Waamuzi 16 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waamuzi 16:1-31

Samsoni Na Delila

116:1 Amu 16:28; Mwa 10:19; 38:15Siku moja Samsoni alienda Gaza, akamwona mwanamke kahaba, naye akaingia kwake. 216:2 Yos 2:5; 1Sam 19:11; Mdo 9:24Watu wa Gaza wakaambiwa, “Samsoni amekuja huku!” Hivyo wakapazingira mahali pale nao wakamvizia usiku kucha, penye lango la mji. Wakanyamaza kimya usiku kucha, wakisema, “Tumvizie hadi mapambazuko, ndipo tutamuua.”

316:3 Yos 10:36Samsoni akalala mpaka usiku wa manane. Akaondoka katikati ya usiku, akashika milango ya lango la mji pamoja na miimo yake miwili, akaingʼoa, makomeo yake na vyote. Akaviweka mabegani mwake na kuvipeleka mpaka kwenye kilele cha mlima ule unaokabili Hebroni.

416:4 Mwa 24:67; 34:3Baada ya hayo akampenda mwanamke mmoja katika Bonde la Soreki aliyeitwa Delila. 516:5 Yos 13:3; Kut 10:7; Amu 14:15Viongozi wa Wafilisti wakamwendea yule mwanamke na kumwambia, “Umbembeleze ili upate kujua siri za nguvu zake zilizo nyingi na jinsi tutakavyoweza kumshinda ili tuweze kumfunga na kumtiisha. Nasi kila mmoja wetu tutakupa shekeli 1,100 za fedha.”16:5 Shekeli 1,100 za fedha ni sawa na kilo 13 za fedha.

6Hivyo Delila akamwambia Samsoni, “Naomba niambie siri ya hizi nguvu zako nyingi na jinsi utakavyoweza kufungwa ili kukutiisha.”

7Samsoni akamjibu, “Kama wakinifunga kwa kamba saba za upinde ambazo hazijakauka bado, hapo ndipo nitakapokuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.”

8Viongozi wa Wafilisti wakamletea yule mwanamke kamba saba za upinde ambazo hazijakauka bado, akamfunga nazo Samsoni. 9Wakati watu wakiwa wanamvizia katika chumba cha ndani, yule mwanamke akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Lakini yeye akazikata zile kamba za upinde, kama vile uzi wa pamba unapoguswa na moto. Hivyo siri ya nguvu zake haikujulikana.

10Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Umenifanyia mzaha na kuniambia uongo. Tafadhali niambie waweza kufungwa kwa kitu gani?”

1116:11 Amu 15:13Akamwambia, “Wakinifunga kwa uthabiti kwa kamba mpya ambazo hazijatumika, basi nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.”

12Hivyo Delila akachukua kamba mpya na kumfunga nazo. Kisha akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Wale watu waliokuwa wanamvizia walikuwa katika chumba cha ndani. Lakini akazikata zile kamba zilizokuwa zimefunga mikono yake kama akatavyo uzi.

13Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Mpaka sasa, umenifanyia mzaha na kuniambia uongo. Nieleze ni jinsi gani utakavyoweza kufungwa.”

Samsoni akamwambia, “Kama ukivisuka hivi vishungi saba vya nywele za kichwa changu katika mtande wa nguo na kukaza kwa msumari, ndipo nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote.” Hivyo Samsoni alipokuwa amelala, Delila akachukua vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake na kuvifunga kwenye mtande wa nguo, 14na kuvikaza kwa msumari.

Kisha akamwambia, “Samsoni, Wafilisti wanakujia!” Lakini akaamka kutoka usingizini na kuungʼoa ule msumari na ule mtande.

1516:15 Hes 24:10; Amu 14:16Ndipo Delila akamwambia, “Wawezaje kusema, ‘Nakupenda,’ wakati moyo wako haupo pamoja nami? Umenifanyia mzaha mara hizi tatu na hujaniambia siri ya hizi nguvu zako nyingi.” 16Hatimaye, baada ya kuwa anamsumbua kwa maneno siku kwa siku na kumuudhi, roho yake ikataabika hata kufa.

1716:17 Hes 6:2; 15:9; Amu 13:5Hivyo akamwambia yule mwanamke siri yake yote, akamwambia, “Wembe haujapita kamwe kichwani mwangu, kwa kuwa mimi ni Mnadhiri wa Mungu tangu tumboni mwa mama yangu. Kama nywele za kichwa changu zikinyolewa, nguvu zangu zitanitoka, na nitakuwa dhaifu kama mtu mwingine yeyote!”

