Mwanzo 18 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 18:1-33

Wageni Watatu

118:1 Mwa 12:7; 13:18; 14:13; 19:1; 23:10, 18; 34:20-24; Rut 4:1; Ebr 11:9; Za 69:12Bwana akamtokea Abrahamu karibu na mialoni ya Mamre wakati alipokuwa ameketi kwenye ingilio la hema lake wakati wa adhuhuri. 218:2 Mwa 17:2-3; 19:1, 10; 24:63; 32:24; 43:28; Yos 5:13; Ebr 13:2; Amu 13:6-11; Hos 12:2-4Abrahamu akainua macho akaona watu watatu wamesimama karibu naye. Alipowaona, aliharakisha kutoka kwenye ingilio la hema lake kuwalaki na kuwasujudia hadi nchi.

3Akasema, “Kama nimepata kibali machoni penu, ee bwana wangu, usimpite mtumishi wako. 418:4 Mwa 19:2; 24:32; 43:24; Amu 19:21; 2Sam 11:8; Lk 7:44Acha yaletwe maji kidogo, kisha ninyi nyote mnawe miguu yenu na mpumzike chini ya mti huu. 518:5 Amu 13:15; 19:5Niruhusuni niwapatie chakula kidogo mle, ili mpate nguvu mwendelee na safari yenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.”

Nao wakamjibu, “Vema sana, fanya kama unavyosema.”

618:6 Mwa 19:3; 2Sam 13:8Hivyo Abrahamu akaharakisha akaingia hemani kwa Sara, akamwambia, “Chukua vipimo vitatu vya unga laini haraka, ukande na uoke mikate.”

718:7 1Sam 28:24; Lk 15:23Kisha Abrahamu akakimbia kwenda kwenye kundi, akachagua ndama mzuri, laini na akampa mtumishi, ambaye aliharakisha kumtayarisha. 818:8 Isa 7:15, 22; Amu 4:19; 5:25; 6:19Kisha akaleta jibini, maziwa na nyama ya yule ndama iliyoandaliwa, akaviweka mbele ya wageni. Walipokuwa wakila, alisimama karibu nao chini ya mti.

918:9 Mwa 3:9; 24:67; Ebr 11:9Wakamuuliza, “Yuko wapi Sara mkeo?”

Akasema, “Yuko huko, ndani ya hema.”

1018:10 Mwa 17:6, 21; 21:2; 2Fal 4:16; Rum 6:6Kisha Bwana akasema, “Hakika nitakurudia tena majira kama haya mwakani na Sara mkeo atakuwa ana mwana.”

Sara alikuwa akiwasikiliza kwenye ingilio la hema, lililokuwa nyuma yake. 1118:11 Mwa 11:30; 17:17; Lk 1:18; Rum 4:19; Ebr 11:11-12Abrahamu na Sara walikuwa wazee tena waliosogea miaka, naye Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake. 1218:12 Mwa 17:17; 21:6; 1Pet 3:6Hivyo Sara akacheka kimoyomoyo alipokuwa akiwaza, “Baada ya mimi kuwa mkongwe hivi na bwana wangu amezeeka, je, nitaweza kufurahia jambo hili?”

1318:13 Mwa 17:17Ndipo Bwana akamwambia Abrahamu, “Kwa nini Sara amecheka na kusema, ‘Kweli nitazaa mtoto nami sasa ni mzee?’ 1418:14 Ay 42:2; Isa 40:29; 50:2; 51:9; Gal 4:23; Yer 32:17; Mt 19:26; Rum 4:21; 9:9; Mwa 17:19Je, kuna jambo lolote gumu lisilowezekana kwa Bwana? Nitakurudia mwakani majira kama haya, naye Sara atakuwa na mwana.”

15Sara akaogopa kwa kuwa alidanganya na kusema, “Mimi sikucheka.”

Lakini Bwana akasema, “Ndiyo, ulicheka!”

Abrahamu Aiombea Sodoma

16Wakati watu hao waliposimama ili waondoke, walielekeza nyuso zao Sodoma, Abrahamu akawatoa kitambo kidogo ili awasindikize. 1718:17 Amo 3:7; Mwa 19:24; Ay 1:16; Za 107:34Ndipo Bwana akasema, “Je, nimfiche Abrahamu jambo ninalokusudia kufanya? 1818:18 Mwa 12:2; Gal 3:8Hakika Abrahamu atakuwa taifa kubwa na lenye nguvu, kupitia kwake mataifa yote ya dunia yatabarikiwa. 1918:19 Mwa 16:11; 17:9; 22:12, 18; 26:5; Kum 4:9-10; 6:7; Isa 14:1; Efe 6:4; Yos 24:15; Yer 23:5; 2Sam 8:15; Za 17:2; 99:4Kwa maana nimemchagua yeye, ili awaongoze watoto wake na jamaa yake kufuata njia ya Bwana, kwa kuwa waadilifu na kutenda haki, ili Bwana atimize ahadi yake kwa Abrahamu.”

