Mwanzo 49 – NEN & OL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 49:1-33

Yakobo Abariki Wanawe

149:1 Hes 24:14; Kum 31:29Ndipo Yakobo akawaita wanawe na kusema: “Kusanyikeni kunizunguka ili niweze kuwaambia lile litakalowatokea siku zijazo.

249:2 Yos 24:1; Za 34:11“Kusanyikeni na msikilize, enyi wana wa Yakobo,

msikilizeni baba yenu Israeli.

349:3 Mwa 29:32; Kum 21:17; Za 78:51“Reubeni, wewe ni mzaliwa wangu wa kwanza,

nguvu zangu, tunda la kwanza la nguvu zangu,

umepita kwa heshima, umepita kwa uwezo.

4Usiyezuiwa kama maji, basi hutakuwa mkuu tena,

kwa kuwa ulipanda kwenye kitanda cha baba yako,

kwenye kitanda changu na kukinajisi.

549:5 Mwa 29:33; Mit 4:17“Simeoni na Lawi ni wana ndugu:

panga zao ni silaha za jeuri.

649:6 Mit 1:15; Efe 5:11Mimi na nisiingie katika baraza lao,

nami nisiunganike katika kusanyiko lao,

kwa kuwa wamewaua watu katika hasira yao,

walikata mishipa ya miguu ya mafahali

kama walivyopenda.

749:7 Yos 19:1, 9; Mwa 29:35Hasira yao na ilaaniwe, kwa kuwa ni kali mno,

nayo ghadhabu yao ni ya ukatili!

Nitawatawanya katika Yakobo

Na kuwasambaza katika Israeli.

849:8 1Nya 5:2; Kum 28:48“Yuda, ndugu zako watakusifu;

mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako;

wana wa baba yako watakusujudia.

949:9 Hes 24:9; Ay 38:39Ee Yuda, wewe ni mwana simba;

unarudi toka mawindoni, mwanangu.

Kama simba hunyemelea na kulala chini,

kama simba jike: nani athubutuye kumwamsha?

1049:10 Eze 21:27; Isa 42:1Fimbo ya ufalme haitaondoka kwa Yuda,

wala fimbo ya mtawala kati ya miguu yake,

hadi aje yeye ambaye milki ni yake,

ambaye utii wa mataifa ni wake.

11Atamfunga punda wake katika mzabibu,

naye mwana-punda wake kwenye tawi lililo bora zaidi;

atafua mavazi yake katika divai,

majoho yake katika damu ya mizabibu.

12Macho yake yatakuwa mekundu kwa divai,

meno yake yatakuwa meupe kwa maziwa.

1349:13 Mwa 30:20; 10:19“Zabuloni ataishi pwani ya bahari

na kuwa bandari za kuegesha meli;

mpaka wake utapanuka kuelekea Sidoni.

14“Isakari ni punda mwenye nguvu

ambaye amelala kati ya mizigo yake.

1549:15 Yos 19:17-23; Eze 29:18Aonapo palivyo pazuri mahali pake pa kupumzika

na jinsi nchi yake inavyopendeza,

atainamisha bega lake kwenye mzigo

na kujitolea kwa ajili ya kazi ngumu.

16“Dani atahukumu watu wake kwa haki

kama mmoja wa makabila ya Israeli.

1749:17 Amu 18:27; Yer 8:17Dani atakuwa nyoka kando ya barabara,

nyoka mwenye sumu kando ya njia,

yule aumaye visigino vya farasi

ili yule ampandaye aanguke chali.

18“Ee Bwana, nautafuta wokovu wako.

19“Gadi atashambuliwa ghafula na kundi la washambuliaji,

lakini yeye atawageukia na kuwashinda kabisa.

2049:20 Mwa 30:13; Isa 25:6; Ay 29:6“Chakula cha Asheri kitakuwa kinono,

naye atatoa chakula kitamu kimfaacho mfalme.

21“Naftali ni kulungu jike aliyeachiwa huru

azaaye watoto wazuri.

2249:22 Mwa 30:24; Eze 19:10“Yosefu ni mzabibu uzaao,

mzabibu uzaao ulio kando ya chemchemi,

ambao matawi yake hutanda ukutani.

23Kwa uchungu wapiga mshale walimshambulia,

wakampiga mshale kwa ukatili.

2449:24 Za 18:34; Isa 1:24Lakini upinde wake ulibaki imara,

mikono yake ikatiwa nguvu,

na mkono wa Mwenye Nguvu wa Yakobo,

kwa sababu ya Mchungaji, Mwamba wa Israeli,

2549:25 Kut 18:4; Mwa 27:28kwa sababu ya Mungu wa baba yako, anayekusaidia,

kwa sababu ya Mwenyezi,49:25 Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania. yeye anayekubariki

kwa baraka za mbinguni juu,

baraka za kilindi kilichoko chini,

baraka za matitini na za tumbo la uzazi.

26Baraka za baba yako ni kubwa

kuliko baraka za milima ya kale,

nyingi kuliko vilima vya kale.

Baraka hizo zote na zikae juu ya kichwa cha Yosefu,

juu ya paji la yule mkuu miongoni mwa ndugu zake.

2749:27 Amu 20:12-13; Ebr 1:8; Hes 31:11“Benyamini ni mbwa mwitu mlafi mwenye njaa kuu;

asubuhi hurarua mawindo yake,

jioni hugawa nyara.”

28Haya yote ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hivi ndivyo baba yao alivyowaambia alipowabariki, akimpa kila mmoja baraka inayomfaa.

