Nehemia 12 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Nehemia 12:1-47

Makuhani Na Walawi Waliorudi Na Zerubabeli

112:1 Neh 10:2-8; Zek 4:6-10; Ezr 3:2Hawa wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua:

Seraya, Yeremia, Ezra,

2Amaria, Maluki, Hatushi,

3Shekania, Rehumu, Meremothi,

412:4 Lk 1:5; 1Nya 24:10Ido, Ginethoni, Abiya,

5Miyamini, Moadia, Bilga,

612:6 1Nya 24:7Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,

712:7 Hag 1:1; Zek 5:1; Ezr 3:2Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya.

Hawa walikuwa viongozi wa makuhani na wenzao wakati wa Yeshua.

812:8 Neh 11:17; 1Nya 16:8Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani. 9Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.

1012:10 Ezr 10:24; Neh 3:20Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada, 11Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.

12Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani:

wa jamaa ya Seraya, Meraya;

wa jamaa ya Yeremia, Hanania;

13wa jamaa ya Ezra, Meshulamu;

wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;

14wa jamaa ya Maluki, Yonathani;

wa jamaa ya Shebania, Yosefu;

15wa jamaa ya Harimu, Adna;

wa jamaa ya Meremothi, Helkai;

1612:16 Neh 12:4wa jamaa ya Ido, Zekaria;

wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;

1712:17 1Nya 24:10wa jamaa ya Abiya, Zikri;

wa jamaa ya Miniamini na ya Maazia, Piltai;

18wa jamaa ya Bilgai, Shamua;

wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;

19wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai;

wa jamaa ya Yedaya, Uzi;

20wa jamaa ya Salu, Kalai;

wa jamaa ya Amoki, Eberi;

21wa jamaa ya Hilkia, Hashabia;

wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.

22Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario, Mwajemi. 2312:23 1Nya 9:14Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu. 2412:24 Ezr 2:40; 3:11; 1Nya 23:1Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.

25Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu. 2612:26 Neh 8:9; Ezr 7:6, 11Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.

Kuwekwa Wakfu Ukuta Wa Yerusalemu

2712:27 Kum 20:5; 2Sam 6:5; 1Nya 25:6; Za 81:1-3; 92:3Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe huko kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze. 2812:28 1Nya 2:54; 9:16Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi, 29kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu. 3012:30 Kut 19:10; Ay 1:5Wakati makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kwa kufuatana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.

3112:31 Neh 2:13; Ezr 3:10; Hes 10:2; 2Nya 5:12Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi. 32Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata, 33pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu, 3412:34 Ezr 1:5Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia, 3512:35 Ezr 3:10pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu, 3612:36 1Nya 23:5; 15:16; 2Nya 8:14pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano. 3712:37 Neh 2:14; 3:3-15; 3:26; 2Sam 5:7-9Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.

3812:38 Neh 3:8-11Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru mpaka kwenye Ukuta Mpana, 3912:39 2Fal 14:13; Neh 8:16; 2Nya 33:14; Neh 3:1-6juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, mpaka kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.

4012:40 Za 42:4Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa, 41na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao, 42na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia. 4312:43 Za 9:2; 92:4Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.

4412:44 Neh 13:4, 13; Law 27:30; Kum 18:8Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka kwenye yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi. 4512:45 1Nya 25:1; 2Nya 8:14; 1Nya 6:31; 23:5Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Solomoni mwanawe. 4612:46 2Nya 35:15; 29:27Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, walikuwepo viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu. 4712:47 Hes 18:21; Kum 18:8Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Aroni.

New International Reader’s Version

Nehemiah 12:1-47

The Priests and Levites Who Returned to Judah

1Some priests and Levites returned to Judah with Zerubbabel and Joshua. Zerubbabel was the son of Shealtiel. Here are the names of those priests and Levites.

Seraiah, Jeremiah, Ezra,

2Amariah, Malluk, Hattush,

3Shekaniah, Rehum, Meremoth,

4Iddo, Ginnethon, Abijah,

5Mijamin, Moadiah, Bilgah,

6Shemaiah, Joiarib, Jedaiah,

7Sallu, Amok, Hilkiah, Jedaiah

All of them were the leaders of the priests and those who helped them. They lived in the days of Joshua.

8The Levites were Jeshua, Binnui, Kadmiel, Sherebiah and Judah. There were also Mattaniah and those who helped him. They were in charge of the songs for giving thanks. 9Bakbukiah and Unni helped them. They stood and sang across from them during the services.

10Joshua was the father of Joiakim.

Joiakim was the father of Eliashib.

Eliashib was the father of Joiada.

11Joiada was the father of Jonathan.

And Jonathan was the father of Jaddua.

12Here are the names of the family leaders of the priests. They were the leaders in the days of Joiakim.

Meraiah was from Seraiah’s family.

Hananiah was from Jeremiah’s family.

13Meshullam was from Ezra’s family.

Jehohanan was from Amariah’s family.

14Jonathan was from Malluk’s family.

Joseph was from Shekaniah’s family.

15Adna was from Harim’s family.

Helkai was from Meremoth’s family.

16Zechariah was from Iddo’s family.

Meshullam was from Ginnethon’s family.

