Mwanzo 26 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 26:1-35

Isaki Na Abimeleki

126:1 Mwa 12:10; 20:1Basi njaa kubwa ikawa katika nchi hiyo, kuliko ile njaa iliyotangulia iliyotokea wakati wa Abrahamu. Isaki akamwendea Abimeleki mfalme wa Wafilisti huko Gerari. 226:2 Mwa 12:1, 7; 46:3Bwana akamtokea Isaki, akamwambia, “Usiende Misri, bali ukae katika nchi nitakayokuambia. 326:3 Kut 3:12; Mwa 12:2, 7Kaa katika nchi hii kwa kitambo, mimi nitakuwa pamoja na wewe na nitakubariki. Kwa maana nitakupa wewe na uzao wako nchi hizi zote na nitatimiza kiapo nilichomwapia Abrahamu baba yako. 426:4 Mwa 26:24; 48:4; 12:2Nitafanya wazao wako kuwa wengi kama nyota za angani, nami nitawapa nchi hizi zote na kutokana na uzao wako mataifa yote yatabarikiwa, 526:5 Mwa 18:19; Za 119:80, 112; Eze 18:21kwa sababu Abrahamu alinitii mimi akatunza kanuni zangu na maagizo yangu, amri zangu pamoja na sheria zangu.” 626:6 Mwa 20:1Hivyo Isaki akaishi huko Gerari.

726:7 Mwa 12:13Watu wa mahali pale walipomuuliza habari za mke wake, akasema, “Huyu ni dada yangu,” kwa sababu aliogopa kusema, “Huyu ni mke wangu.” Alifikiri, “Watu wa mahali pale wataweza kumuua kwa sababu ya Rebeka, kwa kuwa alikuwa mzuri wa sura.”

8Wakati Isaki alipokuwa amekaa huko siku nyingi, Abimeleki mfalme wa Wafilisti akachungulia dirishani, akaona jinsi Isaki alivyomkumbatia Rebeka mke wake. 9Abimeleki akamwita Isaki akamwambia, “Hakika huyu ni mke wako! Mbona uliniambia, ‘Huyu ni dada yangu?’ ”

Isaki akamjibu, “Kwa sababu nilifikiri ningeweza kuuawa kwa sababu yake.”

1026:10 Mwa 12:8Ndipo Abimeleki akamjibu, “Ni nini hiki ulichotufanyia? Ingewezekana mtu yeyote akawa amekutana kimwili na mke wako, nawe ungeleta hatia juu yetu.”

1126:11 1Sam 24:6; 26:9; Za 105:15Hivyo Abimeleki akatoa amri kwa watu wote, akisema, “Yeyote atakayemnyanyasa mtu huyu au mkewe hakika atauawa.”

1226:12 Mt 13:8; Mwa 26:3Isaki akapanda mazao katika nchi hiyo, kwa mwaka huo huo, akavuna mara mia, kwa sababu Bwana alimbariki. 1326:13 Mwa 13:2; Kum 8:18Isaki akawa tajiri, mali zake zikaendelea kuongezeka mpaka akawa tajiri sana. 1426:14 Mwa 12:16; 24:36Akawa na mifugo ya kondoo na ngʼombe, na watumishi wengi sana, kiasi kwamba Wafilisti wakamwonea wivu. 1526:15 Mwa 21:30; 21:25Kwa hiyo visima vyote vilivyochimbwa na watumishi wakati wa Abrahamu baba yake, Wafilisti wakavifukia, wakavijaza udongo.

16Ndipo Abimeleki akamwambia Isaki, “Ondoka kwetu, kwa maana umetuzidi nguvu sana.”

17Basi Isaki akatoka huko akajenga kambi katika Bonde la Gerari, akaishi huko. 18Ndipo Isaki akavichimbua tena vile visima vya maji ambavyo vilichimbwa siku zile za Abrahamu baba yake, ambavyo Wafilisti walivifukia baada ya kufa Abrahamu, akavipa majina yale yale ambayo baba yake alikuwa amevipa.

19Watumishi wa Isaki wakachimba katika lile bonde wakagundua huko kisima chenye maji safi. 20Lakini wachungaji wa Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaki wakisema, “Maji haya ni yetu!” Ndipo akakiita kile kisima Eseki,26:20 Eseki maana yake ni Ugomvi. kwa sababu waligombana naye. 21Kisha wakachimba kisima kingine, lakini hata hicho pia wakakigombania, akakiita Sitna.26:21 Sitna maana yake Upinzani. 2226:22 Kut 18:19; Mwa 17:6Akaondoka huko, akachimba kisima kingine, wala hakuna yeyote aliyekigombania. Akakiita Rehobothi,26:22 Rehobothi maana yake ni Mungu ametufanyia nafasi. akisema, “Sasa Bwana ametufanyia nafasi, nasi tutastawi katika nchi.”