1816:18 Yos 13:3; 1Sam 5:8Delila alipoona kuwa amemweleza siri yake yote, akatuma ujumbe kwa viongozi wa Wafilisti na kusema, “Njooni tena mara nyingine, maana amenieleza siri yake yote.” Basi viongozi wa Wafilisti wakaja kwa Delila, wakiwa na fedha mikononi mwao. 1916:19 Mit 7:26-27Delila akamfanya alale usingizi magotini pake, akamwita mtu akamnyoa vile vishungi saba vya nywele za kichwa chake. Akaanza kumsumbua ili aamke nazo nguvu zake zikamtoka.

2016:20 Hes 14:42; Yos 7:12; 1Sam 16:14; 18:12; 28:15Yule mwanamke akamwita, “Samsoni, hao Wafilisti wanakujia!”

Akaamka toka usingizini akasema, “Nitatoka nje kama hapo awali, nitawakungʼutia mbali na kuwa huru.” Lakini hakujua kuwa Bwana amemwacha.

2116:21 Yer 47:1; Hes 16:14; Mwa 10:19; Ay 31:10; Isa 47:2Basi Wafilisti wakamkamata, wakamngʼoa macho yake, wakamchukua wakamteremsha mpaka Gaza. Wakiwa wamemfunga kwa pingu za shaba, wakamweka ili asage ngano huko gerezani. 22Wakati huo nywele za kichwa chake zikaanza kukua tena baada ya kunyolewa.

Kifo Cha Samsoni

2316:23 1Sam 5:3; 1Nya 10:10Basi viongozi wa Wafilisti wakakusanyika pamoja ili kutoa kafara kwa mungu wao Dagoni na kufanya karamu, wakisema, “Mungu wetu amemtia adui yetu Samsoni mikononi mwetu.”

2416:24 Dan 5:4; 1Sam 31:9; 1Nya 10:9Watu walipomwona Samsoni wakamsifu mungu wao, wakisema:

“Sasa mungu wetu amemtia adui yetu

mikononi mwetu,

yule aliyeharibu nchi yetu

na kuwaua watu wengi miongoni mwetu.”

2516:25 Amu 9:27; 19:6-9, 22; Rut 3:7; Es 1:10Mioyo yao ilipokuwa imefurahishwa wakasema, “Mleteni Samsoni aje acheze ili tufurahi.” Basi wakamleta Samsoni kutoka mle gerezani naye akacheza mbele yao.

Wakamweka kati ya nguzo mbili. 26Samsoni akamwambia mtumishi aliyeshika mkono wake, “Niweke mahali ambapo ninaweza kuzigusa nguzo ambazo zinategemeza jengo ili nipate kuziegemea.” 2716:27 Yos 2:8; Kum 22:8Basi lile jengo lilikuwa na wingi wa watu waume kwa wake; viongozi wote wa Wafilisti walikuwamo humo, na kwenye sakafu ya juu walikuwepo watu 3,000 waume kwa wake, waliokuwa wakimtazama Samsoni wakati anacheza. 2816:28 Yos 15:18; Yer 15:15Ndipo Samsoni akamwomba Bwana, akasema, “Ee Bwana Mwenyezi, unikumbuke. Ee Mungu, nakusihi ukanitie nguvu mara hii moja tena, ili kwa tendo hili nipate kulipiza kisasi juu ya Wafilisti kwa ajili ya macho yangu mawili.” 29Ndipo Samsoni akazikaribia zile nguzo mbili za katikati ambazo lile jengo lilikuwa linazitegemea. Akazishika moja kwa mkono wa kuume na nyingine mkono wa kushoto. 30Samsoni akasema, “Nife pamoja na Wafilisti!” Ndipo akazisukuma zile nguzo kwa nguvu zake zote, lile jengo likaanguka juu ya viongozi na watu wote waliokuwamo mle ndani yake. Hivyo akawaua watu wengi wakati wa kufa kwake kuliko siku za uhai wake.

3116:31 Amu 13:2; Rut 1:1; 1Sam 7:6; Amu 15:20Basi ndugu zake na jamaa yote ya baba yake wakateremka kwenda kumchukua. Wakampandisha na kumzika kati ya Sora na Eshtaoli kwenye kaburi la Manoa baba yake. Naye Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka ishirini.

New International Reader’s Version

Judges 16:1-31

Samson and Delilah

1One day Samson went to Gaza. There he saw a prostitute. He went in to spend the night with her. 2The people of Gaza were told, “Samson is here!” So they surrounded the place. They hid and waited for him at the city gate all night long. They didn’t make any move against him during the night. They said, “Let’s wait until the sun comes up. Then we’ll kill him.”

3But Samson stayed there only until the middle of the night. Then he got up. He took hold of the doors of the city gate. He also took hold of the two doorposts. He tore them loose, together with their metal bar. He picked them up and put them on his shoulders. Then he carried them to the top of the hill that faces Hebron.

