Tito 3 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Tito 3:1-15

Kutenda Mema

13:1 Rum 13:1; 2Tim 2:21Wakumbushe watu kuwanyenyekea watawala na kuwatii wenye mamlaka, wawe tayari kutenda kila lililo jema. 23:2 Efe 4:31; 2Tim 2:24Wasimnenee mtu yeyote mabaya, wasiwe wagomvi, bali wawe wapole, wakionyesha unyenyekevu kwa watu wote.

33:3 Efe 2:2, 5, 8; 1Kor 6:11Maana sisi wenyewe wakati fulani tulikuwa wajinga, wasiotii, tukiwa watumwa wa tamaa mbaya na anasa za kila aina. Tuliishi katika uovu na wivu, tukichukiwa na kuchukiana sisi kwa sisi. 43:4 Efe 2:7; Tit 2:11; Mit 8:31; 1Tim 2:3Lakini wema na upendo wa Mungu Mwokozi wetu ulipofunuliwa, 53:5 Efe 2:9; Rum 12:2; 3:20; 9:11; Gal 2:16; 2Tim 1:9; Yn 3:3, 5alituokoa, si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyotenda, bali kwa sababu ya rehema zake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa mara ya pili na kwa kufanywa wapya kwa njia ya Roho Mtakatifu, 63:6 Rum 5:5; Eze 36:25; Yoe 2:28; Yn 1:16; Mdo 2:33; 10:45ambaye Mungu alitumiminia kwa wingi kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu, 73:7 Rum 3:24; 8:24; Tit 1:2ili kwamba, tukiisha kuhesabiwa haki kwa neema yake, tupate kuwa warithi tukiwa na tumaini la uzima wa milele. 83:8 1Tim 1:15; Tit 2:14Hili ni neno la kuaminiwa. Nami nataka uyasisitize mambo haya, ili wale ambao wamemwamini Mungu wapate kuwa waangalifu kujitoa kwa ajili ya kutenda mema wakati wote. Mambo haya ni mazuri tena ya manufaa kwa kila mtu.

93:9 1Tim 1:14; 2Tim 2:14Lakini jiepushe na maswali ya kipuzi, mambo ya koo, mabishano na ugomvi kuhusu sheria, kwa sababu hayana faida, tena ni ubatili. 103:10 Rum 16:17; 2Kor 13:2; Mt 18:17; 2The 3:6, 14; 2Tim 3:5; Yn 10Mtu anayesababisha mafarakano, mwonye mara ya kwanza, kisha mwonye mara ya pili. Baada ya hapo, usihusike naye tena. 113:11 Mdo 13:46; 1Tim 6:4, 5Kwa kuwa unajua kwamba mtu kama huyo amepotoka na tena ni mwenye dhambi. Yeye amejihukumu mwenyewe.

Maneno Ya Mwisho Na Kumtamkia Baraka

123:12 Mdo 20:4; 2Tim 4:9, 21Mara nitakapomtuma Artema au Tikiko kwako, jitahidi kuja unione huko Nikopoli, kwa sababu nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi. 133:13 Mdo 18:24Fanya kila uwezalo uwasafirishe Zena yule mwanasheria na Apolo na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji katika safari yao. 14Watu wetu hawana budi kujifunza kutenda mema, ili waweze kuyakimu mahitaji ya kila siku, wasije wakaishi maisha yasiyokuwa na matunda.

153:15 1Tim 1:2; Kol 4:18Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale wanaotupenda katika imani.

Neema iwe nanyi nyote. Amen.

New International Reader’s Version

Titus 3:1-15

Do What Is Good Because You Are Saved

1Remind God’s people to obey rulers and authorities. Remind them to be ready to do what is good. 2Tell them not to speak evil things against anyone. Remind them to live in peace. They must consider the needs of others. They must always be gentle toward everyone.

3At one time we too acted like fools. We didn’t obey God. We were tricked. We were controlled by all kinds of desires and pleasures. We were full of evil. We wanted what belongs to others. People hated us, and we hated one another. 4But the kindness and love of God our Savior appeared. 5He saved us. It wasn’t because of the good things we had done. It was because of his mercy. He saved us by washing away our sins. We were born again. The Holy Spirit gave us new life. 6God poured out the Spirit on us freely. That’s because of what Jesus Christ our Savior has done. 7His grace made us right with God. So now we have received the hope of eternal life as God’s children. 8You can trust this saying. These things are important. Treat them that way. Then those who trust in God will be careful to commit themselves to doing good. These things are excellent. They are for the good of everyone.

9But keep away from foolish disagreements. Don’t argue about family histories. Don’t make trouble. Don’t fight about what the law teaches. Don’t argue about things like that. It doesn’t do any good. It doesn’t help anyone. 10Warn anyone who tries to get believers to separate from one another. Warn that person more than once. After that, have nothing to do with them. 11You can be sure that people like this are twisted and sinful. Their own actions judge them.

Final Words

12I will send Artemas or Tychicus to you. Then do your best to come to me at Nicopolis. I’ve decided to spend the winter there. 13Do everything you can to help Zenas the lawyer and Apollos. Send them on their way. See that they have everything they need.

14Our people must learn to commit themselves to doing what is good. Then they can provide for people when they are in great need. If they do that, their lives won’t turn out to be useless.

15Everyone who is with me sends you greetings.

Greet those who love us in the faith.

May God’s grace be with you all.