23Kutoka pale akaenda Beer-Sheba. 2426:24 Mwa 24:12; 17:7Usiku ule Bwana akamtokea, akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa Abrahamu baba yako. Usiogope, kwa maana mimi niko pamoja nawe, nitakubariki na kuongeza idadi ya wazao wako kwa ajili ya Abrahamu mtumishi wangu.”

25Isaki akajenga madhabahu huko, akaliitia jina la Bwana. Akapiga hema lake huko, nao watumishi wake wakachimba kisima.

2626:26 Mwa 21:22Wakati huo, Abimeleki alikuwa amemjia kutoka Gerari, akifuatana na Ahuzathi mshauri wake, pamoja na Fikoli jemadari wa majeshi yake. 27Isaki akawauliza, “Mbona mmekuja kwangu na ninyi mlinichukia na kunifukuza?”

2826:28 Mwa 21:22Wakamjibu, “Tuliona wazi kuwa Bwana alikuwa pamoja nawe, kwa hiyo tukasema, ‘Inabidi kuwe na kiapo cha mapatano kati yetu, kati yetu na wewe. Na tufanye mkataba pamoja nawe 2926:29 Mwa 31:29, 52; 24:31kwamba hutatudhuru, kama jinsi nasi hatukuwanyanyasa bali tuliwatendea mema wakati wote na kuwaondoa kwetu kwa amani. Tena sasa umebarikiwa na Bwana.’ ”

3026:30 Mwa 31:54; Kut 18:12Basi Isaki akawaandalia karamu, nao wakala na kunywa. 3126:31 Mwa 21:23, 27Kesho yake asubuhi na mapema, wakaapizana wao kwa wao. Kisha Isaki akawaruhusu waende zao, wakamwacha Isaki kwa amani.

3226:32 Mwa 21:30Siku hiyo watumishi wa Isaki wakaja wakampa habari kuhusu kisima walichokuwa wamekichimba, wakamwambia, “Tumepata maji!” 3326:33 Mwa 21:14Naye akakiita Shiba,26:33 Shiba kwa Kiebrania maana yake ni Saba. mpaka leo mji huo unaitwa Beer-Sheba.26:33 Beer-Sheba maana yake ni Kisima cha wale saba, yaani wale kondoo saba ambao Abrahamu aliwatoa kama ushahidi kati yake na Abimeleki.

3426:34 Mwa 36:2Esau alipokuwa na umri wa miaka arobaini, akamwoa Yudithi binti Beeri Mhiti, kisha akamwoa Basemathi binti Eloni Mhiti. 3526:35 Mwa 27:46; Ay 7:16Hawa walikuwa chanzo cha huzuni ya Isaki na Rebeka.

La Bible du Semeur

Genèse 26:1-35

Isaac à Guérar

1A cette époque-là, il y eut de nouveau une famine dans le pays, comme naguère au temps d’Abraham. Alors Isaac se rendit à Guérar chez Abimélek26.1 Sans doute, un nom héréditaire (comme pharaon en Egypte) puisqu’un roi du même nom a régné sur cette contrée environ quatre-vingts ans auparavant (20.2)., roi des Philistins26.1 Voir note 10.14.. 2En effet, l’Eternel lui était apparu et lui avait dit : Ne descends pas en Egypte26.2 Où l’on se rendait généralement en cas de famine (12.10 ; 41.57). ! Fixe-toi dans le pays que je te désignerai. 3Séjourne dans ce pays-ci. Je serai avec toi et je te bénirai. Car c’est à toi et à ta descendance que je donnerai tous ces territoires. J’accomplirai ainsi le serment que j’ai fait à ton père Abraham. 4Je rendrai ta descendance aussi nombreuse que les étoiles du ciel et je lui donnerai tous ces territoires-ci, et tous les peuples de la terre seront bénis en ta descendance26.4 Autre traduction : se béniront en citant l’exemple de ta descendance.. 5Je le ferai parce qu’Abraham m’a obéi et qu’il a observé mes prescriptions, mes commandements, mes préceptes et mes lois. 6C’est pourquoi Isaac resta à Guérar.

7Lorsque les hommes de l’endroit s’enquéraient au sujet de sa femme, il répondait : C’est ma sœur.

