Ufunuo 19 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 19:1-21

Shangwe Huko Mbinguni

119:1 Ufu 11:15; 7:10; 4:11Baada ya haya nikasikia sauti kama ya umati mkubwa mbinguni wakipiga kelele wakisema:

“Haleluya!

Wokovu na utukufu na uweza ni vya Mungu wetu,

219:2 Kum 32:43; Ufu 6:10kwa maana hukumu zake

ni za kweli na za haki.

Amemhukumu yule kahaba mkuu

aliyeuharibu ulimwengu kwa uzinzi wake.

Mungu amemlipiza kisasi

kwa ajili ya damu ya watumishi wake.”

319:3 Isa 34:10; Ufu 14:11Wakasema tena kwa nguvu:

“Haleluya!

Moshi wake huyo kahaba unapanda juu

milele na milele.”

419:4 Ufu 4:4-6; 5:14Wale wazee ishirini na wanne pamoja na wale viumbe wanne wenye uhai wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu, aliyekuwa ameketi kwenye kile kiti cha enzi. Wakasema kwa sauti kuu:

“Amen, Haleluya!”

519:5 Za 134:1; Ufu 11:18Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema:

“Msifuni Mungu wetu,

ninyi watumishi wake wote,

ninyi nyote mnaomcha,

wadogo kwa wakubwa!”

619:6 Ufu 11:15Kisha nikasikia sauti kama ya umati mkubwa, kama sauti ya maji mengi yaendayo kasi na kama ngurumo kubwa ya radi wakipiga kelele wakisema:

“Haleluya!

Kwa maana Bwana Mungu wetu Mwenyezi anatawala.

719:7 Mt 25:10; Efe 5:32; Ufu 21:2, 9Tufurahi, tushangilie

na kumpa utukufu!

Kwa maana arusi ya Mwana-Kondoo imewadia

na bibi arusi wake amejiweka tayari.

819:8 Ufu 15:4; 19:14; 15:6; Isa 61:10; Eze 44:17; Zek 3:4Akapewa kitani safi, nyeupe

inayongʼaa, ili avae.”

(Hiyo kitani safi inawakilisha matendo ya haki ya watakatifu.)

919:9 Ufu 1:19; Lk 14:15; Ufu 21:5; 22:6Ndipo malaika akaniambia, “Andika: ‘Wamebarikiwa wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo!’ ” Naye akaongeza kusema, “Haya ndiyo maneno ya kweli ya Mungu.”

1019:10 Ufu 22:8; Mdo 10:25, 26; Ufu 22:9; 12:17Ndipo nikaanguka kifudifudi miguuni pake ili kumwabudu, lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi mwenzako pamoja na ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.”

Aliyepanda Farasi Mweupe

1119:11 Ufu 6:2; 3:14; Kut 15:3Kisha nikaona mbingu imefunguka na hapo mbele yangu akiwepo farasi mweupe, ambaye yeye aliyempanda aliitwa Mwaminifu na Kweli. Yeye huhukumu kwa haki na kufanya vita. 1219:12 Ufu 1:14; 6:2; 2:17Macho yake ni kama miali ya moto na juu ya kichwa chake kuna taji nyingi. Ana jina lililoandikwa ambalo hakuna mtu yeyote anayelijua isipokuwa yeye mwenyewe. 1319:13 Isa 63:2, 3; Yn 1:1Amevaa joho lililochoviwa katika damu, na Jina lake ni “Neno la Mungu.” 1419:14 Ufu 19:8; 3:4; 17:14Majeshi ya mbinguni walikuwa wakimfuata, wakiwa wamepanda farasi weupe, hali wamevaa mavazi ya kitani safi, nyeupe na nzuri. 1519:15 Ufu 1:16; 12:5; 14:20; Isa 11:4; 2The 2:8; Za 2:9Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao kwa huo atayaangusha mataifa. “Atayatawala kwa fimbo yake ya utawala ya chuma.” Hulikanyaga shinikizo la mvinyo wa ghadhabu ya Mungu Mwenyezi. 1619:16 Ufu 17:14; 19:12; 1Tim 6:15Kwenye joho lake na paja lake pameandikwa jina hili:

Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.

Mnyama Na Majeshi Yake Yashindwa

1719:17 Ufu 8:13; Eze 39:17Nami nikamwona malaika amesimama ndani kwenye jua, akaita ndege wote warukao angani kwa sauti kuu, “Njooni, kusanyikeni kwa ajili ya karamu kubwa ya Mungu, 1819:18 Eze 39:18-20ili mpate kula nyama ya wafalme na ya majemadari, ya mashujaa, ya farasi na ya wapanda farasi, nyama ya wanadamu, wote walio huru na watumwa, wadogo na wakubwa.”

