Nehemia 5 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Nehemia 5:1-19

Nehemia Awasaidia Maskini

15:1 Kum 15:7; Law 25:35; Isa 5:7Wakati huu wanaume na wake zao wakalia kilio kikuu dhidi ya ndugu zao Wayahudi. 25:2 Mwa 41:57; Hag 1:6Baadhi yao walikuwa wakisema, “Sisi na wana wetu na binti zetu tuko wengi. Ili tuweze kula na kuishi, ni lazima tupate nafaka.”

35:3 Mwa 47:23; Za 109:11Wengine walikuwa wakisema, “Tunaweka rehani mashamba yetu, mashamba ya mizabibu, na nyumba zetu ili tupate nafaka wakati wa njaa.”

45:4 Ezr 4:13Bado kukawa na wengine waliokuwa wakisema, “Ilitubidi tukope fedha ili kulipa kodi ya mfalme kwa ajili ya mashamba yetu na mashamba yetu ya mizabibu. 55:5 Mwa 37:27; 29:14; Kum 15:7-11; 2Fal 4:1; Mt 18:25Ingawa sisi ni mwili na damu moja sawa na watu wa nchi yetu, na ijapo wana wetu ni wazuri kama wana wao, bado inatupasa kuwatoa wana wetu na binti zetu kwenye utumwa. Baadhi ya binti zetu wameshakuwa watumwa tayari, lakini hatuna uwezo wa kuwakomboa, kwa sababu mashamba yetu na mashamba ya mizabibu yetu ni mali ya wengine.”

65:6 Kut 11:8; Neh 13:8; Mk 3:5; Efe 4:26Niliposikia kilio chao na malalamiko haya, nilikasirika sana. 75:7 Kut 22:25-27; Kum 24:10-13; Law 19:17Nikayatafakari katika akili yangu, nikiwalaumu wakuu na maafisa. Nikawaambia, “Mnawaonea ndugu zenu kwa kuwatoza riba!” Basi nikaitisha mkutano mkubwa ili kuwashughulikia 85:8 Law 25:47-48; Yer 34:8na kusema: “Kulingana na uwezo wetu, tumewakomboa ndugu zetu Wayahudi waliokuwa wameuzwa kwa watu wasioamini. Sasa mnawauza ndugu zenu, ili wauzwe tena kwetu!” Walinyamaza kimya, kwa sababu hawakupata chochote cha kusema.

95:9 Mwa 13:7-8; Rum 2:24; Isa 52:5; 1Pet 2:12Basi nikaendelea kusema, “Mnachokifanya si sawa. Je, haikuwapasa kutembea katika hofu ya Mungu wetu ili tuepukane na shutuma za adui zetu wasioamini? 105:10 Kut 22:25Mimi na ndugu zangu na watu wangu tunawakopesha watu fedha na nafaka. Lakini jambo hili la kutoza riba likome! 115:11 Isa 58:6Warudishieni mara moja mashamba yao, mashamba yao ya mizabibu, mashamba yao ya mizeituni, na nyumba zao, pia riba yao mnayowatoza na sehemu ya fungu la mia la fedha, nafaka, divai mpya na mafuta.”

125:12 Ezr 10:5; Yer 34:8-9Wakasema, “Tutawarudishia na hatutataka kitu chochote zaidi kutoka kwao. Tutafanya kama ulivyosema.”

Kisha nikawaita makuhani na kuwafanya wakuu na maafisa kuapa kufanya kile walichoahidi. 135:13 Mt 10:14; Mdo 13:51; 18:6; Kum 27:15-26Pia nikakungʼuta makunjo ya vazi langu na kusema, “Kila mtu ambaye hatatimiza ahadi hii, Mungu na amkungʼute hivi kutoka nyumba yake na katika mali zake. Basi mtu wa namna hiyo akungʼutiwe nje na aachwe bila kitu!”

Waliposikia hili, mkutano wote ukasema, “Amen,” na wakamtukuza Bwana. Nao watu wakafanya kama walivyokuwa wameahidi.

