Mithali 23 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 23:1-35

1Uketipo kula chakula na mtawala,

angalia vyema kile kilicho mbele yako,

2na utie kisu kooni mwako

kama ukiwa mlafi.

323:3 Za 141:4Usitamani vyakula vyake vitamu

kwa kuwa chakula hicho ni cha hila.

423:4 Yn 6:27; 1Tim 6:9; Rum 12:16Usijitaabishe ili kuupata utajiri,

uwe na hekima kuonyesha kujizuia.

523:5 Mt 6:19; Mit 27:24Kufumba na kufumbua utajiri hutoweka,

huwa kama umepata mabawa ghafula,

ukaruka na kutoweka angani kama tai.

623:6 Za 141:4; Kum 15:9Usile chakula cha mtu mchoyo,

usitamani vyakula vyake vitamu,

723:7 Za 12:2kwa maana yeye ni aina ya mtu

ambaye kila mara anafikiri juu ya gharama.

Anakuambia, “Kula na kunywa,”

lakini moyo wake hauko pamoja nawe.

8Utatapika kile kidogo ulichokula,

nawe utakuwa umepoteza bure

maneno yako ya kumsifu.

923:9 Mit 9:7Usizungumze na mpumbavu,

kwa maana atadhihaki hekima ya maneno yako.

1023:10 Kum 19:14; Mit 22:28Usisogeze jiwe la mpaka wa zamani

wala kunyemelea kwenye mashamba ya yatima,

1123:11 Ay 19:25; Kut 22:22-24; Yer 50:34; Mit 15:25kwa kuwa Mtetezi wao ni mwenye nguvu,

atalichukua shauri lao dhidi yako.

1223:12 Mit 2:2Elekeza moyo wako kwenye mafundisho

na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.

1323:13 Mit 13:24; 19:18; 22:18; 22:15; 29:15, 16Usimnyime mtoto adhabu,

ukimwadhibu kwa fimbo, hatakufa.

1423:14 Mit 13:24; 19:18Mwadhibu kwa fimbo

na kuiokoa nafsi yake kutoka mautini.23:14 Mautini maana yake ni Kuzimu.

1523:15 Mit 23:24, 25; 29:3Mwanangu, kama moyo wako una hekima,

basi moyo wangu utafurahi,

1623:16 Mit 23:24utu wangu wa ndani utafurahi,

wakati midomo yako

itakapozungumza lililo sawa.

1723:17 Za 73:3; Mit 28:14Usiuruhusu moyo wako kuwaonea wivu wenye dhambi,

bali kila mara uwe na bidii katika kumcha Bwana.

1823:18 Za 37:1-4; Mit 24:14-20Hakika kuna tumaini la baadaye kwa ajili yako,

nalo tarajio lako halitakatiliwa mbali.

1923:19 Kum 4:9; Mit 28:7Sikiliza, mwanangu na uwe na hekima,

weka moyo wako kwenye njia iliyo sawa.

2023:20 Hab 2:15; Rum 13:13; Isa 5:22Usiwe miongoni mwa wanywao mvinyo,

au wale walao nyama kwa pupa,

2123:21 Mit 21:17; 19:23; 19:15kwa maana walevi na walafi huwa maskini,

nako kusinzia huwavika matambara.

2223:22 Law 19:32; Efe 6:1-2Msikilize baba yako, aliyekuzaa,

wala usimdharau mama yako atakapokuwa mzee.

2323:23 Mit 4:7; 17:16; Mt 13:44Nunua kweli wala usiiuze,

pata hekima, adabu na ufahamu.

2423:24 Mit 23:15-16; 10:1; 15:20Baba wa mwenye haki ana furaha kubwa,

naye aliye na mwana mwenye hekima humfurahia.

2523:25 Mit 10:1Baba yako na mama yako na wafurahi,

mama aliyekuzaa na ashangilie!

2623:26 Mit 5:1-6; Za 18:21Mwanangu, nipe moyo wako,

macho yako na yafuate njia zangu,

2723:27 Mit 22:14kwa maana kahaba ni shimo refu

na mwanamke mpotovu ni kisima chembamba.

