Mwanzo 47 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 47:1-31

Yakobo Ambariki Farao

147:1 Mwa 46:31Yosefu akaenda na kumwambia Farao, “Baba yangu na ndugu zangu wamekuja kutoka nchi ya Kanaani wakiwa na makundi yao ya kondoo, mbuzi na ngʼombe, pamoja na kila kitu walicho nacho, nao sasa wapo huko Gosheni.” 2Akachagua ndugu zake watano na kuwaonyesha kwa Farao.

347:3 Mwa 46:33Farao akawauliza hao ndugu zake, “Kazi yenu ni nini?”

Wakamjibu, “Watumishi wako ni wachunga mifugo, kama vile baba zetu walivyokuwa.” 447:4 Mwa 46:34Pia wakamwambia Farao, “Tumekuja kukaa huku kwa muda mfupi, kwa sababu njaa ni kali huko Kanaani, na mifugo ya watumishi wako haina malisho. Kwa hiyo sasa, tafadhali uruhusu watumishi wako wakae huko Gosheni.”

5Farao akamwambia Yosefu, “Baba yako na ndugu zako wamekuja kwako, 647:6 Kut 18:21nayo nchi ya Misri ipo mbele yako, uwakalishe baba yako na ndugu zako katika sehemu iliyo bora kupita zote katika nchi. Na waishi Gosheni. Kama unamfahamu yeyote miongoni mwao mwenye uwezo maalum, waweke wawe wasimamizi wa mifugo yangu.”

747:7 2Sam 14:22Ndipo Yosefu akamleta Yakobo baba yake na kumtambulisha mbele ya Farao. Baada ya Yakobo kumbariki Farao, 8Farao akamuuliza, “Je una umri gani?”

947:9 Mwa 25:7Naye Yakobo akamwambia Farao, “Siku za miaka ya kusafiri kwangu ni miaka 130. Miaka yangu imekuwa michache na ya taabu, wala haikufikia miaka ya kusafiri ya baba zangu.” 1047:10 Mwa 47:7Kisha Yakobo akambariki Farao, naye akaondoka mbele ya uso wake.

1147:11 Hes 33:3, 5Ndipo Yosefu akawakalisha baba yake na ndugu zake katika nchi ya Misri na kuwapa milki katika sehemu bora sana ya nchi, wilaya ya Ramesesi, kama Farao alivyoelekeza. 1247:12 Mwa 45:11Pia Yosefu akampa baba yake, na ndugu zake na wote wa nyumbani mwa baba yake vyakula, kwa kulingana na hesabu ya watoto wao.

Uongozi Wa Yosefu Wakati Wa Njaa

1347:13 Mwa 12:10Hata hivyo, hapakuwepo chakula katika sehemu yote kwa kuwa njaa ilikuwa kali sana; Misri na Kanaani zote zikaharibiwa kwa sababu ya njaa. 1447:14 Kut 7:23Yosefu akakusanya fedha zote zilizopatikana kutoka mauzo ya nafaka huko Misri na Kanaani, akazileta kwenye jumba la kifalme la Farao. 1547:15 Kut 16:3Fedha za watu wa Misri na Kanaani zilipokwisha, Wamisri wote wakamjia Yosefu na kumwambia, “Tupatie chakula. Kwa nini tufe mbele ya macho yako? Fedha zetu zimekwisha.”

1647:16 Mwa 47:18, 19Yosefu akawaambia, “Basi leteni mifugo yenu, nitawauzia chakula kwa kubadilisha na mifugo yenu, kwa kuwa fedha zenu zimekwisha.” 1747:17 Kut 14:9Kwa hiyo wakaleta mifugo yao kwa Yosefu, naye akawapa chakula kwa kubadilishana na farasi zao, kondoo na mbuzi zao, ngʼombe na punda zao. Katika mwaka huo wote Yosefu akawapa chakula kwa kubadilishana na mifugo yao yote.

18Mwaka ule ulipokwisha, wakamjia mwaka uliofuata na kumwambia, “Hatuwezi kuficha ukweli mbele za bwana wetu kwamba, kwa kuwa fedha zetu zimekwisha na wanyama wetu ni mali yako, sasa hakuna chochote kilichosalia kwa ajili ya bwana wetu isipokuwa miili yetu na ardhi yetu. 19Kwa nini tuangamie mbele ya macho yako, sisi pamoja na nchi yetu? Utununue sisi pamoja na ardhi yetu ili kubadilishana kwa chakula. Nasi pamoja na nchi yetu tutakuwa watumwa wa Farao. Tupe sisi mbegu ili tuweze kuishi wala tusife, nchi yetu isije ikawa ukiwa.”