145:14 Neh 2:6; 13:6; Mwa 42:6; 1Kor 9:4Zaidi ya hayo, kutoka mwaka wa ishirini wa Mfalme Artashasta, wakati nilipoteuliwa kuwa mtawala wao katika nchi ya Yuda, mpaka mwaka wake wa thelathini na mbili, yaani miaka kumi na miwili, mimi wala ndugu zangu hatukula chakula ambacho kwa kawaida hupewa watawala. 155:15 Mwa 42:18; 20:11; Ay 31:23; Lk 18:2-4Lakini watawala wa mwanzoni, wale walionitangulia, waliwalemea watu na kuchukua kutoka kwao shekeli arobaini za fedha,5:15 Shekeli 40 za fedha ni sawa na gramu 456. pamoja na chakula na mvinyo. Wasaidizi wao pia walijifanya wakuu juu ya watu. Lakini kwa kumheshimu Mungu sikufanya hivyo. 165:16 2The 3:7-10Badala yake, nilijitoa kwa bidii katika kazi ya ukuta huu. Watu wangu wote walikutanika pale kwa ajili ya kazi. Hatukujipatia shamba lolote.

17Zaidi ya hayo, Wayahudi na maafisa 150 walikula mezani pangu, pamoja na wale waliotujia kutoka mataifa jirani. 185:18 1Fal 4:22-23Kila siku niliandaliwa maksai mmoja, kondoo sita wazuri, na kuku, na mvinyo wa kila aina kwa wingi kila baada ya siku kumi. Licha ya mambo haya yote, sikudai chakula kilichokuwa fungu la mtawala, kwa sababu madai yalikuwa mazito sana kwa watu hawa.

195:19 Mwa 8:1; Neh 13:22; 2Fal 20:3Unikumbuke kwa fadhili, Ee Mungu wangu, kwa yote niliyofanya kwa ajili ya watu hawa.

New International Reader’s Version

Nehemiah 5:1-19

Nehemiah Helps Some Poor People

1Some men and their wives cried out against their Jewish brothers and sisters. 2Some of them were saying, “There are now many of us. We have many sons and daughters. We have to get some grain so we can eat and stay alive.”

3Others were saying, “We’re being forced to sell our fields, vineyards and homes. We have to do it to buy grain. There isn’t enough food for everyone.”

4Still others were saying, “We’ve had to borrow money. We needed it to pay the king’s tax on our fields and vineyards. 5We belong to the same family lines as the rest of our people. Our children are as good as theirs. But we’ve had to sell them off as slaves. Some of our daughters have already been made slaves. But we can’t do anything about it. That’s because our fields and vineyards now belong to others.”

6I heard them when they cried out. And I was very angry when I heard what they were saying. 7I thought it over for a while. Then I accused the nobles and officials of breaking the law. I told them, “You are charging your own people interest!” So I called together a large group of people to handle the matter. 8I said, “Our Jewish brothers and sisters were sold to other nations. We’ve done everything we could to buy them back and bring them home. But look at what you are doing! You are actually selling your own people! Now we’ll have to buy them back too!” The people kept quiet. They couldn’t think of anything to say.

9So I continued, “What you are doing isn’t right. Shouldn’t you show respect for our God? Shouldn’t you live in a way that will keep our enemies from saying bad things about us? 10I’m lending the people money and grain. So are my relatives and my men. But we must stop charging interest! 11Give the people’s fields back to them. Give them back their vineyards, olive groves and houses. Do it right away. Give everything back to them. Also give them back the one percent on the money, grain, fresh wine and olive oil you have charged them.”

12“We’ll give it back,” they said. “And we won’t require anything more from them. We’ll do exactly as you say.”

Then I sent for the priests. I made the nobles and officials promise to do what they had said. 13I also shook out my pockets and emptied them. I said, “Someone might decide not to keep this promise they have made. If that happens, may God shake them out of their house! May he empty them of everything they own!”

The whole community said, “Amen.” They praised the Lord. And the leaders did what they had promised to do.

14And that’s not all. I was appointed as governor of Judah in the 20th year that Artaxerxes was king of Persia. I remained in that position until his 32nd year. During those 12 years, I and my relatives didn’t eat the food that was provided for my table. 15But there had been governors before me. They had put a heavy load on the people. They had taken a pound of silver from each of them. They had also taken food and wine from them. Their officials had acted like high and mighty rulers over them. But because of my great respect for God, I didn’t act like that. 16Instead, I spent all my time working on this wall. All my men were gathered there to work on it too. We didn’t receive any land for ourselves.

17Many people ate at my table. They included 150 Jews and officials. They also included leaders who came to us from the nations that were around us. 18Each day one ox, six of the best sheep and some birds were prepared for me. Every ten days plenty of wine of all kinds was brought in as well. In spite of all that, I never asked for the food that was provided for my table. That’s because the people were already paying too many taxes.

19You are my God. Please remember me and help me. Keep in mind everything I’ve done for these people.