mwa 31:19; Amu 17:5Ndipo wale watu watano waliopeleleza nchi ya Laishi wakawaambia ndugu zao, “Je, mwajua kuwa mojawapo ya nyumba hizi kuna naivera, sanamu ndogo za nyumbani, sanamu ya kuchonga na sanamu ya kusubu? Sasa basi fikirini mtakalofanya.” 15Basi wakaingia humo na kwenda kwenye nyumba ya yule kijana Mlawi katika nyumba ya Mika na kumsalimu. 16Wale Wadani 600, waliovaa silaha za vita, wakasimama penye ingilio la lango. 1718:17 Mwa 31:19; Mik 5:13Wale watu watano waliokwenda kupeleleza nchi wakaingia ndani na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani pamoja na ile sanamu ya kusubu, wakati yule kuhani akiwa amesimama pale penye ingilio la lango pamoja na wale watu 600 waliokuwa wamejifunga silaha za vita.

1818:18 Isa 46:2; Yer 43:11; 48:7; 49:3; Hos 10:5; Mwa 31:19Hao watu walipoingia katika nyumba ya Mika na kuchukua ile sanamu ya kuchonga, ile naivera, na zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, pamoja na ile sanamu ya kusubu, yule kuhani akawauliza, “Mnafanya nini?”

1918:19 Ay 13:5; 21:5; 29:9; 40:4; Isa 52:15; Mik 7:16; Amu 17:10; Hes 26:42Wakamjibu, “Nyamaza kimya! Weka mkono wako juu ya kinywa chako na ufuatane nasi, uwe baba yetu na kuhani wetu. Si ni afadhali utumikie kabila na ukoo katika Israeli kama kuhani kuliko kumtumikia mtu mmoja na watu wa nyumbani mwake?” 20Yule kuhani akafurahi. Akachukua ile naivera, zile sanamu nyingine ndogo za nyumbani, na sanamu ya kuchonga, naye akaenda pamoja na wale watu. 21Ndipo wakageuka na kuondoka wakiwatanguliza mbele watoto wao wadogo, wanyama wao wa kufugwa na mali zao.

22Walipokuwa wamesafiri umbali kidogo toka nyumbani kwa Mika, watu walioishi karibu na Mika wakaitwa wakakusanyika pamoja, nao wakawafikia Wadani. 23Walipofuatilia wakipiga kelele Wadani wakawageukia na kumwambia Mika, “Una nini wewe hata ukaja na kundi la watu namna hii ili kupigana?”

24Akawajibu, “Mmechukua miungu yote niliyoitengeneza, mkachukua na kuhani wangu, nanyi mkaondoka. Nimebaki na nini kingine? Mnawezaje kuniuliza, ‘Una nini wewe?’ ”

25Wadani wakamjibu, “Usibishane na sisi, la sivyo watu wenye hasira kali watakushambulia, nawe na watu wa nyumbani mwako mtapoteza maisha.” 2618:26 2Sam 3:39; Za 18:17; 35:10Basi Wadani wakaenda zao, naye Mika alipoona kuwa wana nguvu kumliko yeye, akageuka na kurudi nyumbani kwake.

2718:27 Mwa 34:25; Hes 31:10; Mwa 49:17; Yos 19:47Kisha wakachukua vile Mika alivyokuwa ametengeneza, na kuhani wake, wakaendelea hadi Laishi, dhidi ya watu walio na amani, wasiokuwa na wasiwasi. Wakawashambulia kwa upanga na kuuteketeza mji wao kwa moto. 28Hapakuwa na yeyote wa kuwaokoa, kwa kuwa kulikuwa mbali sana na Sidoni na hawakuwa na ushirikiano na mtu mwingine yeyote. Mji ulikuwa kwenye bonde karibu na Beth-Rehobu.

Wadani wakaujenga upya huo mji na kuishi humo. 29Wakauita ule mji Dani kwa kufuata jina la baba yao aliyezaliwa na Israeli, ingawa mji huo ulikuwa ukiitwa Laishi hapo kwanza. 3018:30 Kut 2:22; Amu 17:3-5Kisha Wadani wakajisimamishia sanamu ile ya kuchonga, naye Yonathani mwana wa Gershomu, mwana wa Mose pamoja na wanawe walikuwa makuhani wa kabila la Wadani mpaka nchi hiyo ilipotekwa. 3118:31 Amu 19:18; 20:18; Yos 18:1; Yer 7:14Wakaisimamisha na kuiabudu hiyo sanamu ya kuchonga ya Mika aliyokuwa ameitengeneza, wakati wote ule nyumba ya Mungu ilipokuwa huko Shilo.