Kifo Cha Yakobo

2949:29 Mwa 25:8; 2Sam 2:32Ndipo alipowapa maelekezo haya: “Mimi niko karibu kukusanywa kwa watu wangu. Mnizike pamoja na baba zangu kwenye pango katika shamba la Efroni, Mhiti, 30pango lililoko katika shamba la Makpela, karibu na Mamre huko Kanaani, ambalo Abrahamu alinunua kwa ajili ya mahali pa kuzikia kutoka kwa Efroni, Mhiti, pamoja na shamba. 3149:31 Mwa 25:9; 23:19Huko ndiko Abrahamu na Sara mkewe walikozikwa, huko akazikwa Isaki na Rebeka mkewe, na huko nilimzika Lea. 32Shamba hilo na pango lililoko ndani yake lilinunuliwa kutoka kwa Wahiti.”

3349:33 Mwa 25:8; Mdo 7:15Baada ya Yakobo kumaliza kutoa maelekezo hayo kwa wanawe, akarudisha miguu yake kitandani, akapumua pumzi ya mwisho, na akakusanywa kwa watu wake.

O Livro

Génesis 49:1-33

Jacob abençoa os filhos

1Então Jacob chamou todos os seus filhos e disse-lhes: “Juntem-se aqui, perto de mim e dir-vos-ei o que será de vocês no futuro.

2Ouçam-me, ó filhos de Jacob,

escutem Israel, o vosso pai!

3Rúben, tu és o mais velho,

o filho que eu tive na maturidade do meu vigor;

és o primeiro em categoria e em honra.

4Mas inconstante como és, semelhante às vagas do mar,

deixarás de ser o mais excelente porque me desonraste,

deitando-te com uma das minhas mulheres,

profanando o meu leito.

5Simeão e Levi são dois da mesma espécie;

são homens de violência e injustiça.

6A minha alma manteve-se afastada deles,

não quis participar nos seus intentos secretos,

porque no seu ódio mataram homens,

na sua excitação mutilaram bois.

7Maldita seja a sua fúria, pois foi feroz e cruel.

Por isso, espalharei os seus descendentes por todo o Israel.

8Judá, os teus irmãos te louvarão.

Destruirás os teus inimigos.

Os filhos do teu pai se inclinarão perante ti.

9És como um pequeno leão

que acabou de tragar a sua presa.

Assenta-se como um forte leão e deita-se como uma leoa;

quem ousará despertá-lo?

10O cetro real não deixará de lhe pertencer,

até que venha Silo, a quem todo o mundo obedecerá.

11Ele amarra o seu jumentinho à melhor videira,

e lava os seus fatos no vinho.

12Seus olhos são mais escuros do que o vinho,

seus dentes mais brancos que o leite.

13Zebulão habitará à beira do mar

e terá os portos de que se servirão os navios.

Os seus limites estender-se-ão até Sídon.

14Issacar é um possante animal de carga

que repousa no meio dos fardos.

15Quando vê que o seu repouso é bom,

e a terra é agradável para se viver,

de boa vontade se entregou ao trabalho

e aceitou a tarefa que lhe era imposta.

16Dan governará o seu povo

tal como qualquer outra tribo de Israel.

17Ele será como uma serpente no caminho,

como uma víbora à beira da estrada

que morde as patas do cavalo,

o qual lança o cavaleiro ao chão.

18Eu confio na tua salvação, Senhor!

19Gad será atacado por um bando de guerrilheiros,

mas ele os atacará pelos calcanhares.

20Aser produzirá alimento abundante

e de finíssima qualidade, próprio de reis.

21Naftali é como uma gazela à solta,

produzindo lindas crias.

22José é como uma árvore frutífera,

produzindo frutos junto duma fonte.

Os seus ramos passam acima do muro.

23Foi gravemente ferido por aqueles

que se atiraram sobre ele e o perseguiram.

24Mas o seu arco permeneceu firme,

e os seus braços jamais esmoreceram,

diante do Poderoso de Jacob,

o seu Pastor, o Rochedo de Israel.

25Que o Deus dos teus pais, o Todo-Poderoso,

te abençoe com as bênçãos dos céus

e também com as da Terra,

as bênçãos dos seios, assim como as da madre,

26Que as bênçãos do teu pai ultrapassem as bênçãos das antigas montanhas,

que chegam às alturas das colinas eternas.

Estas serão as bênçãos que descerão sobre a cabeça de José,

que teve de se separar dos irmãos.

27Benjamim é um lobo que devora a sua presa.

Devora os seus inimigos logo de manhã

e pela tarde reparte os despojos.”

28Estas são as bênçãos que Israel deu aos doze filhos.

A morte de Jacob

29-30Depois disse-lhes: “Vou morrer em breve. Vocês deverão pôr-me junto dos meus pais na terra de Canaã, na gruta que está no campo de Macpela, diante de Mamre, o campo que Abraão comprou a Efrom, o hitita, como terreno para sepultura. 31Foi lá que sepultaram Abraão e Sara, a sua mulher; e ainda Isaque mais a sua mulher Rebeca; eu próprio ali coloquei o corpo de Leia. 32Essa gruta e o campo foram comprados pelo meu avô Abraão aos filhos de Hete.”

33Tendo acabado de dar aquelas profecias e estas indicações aos filhos, deitou-se, acomodou-se na cama, deu um último suspiro e faleceu, juntando-se aos seus antepassados.