Ufunuo 13 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 13:1-18

113:1 Dan 7:1-6; Ufu 16:13; 12:3; Dan 11:36; Ufu 17:3Yule joka akajikita katika mchanga ulioko ufuoni mwa bahari.

Mnyama Kutoka Baharini

Nami nikamwona mnyama akitoka ndani ya bahari. Mnyama huyo alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, akiwa na taji kumi kwenye hizo pembe zake, na juu ya kila kichwa kulikuwa na jina la kukufuru. 213:2 Dan 7:6; 7:5; 7:4; Ufu 16:10Mnyama yule niliyemwona alifanana na chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kichwa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu zake, kiti chake cha enzi na mamlaka makubwa. 313:3 Ufu 17:8Kimojawapo ya vichwa vya huyo mnyama kilikuwa kama kilichokwisha kupata jeraha la mauti, lakini jeraha hilo la mauti likapona. Ulimwengu wote ukashangaa ukamfuata huyo mnyama. 413:4 Kut 15:11Watu wakaliabudu lile joka kwa sababu lilikuwa limempa huyo mnyama mamlaka yake, pia wakamwabudu huyo mnyama na kuuliza, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana vita naye?”

513:5 Dan 11:36; 2The 2:4; Ufu 11:2Huyo mnyama akapewa kusema maneno ya kiburi na kukufuru na kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na miwili. 613:6 Ufu 12:12Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wakaao mbinguni. 713:7 Dan 7:21; Ufu 11:7; 5:9Pia akaruhusiwa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda. Akapewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa. 813:8 Ufu 3:10; 3:5; 20:12; Mt 25:34Nao watu wote waishio duniani watamwabudu huyo mnyama, yaani, wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.

913:9 Ufu 2:7Yeye aliye na sikio na asikie.

1013:10 Yer 15:2; 43:11; Hes 6:12; Ufu 14:12Ikiwa mtu ni wa kuchukuliwa mateka,

atachukuliwa mateka.

Ikiwa mtu ni wa kuuawa kwa upanga,

atauawa kwa upanga.

Hapa ndipo penye wito wa subira na imani ya watakatifu.

Mnyama Kutoka Dunia

1113:11 Ufu 13:1, 2Kisha nikamwona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka dunia. Alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akanena kama joka. 1213:12 Ufu 19:20; 20:4Akatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza kwa niaba yake, naye akawafanya wote wakaao duniani kumwabudu yule mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona. 1313:13 Mt 24:24; 2Fal 1:10; Lk 9:54Naye akafanya ishara kuu na za ajabu, hata kusababisha moto kushuka toka mbinguni kuja duniani watu wakiona waziwazi. 1413:14 2The 2:9, 10; Ufu 12:9Kwa sababu ya zile ishara alizokuwa amepewa uwezo wa kuzifanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, akawadanganya wakaao duniani. Akawaamuru wasimamishe sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi. 1513:15 Dan 3:3-6Akapewa uwezo wa kuipa pumzi ile sanamu ya yule mnyama wa kwanza, ili iweze kusema na kuwasababisha wale wote waliokataa kuiabudu hiyo sanamu kuuawa. 1613:16 Ufu 19:5; 14:9Pia alimlazimisha kila mmoja, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, mtu huru na mtumwa, atiwe chapa kwenye mkono wake wa kuume au kwenye kipaji chake cha uso, 1713:17 Ufu 14:9; 14:11; 15:2ili kwamba mtu yeyote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa amekuwa na hiyo chapa, ambayo ni jina la huyo mnyama au tarakimu za jina lake.

1813:18 Ufu 17:9; 15:2; 21:17Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na ufahamu na ahesabu tarakimu za huyo mnyama, kwa maana ni tarakimu za kibinadamu. Tarakimu zake ni 666.

Knijga O Kristu

Otkrivenje 13:1-18

Zvijer iz mora

1I stane na morski žal. Ugledam kako iz mora izlazi Zvijer s deset rogova i sedam glava. Na rogovima je imala deset kruna, a na glavama bogohulna imena. 2Sličila je leopardu, ali su joj noge bile kao medvjeđe, a usta poput lavljih. Zmaj joj dade svoju silu, svoje prijestolje i veliku vlast.

3Opazio sam da joj je jedna glava kao nasmrt ranjena—ali smrtna joj rana zacijeli. Sav svijet, začuđen, zadivljeno počne slijediti Zvijer 4i svi se poklone Zmaju koji joj je dao takvu vlast. Poklone se i Zvijeri. “Tko je kao Zvijer?” govorili su. “Tko može ratovati s njom?”

5Zvijeri je bilo dopušteno govoriti drskosti i hule protiv Boga i vlast da djeluje četrdeset dva mjeseca. 6Hulila je na Boga, na njegovo ime, na mjesto njegova prebivališta i na sve one što žive u nebu. 7Dopušteno joj je zaratiti protiv svetih i pobijediti ih. Dobila je vlast nad svakim plemenom i pukom, svakim jezikom i narodom. 8Poklonili su joj se svi koji pripadaju ovomu svijetu, kojih imena nisu zapisana u Knjizi života što pripada zaklanomu Jaganjcu od postanka svijeta.

9Slušajte, kad već imate uši! 10Kojima je određeno da odu u ropstvo, otići će u ropstvo. Kojima je određeno da poginu od mača, poginut će od mača. U tomu je postojanost i vjera svetih.

Zvijer iz zemlje

11Ugledam tada još jednu zvijer kako izlazi iz zemlje. Ima dva roga poput jaganjca, a govori kao Zmaj. 12Vrši svu vlast prve Zvijeri u njezinoj nazočnosti. Primorava sve stanovnike zemlje da se klanjaju prvoj Zvijeri, kojoj je zacijelila smrtna rana. 13Činila je veliko znamenje: da oganj sune s neba na zemlju naočigled svih ljudi. 14Zavodila je tako stanovnike zemlje čudesima koje joj je bilo dopušteno činiti u nazočnosti prve Zvijeri. Rekla im je da načine kip Zvijeri koja je bila smrtno ranjena, ali je preživjela. 15Dopušteno joj je udahnuti život kipu Zvijeri tako da progovori. Kip progovori i zapovjedi da se smaknu svi koji mu se ne klanjaju.

16Druga zvijer učinila je da svi—veliki i mali, bogati i siromašni, robovi i slobodni ljudi—daju sebi udariti žig na desnu ruku ili na čelo. 17Nitko nije mogao ništa prodati ni kupiti ako nije imao žig s imenom Zvijeri ili s brojem njezina imena. 18Tko je mudar, neka odgonetne broj Zvijeri. To je broj čovjeka: 666.