Mithali 2 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 2:1-22

Faida Za Hekima

12:1 Mit 1:8Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu

na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,

22:2 Mit 22:17kutega sikio lako kwenye hekima

na kuweka moyo wako katika ufahamu,

32:3 Yak 1:5na kama ukiita busara

na kuita kwa sauti ufahamu,

42:4 Ay 3:21; Mt 13:44; 6:19-21na kama utaitafuta kama fedha

na kuitafuta sana kama hazina iliyofichwa,

52:5 Kum 4:6ndipo utakapoelewa kumcha Bwana

na kupata maarifa ya Mungu.

62:6 Ay 12:13; Lk 21:15; Yak 1:5Kwa maana Bwana hutoa hekima,

na kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.

72:7 Mwa 6:9; 15:1; Mit 30:5-6; Za 84:11Anahifadhi ushindi kwa ajili ya mwadilifu,

yeye ni ngao kwa wale wasio na lawama,

82:8 1Sam 2:9; Za 18:25kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki

na kuhifadhi njia ya waaminifu wake.

92:9 Kum 1:16Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki

na sawa: yaani kila njia nzuri.

102:10 Mit 14:33Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako,

nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako.

112:11 Mit 4:6Busara itakuhifadhi

na ufahamu utakulinda.

122:12 Mit 2:16; 3:13-18; 4:5Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu,

kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka,

132:13 Mit 4:19; Yn 3:19; Efe 4:18wale waachao mapito yaliyonyooka

wakatembea katika njia za giza,

142:14 Mit 15:21; Yer 11:15wale wapendao kutenda mabaya

na kufurahia upotovu wa ubaya,

152:15 Za 125:5; Mit 21:8ambao mapito yao yamepotoka

na ambao ni wapotovu katika njia zao.

162:16 Mit 6:20-29; 7:5-27Itakuokoa pia kutokana na mwanamke kahaba,

kutokana na mke aliyepotoka mwenye maneno

ya kushawishi kutenda ubaya,

172:17 Mal 2:14; Mwa 2:24aliyemwacha mwenzi wa ujana wake

na kupuuza agano alilofanya mbele ya Mungu.

182:18 Mit 5:5; 7:27; 9:18Kwa maana nyumba yake huelekea kwenye kifo

na mapito yake kwenye roho za waliokufa.

192:19 Mit 5:8; Mhu 7:26; Ebr 13:4Hakuna yeyote aendaye kwake akarudi,

au kufikia mapito ya uzima.

202:20 Ebr 6:12Hivyo utatembea katika njia za watu wema

na kushikamana na mapito ya wenye haki.

212:21 Za 37:29Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi,

nao wasio na lawama watabakia ndani yake.

222:22 Ay 18:17; Za 37:38; Kum 29:28Bali waovu watakatiliwa mbali kutoka nchi,

nao wasio waaminifu watangʼolewa kutoka humo.

Het Boek

Spreuken 2:1-22

1Mijn zoon, luister naar wat ik zeg en schat mijn aanwijzingen op hun waarde.

2Dan krijg je een oor voor de echte wijsheid en zal je verstand worden gescherpt.

3Als je inzicht probeert te krijgen en er wijsheid in je woorden doorklinkt,

4als je dat beschouwt als een zeer groot goed en moeite doet om het te verkrijgen,

5zul je merken wat eerbiedig ontzag voor de Here betekent. Dan zul je God werkelijk leren kennen.

6Want de Here is de bron van alle wijsheid. Uit alles wat Hij zegt, spreekt wijsheid en verstand.

7Hij geeft oprechte mensen houvast en is een beschermer van hen die zuiver leven.

8Die mensen blijven op de goede weg, de weg die Hij voor hen effent.

9Zo leer je begrijpen wat rechtvaardigheid is, wat eerlijkheid is en welke levensweg de juiste is.

10Wanneer je je die wijsheid eigen hebt gemaakt en geniet van je kennis,

11dan denk je na voordat je iets zegt en die bedachtzaamheid zal je beschermen.

12Beschermen tegen de man die slechte dingen zegt.

13Beschermen tegen hen die niet in oprechtheid geloven.

14Beschermen ook tegen de boosdoeners die lachen om allerlei wandaden,

15die de goede weg verlieten en kozen voor hun eigen kronkelpad.

16Beschermen ook tegen de vrouw die niet de jouwe is, maar met gevlei probeert jou in te palmen.

17Die vrouw die haar eigen man verlaat en daardoor zowel haar man als God ontrouw is.

18Want wat zij doet, leidt naar de dood.

19Wie met haar naar bed gaat, komt niet meer terug en zal de weg naar het leven niet vinden.

20Blijf dus de goede weg bewandelen en volg het voorbeeld dat oprechte mensen je geven.

21Want de aarde is voor hen die zuiver leven en God zal de oprechten nooit verlaten.

22Maar hun die zonder God door het leven gaan en zich niet aan Hem of aan hun naaste storen, staat uitroeiing te wachten. Zij worden vernietigd.