Mithali 14 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 14:1-35

114:1 Rut 3:11; Mit 24:3Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake,

bali mpumbavu huibomoa nyumba yake

kwa mikono yake mwenyewe.

214:2 Ay 12:4Yeye ambaye njia zake ni nyofu humcha Bwana,

bali yeye ambaye njia zake zimepotoka humdharau Mungu.

314:3 Mit 12:6; 10:13Mazungumzo ya mpumbavu huleta fimbo mgongoni mwake,

bali mwenye hekima hulindwa na maneno ya midomo yake.

414:4 Za 12:2; Mit 12:17Pale ambapo hakuna mafahali, hori ni tupu,

bali kutokana na nguvu za fahali huja mavuno mengi.

514:5 Kut 20:16; Za 12:2; Mit 6:19Shahidi mwaminifu hadanganyi,

bali shahidi wa uongo humimina uongo.

614:6 Mit 9:9; 17:24Mwenye mzaha huitafuta hekima na haipati,

bali maarifa huja kwa urahisi kwa anayepambanua.

7Kaa mbali na mtu mpumbavu,

kwa maana hutapata maarifa katika midomo yake.

814:8 Lk 12:20; 1Kor 3:19; Mit 15:28; 21:29Hekima ya mwenye busara ni kufikiria njia zake,

bali upumbavu wa wapumbavu ni udanganyifu.

914:9 Mit 1:22; 10:23Wapumbavu hudhihaki kujirekebisha kutoka dhambi,

bali wema hupatikana miongoni mwa wanyofu.

10Kila moyo hujua uchungu wake wenyewe,

wala hakuna yeyote awezaye kushiriki furaha yake.

1114:11 Za 72:7; Ay 8:15; Mit 3:33Nyumba ya mwovu itaangamizwa,

bali hema la mnyofu litastawi.

1214:12 Rum 6:21; Mit 12:15; 16:25Iko njia ionekanayo kuwa sawa kwa mtu,

bali mwisho wake huelekeza mautini.

1314:13 Mhu 2:2; 7:3-6Hata katika kicheko moyo waweza kuuma,

nayo furaha yaweza kuishia katika majonzi.

1414:14 2Nya 15:7; Mit 12:14Wasio na imani watapatilizwa kikamilifu kwa ajili ya njia zao,

naye mtu mwema atapewa thawabu kwa ajili ya njia yake.

1514:15 Mit 14:8Mtu mjinga huamini kila kitu,

bali mwenye busara hufikiria hatua zake.

1614:16 Kut 20:20; Mit 22:3Mtu mwenye hekima humcha Bwana na kuepuka mabaya,

bali mpumbavu hukasirika kwa hamaki na uzembe.

1714:17 Mit 28:25; 29:22Mtu anayekasirika kwa haraka hufanya mambo ya upumbavu,

naye mtu wa hila huchukiwa.

18Mjinga hurithi upumbavu,

bali wenye busara huvikwa maarifa kichwani kama taji.

1914:19 Mit 11:29Watu wabaya watasujudu mbele ya watu wema,

nao waovu kwenye malango ya wenye haki.

2014:20 Mit 19:4, 7Maskini huepukwa hata na majirani zao,

bali matajiri wana marafiki wengi.

2114:21 Mit 11:12; 19:17; Za 41:1Yeye anayemdharau jirani yake hutenda dhambi,

bali amebarikiwa yeye aliye na huruma kwa mhitaji.

2214:22 Mit 4:16-17Je, wale wanaopanga ubaya hawapotoki?

Bali wale wanaopanga kilicho chema

hupata upendo na uaminifu.

23Kazi zote zinazofanywa kwa bidii huleta faida,

bali mazungumzo matupu huelekea umaskini tu.

2414:24 Mit 14:8Utajiri wa wenye hekima ni taji yao,

bali upumbavu wa wapumbavu huzaa upumbavu.

2514:25 Mit 12:17Shahidi wa kweli huokoa maisha,

bali shahidi wa uongo ni mdanganyifu.

2614:26 Mit 19:23; Isa 33:6Yeye amchaye Bwana ana ngome salama,

na kwa watoto wake itakuwa kimbilio.

2714:27 Za 18:5; Mit 13:14Kumcha Bwana ni chemchemi ya uzima,

ili kumwepusha mtu na mitego ya mauti.

2814:28 2Sam 19:7Wingi wa watu ni utukufu wa mfalme,

bali pasipo watu mkuu huangamia.