4Some time later, Samson fell in love again. The woman lived in the Valley of Sorek. Her name was Delilah. 5The rulers of the Philistines went to her. They said, “See if you can get him to tell you the secret of why he’s so strong. Find out how we can overpower him. Then we can tie him up. We can bring him under our control. Each of us will give you 28 pounds of silver.”

6So Delilah said to Samson, “Tell me the secret of why you are so strong. Tell me how you can be tied up and controlled.”

7Samson answered her, “Let someone tie me up with seven new bowstrings. They must be strings that aren’t completely dry. Then I’ll become as weak as any other man.”

8So the Philistine rulers brought seven new bowstrings to her. They weren’t completely dry. Delilah tied Samson up with them. 9Men were hiding in the room. She called out to him, “Samson! The Philistines are attacking you!” But he snapped the bowstrings easily. They were like pieces of string that had come too close to a flame. So the secret of why he was so strong wasn’t discovered.

10Delilah spoke to Samson again. “You have made me look foolish,” she said. “You told me a lie. Come on. Tell me how you can be tied up.”

11Samson said, “Let someone tie me tightly with new ropes. They must be ropes that have never been used. Then I’ll become as weak as any other man.”

12So Delilah got some new ropes. She tied him up with them. Men were hiding in the room. She called out to him, “Samson! The Philistines are attacking you!” But he snapped the ropes off his arms. They fell off just as if they were threads.

13Delilah spoke to Samson again. “All this time you have been making me look foolish,” she said. “You have been telling me lies. This time really tell me how you can be tied up.”

He replied, “Weave the seven braids of my hair into the cloth on a loom. Then tighten the cloth with a pin. If you do, I’ll become as weak as any other man.” So while Samson was sleeping, Delilah took hold of the seven braids of his hair. She wove them into the cloth on a loom. 14Then she tightened the cloth with a pin.

Again she called out to him, “Samson! The Philistines are attacking you!” He woke up from his sleep. He pulled up the pin and the loom, together with the cloth.

15Then she said to him, “How can you say, ‘I love you’? You won’t even share your secret with me. This is the third time you have made me look foolish. And you still haven’t told me the secret of why you are so strong.” 16She continued to pester him day after day. She nagged him until he was sick and tired of it.

17So he told her everything. He said, “My hair has never been cut. That’s because I’ve been a Nazirite since the day I was born. A Nazirite is set apart to God. If you shave my head, I won’t be strong anymore. I’ll become as weak as any other man.”

18Delilah realized he had told her everything. So she sent a message to the Philistine rulers. She said, “Come back one more time. He has told me everything.” So the rulers returned. They brought the silver with them. 19Delilah got Samson to go to sleep on her lap. Then she called for someone to shave off the seven braids of his hair. That’s how she began to bring Samson under her control. And he wasn’t strong anymore.

20She called out, “Samson! The Philistines are attacking you!”

He woke up from his sleep. He thought, “I’ll go out just as I did before. I’ll shake myself free.” But he didn’t know that the Lord had left him.

21Then the Philistines grabbed him. They poked his eyes out. They took him down to Gaza. They put bronze chains around him. Then they made him grind grain in the prison. 22His head had been shaved. But the hair on it began to grow again.

Samson Dies

23The rulers of the Philistines gathered together. They were going to offer a great sacrifice to their god Dagon. They were going to celebrate. They said, “Our god has handed our enemy Samson over to us.”

24When the people saw Samson, they praised their god. They said,

“Our god has handed our enemy over to us.

Our enemy has destroyed our land.

He has killed large numbers of our people.”

25After they had drunk a lot of wine, they shouted, “Bring Samson out. Let him put on a show for us.” So they called Samson out of the prison. He put on a show for them.

They had him stand near the temple pillars. 26Then he spoke to the servant who was holding his hand. He said, “Put me where I can feel the pillars. I’m talking about the ones that hold up the temple. I want to lean against them.” 27The temple was crowded with men and women. All the Philistine rulers were there. About 3,000 men and women were on the roof. They were watching Samson put on a show. 28Then he prayed to the Lord. Samson said, “Lord and King, show me that you still have concern for me. Please, God, make me strong just one more time. Let me pay the Philistines back for what they did to my two eyes. Let me do it with only one blow.” 29Then Samson reached toward the two pillars that were in the middle of the temple. They were the ones that held up the temple. He put his right hand on one of them. He put his left hand on the other. He leaned hard against them. 30Samson said, “Let me die together with the Philistines!” Then he pushed with all his might. The temple came down on the rulers. It fell on all the people in it. So Samson killed many more Philistines when he died than he did while he lived.

31Then his brothers went down to get him. So did his father’s whole family. All of them brought Samson back home. They buried him in the tomb of his father Manoah. It’s between Zorah and Eshtaol. Samson had led Israel for 20 years.