2047:20 Mwa 12:10Kwa hiyo Yosefu akamnunulia Farao nchi yote ya Misri. Wamisri, mmoja baada ya mwingine, waliuza mashamba yao, kwa sababu njaa ilikuwa kali sana kwao. Nchi ikawa mali ya Farao, 21naye Yosefu akawafanya watu watumike kama watumwa, kuanzia upande mmoja wa Misri hadi upande mwingine. 2247:22 Kum 14:28-29Hata hivyo, hakununua nchi ya makuhani, kwa sababu walikuwa wanapata mgawo wao wa kawaida kutoka kwa Farao, nao walikuwa na chakula cha kuwatosha kutokana na mgawo waliopewa na Farao. Hii ndiyo sababu hawakuuza ardhi yao.

2347:23 Neh 5:3Yosefu akawaambia watu, “Kwa vile nimewanunua ninyi pamoja na nchi yenu leo kuwa mali ya Farao, hapa kuna mbegu kwa ajili yenu ili mweze kuziotesha. 2447:24 Mwa 41:34Lakini wakati mazao yatakapokuwa tayari, mpeni Farao sehemu ya tano. Sehemu hizo nne zitakazobaki mtaziweka kama mbegu kwa ajili ya mashamba na kwa ajili ya chakula chenu wenyewe na cha watu wa nyumbani mwenu na watoto wenu.”

2547:25 Mwa 32:5Wakamwambia, “Umeokoa maisha yetu. Basi na tupate kibali mbele ya macho ya bwana wetu; tutakuwa watumwa wa Farao.”

2647:26 Mwa 41:34Basi Yosefu akaiweka iwe sheria kuhusu nchi ya Misri, ambayo inatumika mpaka leo, kwamba, sehemu ya tano ya mazao ni mali ya Farao. Ni nchi ya makuhani tu ambayo haikuwa ya Farao.

2747:27 Mwa 1:22Basi Waisraeli wakaishi Misri katika nchi ya Gosheni. Wakapata mali huko wakastawi na kuongezeka kwa wingi sana.

2847:28 Za 105:23Yakobo akaishi Misri miaka kumi na saba, nayo miaka ya maisha yake ilikuwa 147. 2947:29 Mwa 24:32Wakati ulipokaribia wa Israeli kufa, akamwita mwanawe Yosefu na kumwambia, “Kama nimepata kibali machoni pake, weka mkono wako chini ya paja langu na uniahidi kuwa utanifanyia fadhili na uaminifu. Usinizike Misri, 3047:30 Yos 24:32lakini nitakapopumzika na baba zangu, unichukue kutoka Misri, ukanizike walipozikwa.”

Yosefu akamwambia, “Nitafanya kama unavyosema.”

3147:31 Amu 15:12Akamwambia, “Niapie.” Ndipo Yosefu akamwapia, naye Israeli akaabudu, akiwa ameegemea juu ya kichwa cha fimbo yake.

Swedish Contemporary Bible

1 Moseboken 47:1-31

1Josef gick och berättade för farao: ”Min far och mina bröder har kommit hit från Kanaans land med alla sina hjordar och tillhörigheter. De befinner sig nu i Goshens land.”

2Han hade tagit med sig fem av sina bröder och presenterade dem för farao. 3Farao frågade dem: ”Vad har ni för yrke?” De svarade: ”Vi, dina tjänare, är herdar, som våra förfäder. 4Vi har kommit för att bo en tid här i Egypten, för det finns inget bete för våra hjordar i Kanaan. Hungersnöden har varit mycket svår där. Vi ber dig om tillstånd att få bosätta oss i Goshens land.”

5Farao sa då till Josef: ”Din far och dina bröder har alltså kommit till dig. 6Hela landet är öppet för dig. Låt dem bo i den bästa delen av landet – Goshen passar utmärkt. Och om du vet några av dem som är skickliga nog, så ge dem ansvaret också för mina hjordar.”