Il ne disait pas qu’elle était sa femme : il avait peur que les gens de l’endroit le tuent à cause d’elle, car elle était belle. 8Comme il était déjà depuis assez longtemps dans le pays, Abimélek, le roi des Philistins, regardant par la fenêtre, surprit Isaac en train de s’amuser avec Rébecca sa femme. 9Alors il le fit appeler et lui dit : C’est sûrement ta femme. Pourquoi as-tu dit : « C’est ma sœur » ?

Isaac lui répondit : Je me disais que je risquais de mourir à cause d’elle.

10Abimélek rétorqua : Te rends-tu compte de ce que tu nous as fait là ? Il s’en est fallu de peu qu’un homme de ce peuple couche avec ta femme ; dans ce cas, tu nous aurais chargés d’une lourde culpabilité.

11Alors Abimélek fit publier ce décret à tout le peuple : Quiconque fera du mal à cet homme ou à sa femme sera puni de mort.

L’installation à Beer-Sheva

12Isaac fit des semailles dans le pays et récolta cette année-là le centuple de ce qu’il avait semé. L’Eternel le bénissait.

13Isaac devint un personnage important. Son importance s’accrut encore et il devint même un homme très puissant. 14Il possédait des troupeaux de moutons, de chèvres et de bovins, et beaucoup de serviteurs, de sorte que les Philistins devinrent jaloux de lui. 15Ils comblèrent tous les puits que les serviteurs de son père Abraham avaient creusés à son époque en les remplissant de terre. 16Alors Abimélek dit à Isaac : Va, quitte ce pays, car tu es devenu beaucoup plus puissant que nous.

17Isaac partit et alla dresser son camp dans la vallée de Guérar où il s’établit. 18Il s’installa et fit déboucher les puits qu’on avait creusés du temps de son père Abraham et que les Philistins avaient comblés après la mort d’Abraham, et il leur donna les mêmes noms que son père. 19En creusant dans la vallée, les serviteurs d’Isaac découvrirent une source d’eau vive. 20Les bergers de Guérar cherchèrent querelle aux bergers d’Isaac en prétendant : « Cette eau est à nous. » Isaac donna à ce puits le nom d’Eseq (Dispute) parce qu’on s’était disputé avec lui à son sujet. 21Ensuite ils creusèrent un autre puits, pour lequel on lui chercha de nouveau querelle ; il le nomma Sitna (Opposition). 22Puis il partit de là et creusa un autre puits pour lequel on ne lui chercha pas querelle ; il l’appela donc Rehoboth (Larges espaces), car, dit-il, maintenant l’Eternel nous a mis au large et nous prospérerons dans le pays. 23De là, il remonta à Beer-Sheva.

Isaac fait alliance avec Abimélek

24La nuit de son arrivée, l’Eternel lui apparut et lui dit : Je suis le Dieu de ton père Abraham. Sois sans crainte car je suis avec toi ; je te bénirai et je te donnerai une nombreuse descendance à cause d’Abraham, mon serviteur.

25Isaac bâtit un autel à cet endroit, il y invoqua l’Eternel et y dressa sa tente. Les serviteurs d’Isaac y creusèrent un autre puits.

26Abimélek vint le trouver depuis Guérar avec Ahouzath son conseiller, et Pikol, le chef de son armée. 27Isaac leur demanda : Pourquoi êtes-vous venus me trouver, alors que vous me détestez et que vous m’avez renvoyé de chez vous ?

28Ils lui répondirent : Nous avons bien vu que l’Eternel est avec toi, et nous nous sommes dit : Nous devrions nous engager, nous et toi, par serment ! Nous voudrions donc faire alliance avec toi. 29Promets-nous, en le jurant, de ne pas nous faire de mal, comme nous ne t’avons pas fait de mal, car nous t’avons toujours bien traité et nous t’avons laissé partir sain et sauf. A présent tu es béni par l’Eternel.

30Isaac leur fit préparer un grand festin ; ils mangèrent et burent 31et, le lendemain de bon matin, ils s’engagèrent l’un envers l’autre par serment, puis Isaac les reconduisit et ils le quittèrent en bons termes.

32Or, ce même jour, les serviteurs d’Isaac vinrent lui annoncer qu’ils avaient trouvé de l’eau dans le puits qu’ils étaient en train de creuser. 33Alors Isaac appela ce puits Shibea (Serment). C’est pour cela que la ville se nomme Beer-Sheva (le Puits du Serment) jusqu’à ce jour.

Les mariages d’Esaü

34A l’âge de quarante ans, Esaü épousa Judith, fille de Beéri le Hittite, et Basmath, fille d’Elôn le Hittite. 35Elles rendirent toutes deux la vie amère à Isaac et à Rébecca.