2018:20 Isa 1:10; Yer 23:14; Eze 16:46; Mwa 13:13; 19:13Basi Bwana akasema, “Kilio dhidi ya Sodoma na Gomora ni kikubwa sana na dhambi yao inasikitisha sana, 2118:21 Mwa 11:5kwamba nitashuka nione kama waliyoyatenda ni mabaya kiasi cha kilio kilichonifikia. Kama sivyo, nitajua.”

2218:22 Mwa 19:1, 27Basi wale watu wakageuka wakaenda kuelekea Sodoma, lakini Abrahamu akabaki amesimama mbele za Bwana. 2318:23 Kut 23:7; 2Pet 2:9; Law 4:3, 22, 27; Hes 16:22; Eze 18:4; Kum 27:25; 2Sam 24:17; Za 11:4-7; 94:21Ndipo Abrahamu akamsogelea akasema: “Je, utawaangamiza wenye haki na waovu? 2418:24 Yer 5:1Je, ikiwa watakuwepo watu wenye haki hamsini katika mji huo, hivi kweli utauangamiza na wala hutauacha kwa ajili ya hao watu hamsini wenye haki waliomo ndani yake? 2518:25 Mwa 20:4; 44:7; Kum 32:4; 1:16-17; Rum 3:6; Ay 8:3-7; 9:15; 34:10; 36:23; Isa 3:10-11; 5:20; Amo 5:15; Mal 2:17; 3:18; Amu 11:27; Za 7:11; 58:11; 75:7; 94:2; 119:137; Ebr 12:23; 2Nya 19:7; Ezr 9:15; Neh 9:33; Eze 18:25; Dan 4:37; 9:14Hilo na liwe mbali nawe, kufanya jambo kama hilo, kuwaua wenye haki pamoja na waovu, kuwatendea wenye haki sawasawa na waovu. Iwe mbali nawe! Je, Mwamuzi wa dunia yote hatafanya lililo sawa?”

26Bwana akasema, “Kama nikipata watu hamsini wenye haki katika mji wa Sodoma, nitausamehe huo mji wote kwa ajili yao.”

2718:27 Mwa 2:7; Ay 2:8Kisha Abrahamu akasema tena: “Sasa kwa kuwa nimekuwa na ujasiri wa kuzungumza na Bwana, ingawa mimi si kitu bali ni mavumbi na majivu; 28je, kama hesabu ya wenye haki imepungua watano katika hamsini, utauangamiza huo mji wote kwa ajili ya hao watano waliopungua?”

Bwana akamwambia, “Kama nikiwakuta huko watu arobaini na watano, sitauangamiza.”

29Abrahamu akazungumza naye kwa mara nyingine, “Je, kama huko watapatikana watu arobaini tu?”

Akamjibu, “Kwa ajili ya hao arobaini, sitauangamiza.”

3018:30 Mwa 44:18; Kut 32:22Ndipo akasema, “Bwana na asikasirike, lakini niruhusu nizungumze. Je, kama huko watakuwepo thelathini tu?”

Akajibu, “Sitapaangamiza ikiwa nitawakuta huko watu thelathini.”

31Abrahamu akasema, “Sasa kwa kuwa nimekuwa na ujasiri sana kuzungumza na Bwana, je, kama wakipatikana huko watu ishirini tu?”

Bwana akajibu, “Kwa ajili ya hao ishirini, sitauangamiza.”

3218:32 Amu 6:39; Yer 5:1Abrahamu akasema, “Bwana na asikasirike, lakini niruhusu nizungumze tena mara moja tu. Itakuwaje kama watapatikana huko watu kumi tu?”

Bwana akajibu, “Kwa ajili ya hao kumi, sitauangamiza.”

3318:33 Kut 31:18; Mwa 17:22; 31:55Bwana alipomaliza kuzungumza na Abrahamu, akaondoka, naye Abrahamu akarudi nyumbani kwake.

Bibelen på hverdagsdansk

1. Mosebog 18:1-33

Gud besøger Abraham og gentager løftet om en søn

1Mens Abraham boede i Mamres egelund, viste Herren sig for ham igen. En dag sad Abraham i teltåbningen på den varmeste tid af dagen. 2Pludselig lagde han mærke til, at der stod tre mænd i nærheden. Han løb dem i møde og bød dem velkommen ved at bøje sig dybt til jorden.