2823:28 Mit 7:11-12; Mhu 7:26Kama mnyangʼanyi, hungojea akivizia,

naye huzidisha wasio waaminifu miongoni mwa wanaume.

2923:29 1Fal 20:16; Mit 20:1; Isa 5:11; Nah 1:10; Mt 24:49, 50; Efe 5:18Ni nani mwenye ole?

Ni nani mwenye huzuni?

Ni nani mwenye ugomvi?

Ni nani mwenye malalamiko?

Ni nani aliye na majeraha yasiyo na sababu?

Ni nani mwenye macho mekundu?

3023:30 Za 75:8; Efe 5:18; Mit 20:1; Efe 5:18; Za 75:8; Mit 9:2Ni hao wakaao sana kwenye mvinyo,

hao waendao kuonja mabakuli ya mvinyo uliochanganywa.

31Usiukodolee macho mvinyo wakati ukiwa mwekundu,

wakati unapometameta kwenye bilauri,

wakati ushukapo taratibu!

32Mwishowe huuma kama nyoka

na kutia sumu yake kama nyoka mwenye sumu.

33Macho yako yataona mambo mageni

na moyo wako kuwazia mambo yaliyopotoka.

34Utakuwa kama alalaye katikati ya bahari,

alalaye juu ya kamba ya merikebu.

3523:35 Mit 27:22; Yer 5:3; Kum 29:19; Isa 56:12; 2Pet 2:22Utasema, “Wamenipiga lakini sikuumia!

Wamenichapa, lakini sisikii!

Nitaamka lini

ili nikanywe tena?”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

箴言 23:1-35

1你若與官長同席,

要注意面對的是誰。

2如果你是貪吃的人,

就要節制食慾23·2 節制食慾」希伯來文是「把刀放在喉嚨上」。

3不可貪戀他的美食,

這美食是圈套。

4別為錢財耗盡心力,

要明智,適可而止。

5錢財眨眼之間消逝無蹤,

它必長出翅膀如鷹飛去。

6不要吃吝嗇人的飯,

不可貪圖他的美味。

7因為他總是精於算計,

嘴上說「請吃,請喝」,

心裡卻另有盤算。

8你必嘔出所吃的那點飯,

你說的美言都必枉費。

9不要和愚人說話,

他必藐視你的智言。

10不可挪移古時的界石,

不可侵佔孤兒的田地。

11因他們的救贖主強大,

祂必對付你,替他們伸冤。

12你要專心接受教誨,

側耳傾聽智言。

13不要疏於管教孩子,

杖責不會使他斃命,

14杖責能救他脫離死亡。

15孩子啊,

你若心裡有智慧,

我心裡也會歡喜。

16你的口若說正直的話,

我的內心也歡暢不已。

17不要心裡羡慕罪人,

要終日敬畏耶和華。

18這樣,你必前途光明,

你的盼望不會幻滅。

19孩子啊,聽我的話,

要有智慧,心守正道。

20不要結交酒肉朋友,

21因為好酒貪吃者必窮困,

貪睡的人必穿破衣爛衫。

22要聽從生養你的父親,

不可輕視年老的母親。

23要買真理、智慧、教誨和悟性,

不可賣掉。

24義人的父親喜樂無限,

智慧之子使父母歡欣。

25你要使父母快樂,

叫生你的人歡欣。

26孩子啊,把你的心交給我,

歡然走我的道路。

27妓女是深坑,淫婦是陷阱;

28她像強盜般埋伏,

使世間增添奸徒。

29誰有災禍?誰有憂傷?

誰有爭吵?誰有怨言?

誰無故受傷?誰兩眼發紅?

30就是那些沉迷醉鄉,

品嚐醇和之酒的人!

31雖然鮮紅的酒在杯中閃爍,

喝下去痛快,但不要盯著它。

32它終必像蛇一樣傷你,

像毒蛇一樣咬你。

33你的眼會看見怪異的景象,

你會神智不清,胡言亂語。

34你好像躺在怒海中,

又像臥在桅杆頂上。

35你會說:「人打我,我不痛;

人揍我,我不知。

什麼時候醒了,再乾一杯!」