7Sedan tog Josef sin far Jakob till farao och Jakob hälsade farao med en välsignelse. 8”Hur gammal är du?” frågade farao honom. 9Jakob svarade: ”Min vandringstid har bara blivit 130 få och hårda år, inte alls som mina förfäders.” 10Sedan välsignade Jakob farao innan han gick därifrån.

11Josef lät sin far och sina bröder bosätta sig i Egypten och gav dem land i de bästa områdena, i Ramses land, precis som farao hade befallt. 12Josefs far och bröder och hela hans fars husfolk fick också sitt underhåll av Josef, alltefter familjernas storlek.

13Hungersnöden blev allt värre i hela regionen, hela Egypten och Kanaans land var utan mat och höll på att gå under av svält. 14Josef tog emot alla de pengar som fanns i Egypten och Kanaan i utbyte mot säd och förde dem till faraos palats. 15När även pengarna tog slut både i Egypten och i Kanaan, kom egypterna till Josef och sa:

”Våra pengar är slut, men ge oss bröd! Varför ska vi behöva dö här inför dig?” 16”Nåväl”, svarade Josef. ”Om era pengar är slut, får ni ge mig era djur i utbyte mot mat.”

17Då förde de sin boskap till Josef i utbyte mot mat. Josef försörjde dem det året i utbyte mot alla hästar, hjordar, kreatur och åsnor i hela Egypten.

18Följande år kom de tillbaka igen och sa: ”Vi kan inte dölja detta för dig, herre. Våra pengar är slut och vår boskap är borta, och det finns inget vi kan erbjuda dig annat än oss själva och den mark vi äger. 19Varför ska vi behöva förgås här inför dig, både vi och vår jord? Köp oss och marken vi äger, i utbyte mot mat, så ska vi med vår mark bli slavar åt farao. Vi överlämnar oss själva i utbyte mot mat, så att vi får leva och så att vårt land inte blir ödelagt.”

20Då köpte Josef upp all mark i Egypten åt farao. Alla egypter sålde sina åkrar till honom, eftersom svälten var så svår, och till slut ägde farao hela landet. 21På så sätt blev hela Egyptens folk faraos slavar47:21 Enligt den samaritanska texten och Septuaginta (och även den latinska Vulgata). Enligt den masoretiska texten blir översättningen: …förflyttades människorna till städer.. 22Det enda land han inte köpte var prästernas, för de fick sitt underhåll från farao och fick således mat av farao och behövde alltså inte sälja sin jord.

23Sedan sa Josef till folket: ”Nu har jag köpt både er och all mark åt farao. Här får ni utsäde till åkrarna. 24Men när ni skördar, så tillhör en femtedel av allt ni får farao. Behåll de resterande fyra femtedelarna till utsäde och till mat åt er själva och era familjer och era barn.” 25”Du har räddat våra liv”, sa de. ”Låt oss alltid få möta din välvilja, herre! Vi blir gärna faraos slavar.”

26Då stiftade Josef en lag för hela Egyptens land och den gäller fortfarande: farao ska ha en femtedel av all skörd som skatt. Detta gällde dock inte det land som ägdes av prästerna.

Jakob och Josef dör i Egypten

Jakob välsignar Josef

27Israeliterna47:27 Israel var det namn Gud gav Jakob i 32:28. Israeliterna betyder alltså Jakobs släkt. bodde alltså i Goshens land i Egypten och skaffade sig mark där. De var fruktsamma och förökade sig mycket.

28Jakob levde sjutton år i Egypten och blev 147 år gammal. 29När tiden närmade sig för honom att dö, kallade han på sin son Josef och sa till honom: ”Visa mig den välviljan att lägga handen under min höft och svär47:29 Se not till 24:3. att du ska visa mig den godheten och trofastheten att du inte begraver mig i Egypten, 30utan när jag gått till vila hos mina fäder47:30 Gå till vila hos sina fäder var ett vanligt sätt att beteckna döden., ta mig ut ur Egypten och begrav mig i deras grav.” Och Josef lovade att göra som han sa. 31”Lova det med en ed”, fortsatte Jakob. Då svor Josef eden, och Israel böjde sig ner, lutad mot sin stav47:31 Enligt Septuaginta och Heb 11:21. Enligt den masoretiska texten: Israel böjde knä vid sängens huvudgärd..