Mwanzo 22 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 22:1-24

Kujua Uthabiti Wa Abrahamu

122:1 Kut 15:25; 16:4; 20:20; Kum 8:2, 16; 13:3; Amu 2:22; 3:1; 2Nya 32:31; Za 66:10; Ebr 11:17; Yak 1:12-13; Mwa 31:11; 46:2; 1Sam 3:4-8; Isa 6:8Baadaye Mungu akamjaribu Abrahamu. Akamwambia, “Abrahamu!”

Abrahamu akajibu, “Mimi hapa.”

222:2 Yn 3:16; Ebr 11:17; 1Yn 4:9; Mwa 8:20Kisha Mungu akamwambia, “Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, Isaki umpendaye, uende katika nchi ya Moria. Mtoe huko kama sadaka ya kuteketezwa juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.”

322:3 Yos 8:10Abrahamu akaamka asubuhi na mapema siku iliyofuata, akamtayarisha punda wake. Akawachukua watumishi wake wawili pamoja na Isaki mwanawe. Baada ya kuchanja kuni za kutosha kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka kuelekea mahali Mungu alipokuwa amemwambia. 4Siku ya tatu Abrahamu akainua macho, akapaona mahali pale kwa mbali. 522:5 Kut 24:14Akawaambia watumishi wake, “Kaeni hapa pamoja na punda, wakati mimi na kijana tunakwenda kule. Tutakwenda kuabudu na kisha tutawarudia.”

622:6 Yn 19:17; Amu 19:29Abrahamu akachukua kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, akamtwika Isaki mwanawe, yeye mwenyewe akachukua moto na kisu. Walipokuwa wakienda pamoja, 722:7 Kut 29:38-42; Law 1:10; Ufu 13:8Isaki akanena akamwambia Abrahamu baba yake, “Baba yangu!”

Abrahamu akaitika, “Mimi hapa, mwanangu.”

Isaki akasema, “Moto na kuni zipo, Je, yuko wapi mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa?”

822:8 Yn 1:29Abrahamu akajibu, “Mwanangu, Mungu mwenyewe atajipatia mwana-kondoo kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa.” Nao hawa wawili wakaendelea mbele pamoja.

922:9 Mwa 4:26; 8:20; Law 1:7; 1Fal 18:33; Ebr 11:17-19; Yak 2:21Walipofika mahali pale alipokuwa ameambiwa na Mungu, Abrahamu akajenga madhabahu hapo, akaziweka kuni juu yake. Akamfunga Isaki mwanawe na akamlaza kwenye madhabahu, juu ya zile kuni. 1022:10 Mwa 18:19Kisha akanyoosha mkono wake na akachukua kisu ili amchinje mwanawe. 1122:11 Mwa 16:7; 21:17; 46:2Lakini malaika wa Bwana akamwita kutoka mbinguni, akamwambia, “Abrahamu! Abrahamu!”

Akajibu, “Mimi hapa.”

1222:12 Mwa 18:19; 42:18; Kut 18:21; 1Sam 15:22; Ay 1:1; 37:24; Mit 8:13; Yak 2:21-23; Yn 3:16; 1Yn 4:9Akamwambia, “Usimdhuru kijana, wala usimtendee jambo lolote. Sasa ninajua kwamba unamcha Mungu, kwa sababu hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee.”

1322:13 Mwa 8:20; Rum 8:32Abrahamu akainua macho yake, akaona kondoo dume amenaswa pembe zake nyuma yake katika kichaka. Akaenda akamchukua huyo kondoo dume, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe. 1422:14 Kut 17:15; Amu 6:24; Isa 30:29Abrahamu akapaita mahali pale Yehova-Yire.22:14 Yehova-Yire maana yake Bwana atatupa. Mpaka siku ya leo inasemekana, “Katika mlima wa Bwana itapatikana.”

1522:15 Mwa 21:17Basi malaika wa Bwana akamwita Abrahamu kutoka mbinguni mara ya pili, 1622:16 Kut 13:11; 32:13; 33:1; Isa 45:23; 62:8; Yer 22:5; 44:26; 49:13; 51:14; Amo 6:8; Ebr 6:13; Lk 1:73akasema, “Ninaapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, kwamba kwa sababu umefanya jambo hili na hukunizuilia mwanao, mwana wako wa pekee, 1722:17 Mwa 12:2; 15:5; 26:24; 24:60; Ebr 6:14; Kut 32:13; Kum 7:7; 28:62; Hos 1:10; Rum 9:27; Ebr 11:12; Es 9:2hakika nitakubariki, na nitauzidisha uzao wako kama nyota za angani na kama mchanga ulioko pwani. Wazao wako watamiliki miji ya adui zao, 1822:18 Mwa 12:2-3; 17:2, 9; Mdo 3:25; Gal 3:8; Za 105:9na kupitia uzao wako mataifa yote duniani yatabarikiwa, kwa sababu umenitii.”

1922:19 Mwa 21:14; 26:23; 28:10Ndipo Abrahamu akawarudia watumishi wake, wakaondoka wakaenda wote pamoja mpaka Beer-Sheba. Abrahamu akaishi huko Beer-Sheba.