2914:29 Mhu 7:8-9; Mit 15:18; Yak 1:19Mtu mwenye subira ana ufahamu mwingi,

bali anayekasirika haraka huonyesha upumbavu.

3014:30 Ay 5:2; Mdo 7:9; Mit 12:4Moyo wenye amani huupa mwili uzima,

bali wivu huozesha mifupa.

3114:31 Ay 31:15-16; Mit 17:5Yeye amwoneaye maskini huonyesha dharau kwa Muumba wao,

bali yeyote anayemhurumia mhitaji humheshimu Mungu.

3214:32 Za 34:21; Mit 6:15; Ay 13:15; 2Tim 4:18Waovu huangamizwa kwa matendo yao maovu,

bali hata katika kifo wenye haki hupata kimbilio.

3314:33 Mit 2:6-10Hekima hukaa katika moyo wa mwenye ufahamu

bali haijulikani miongoni mwa wapumbavu.

3414:34 Mit 11:11Haki huinua taifa,

bali dhambi ni aibu kwa watu wote.

3514:35 Es 8:2; Mt 25:14-30Mfalme hupendezwa na mtumishi mwenye hekima,

bali ghadhabu yake humwangukia

mtumishi mwenye kuaibisha.

Japanese Contemporary Bible

箴言 知恵の泉 14:1-35

14

1知恵のある女は自分の家を建て、

愚かな女は自分の家を自分で壊します。

2正しいこととは主をたたえること、

罪を犯すことは主をさげすむことです。

3高慢な者はむだ口をたたいて自分の尊厳を傷つけ、

知恵のある人は役に立つことを語って

人から尊敬されます。

4働かなければ、

手を汚さない代わりに収入もありません。

5真実な証人はうそをつかず、

偽りの証人はうそを語ります。

6人をさげすむ者に知恵は寄りつかず、

思慮のある人には、知恵のほうからやって来ます。

7正しい忠告をもらいたいなら、

愚か者を相手にしてはなりません。

8知恵のある人は先を見越し、

愚か者は自分をごまかして事実を直視しません。

9神の教えに背く者たちは過ちを犯し、

神を恐れる者たちは人を思いやります。

10悲しみも喜びも、真にわかるのはその人自身で、

他の人が完全に共有することはできません。

11悪者の働きは失敗し、

神を恐れる人だけが成功します。

12だれでも、広く歩きやすい道が正しい道と考えますが、

それは死に通じる道です。

13笑っても苦しみは隠せません。

笑ったあと、悲しみがそのまま残っています。

14信仰をなくした人は自分に嫌気がさしますが、

神を恐れる人の生活には活気があります。

15わきまえのない人は言われたことを鵜呑みにし、

慎重な人は将来をよく考えて行動します。

16賢い人は用心深く危険を避け、

愚か者は自信満々につき進みます。

17短気な人は愚かなことをし、

忍耐強い人をきらいます。

18愚か者は愚かさを報いとして得ますが、

賢い人は知識を得ます。

19悪人は、いつかは神を恐れる人に

頭を下げることになります。

20貧しい人は隣近所にさえ相手にされず、

金持ちは友に不自由しません。

21貧しい人を軽蔑してはいけません。

貧しい人に親切にすれば、自分も幸せになります。

22悪いことを企む者は道に迷い、

良いことを計画する人は神に愛されて安全です。

23まじめに働けば収入は増え、

むだ話ばかりしていると貧しくなります。

24知恵のある人は知恵をほめられ、

愚か者は愚かさを軽蔑されます。

25真実を言う証人は

無実の罪をはらしてくれますが、

偽りの証人は平気で人を裏切ります。

26神を恐れる人は頑健で、

子どもたちは安心して、その人に頼ります。

27主を恐れることはいのちの泉です。

その水を飲めば生きる力がわいてきます。

28民が増えるのは王にとって栄光であり、

民が減るのは王座の揺らぐしるしです。

29利口な人は腹を立てるのは愚かだと知っているので、

自分の感情を抑えます。

30心がおおらかだと長生きし、

激しやすい人は寿命を縮めます。

31貧しい人をいじめるのは、

その人たちを造った神をさげすむこと、

貧しい人を助けるのは神をほめたたえることです。

32神を信じる人には、

死ぬ時にも心の拠り所がありますが、

悪者は罪に押しつぶされます。

33知恵は聡明な人の心に住み、

愚か者がそれを聞くには

大声で叫ばなければなりません。

34神を敬うことは国を高め、

罪は民をおとしめます。

35やるべきことを心得ている召使は王に好かれ、

やっかいな召使は王の怒りを買います。