Mwanzo 4 – NEN & HOF

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 4:1-26

Kaini Na Abeli

14:1 Mwa 2:20; Ebr 11:4; 1Yn 3:12; Yud 11Adamu akakutana kimwili na mkewe Eva, naye akapata mimba, akamzaa Kaini. Eva akasema, “Kwa msaada wa Bwana nimemzaa mwanaume.” 24:2 Mt 23:35; Lk 11:51; Ebr 11:4; 12:24; Mwa 2:7Baadaye akamzaa Abeli ndugu yake.

Basi Abeli akawa mfugaji, na Kaini akawa mkulima. 34:3 Law 2:1-2; Isa 43:23; Yer 41:5; Hes 18:12Baada ya muda Kaini akaleta baadhi ya mazao ya shamba kama sadaka kwa Bwana. 44:4 Law 3:16; 2Nya 29:35; Kut 13:2, 12; Kum 15:19; Ebr 11:4Lakini Abeli akaleta fungu nono kutoka baadhi ya wazaliwa wa kwanza wa mifugo yake. Bwana akamkubali Abeli pamoja na sadaka yake, 5lakini Mungu hakumkubali Kaini pamoja na sadaka yake. Kwa hiyo Kaini akakasirika sana, uso wake ukawa na huzuni.

6Kisha Bwana akamwambia Kaini, “Kwa nini umekasirika? Kwa nini uso wako una huzuni? 74:7 Mwa 44:16; Hes 32:23; Isa 59:12; Ay 11:15; 22:27; Za 27:3; 46:2; Rum 6:16Ukifanya lililo sawa, je, hutakubalika? Lakini usipofanya lililo sawa, dhambi inakuvizia mlangoni mwako, inakutamani wewe, lakini inakupasa uishinde.”

84:8 Mt 23:35; Lk 11:51; 1Yn 3:12; Yud 11Basi Kaini akamwambia ndugu yake Abeli, “Twende shambani.” Walipokuwa shambani, Kaini akamshambulia Abeli ndugu yake, akamuua.

94:9 Mwa 3:9; Yn 8:44Kisha Bwana akamuuliza Kaini, “Ndugu yako Abeli yuko wapi?”

Akamjibu, “Sijui, je, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?”

104:10 Mwa 9:5; 37:20, 26; Kut 21:12; Hes 35:33; Kum 21:7-9; 2Sam 4:11; Ay 16:18; 24:2; 31:38; Za 9:12; 106:38; Ebr 12:24; Ufu 6:9-10Bwana akasema, “Umefanya nini? Sikiliza! Damu ya ndugu yako inanililia mimi kutoka ardhini. 114:11 Kum 11:28; 2Fal 2:24Sasa umelaaniwa na umehamishwa kutoka ardhi, ambayo imefungua kinywa chake na kupokea damu ya ndugu yako kutoka mkononi mwako. 124:12 Kum 28:15-24; Za 37:25; 59:15; 109:10Utakapoilima ardhi, haitakupa tena mazao yake. Utakuwa mtu wa kutangatanga duniani asiye na utulivu.”

13Kaini akamwambia Bwana, “Adhabu yangu ni zaidi ya niwezavyo kustahimili. 144:14 2Fal 17:18; Za 51:11; 139:7-12; Yer 7:15; 52:3; Kum 28:64-67; Mwa 9:6; Kut 21:12-14; Law 24:17; Hes 35:19-21, 27; 1Fal 2:32; 2Fal 11:16Leo unanifukuza kutoka nchi, nami nitafichwa mbali na uwepo wako. Nitakuwa mtu wa kutangatanga asiyetulia duniani na yeyote anionaye ataniua.”

