Ole Wa Ninawi
13:1 Eze 22:2; Mik 3:10; Za 12:2Ole wa mji umwagao damu,
uliojaa uongo,
umejaa nyara,
usiokosa kuwa na vitu vya kuteka nyara.
23:2 Isa 34:3; Yer 47:3Kelele za mijeledi,
vishindo vya magurudumu,
farasi waendao mbio
na mshtuo wa magari ya vita!
3Wapanda farasi wanaenda mbio,
panga zinameremeta,
na mikuki inangʼaa!
Majeruhi wengi,
malundo ya maiti,
idadi kubwa ya miili isiyohesabika,
watu wanajikwaa juu ya mizoga:
43:4 Isa 47:9; 23:17; 2The 2:9, 10; Dan 2:2; Ufu 9:20, 21; Eze 16:25-29yote haya kwa sababu ya wingi wa tamaa za kahaba,
anayeshawishi, bibi wa mambo ya uchawi,
anayewatia utumwani mataifa kwa ukahaba wake
na pia jamaa za watu kwa ulozi wake.
53:5 Nah 2:13; Isa 47:2-3; 20:4; Yer 13:22Bwana Mwenye Nguvu Zote anasema,
“Mimi ni kinyume na ninyi.
Nitafunika uso wako kwa gauni lako.
Nitaonyesha mataifa uchi wako
na falme aibu yako.
63:6 Kut 29:14; Ay 9:31; 1Sam 2:30; Yer 51:37; Isa 14:16Nitakutupia uchafu,
nitakufanyia dharau
na kukufanya kioja.
73:7 Isa 13:14; 31:9; Nah 1:1; Ay 3:14; Yer 51:37Wote wanaokuona watakukimbia na kusema,
‘Ninawi ipo katika kuangamia:
ni nani atakayeomboleza kwa ajili yake?’
Nitampata wapi yeyote wa kukufariji?”
83:8 Amo 6:2; Yer 46:25; Isa 19:6-9Je, wewe ni bora kuliko No-Amoni,
uliopo katika Mto Naili,
uliozungukwa na maji?
Mto ulikuwa kinga yake,
nayo maji yalikuwa ukuta wake.
93:9 Mwa 10:6; 2Nya 12:3; Eze 27:10; 30:5Kushi3:9 Kushi ni Ethiopia. na Misri walikuwa nguvu zake zisizo na mpaka;
Putu na Libia walikuwa miongoni mwa wale walioungana naye.
103:10 Isa 20:4; 2Fal 8:12; Isa 13:16; Hos 13:16; Ay 6:26-27; Eze 24:6; Yer 40:1; Yoe 3:3; Oba 1:11Hata hivyo alichukuliwa mateka
na kwenda uhamishoni.
Watoto wake wachanga walivunjwa vunjwa vipande
kwenye mwanzo wa kila barabara.
Kura zilipigwa kwa watu wake wenye heshima,
na watu wake wote wakuu walifungwa kwa minyororo.
113:11 Isa 49:26; 2:10Wewe pia utalewa;
utakwenda mafichoni
na kutafuta kimbilio kutoka kwa adui.
123:12 Wim 2:13; Ufu 6:13; Isa 28:4Ngome zako zote ni kama mitini
yenye matunda yake ya kwanza yaliyoiva;
wakati inapotikiswa,
tini huanguka kwenye kinywa chake alaye.
133:13 Isa 19:16; 45:2; Yer 50:37; Nah 2:6Tazama vikosi vyako:
wote ni wanawake!
Malango ya nchi yako
yamekuwa wazi kwa adui zako;
moto umeteketeza mapingo yake.
143:14 2Nya 32:4; Nah 2:1Teka maji kwa ajili ya kuzingirwa kwako,
imarisha ulinzi wako,
Ufanyie udongo wa mfinyanzi kazi,
yakanyage matope,
karabati tanuru la kuchomea matofali!