1919:19 Ufu 16:14, 16Kisha nikamwona yule mnyama na wafalme wa dunia pamoja na majeshi yao wakiwa wamekusanyika pamoja ili kufanya vita dhidi ya yule aliyempanda farasi pamoja na jeshi lake. 2019:20 Ufu 16:13; 13:12; Dan 7:11; Ufu 21:8; 14:19Lakini yule mnyama akakamatwa pamoja na huyo nabii wa uongo ambaye alikuwa amefanya ishara kwa niaba ya huyo mnyama, ambaye kwa ishara hizi aliwadanganya wale waliopokea chapa ya huyo mnyama na kuiabudu sanamu yake. Hawa wawili wakatupwa wakiwa hai ndani ya ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. 21Wale waliosalia waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa yule aliyekuwa amempanda farasi nao ndege wote wakajishibisha kwa nyama yao.

Knijga O Kristu

Otkrivenje 19:1-21

Pobjednička pjesma u nebu

1Začujem zatim silno mnoštvo u nebu kako viče: “Aleluja! Spasenje je djelo našega Boga. Slava i moć njemu pripadaju! 2Njegovi su sudovi istiniti i pravedni. Kaznio je veliku Bludnicu koja je pokvarila zemlju svojim bludom i osvetio je krv svojih slugu.” 3I opet: “Aleluja! Dim s njezina zgarišta dizat će se u vijeke vjekova!”

4Nato dvadeset četvorica starješina i četiri bića padnu ničice i poklone se Bogu koji sjedi na prijestolju govoreći: “Amen! Aleluja!”

5S prijestolja se začuje glas: “Hvalite našega Boga, sve njegove sluge, svi koji ga se bojite, od najmanjega do najvećega!”

6Začujem potom opet glas silnog mnoštva, poput silnoga huka vode i praska silnih gromova: “Aleluja! Naš Gospodin Bog Svemogući kraljuje! 7Radujmo se i veselimo i slavu mu dajmo jer je došao trenutak Jaganjčeve svadbe i njegova je zaručnica pripravna! 8Dopušteno joj je da se odjene u fini, blistavi i čisti lan.”

A lan predstavlja pravedna djela Božjega naroda.

9Anđeo mi reče: “Napiši: Blago onima koji su pozvani na Jaganjčevu svadbenu gozbu!” I još doda: “Ove su riječi istinite, Božje.”

10Pao sam do njegovih nogu da mu se poklonim, ali on reče: “Ne klanjaj mi se! Ta ja sam samo Božji sluga kao i ti, kao i ostala tvoja braća koja svjedoče o svojoj vjeri u Isusa. Bogu se klanjaj! Jer koji svjedoče o Isusu, imaju proročkog duha.”

Jahač na bijelome konju

11Ugledam zatim otvoreno nebo i ondje konja bijelca. Na njemu je sjedio On, zvan Vjerni i Istiniti, koji pravedno sudi i ratuje. 12Oči su mu bile poput ognjenih plamenova, na glavi mnoge krune. Nosio je napisano ime koje samo on zna. 13Ogrtač mu je bio natopljen krvlju. Ime mu je: Riječ Božja. 14Za njim su išle nebeske vojske odjevene u fini, bijeli i čisti lan. 15Iz usta mu je izlazio oštar mač kojim će posjeći narode. Vladat će njima željeznom palicom. On gazi u tijesku gnjevne srdžbe Svemogućega Boga. 16Na boku ogrtača piše mu ime:

“Kralj kraljeva i Gospodar gospodara”.

17Ugledam zatim anđela kako stoji na suncu i kako na sav glas viče lešinarima što lete nebom: “Dođite! Skupite se na veliku gozbu koju vam je Bog priredio 18da se najedete mesa kraljeva, vojskovođa i moćnika, mesa konja i konjanika, mesa svih ljudi—slobodnih i robova, malih i velikih!”

19I vidim: Zvijer i svi zemaljski kraljevi okupili su se s vojskama da zarate s Onim što sjedi na konju i s njegovom vojskom. 20Ali zarobljeni su Zvijer i lažni prorok koji je u njezinoj nazočnosti činio čudesa i njima zavodio ljude koji su primili žig Zvijeri i klanjali se njezinome kipu. I Zvijer i lažni prorok bačeni su u ognjeno jezero s gorućim sumporom. 21Ostatak njihove vojske posjekao je mač izišao iz usta Onoga koji sjedi na bijelome konju. I svi su se lešinari nasitili njihova mesa.