154:15 Eze 9:4, 6; Kut 21:20; Law 26:21; Za 79:12Lakini Bwana akamwambia, “La sivyo, ikiwa mtu yeyote atamuua Kaini atalipizwa kisasi mara saba zaidi.” Kisha Bwana akamwekea Kaini alama ili mtu yeyote ambaye angemwona asimuue. 164:16 Yud 11; Mwa 2:8Kwa hiyo Kaini akaondoka mbele za Bwana akaenda kuishi katika nchi ya Nodi, iliyoko mashariki ya Edeni.

174:17 Za 55:9; 49:11Kaini akakutana kimwili na mkewe, naye akapata mimba na akamzaa Enoki. Wakati huo Kaini alikuwa anajenga mji, akauita Enoki jina la mtoto wake. 18Enoki akamzaa Iradi, Iradi akamzaa Mehuyaeli, Mehuyaeli akamzaa Methushaeli, na Methushaeli akamzaa Lameki.

194:19 Mwa 2:9; 29:28; Kum 21:15; Rut 4:11; 1Sam 1:2Lameki alioa wanawake wawili, mmoja aliitwa Ada, na mwingine Sila. 20Ada akamzaa Yabali ambaye ni baba wa wale walioishi katika mahema na kufuga wanyama. 214:21 Mwa 31:27; Kut 15:20; 1Sam 16:16; 1Nya 25:3; Za 33:2; 43:4; 150:4; Isa 16:11; Dan 3:5; Ay 21:12; 30:31Kaka yake aliitwa Yubali, aliyekuwa baba wa wote wapigao zeze na filimbi. 224:22 Kut 35:35; 1Sam 13:19; 2Fal 24:14Pia Sila alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Tubali-Kaini ambaye alifua vifaa vya aina mbalimbali vya shaba na chuma. Naama alikuwa dada wa Tubali-Kaini.

234:23 Mwa 9:6-9; Kut 20:13; 21:12; 23:7; Law 19:18; 24:17; Kum 27:24Lameki akawaambia wake zake,

“Ada na Sila nisikilizeni mimi;

wake wa Lameki sikieni maneno yangu.

Nimemuua mtu kwa kunijeruhi,

kijana mdogo kwa kuniumiza.

244:24 Kum 32:35; 2Fal 9:7; Za 18:47; Isa 35:4; Yer 51:56; Mt 18:22; Nah 1:2Kama Kaini atalipizwa kisasi mara saba,

basi Lameki itakuwa mara sabini na saba.”

254:25 Mwa 5:3; 1Nya 1:1Adamu akakutana kimwili na mke wake tena, akamzaa mwana, akamwita Sethi, akisema, “Mungu amenijalia mwana mwingine badala ya Abeli, kwa kuwa Kaini alimuua.” 264:26 Mwa 5:3; 12:8; 13:4; 21:33; 22:9; 26:25; 33:20; Lk 3:38; Kut 17:15; Sef 3:9; 1Fal 18:24; Za 116:17; Yoe 2:32; Mdo 2:21Naye Sethi akamzaa mwana, akamwita Enoshi.

Wakati huo watu wakaanza kuliitia jina la Bwana.

Hoffnung für Alle

1. Mose 4:1-26

Neid und seine Folgen

1Adam schlief mit seiner Frau Eva, sie wurde schwanger und brachte einen Sohn zur Welt. »Mit der Hilfe des Herrn habe ich einen Sohn bekommen!«, rief sie aus. Darum nannte sie ihn Kain (»Gewinn«). 2Ihren zweiten Sohn nannte sie Abel. Die beiden wuchsen heran; Abel wurde ein Hirte, Kain ein Bauer.