153:15 Isa 27:1; 2Sam 2:26; Yer 51:14; Yoe 1:4Huko moto utakuteketeza,
huko upanga utakuangusha chini
na kama vile panzi, watakumaliza.
Ongezeka kama panzi,
ongezeka kama nzige!
163:16 Kut 10:13Umeongeza idadi ya wafanyabiashara wako
mpaka wamekuwa wengi kuliko nyota za angani,
lakini kama nzige wanaacha nchi tupu
kisha huruka na kwenda zake.
173:17 Ufu 9:7; Yer 51:17Walinzi wako ni kama nzige,
maafisa wako ni kama makundi ya nzige
watuao kwenye kuta wakati wa siku ya baridi:
lakini wakati jua linapotokea wanaruka kwenda zao,
na hakuna ajuaye waendako.
183:18 Za 76:5-6; Yer 25:27; 50:18; Eze 31:3; Isa 56:10; 1Fal 22:17Ee mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wanasinzia;
wakuu wako wanalala chini mavumbini kupumzika.
Watu wako wametawanyika juu ya milima
bila kuwa na mtu yeyote wa kuwakusanya.
193:19 Yer 30:13; Mik 1:9; Ay 27:23; Mao 2:15; Sef 2:15; Isa 14:8; 37:18Hakuna kitu kinachoweza kuponya jeraha lako;
jeraha lako ni la kukuua.
Kila anayesikia habari zako,
hupiga makofi kwa kuanguka kwako,
kwa kuwa ni nani ambaye hajaguswa
na ukatili wako usio na mwisho?
Woe to Nineveh
1Woe to the city of blood,
full of lies,
full of plunder,
never without victims!
2The crack of whips,
the clatter of wheels,
galloping horses
and jolting chariots!
3Charging cavalry,
flashing swords
and glittering spears!
Many casualties,
piles of dead,
bodies without number,
people stumbling over the corpses –
4all because of the wanton lust of a prostitute,
alluring, the mistress of sorceries,
who enslaved nations by her prostitution
and peoples by her witchcraft.
5‘I am against you,’ declares the Lord Almighty.
‘I will lift your skirts over your face.
I will show the nations your nakedness
and the kingdoms your shame.
6I will pelt you with filth,
I will treat you with contempt
and make you a spectacle.
7All who see you will flee from you and say,
“Nineveh is in ruins – who will mourn for her?”
Where can I find anyone to comfort you?’
8Are you better than Thebes,
situated on the Nile,
with water around her?
The river was her defence,
the waters her wall.
9Cush3:9 That is, the upper Nile region and Egypt were her boundless strength;
Put and Libya were among her allies.
10Yet she was taken captive
and went into exile.
Her infants were dashed to pieces
at every street corner.
Lots were cast for her nobles,
and all her great men were put in chains.
11You too will become drunk;
you will go into hiding
and seek refuge from the enemy.
12All your fortresses are like fig-trees
with their first ripe fruit;
when they are shaken,
the figs fall into the mouth of the eater.
13Look at your troops –
they are all weaklings.
The gates of your land
are wide open to your enemies;
fire has consumed the bars of your gates.
14Draw water for the siege,
strengthen your defences!
Work the clay,
tread the mortar,
repair the brickwork!
15There the fire will consume you;
the sword will cut you down –
and it will devour you like a swarm of locusts.
Multiply like grasshoppers,
multiply like locusts!
16You have increased the number of your merchants
till they are more numerous than the stars in the sky,
but like locusts they strip the land
and then fly away.
17Your guards are like locusts,
your officials like swarms of locusts
that settle in the walls on a cold day –
but when the sun appears they fly away,
and no-one knows where.
18King of Assyria, your shepherds3:18 That is, rulers slumber;
your nobles lie down to rest.
Your people are scattered on the mountains
with no-one to gather them.
19Nothing can heal you;
your wound is fatal.
All who hear the news about you
clap their hands at your fall,
for who has not felt
your endless cruelty?