3„Herre,” sagde han, „vis mig den gunst ikke at gå din tjeners dør forbi, men tag imod min gæstfrihed. 4Lad mig sørge for, at I får vand til at vaske støvet af jeres fødder. I kan hvile jer under træet her. 5Så kommer jeg med lidt mad, som I kan styrke jer på. Siden I nu er kommet denne vej, håber jeg, I vil gøre mig den ære at blive lidt, inden I rejser videre.” „Tak, det vil vi gerne,” svarede de.

6Abraham skyndte sig tilbage til teltet og gav besked til Sara: „Hurtigt! tag det bedste mel, vi har, og lav noget brød af det.” 7Så løb han videre ud til kvægflokken, hvor han udvalgte en fedekalv og gav den til en tjener, som skyndte sig at slagte den. 8Da maden var klar, tog Abraham syrnet mælk og sødmælk samt noget af den stegte kalv og serverede det for mændene. Han vartede selv op, mens mændene sad og spiste ude under træerne.

9„Hvor er Sara, din kone?” spurgte en af mændene. „Inde i teltet,” svarede Abraham. 10Da sagde manden: „Næste år ved denne tid kommer jeg igen, og da har Sara født en søn!”

Sara stod i teltdøren bagved og hørte det hele. 11Både hun og Abraham var gamle, og hun vidste jo godt, at hun var alt for gammel til at få børn. 12Hun lo ved sig selv og tænkte: „Skulle jeg virkelig opleve den glæde, nu da både jeg og min mand er blevet for gamle?”

13Da sagde Herren til Abraham: „Hvorfor ler Sara og tænker, at hun umuligt kan få et barn? 14Skulle noget være umuligt for Gud? Næste år ved denne tid kommer jeg igen, og da har Sara en søn!”

15Da Sara hørte det, blev hun bange og forsvarede sig. „Jeg lo ikke!” løj hun. „Jo, du gjorde!” svarede Herren.

Abraham går i forbøn for Sodoma

16Så rejste mændene sig fra måltidet og gik videre i retning af Sodoma, og Abraham fulgte dem på vej. 17Undervejs sagde Herren til sig selv: „Hvorfor skulle jeg ikke indvi Abraham i mine planer? 18Abrahams efterkommere vil jo blive et mægtigt folk, og alle jordens folkeslag vil opnå velsignelse gennem ham. 19Jeg har jo netop udvalgt ham, for at han skal indprente sine efterkommere lydighed mod mig, ærlighed og godhed, så jeg kan lade det ske, jeg har lovet ham.”

20Herren sagde derfor til Abraham: „Jeg har hørt klageskrig fra Sodoma og Gomorra. Indbyggerne er frygtelig onde, og alt hvad de gør er ondt. 21Jeg er nu på vej derned for at se, om deres handlinger virkelig er så forfærdelige, som det lyder til.” 22De to andre mænd gik nu videre mod Sodoma, mens Abraham blev stående foran Herren. 23Så trådte han et skridt nærmere Gud og sagde: „Vil du virkelig udrydde de gode mennesker sammen med de onde? 24Hvis nu der findes 50 uskyldige mennesker i byen—vil du da stadig ødelægge den? Kan du ikke skåne byen for de 50 menneskers skyld? 25Du vil da vel ikke behandle de gode og de onde lige? Skulle han, som dømmer hele verden, ikke være retfærdig?”

26Herren svarede: „Hvis der findes 50 retsindige mennesker, vil jeg for deres skyld skåne byen.”

27Men Abraham fortsatte: „Siden jeg nu er begyndt at tale med min Herre, så lad mig fortsætte—vel vidende, at jeg kun er støv og aske. 28Hvad nu, hvis der kun er 45 retsindige? Vil du så ødelægge byen, bare fordi der mangler fem?” „Nej, jeg vil ikke ødelægge byen, hvis der er 45 retsindige.”

29„Hvad nu, hvis der kun er 40?” „Nej, heller ikke, hvis der er 40.”

30„Tag mig det ikke ilde op,” blev Abraham ved. „Hvad nu, hvis der kun er 30?” „Jeg vil skåne hele byen, hvis jeg finder 30,” svarede Herren.

31„Siden jeg har taget mig den frihed at tale til min Herre,” fortsatte Abraham, „tillad mig da at spørge nok en gang: Hvad nu, hvis der kun er 20?” „Så vil jeg for disse 20 retsindiges skyld skåne byen.”

32Da sagde Abraham: „Herre, bliv ikke vred! Dette er sidste gang: Hvad nu, hvis der kun findes ti?” Og Herren svarede: „Så vil jeg for disse ti uskyldiges skyld skåne hele byen.”

33Da Herren var færdig med at tale med Abraham, gik han videre, mens Abraham vendte hjem til sit telt.