Waamuzi 11 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waamuzi 11:1-40

111:1 Amu 12:1; 1Sam 12:11; Ebr 11:32; Amu 6:12; Hes 26:29; Mwa 38; 15Basi Yefta Mgileadi alikuwa mtu shujaa. Baba yake alikuwa Gileadi, naye mama yake alikuwa kahaba. 2Mke wa Gileadi akamzalia wana wengine, nao watoto hao walipokua, wakamfukuza Yefta na kumwambia, “Wewe huwezi kupata urithi katika jamii yetu, kwa sababu wewe ni mwana wa mwanamke mwingine.” 311:3 2Sam 10:6-8; Amu 9:4Basi Yefta akawakimbia ndugu zake akaenda kuishi katika nchi ya Tobu, mahali ambako watu waasi walijiunga naye na kumfuata.

411:4 Amu 10:9Baada ya muda Waamoni wakafanya vita na Israeli, 5viongozi wa Gileadi wakaenda kumchukua Yefta katika nchi ya Tobu. 6Wakamwambia Yefta, “Uwe jemadari wetu, ili tuweze kupigana na Waamoni.”

711:7 Mwa 26:16, 27Yefta akawaambia, “Je, hamkunichukia mimi na kunifukuza katika nyumba ya baba yangu? Kwa nini mnanijia sasa, wakati mna matatizo.”

811:8 Amu 10:18Viongozi wa Gileadi wakamwambia Yefta, “Lakini sasa tumegeuka kukuelekea wewe, ili uende pamoja nasi kupigana na Waamoni, nawe utakuwa kiongozi wetu juu ya watu wote wa Gileadi.”

9Yefta akawaambia, “Ikiwa mtanirudisha kwetu kupigana na Waamoni, naye Bwana akanisaidia kuwashinda, Je, ni kweli nitakuwa kiongozi wenu?”

1011:10 Mwa 31:50; Isa 1:2; Yer 42:5Viongozi wa Gileadi wakamjibu Yefta, “Bwana ndiye shahidi yetu. Kwa hakika tutafanya kama usemavyo.” 1111:11 1Sam 9:4; 2Sam 3:17; Kut 19:9; 1Sam 8; 21; Yos 11:3Basi Yefta akaenda na viongozi wa Gileadi, nao watu wakamfanya kiongozi na jemadari wao. Naye akarudia maneno yake yote mbele za Bwana huko Mispa.

12Ndipo Yefta akatuma wajumbe kwa mfalme wa Waamoni akisema, “Una nini juu yetu, hata umekuja kushambulia nchi yetu?”

1311:13 Hes 21:13; 21:24; Mwa 32:22Mfalme wa Waamoni akawajibu wajumbe wale wa Yefta, “Wakati Waisraeli walipopanda kutoka Misri, waliichukua nchi yangu kuanzia Arnoni mpaka Yaboki, hadi kufikia Yordani. Sasa rudisha kwa amani.”

14Yefta akarudisha wajumbe kwa mfalme wa Waamoni, 1511:15 Kum 2:9; 1:19kusema:

“Hili ndilo asemalo Yefta, Israeli hawakuchukua nchi ya Moabu wala ya Waamoni. 1611:16 Hes 14:25; Kum 1:40; Mwa 14:7; Hes 20:1Lakini walipopanda kutoka Misri, Israeli walipitia katika jangwa hadi Bahari ya Shamu na wakafika Kadeshi. 1711:17 Mwa 32:3; Hes 20:14-17; Yer 48:1; Yos 24:9Ndipo Israeli wakatuma wajumbe kwa mfalme wa Edomu, wakisema, ‘Tupe ruhusa kupita katika nchi yako,’ Lakini mfalme wa Edomu hakutusikia. Wakapeleka pia wajumbe kwa mfalme wa Moabu, naye akakataa. Kwa hiyo Israeli wakakaa huko Kadeshi.

1811:18 Hes 20:21; Kum 2:8; Hes 21:13; 21:4“Baadaye wakasafiri kupitia jangwa, wakiambaa na nchi za Edomu na Moabu, wakapitia upande wa mashariki wa nchi ya Moabu na kupiga kambi upande mwingine wa Arnoni. Hawakuingia katika nchi ya Moabu, kwa kuwa Arnoni ilikuwa mpaka wake.

1911:19 Hes 21:21-22; Yos 12:2; Kum 2:26-27“Kisha Israeli wakatuma wajumbe kwa Sihoni mfalme wa Waamori, aliyetawala Heshboni, na kumwambia, ‘Tupe ruhusa kupita katika nchi yako ili kufikia mahali petu.’ 2011:20 Hes 21:23; Kum 2:32Hata hivyo, Sihoni hakuwaamini Waisraeli kupita katika nchi yake. Akaandaa jeshi lake lote na kupiga kambi huko Yahasa, nao wakapigana na Israeli.

