Mithali 5 – NEN & AKCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 5:1-23

Onyo Dhidi Ya Uzinzi

15:1 Mit 1:8Mwanangu, sikiliza kwa makini hekima yangu,

sikiliza vizuri maneno yangu ya busara,

25:2 Mwa 2:7ili uweze kutunza busara

na midomo yako ihifadhi maarifa.

35:3 Za 55:21; Mit 2:16Kwa maana midomo ya mwanamke kahaba

hudondoza asali,

na maneno ya kinywa chake

ni laini kuliko mafuta;

45:4 Mhu 7:26; Ebr 4:12lakini mwisho wake ni mchungu kama nyongo,

mkali kama upanga ukatao kuwili.

55:5 Za 9:17; Mit 2:18Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo;

hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini.5:5 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

65:6 Mit 9:13; 30:20Yeye hafikiri juu ya njia ya uzima;

njia zake zimepotoka, lakini yeye hajui.

75:7 Mit 1:8-9Sasa basi wanangu, nisikilizeni;

msiache ninalowaambia.

85:8 Mit 6:20-29; 7:1-27Njia zenu ziwe mbali naye,

msiende karibu na mlango wa nyumba yake,

9usije ukatoa nguvu zako nzuri kwa wengine

na miaka yako kwa aliye mkatili,

105:10 Mit 29:3wageni wasije wakasherehekea utajiri wako

na jitihada yako ikatajirisha

nyumba ya mwanaume mwingine.

11Mwishoni mwa maisha yako utalia kwa uchungu,

wakati nyama na mwili wako vimechakaa.

12Utasema, “Tazama jinsi gani nilivyochukia adhabu!

Tazama jinsi moyo wangu ulivyodharau maonyo!

13Sikuwatii walimu wangu

wala kuwasikiliza wakufunzi wangu.

145:14 Mit 1:24-27; 6:33; 31:3Nimefika ukingoni mwa maangamizi kabisa

katikati ya kusanyiko lote.”

15Kunywa maji kutoka kwenye kisima chako mwenyewe,

maji yanayotiririka kutoka kwenye kisima chako mwenyewe.

16Je, chemchemi zako zifurike katika barabara za mji

na vijito vyako vya maji viwanjani?

17Na viwe vyako mwenyewe,

kamwe visishirikishwe wageni.

185:18 Wim 4:12-15; Kum 20:7; Mal 2:14Chemchemi yako na ibarikiwe

na umfurahie mke wa ujana wako.

195:19 Wim 2:9; 8:14Kulungu jike apendaye, kulungu mzuri:

matiti yake na yakutosheleze siku zote,

nawe utekwe daima na upendo wake.

205:20 Mit 2:16; 7:5Kwa nini mwanangu, utekwe na mwanamke kahaba?

Kwa nini ukumbatie kifua cha mke wa mwanaume mwingine?

215:21 Za 119:168; Hos 7:2; Yer 16:17; Ay 10:4; Ebr 4:13Kwa maana njia za mtu ni wazi kabisa mbele za Bwana,

naye huyapima mapito yake yote.

225:22 Za 9:16; Hes 32:23; Ay 18:9Matendo mabaya ya mtu mwovu humnasa yeye mwenyewe;

kamba za dhambi yake humkamata kwa nguvu.

235:23 Ay 4:21; 36:12Atakufa kwa kukosa nidhamu,

akipotoshwa kwa upumbavu wake mwenyewe.

Akuapem Twi Contemporary Bible

Mmebusɛm 5:1-23

Aguamammɔ Ho Kɔkɔbɔ

1Me ba, yɛ aso ma me nyansa;

tie me nhumu nsɛm no yiye,

2sɛnea ɛbɛma woahwɛ yiye,

na wʼano akora nimdeɛ.

3Efisɛ ɔbea aguaman ano sosɔ ɛwo,

na ne kasa yɛ fɔmm sen ngo;

4nanso awiei no, ɛyɛ nwen sen bɔnwoma,

ɛyɛ nam sɛ afoa anofanu.

5Nʼanan kɔ owu mu;

nʼanammɔntutu kɔ ɔda mu tee.

6Onsusuw ɔkwan a ɛkɔ nkwa mu ho;

nʼakwan yɛ kɔntɔnkye, nanso onnim.

7Enti afei, me mma, muntie me;

Monntwe mo ho mmfi nea meka ho.

8Ɔkwan a ɛmmɛn no no na momfa so;

mommmɛn ne fi pon ano,

9anyɛ saa a, mode mo ahoɔden bɛma afoforo

na mode mo mfe ama otirimɔdenfo,

10anyɛ saa a, ahɔho bɛfom mo ahonyade

na mo brɛ de ahonya akɔ afoforo fi.

11Mo nkwanna akyi, mubesi apini,

bere a mo honam ne mo nipadua asa no.

12Na moaka se, “Na mikyi ahohyɛso!

Me koma ampɛ nteɛso!

13Manyɛ osetie amma mʼakyerɛkyerɛfo

na mantie me kwankyerɛfo asɛm.

14Madu ɔsɛe ano

wɔ asafo no nyinaa mu.”

15Nom nsu fi wʼankasa ahina mu,

nsu a ɛteɛ fi wʼankasa abura mu.

16So ɛsɛ sɛ wʼasuti yiri fa mmɔnten so

na wo nsuwa kokɔ ɔman aguabɔbea ana?

17Ma ɛnyɛ wo nko ara de,

a wo ne ahɔho nkyɛ da.

18Nhyira nka wʼasubura

na wʼani nnye wo mmrantebere mu yere ho.

19Ɔte sɛ ɔtwe bere dɔfo, ɔwansan nuonyamfo;

ma ne nufu nsɔ wʼani daa

na ne dɔ nkyekyere wo.

20Me ba, adɛn nti na woma ɔbea aguaman kyekyere wo?

Adɛn nti na woda ɔbarima foforo bi yere kokom?

21Awurade hu onipa akwan nyinaa,

na ɔhwehwɛ ne nyinaa mu.

22Omumɔyɛfo nnebɔne sum no afiri;

na ne bɔne ahama kyekyere no papee.

23Wobewu, esiane ahohyɛso a wonni nti,

na wɔayera, esiane wɔn agyennyentwisɛm nti.