17Zikri was from Abijah’s family.

Piltai was from Miniamin’s and Moadiah’s family.

18Shammua was from Bilgah’s family.

Jehonathan was from Shemaiah’s family.

19Mattenai was from Joiarib’s family.

Uzzi was from Jedaiah’s family.

20Kallai was from Sallu’s family.

Eber was from Amok’s family.

21Hashabiah was from Hilkiah’s family.

And Nethanel was from Jedaiah’s family.

22The names of the family leaders of the Levites in the days of Eliashib, Joiada, Johanan and Jaddua were written down. So were the names of the family leaders of the priests. That happened while Darius ruled over Persia. 23The names of the leaders in Levi’s family line up to the time of Johanan were written down. They were written in the official records. Johanan was the son of Eliashib. 24The leaders of the Levites were Hashabiah, Sherebiah and Jeshua. Jeshua was the son of Kadmiel. Those who helped them stood across from them to sing praises and give thanks. One group would sing back to the other. That’s what David, the man of God, had ordered.

25Mattaniah, Bakbukiah, Obadiah, Meshullam, Talmon and Akkub stood at the gates of the temple. They guarded the storerooms at the gates. 26They served in the days of Joiakim. He was the son of Joshua. Joshua was the son of Jozadak. They also served in the days of Nehemiah and Ezra. Nehemiah was the governor. Ezra was a priest and the teacher of the Law.

The Wall of Jerusalem Is Set Apart to God

27The wall of Jerusalem was set apart to God. For that occasion, the Levites were gathered together from where they lived. They were brought to Jerusalem to celebrate that happy occasion. They celebrated the fact that the wall was being set apart to God. They did it by singing and giving their thanks to him. They celebrated by playing music on cymbals, harps and lyres. 28The musicians were also brought together. Some of them came in from the area around Jerusalem. Others came from the villages where the people of Netophah lived. 29Others came from Beth Gilgal. Still others came from the area of Geba and Azmaveth. The musicians had built villages for themselves around Jerusalem. 30The priests and Levites made themselves pure. Then they made the people, the gates and the wall pure and “clean.”

31I, Nehemiah, had the leaders of Judah go up on top of the wall. I also appointed two large choirs to sing and give thanks. I told one of them to walk south on top of the wall. That was toward the Dung Gate. 32Hoshaiah and half of the leaders of Judah followed them. 33Azariah, Ezra, Meshullam, 34Judah, Benjamin, Shemaiah and Jeremiah also followed them. 35Some priests who had trumpets followed them. So did Zechariah. He was the son of Jonathan. Jonathan was the son of Shemaiah. Shemaiah was the son of Mattaniah. Mattaniah was the son of Micaiah. Micaiah was the son of Zakkur. Zakkur was the son of Asaph. 36Those who helped Zechariah also marched along. They were Shemaiah, Azarel, Milalai, Gilalai, Maai, Nethanel, Judah and Hanani. They brought musical instruments with them. That’s what David, the man of God, had ordered. Ezra led the group that was marching south. He was the teacher of the Law. 37At the Fountain Gate they continued straight up the steps of the City of David. The steps went up to the wall. Then the group passed above the place where David’s palace had been. They continued on to the Water Gate on the east.

38The second choir went north. I followed them on top of the wall. Half of the people went with me. They went past the Tower of the Ovens. They went to the Broad Wall. 39They marched over the Gate of Ephraim. They went over the Jeshanah Gate and the Fish Gate. They went past the Tower of Hananel and the Tower of the Hundred. They continued on to the Sheep Gate. At the Gate of the Guard they stopped.

40Then the two choirs that sang and gave thanks took their places in God’s house. So did I. So did half of the officials. 41And so did the priests. They were Eliakim, Maaseiah, Miniamin, Micaiah, Elioenai, Zechariah and Hananiah. They had their trumpets with them. 42Maaseiah, Shemaiah, Eleazar, Uzzi, Jehohanan, Malkijah, Elam and Ezer were also there. The choirs sang under the direction of Jezrahiah. 43On that day large numbers of sacrifices were offered. The people were glad because God had given them great joy. The women and children were also very happy. The joyful sound in Jerusalem could be heard far away.

Nehemiah Makes Some Final Changes

44At that time some men were put in charge of the storerooms. That’s where all the gifts the people brought were placed. Those gifts included the first shares of their crops. They also included a tenth of everything the Law required. Crops were harvested from the fields around the towns. The people had to bring the shares of those crops that were required by the Law. They gave them to the priests and Levites. That’s because the people of Judah were pleased with the priests and Levites who were serving God. 45The priests and Levites did everything their God wanted them to do. They made things pure and “clean.” The musicians and the men who guarded the temple gates also served God. Everything was done just as David and his son Solomon had commanded. 46A long time ago there had been directors for the musicians. There had also been directors for the songs for giving thanks and praise to God. It was in the time of David and Asaph. 47So now in the days of Zerubbabel and Nehemiah, all the people of Israel brought their gifts. They gave the musicians and the men who guarded the gates what they were supposed to give them every day. They also set apart the shares for the other Levites. And the Levites set apart the shares for the priests in the family line of Aaron.