Wana Wa Nahori

2022:20 Mwa 11:29Baada ya muda, Abrahamu akaambiwa, “Milka pia amepata watoto, amemzalia ndugu yako Nahori wana: 2122:21 Mwa 10:23; Ay 32:2; Yer 25:23Usi mzaliwa wake wa kwanza, Buzi nduguye, Kemueli (baba wa Aramu), 2222:22 Mwa 24:15, 47; 25:20Kesedi, Hazo, Pildashi, Yidlafu na Bethueli.” 2322:23 Mwa 24:15; 11:29Bethueli akamzaa Rebeka. Milka alimzalia Nahori nduguye Abrahamu hao wana wanane. 2422:24 Mwa 25:6; 35:22; 36:12; Amu 8:31; 2Sam 3:7; 1Fal 2:22; 11:3; 1Nya 1:32; Wim 6:8Suria wake Nahori aliyeitwa Reuma pia alikuwa na wana: Teba, Gahamu, Tahashi na Maaka.

La Bible du Semeur

Genèse 22:1-24

Isaac sera-t-il sacrifié ?

1Après ces événements, Dieu mit Abraham à l’épreuve22.1 Allusion en Jc 2.21.. Il l’appela : Abraham !

Et celui-ci répondit : Me voici.

2– Prends Isaac, ton fils unique, que tu aimes, lui dit Dieu, et va au pays de Moriya. Là, tu me l’offriras en sacrifice sur l’une des collines, celle que je t’indiquerai22.2 Voir Hé 11.17-19. Moriya: voir 2 Ch 3.1. offriras en sacrifice: allusion en Hé 11.17-19..

3Le lendemain, Abraham se leva de grand matin, sella son âne et emmena deux de ses serviteurs ainsi que son fils Isaac ; il fendit du bois pour l’holocauste, puis il se mit en route en direction de l’endroit que Dieu lui avait indiqué.

4Après trois jours de marche, Abraham, levant les yeux, aperçut le lieu dans le lointain. 5Alors il dit à ses serviteurs : Restez ici avec l’âne ; le garçon et moi, nous irons jusque là-bas pour adorer Dieu, puis nous reviendrons vers vous.

6Abraham chargea le bois de l’holocauste sur son fils Isaac ; il prit lui-même des braises pour le feu et le couteau, puis tous deux s’en allèrent ensemble.

7Isaac s’adressa à son père Abraham et lui dit : Mon père !

Abraham dit : Qu’y a-t-il, mon fils ?

– Voici le feu et le bois, dit-il, mais où est l’agneau pour l’holocauste ?

8Abraham répondit : Mon fils, Dieu pourvoira lui-même à l’agneau pour l’holocauste.

Et ils poursuivirent leur chemin tous deux ensemble.

9Quand ils furent arrivés à l’endroit que Dieu lui avait indiqué, Abraham construisit un autel et y disposa les bûches. Puis il ligota son fils Isaac et le mit sur l’autel par-dessus le bois. 10Alors Abraham prit en main le couteau pour immoler son fils. 11A ce moment-là, l’ange de l’Eternel lui cria du haut du ciel : Abraham ! Abraham !

– Me voici, répondit-il.

12L’ange reprit : Ne porte pas la main sur le garçon, ne lui fais pas de mal, car maintenant je sais que tu crains Dieu puisque tu ne m’as pas refusé ton fils unique.

13Alors Abraham aperçut un bélier qui s’était pris les cornes dans un buisson22.13 D’après certains manuscrits, le Pentateuque samaritain et la version syriaque. Le texte hébreu traditionnel a : derrière lui.. Il s’en saisit et l’offrit en holocauste à la place de son fils. 14Abraham appela ce lieu-là : Adonaï-Yireéh (le Seigneur pourvoira). C’est pourquoi on dit aujourd’hui : Sur la montagne du Seigneur, il sera pourvu.

15Puis l’ange de l’Eternel appela une seconde fois Abraham du haut du ciel 16et lui dit : Je le jure par moi-même, parole de l’Eternel, puisque tu as fait cela, puisque tu ne m’as pas refusé ton fils, ton unique, 17je te comblerai de bénédictions, je multiplierai ta descendance et je la rendrai aussi nombreuse que les étoiles du ciel et que les grains de sable au bord de la mer. Ta descendance dominera sur ses ennemis22.17 Les v. 16-17 sont cités en Hé 6.13-14.. 18Tous les peuples de la terre seront bénis à travers ta descendance parce que tu m’as obéi.

19Abraham revint vers ses serviteurs et ils se remirent ensemble en route pour rentrer à Beer-Sheva où Abraham continua d’habiter.

La descendance de Nahor

20Après ces événements, on annonça à Abraham que Milka avait donné des enfants à Nahor, son frère : 21Outs son premier-né, Bouz le second, Qemouel, père d’Aram, 22Késéd, Hazo, Pildash, Yidlaph et Betouel. 23Betouel fut le père de Rébecca. Ce sont là les huit fils que Milka avait donnés à Nahor, frère d’Abraham. 24Son épouse de second rang Reouma lui donna aussi des enfants : Tébah, Gaham, Tahash et Maaka.