3Eines Tages nahm Kain etwas von dem Ertrag seines Feldes und brachte es dem Herrn als Opfer dar. 4Auch Abel wählte eine Gabe für Gott aus: Er schlachtete einige von den ersten Lämmern seiner Herde und opferte die besten Fleischstücke mitsamt dem Fett daran. Der Herr blickte freundlich auf Abel und nahm sein Opfer an, 5Kain und seinem Opfer hingegen schenkte er keine Beachtung. Darüber wurde Kain sehr zornig und starrte mit finsterer Miene vor sich hin. 6»Warum bist du so zornig und blickst so grimmig zu Boden?«, fragte ihn der Herr. 7»Wenn du Gutes im Sinn hast, kannst du doch jedem offen ins Gesicht sehen. Wenn du jedoch Böses planst, dann lauert die Sünde schon vor deiner Tür. Sie will dich zu Fall bringen, du aber beherrsche sie!«

8Kain forderte seinen Bruder auf: »Komm, wir gehen zusammen aufs Feld!«4,8 »Komm … Feld!« ist nach der griechischen, syrischen und lateinischen Übersetzung ergänzt. Im hebräischen Text fehlt dieser Satz. Als sie dort ankamen, fiel er über Abel her und schlug ihn tot.

9Da fragte der Herr: »Wo ist dein Bruder Abel?« »Woher soll ich das wissen?«, wich Kain aus. »Ist es etwa meine Aufgabe, ständig auf ihn aufzupassen?« 10Aber Gott entgegnete: »Was hast du bloß getan? Das vergossene Blut deines Bruders schreit von der Erde zu mir! 11Darum bist du von nun an verflucht: Weil du deinen Bruder umgebracht und den Acker mit seinem Blut getränkt hast, musst du von diesem fruchtbaren Land fort. 12Wenn du ein Feld bebauen willst, wird es dir kaum noch Ertrag einbringen. Ruhelos musst du von Ort zu Ort ziehen!« 13»Meine Strafe ist zu hart – ich kann sie nicht ertragen!«, erwiderte Kain. 14»Ach, Gott, du verstößt mich von dem Land, das ich zum Leben brauche. Noch dazu muss ich mich vor dir verstecken! Heimatlos werde ich von nun an umherirren, und wenn mich jemand findet, wird er mich umbringen!« 15»Damit dies nicht geschieht«, sagte der Herr, »lege ich Folgendes fest: Wer dich tötet, wird dafür siebenfach bestraft werden!« Er machte ein Zeichen an Kain, damit jeder, der ihm begegnete, wusste: Kain darf man nicht töten. 16Dann verließ Kain die Nähe des Herrn und wohnte im Land Nod (»Land des ruhelosen Lebens«), östlich von Eden.

Kains Nachkommen

17Als Kain mit seiner Frau schlief, wurde sie schwanger und brachte einige Zeit später einen Sohn zur Welt: Henoch. Kain baute eine Stadt und benannte sie nach ihm. 18Henoch hatte einen Sohn namens Irad, Irads Sohn war Mehujaël, dessen Sohn hieß Metuschaël, der war der Vater von Lamech. 19Lamech heiratete zwei Frauen: Ada und Zilla. 20Ein Sohn Adas war Jabal – von ihm stammen alle ab, die mit ihren Herden umherziehen und in Zelten wohnen. 21Sein Bruder hieß Jubal – auf ihn gehen alle die zurück, die Laute und Flöte spielen. 22Auch Zilla bekam einen Sohn: Tubal-Kain; er war der Erste, der Geräte aus Bronze und Eisen herstellte. Seine Schwester hieß Naama.

23Lamech sagte zu seinen Frauen: »Ada und Zilla, meine Frauen, hört mir gut zu: Wenn ein Mann mich verwundet, erschlage ich ihn – ja, für eine einzige Strieme bringe ich ihn um! 24Wenn schon ein Mord an Kain siebenfach bestraft wird – für Lamech wird alles siebenundsiebzigmal gerächt!«

Set und Enosch

25Adam und Eva bekamen noch einen Sohn. Eva nannte ihn Set (»Ersatz«). »Gott hat mir einen anderen Nachkommen geschenkt!«, sagte sie. »Er wird mir Abel ersetzen, den Kain erschlagen hat!« 26Auch Set bekam später einen Sohn und nannte ihn Enosch (»Mensch«). Zu dieser Zeit begannen die Menschen, zum Herrn zu beten.