21“Ndipo Bwana, Mungu wa Israeli, akamtia Sihoni na watu wake wote mikononi mwa Israeli, nao wakawashinda. Israeli wakaitwaa nchi yote ya Waamori, waliokuwa wakiishi katika nchi hiyo, 2211:22 Hes 21:21-22; Kum 2:36wakiiteka nchi yote kuanzia Arnoni mpaka Yaboki, na kutoka jangwani mpaka Yordani.

23“Basi kwa kuwa Bwana, Mungu wa Israeli, amewafukuza Waamori watoke mbele ya watu wake Israeli, wewe unayo haki gani ya kuitamalaki? 2411:24 Hes 21:29; Yos 3:10; Kum 2:3; 1Fal 11:7Je, haikupasi kuchukua kile ambacho mungu wako Kemoshi amekupa? Vivyo hivyo, chochote kile Bwana Mungu wetu alichotupa sisi, tutakimiliki. 2511:25 Hes 22:2; Yos 24:9Je, wewe ni bora kuliko Balaki mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu? Je, yeye alishagombana na Israeli au kupigana nao wakati wowote? 2611:26 Hes 21:25; 32:34; Yos 13:9Kwa maana kwa miaka 300 Israeli wameishi Heshboni na vijiji vyake, Aroeri na vijiji vyake, na katika miji yote iliyo kando ya Arnoni. Kwa nini wewe haukuyachukua wakati huo? 2711:27 Mwa 18:25; 16:5; 2Nya 20; 12; Mwa 31:53; 1Sam 24:12-15Mimi sijakukosea jambo lolote, bali wewe ndiye unayenikosea kwa kufanya vita nami. Basi Bwana, aliye Mwamuzi, leo na aamue ugomvi kati ya Waisraeli na Waamoni.”

28Hata hivyo, Mfalme wa Waamoni, hakuyajali maneno ya ujumbe wa Yefta.

2911:29 Amu 3:10; Mwa 31:49; Amu 10:17; Hes 11:25; Isa 11; 2Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya Yefta. Akapita katikati ya Gileadi na Manase, pia akapita katika Mispa ya Gileadi, na kutokea huko akasonga mbele kushambulia Waamoni. 3011:30 Mwa 28:20; Hes 30:10; 1Sam 1:11; Mit 31:2Naye Yefta akaweka nadhiri mbele za Bwana akisema, “Ikiwa utawatia Waamoni mikononi mwangu, 3111:31 Mwa 28:21; 8:20; Law 1:3; Amu 13:16chochote kile kitakachotoka katika mlango wa nyumba yangu cha kwanza ili kunilaki nirudipo kwa amani katika kuwashinda Waamoni, kitakuwa ni cha Bwana na nitakitoa kuwa sadaka ya kuteketezwa.”

32Ndipo Yefta akavuka kupigana na hao Waamoni, naye Bwana akawatia mkononi mwake. 3311:33 Eze 27:17Akawapiga kwa ushindi mkubwa kuanzia Aroeri mpaka karibu na Minithi na kuendelea mpaka Abel-Keramimu, miji yote iliyopigwa ni ishirini. Basi Israeli wakawashinda Waamoni.

3411:34 Kut 15:20; Mwa 31:27; Yer 31:4; Zek 12; 10Yefta aliporudi nyumbani Mispa, tazama, binti yake akatoka ili kumlaki kwa matari na kucheza. Alikuwa ndiye mtoto pekee, hakuwa na mwana wala binti mwingine. 3511:35 Hes 14:6; 30:2; Kum 23:21; Mhu 5:2-5Alipomwona akararua mavazi yake akalia, “Ee! Binti yangu! Umenifanya niwe na huzuni na kunyongʼonyea sana, kwa kuwa nimeweka nadhiri kwa Bwana, ambayo siwezi kuivunja.”

3611:36 Lk 1:38; Hes 31:3; 2Sam 18:19Akajibu, “Baba yangu, umetoa neno lako kwa Bwana. Nitendee mimi kama vile ulivyoahidi, kwa kuwa Bwana amekupa ushindi dhidi ya adui zako Waamoni.” 37Naye akamwambia baba yake, “Naomba nifanyiwe jambo hili. Nipewe miezi miwili ili kuzunguka vilimani nikaulilie ubikira wangu, mimi na wenzangu.”

38Baba yake akamwambia, “Waweza kwenda.” Naye akamwacha aende kwa miezi miwili. Hivyo akaondoka pamoja na wasichana wenzake, naye akaulilia ubikira wake huko vilimani kwa sababu asingeolewa kamwe. 39Baada ya hiyo miezi miwili, alirejea kwa baba yake, naye baba yake akamtendea kama alivyokuwa ametoa nadhiri yake. Naye alikuwa bikira.