Swedish Contemporary Bible

Domarboken 18:1-31

Mikas avgudar blir stulna

1Det fanns inte någon kung i Israel vid den här tiden. Daniterna försökte fortfarande hitta en plats att slå sig ner på, för de hade ännu inte fått ett eget område bland Israels stammar. 2De valde ut fem tappra män från Sora och Eshtaol att spionera på landet där de skulle bo. De representerade varje släkt i stammen och uppmanades att gå och utforska landet. När de kom till Efraims bergsbygd, stannade de i Mikas hem över natten. 3De lade märke till den unge levitens dialekt och tog honom avsides och frågade: ”Vem förde dig hit? Vad gör du här? Varför har du kommit hit?” 4Då berättade han för dem om vad Mika gjort för honom och att han var dennes personlige präst.

5”Då kan du väl fråga Gud om vår resa kommer att lyckas”, bad de honom. 6”Ja”, svarade prästen. ”Ni kan lugnt gå. Herren kommer att ta hand om er.”

7De fem männen fortsatte och kom till Lajish där de lade märke till hur trygga alla verkade vara. Människorna där uppträdde precis som de lugna och säkra sidonierna. Dessutom saknades ingenting i landet utan de var rika. De levde lugnt och fredligt och bodde långt från Sidon och hade mycket liten eller ingen kontakt med andra människor.

8De fem spionerna återvände så småningom till sitt folk i Sora och Eshtaol. ”Nå, hur var det? Vad säger ni?” frågade man dem.

9Männen svarade: ”Låt oss gå till anfall! Vi har sett landet och det är rikt. Det är bara för oss att inta det. Tveka inte! Inta det! 10När ni kommer dit, kommer ni till ett folk som lever i trygghet och ett land där det finns gott om plats. Gud har gett oss detta land där ingenting saknas.”

11Så drog sexhundra beväpnade män ur Dans stam ut från Sora och Eshtaol. 12De slog läger vid Kirjat-Jearim i Juda och den platsen kallas än i dag för Dans läger. Det ligger väster om Kirjat-Jearim. 13Sedan fortsatte de till Efraims bergsbygd och kom till Mikas hus.

14De fem som varit och spionerat i landet sa till de övriga: ”Det finns en efod därinne, husgudar och en snidad och gjuten gudabild. Det är ju självklart vad ni ska göra!”

15De gick fram till den unge leviten Mikas hus och hälsade på honom. 16De sexhundra beväpnade daniterna ställde sig vid ingången. 17Sedan gick de fem fram som varit och spionerat där och lade beslag på den snidade gudabilden, efoden, husgudarna och den gjutna gudabilden. Prästen stod vid ingången tillsammans med de sexhundra beväpnade männen.

18De fem gick in i Mikas hus och tog den snidade gudabilden, efoden, husgudarna och den gjutna gudabilden. ”Vad gör ni?” frågade prästen.

19”Var tyst och följ med oss”, sa de. ”Bli fader och präst åt oss i stället! Är det inte bättre för dig att vara präst åt en hel stam i Israel än åt bara en enda man i hans privata hus?”

20Prästen blev då mycket glad åt att få följa med dem och han tog med efoden, husgudarna och den snidade avgudabilden. 21De fortsatte sedan sin vandring med barnen, boskapen och de mest värdefulla ägodelarna främst i kolonnen.

22När de hunnit en bit på väg från Mikas hem, kom Mika och hans grannar efter dem 23och ropade till dem att stanna. Daniterna vände sig då till honom och frågade: ”Vad menar du med att förfölja oss på det här sättet?” 24Mika svarade: ”Ni har tagit med er alla mina gudar som jag låtit göra och min präst och jag har ingenting kvar. Sedan undrar ni vad det är fråga om!”

25”Vi vill inte höra ett ord till från dig”, svarade männen. ”Annars kan det hända att någon ilsknar till och dödar dig och er allesammans.”

26De fortsatte sin färd och när Mika såg att de var starkare än han, vände han om hem.

27De nådde snart fram till Lajish med föremålen som Mika hade gjort och med hans präst. De dödade det intet ont anande folket med svärd och brände sedan ner staden. 28Ingen kom för att hjälpa invånarna i staden, för de bodde alldeles för långt borta från Sidon och de hade inte kontakt med andra människor.

Staden låg i dalen nära Bet-Rechov. Dans män byggde upp staden igen och bosatte sig där. 29Staden fick namnet Dan efter deras förfader, Israels son, men ursprungligen hette den Lajish.

30De satte upp avgudabilden och utvalde Jonatan, Gershoms son och Moses18:30 I en del handskrifter och tidiga översättningar Manasse, som var en avfällig kung (2 Kung 21:1-7), möjligen ändrad av fromma skrivare som inte kunde förknippa namnet Mose med en avgudakult. sonson, att tillsammans med sina söner bli deras präster ända till dess att folket blev förvisat 31och Mikas avgudastaty, som de ställde upp, tillbads av Dans stam så länge Guds helgedom var kvar i Shilo.