Nayo ikawa desturi katika Israeli, 40kwamba kila mwaka binti wa Israeli huenda kwa siku nne ili kumkumbuka huyo binti wa Yefta, Mgileadi.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

士師記 11:1-40

士師耶弗他

1基列耶弗他是個英勇的戰士,他父親名叫基列,母親是個妓女。 2基列的妻子還生了幾個兒子,他們長大後,便把耶弗他趕出家門,說:「你是別的女人生的,你休想繼承我們父親的任何產業。」 3耶弗他只好逃走,住在陀伯地區。有一群匪徒跟隨了他。

4後來,亞捫人攻打以色列5基列的眾長老就去陀伯耶弗他6對他說:「請你回來做統帥帶領我們對抗亞捫人。」 7耶弗他說:「從前你們不是厭惡我,把我從父親家趕走的嗎?現在你們遭難,為什麼來找我?」 8基列的眾長老說:「現在我們是來請你跟我們一起回去抵抗亞捫人,你可以做所有基列人的首領。」 9耶弗他說:「如果我跟你們回去與亞捫人作戰,耶和華讓我打敗他們,我就真的可以做你們的首領嗎?」 10基列的首領們說:「我們必聽從你的吩咐,有耶和華為我們作證。」 11於是,耶弗他便跟他們一起回去。民眾擁立他做他們的首領和元帥。耶弗他米斯巴將之前所說的話在耶和華面前重申一遍。

12然後,他派遣使者去問亞捫王:「你與我有什麼相干?為什麼要攻打我的領土?」 13亞捫王對他的使者說:「因為以色列人從埃及出來的時候佔據了我們的土地——從亞嫩河到雅博河,一直到約旦河。現在你們要乖乖地把這些土地還給我們。」 14耶弗他再差遣使者去見亞捫王, 15對他說:「以色列人並沒有佔據摩押亞捫的土地。 16當年以色列人離開埃及,經曠野渡過海來到加低斯17然後派遣使者去見以東王,說,『求你讓我們經過你的領土。』以東王卻不答應。他們又派遣使者去見摩押王,摩押王也不答應。於是,以色列人就住在加低斯18後來,他們走過曠野,繞過以東摩押,到了摩押的東邊,在摩押的邊界亞嫩河東岸紮營,並沒有進入摩押境內。 19以色列人派遣使者去見希實本亞摩利西宏,對他說,『求讓我們經過你的領土前往我們自己的土地。』 20西宏不信任以色列人,拒絕了他們的請求,並招聚全軍駐紮在雅雜,攻打他們。 21以色列的上帝耶和華幫助以色列人戰勝西宏和他的軍隊,佔領了他們所有的土地, 22亞嫩河直到雅博河,從曠野直到約旦河。 23既然是以色列的上帝耶和華為祂的以色列子民趕走了亞摩利人,你憑什麼要奪取這塊土地? 24你擁有你們的神明基抹給你們的土地,我們也要擁有我們的上帝耶和華賜給我們的土地。 25難道你比摩押西撥的兒子巴勒更強嗎?他從未挑戰過以色列人,也未和以色列人交過戰。 26三百年來,以色列人一直住在希實本及其周圍的鄉村、亞羅珥及其周圍的鄉村和亞嫩河沿岸一帶的城邑。在這期間,你們為什麼不收回這些土地呢? 27我們沒有得罪你們,你們卻攻打我們。願審判者耶和華今天在以色列人和亞捫人之間主持公道。」 28可是,亞捫王不理會耶弗他派使者所傳的話。

29那時,耶和華的靈降在耶弗他身上,他便經過基列瑪拿西,來到基列米斯巴,然後從那裡去迎戰亞捫人。 30他向耶和華許願說:「如果你把亞捫人交在我手中, 31讓我凱旋而歸,第一個從我家門出來迎接我的人必歸給你,我必把他獻給你作燔祭。」 32於是,耶弗他率軍與亞捫人作戰,耶和華把敵人交在他手中, 33他大敗敵軍,摧毀了從亞羅珥米匿、遠至亞備勒·基拉明的二十座城。這樣,以色列人征服了亞捫人。

34耶弗他返回自己在米斯巴的家,他的獨生女兒敲著鼓、跳著舞出來迎接他。 35他一見自己的女兒,便撕裂衣服,說:「唉,我的女兒啊,你真讓我傷心欲絕!我向耶和華許了願,不能收回了!」 36他女兒說:「父親啊,你既然向耶和華許了願,就照你許的願對待我吧!因為耶和華幫你打敗了敵軍亞捫人,為你報了仇。 37但求你先給我兩個月的時間,讓我和同伴到山上去為我終身未嫁哀哭。」 38耶弗他答應了,給了她兩個月的時間。於是,她便和同伴到山上為自己終身未嫁哀哭。 39兩個月後,她回到父親那裡。她父親履行了自己所許的願。她終身未嫁。自此以後,在以色列有個習俗: 40每年以色列的女子都去為基列耶弗他的女兒哀哭四天。